TODAYS
JF-Expert Member
- Apr 30, 2014
- 13,749
- 21,202
Mhashamu Askofu Augustino Shao wa Zanzibar ametimiza Jubilei ya miaka 25 katika utumishi wa kanisa la Roman Catholic huko Zanzibar.
Kwenye sherehe zilizohudhuliwa na wananchi mbalimbali wakiwemo viongozi wa kidini, askofu Shao kwenye salamu zake kwa Rais wa Zanzibar, amezungumzia mambo mbalimbali aliyokumbana nayo akiwa katika utumishi wa kanisa, moja au baadhi ni Usafirishaji haramu wa watu kwenda nje ya nchi na uhamiaji wanatumika kutoa pasipoti pasipo utaratibu.
Amesema watu wanasafirishwa nje kwa kuhadaiwa kazi nzuri lakini mbele wanabadilishiwa kile walichoahidiwa na kwenda kufuga nguruwe au kazi za hatari.
Kwa upande mwingine ameongelea kuhusu ardhi ambapo ni tatizo kubwa Zanzibar, yaani mkristo kupata ardhi ni haiwezekani, hasa ukifahamika kutoka bara kama Yohana hupewi.
"Siyo kila mkristo anakuja kujenga kanisa, kanisa halijengwi na familia bali na taasisi kama madhehebu", alisema askofu Shao.
Aliiomba Serikali ifikirie wanapopima viwanja waweke kipaumbele pia kwa mashirika na taasisi za kidini, sababu kanisa linatizama mbele na si kuwapa kiwanja size ya 20x20.
Aliongeza kuwa "Katiba inatoa nafasi kwa raia kuwa na usawa, haiwezekani ukienda bara unachukua ardhi ila ukija Zanzibar hupewi, ifike mahali tuangalie usawa, ukipenda kula vya mwenzako na wewe kubali kuliwa vyako".
Kwenye sherehe zilizohudhuliwa na wananchi mbalimbali wakiwemo viongozi wa kidini, askofu Shao kwenye salamu zake kwa Rais wa Zanzibar, amezungumzia mambo mbalimbali aliyokumbana nayo akiwa katika utumishi wa kanisa, moja au baadhi ni Usafirishaji haramu wa watu kwenda nje ya nchi na uhamiaji wanatumika kutoa pasipoti pasipo utaratibu.
Amesema watu wanasafirishwa nje kwa kuhadaiwa kazi nzuri lakini mbele wanabadilishiwa kile walichoahidiwa na kwenda kufuga nguruwe au kazi za hatari.
Kwa upande mwingine ameongelea kuhusu ardhi ambapo ni tatizo kubwa Zanzibar, yaani mkristo kupata ardhi ni haiwezekani, hasa ukifahamika kutoka bara kama Yohana hupewi.
"Siyo kila mkristo anakuja kujenga kanisa, kanisa halijengwi na familia bali na taasisi kama madhehebu", alisema askofu Shao.
Aliiomba Serikali ifikirie wanapopima viwanja waweke kipaumbele pia kwa mashirika na taasisi za kidini, sababu kanisa linatizama mbele na si kuwapa kiwanja size ya 20x20.
Aliongeza kuwa "Katiba inatoa nafasi kwa raia kuwa na usawa, haiwezekani ukienda bara unachukua ardhi ila ukija Zanzibar hupewi, ifike mahali tuangalie usawa, ukipenda kula vya mwenzako na wewe kubali kuliwa vyako".