Suala la ardhi Zanzibar: Askofu Augustino Shayo apiga msumari wa moto mbele ya Rais Mwinyi

TODAYS

JF-Expert Member
Apr 30, 2014
13,749
21,202
Mhashamu Askofu Augustino Shao wa Zanzibar ametimiza Jubilei ya miaka 25 katika utumishi wa kanisa la Roman Catholic huko Zanzibar.

DSC_0158.JPG

Kwenye sherehe zilizohudhuliwa na wananchi mbalimbali wakiwemo viongozi wa kidini, askofu Shao kwenye salamu zake kwa Rais wa Zanzibar, amezungumzia mambo mbalimbali aliyokumbana nayo akiwa katika utumishi wa kanisa, moja au baadhi ni Usafirishaji haramu wa watu kwenda nje ya nchi na uhamiaji wanatumika kutoa pasipoti pasipo utaratibu.

Amesema watu wanasafirishwa nje kwa kuhadaiwa kazi nzuri lakini mbele wanabadilishiwa kile walichoahidiwa na kwenda kufuga nguruwe au kazi za hatari.

Kwa upande mwingine ameongelea kuhusu ardhi ambapo ni tatizo kubwa Zanzibar, yaani mkristo kupata ardhi ni haiwezekani, hasa ukifahamika kutoka bara kama Yohana hupewi.

"Siyo kila mkristo anakuja kujenga kanisa, kanisa halijengwi na familia bali na taasisi kama madhehebu", alisema askofu Shao.

Aliiomba Serikali ifikirie wanapopima viwanja waweke kipaumbele pia kwa mashirika na taasisi za kidini, sababu kanisa linatizama mbele na si kuwapa kiwanja size ya 20x20.

Aliongeza kuwa "Katiba inatoa nafasi kwa raia kuwa na usawa, haiwezekani ukienda bara unachukua ardhi ila ukija Zanzibar hupewi, ifike mahali tuangalie usawa, ukipenda kula vya mwenzako na wewe kubali kuliwa vyako".
 
hii ndio sababu mojawapo inayonifanya nione kichefuchefu kwenye muungano...na nikikutana na mzanzibari nisiwe na moyo wa kushirikiana naye. mtaniwia radhi kwa kusema ukweli ulioko moyoni mwangu.

kwasababu hata kwa raia wa kawaida achana na institutions, ukienda dsm, kigamboni, kuna wazanzibar wanamiliki ardhi wapendavyo, ukienda mikoani kuna wazanzibar wananunua maeneo wapendavyo. ila sisi tukienda kule, ......., kingine, kuona dini zingine hazitakiwi, kuchapa viboko wakristo wasiofunga wanaokula wakati wa ramadhani....ni jambo ambalo kwa wazanzibar wote wanaona ni sahihi, ila mimi linanitia simanzi sana.
 
Write your reply...mm siwezi kuwalaumu wazanzibar ila nitalaumu mfumo ambao n serikari.maana wao ndio wenye mamlaka ya kutoa ardhi,ila ina kera ukienda kwao wakijua n wa bara kumiliki ardhi ni ngumu sana.
 
Suala la ardhi ni jambo gumu na mtambuka haswa.....

Hivi Zanzibar kuna msikiti gani ambao umepewa mathalani heka 30 ?!!!

Tunajua ardhi ya Zanzibar ni ndogo sasa inakuwaje makanisa kupewa heka nyingi ambazo ndani yake kutakuwa na uzalishaji mali na mambo mengineyo?!!!

Kwani heka ngapi za ardhi zitakazotolewa zitaonekana kuwaridhisha?!!!!

#Siempre JMT🙏
 
Nadhani issue siyo kugawana nao au kujazana unguja au pemba, tatizo ni slogan ya chetu ni chao na chao ni chao.
Hayati baba wa taifa hakuuangalia moyo wake katika masuala mtambuka ya muungano ,ardhi ikiwemo kama unavyouangalia wewe......
 
hii ndio sababu mojawapo inayonifanya nione kichefuchefu kwenye muungano...na nikikutana na mzanzibari nisiwe na moyo wa kushirikiana naye. mtaniwia radhi kwa kusema ukweli ulioko moyoni mwangu. kwasababu hata kwa raia wa kawaida achana na institutions, ukienda dsm, kigamboni, kuna wazanzibar wanamiliki ardhi wapendavyo, ukienda mikoani kuna wazanzibar wananunua maeneo wapendavyo. ila sisi tukienda kule, ......., kingine, kuona dini zingine hazitakiwi, kuchapa viboko wakristo wasiofunga wanaokula wakati wa ramadhani....ni jambo ambalo kwa wazanzibar wote wanaona ni sahihi, ila mimi linanitia simanzi sana.
Watanganyika wakiruhusiwa kununua ardhi Zanzibar si itaisha!!..Kuna ardhi kubwa bara,kimekushinda nini kununua mpaka uvuke maji!!?
 
Back
Top Bottom