chakutaka (Join date: 6th February, 2015),
rallphryder (Join date: 25th January, 2015) na
Bhupe (Join date: 11th February, 2015)...yawezekana wote si wageni hapa JF ila naomba niwafahamishe kuwa wengine Prof. Muhongo tulikuwa na bahati ya kumfahamu toka akiwa shule ya msingi. Kwa majibu ya fedhuli mnayoyatoa hapa mnapokabiliwa na hoja pingamizi, ni vigumu kuwatofautisha na tabia ya Prof. Muhongo kwani zinashabahiana.
Katikati ya mwezi wa
November, 2014 Prof. Muhongo alinukuliwa akitoa kauli hii,
"sitishwi na sitajiuzulu kwa kashfa ya ESCROW." Wengine wetu tuna kumbukumbu ya hii taarifa, nanukuu;
Katika kikao cha ndani ya CCM, Waziri wa Nishati Prof. Sospeter Muhongo amesema bayana kwamba hatishwi na wababaishaji na kamwe hawezi kujiuzulu kutokana na chuki za mafisadi wanaopigania vitalu vya gesi na kama atalazimika kujiuzulu siyo bunge litayumba bali ardhi ya Tanzania itatikisika.
Miezi miwili na nusu baadaye
January 24, 2015, Waziri huyo mtaalamu wa miamba, alilazimika kujiuzulu kufuatia
shinikizo la muda mrefu la kumtaka afanye hivyo au awajibishwe, kufuatia mapendekezo ya bunge lililopita, lililoiagiza Serikali kuchukua hatua dhidi ya viongozi wote na watendaji waliohusika na kashfa ya akaunti ya Tegeta Escrow akiwemo
Prof. Sospeter Muhongo.
chakutaka (Join date: 6th February, 2015),
rallphryder (Join date: 25th January, 2015) na
Bhupe (Join date: 11th February, 2015)...leo ni tarehe
12 Fenruary 2015 na wengi wetu bado tukisubiri ahadi ya Prof. Muhongo, ninyi mnatuletea muziki wa kitoto uliochuja na hauchezeki. Nawashauri muisome hili jamvi letu kwa makini ili angalau muijue na kuielewa...JF inatunza kumbukumbu!
Prof. Muhongo might have been a
powerhouse from wherever Kikwete picked him but to majority of us he is but a
blown out fuse and do you know what we do to a blown fuse? We throw it into its rightful place; the dust bin, trash can or whatever you wanna call it. Please spare us the trouble, money and pain...go back to where you came from; some of us are sick and tired of being reminded of this sick and rotten system.