Kiranga ,sijakuuliza kuhusu watu wa nchi zingine kama wana tabia hizo
Lakini imedaiwa tabia hizi ni za Kitanzania, kitu ambacho kimenifanya nichunguze kama kweli hizi tabia ni za kitanzania? Nakuta zipo dunia nzima, kwa nini zinaitwa za Kitanzania?
'
Pia sijakuuliza ni nchi gani ina watu wengi wenye tabia hizo,wala sijashandanisha nchi na nchi ili kujua nani ni kidedea
Ungekuwa na justification kidoogo kudai tabia hizi ni za Kitanzania kama kungekuwa na utafiti wa kuonesha kwamba Watanzania ndio wanaoongoza katika tabia hizi, ingawa hata hapo napo kama wangekosa monopoly kusema hizi tabia ni za Kitanzania kutakuwa ni kukosea kama vile kusema mchezo wa Marathon ni wa Wakenya. Kwa hiyo hata pale ambapo ungekuwa na a dubious justification, umeikosa.
'
Wala halikua lengo langu kujua hayo,so you can keep all that by yourself,
Hapana, usipotaka kuelezewa kwa mapana usiniulize swali. Kiranga si mtu wa kuelezea vitu juu juu.
nilichokuuliza kama watanzania wana tabia hizo ama la,nashukuru kwa kunijibu
Hilo by the way ndilo lilikuwa jibu la summary, sasa ungepata jibu refu linalokwenda kwenye academic research zinazo debunk the entire notion of the centrality of tribes and the tangibility of nation states sijui ungesemaje.
Sasa nakuuliza,hao wenye tabia hizo ambao umekubali ni watanzania,sasa kuna ubaya gani kwa mtoa mada kuwaita Watanzania?
Kwa sababu hawafanyi mambo hayo kutokana na utanzania wao, wanafanya mambo hayo kwa uchafu, ujinga, upumbavu wao. Kwa hiyo, tusems "Tabia za kipumbavu zinazonikera" etc. Kusema "Tabia za kitanzania zinazonikera" halafu kulist hizi tabia ambazo Watanzania wengine hatuna, kunatutukanisha Watanzania wote, wenye tabia hizo na wasio na tabia hizo, na vivyo hivyo kunawaacha wasio Watanzania wenye tabia hizo.
Ukiongelea kukerwa na "tabia ya Kitanzania" ya kukojoa ovyo, akija M-Nepal ambaye ndiye mara yake ya kwanza kufika Tanzania na hana contact na Watanzania akikojoa ovyo, utaona sawa? Tabia ya Kitanzania kaipata wapi huyu?
Kusema tabia za uchafu, ujinga na upumbavu kwa jina la "tabia za Kitanzania" ni kukosa kuelewa kwamba hizi tabia hazitokani na utanzania, kwani zingetokana na utanzania zisingekuwepo kwa wasio Watanzania na Watanzania wote wangekuwa nazo.