Tabia za Kitanzania zinazonikera...

Tabia za Kitanzania zinazonikera...

Dah hii ni mbaya sana...maana tukiwa watoto nakumbuka tulikuwa twaziokota na kuzipuliza kama maputo...dah!!

Tabia nyingine ya hovyo ni ile ya watu kutupa kondom zilizotumika sehemu za wazi kama vile barabarani/njiani. INAKERA SANA.
 
ila wanaume ndo wanakuwaga na hii tabia haswa mahali ambapo anaogopa kutangaza nia, ama aliwahi kubutuliwa. kuna mdada flani alisemwa na mkaka tukiwa chuo kuwa anatumia chemicals, anajichubua na anachoma sindano kunenepesha miguu coz hakuwaga hivyo akisoma primary. wakati mie ilisoma sekondari na huyo dada na alikuwa mzuri hivyo hivyo.
Yup...halafu sasa hata kukutana na wewe hawajawahi! Hawajui unafananaje....hata hawajui unaitwa nani...wanachojua ni habari za umbea tu wanazopeana.

Wajinga kabisa.
 
Yote hayo ni mazoea ya mtu. Hata umwambie, umweleze yeye kwake sawa na wala haimsumbui kwani ni mazoea yake au kiko kwenye damu. "Ni sawa na mtu kumpigia mbuzi gitaa kwa mategemeo atacheza muziki"
 
paliponikosha ni hapa nimekopi

4. Wale wote wanaotupa hovyo uchafu...

Mtu umemaliza kunywa maji yako ya uhai, au Kiroba n.k...kwa nini usihifadhi hicho kifungashio na ukakiwage sehemu stahiki mbele ya safari...
Yaani sisi Watanzania sijui lini tutajifunza kutumia akili....ndio maana kuna vitu vingi nadhani Mungu kaamua kutunyima kwa sababu ya tabia zetu za ajabu ajabu...
 
na wale wanaopenda kujichokonoa sehemu ambazo ni maalum halafu wanakupa wanakusalimia kwa mkoono huohuo waliojitoko toko huko sehemu nyeti ona hapa kuji.jpg
 
Halafu awe nawe siti moja kwenye daladala na mdomo wake uwe una "aleji" na mswaki,utatamani ushuke!

Hahahahaahahahaaaaa!!!! Umenifanya nicheke sana, halafu awe na harufu ya kwapa, ni lazima utatoa msaada wa siti kwa mzee au mama mwenye mtoto ili uweze kusimama. Duh! nahisi wewe unakaaaaa wapi paleeeee.......?? Mba....
 
Dah hii ni mbaya sana...maana tukiwa watoto nakumbuka tulikuwa twaziokota na kuzipuliza kama maputo...dah!!

Yaani Watu8, usinikumbushe mana nililia siku moja kiasi ilibidi nimpige mswaki mwanangu na kumpeleka hosp saa hiyo hiyo, baada ya kumkuta kaokota hiyo ndude na kulipuliza na kudai ni puto. Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii !!!! sitaki kukumbuka, na walaaniwe wote wanaotupa hizo condom hovyo.
 
Pole, natumai hakukuwa na madhara yoyote kwa ankal...

Yaani Watu8, usinikumbushe mana nililia siku moja kiasi ilibidi nimpige mswaki mwanangu na kumpeleka hosp saa hiyo hiyo, baada ya kumkuta kaokota hiyo ndude na kulipuliza na kudai ni puto. Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii !!!! sitaki kukumbuka, na walaaniwe wote wanaotupa hizo condom hovyo.
 
Mkuu watu8,

Kuna hizi tabia pia,
1. Kuongea na simu sehemu isiyotakiwa au mtu kuanza kupayuka ovyo mf. Hospitali, Benki.

2. Kutonawa mikono mara baada ya kutoka chooni/uani/msalani hasa wanaume watokapo haja ndogo, wanawake wabadilishapo pedi, na kukimbilia kusalimiana na watu.

3.Wanaokohoa/kupiga chafya hovyo bila kujikinga,

4. Kuna watu wenye tabia ya uchafu, wanapotumia "chewing gum/Big G" wanaebandika kwenye makochi, kuta, viti vya ofisi, majumbani.
 
Last edited by a moderator:
4. Kuna watu wenye tabia ya uchafu, wanapotumia "chewing gum/Big G" wanaebandika kwenye makochi, kuta, viti vya ofisi, majumbani.

Hii ya mwisho ni mbaya sana aisee haswa majumbani kwani mara nyingi watoto wadogo huwa wanazibandua na kuanza kuzitafuna tena
 
Wengine walikua wanaandika kwenye kuta...mathalani "Akumbukwe Jodoki Kalimilo"
Ukiwa mtu mzima unabaki unajishangaa ilikuaje na sidhani kama utasema ni wewe hasa ukizingatiwa maandishi yameandikwa chooni tena kwa kinyesi
 
Hawa watu sijui hawajawahi kwenda shule au ni ulimbukeni! Yaani wasimuone mwanafunzi anasogelea gari, kirahisi tu utasikia "Oyaa limeshajaa"...
Magari yenyewe hata sio yao na wala hawana ndoto za kuwa na magari miaka 900!!!! wanabore sana!!!!
 
Back
Top Bottom