Somo kutoka Urusi: Ili Taifa lipate mafanikio lazima kuwe na "consistency" kwa viongozi wa wandamizi na nguli

Nchi zilizofanikiwa ziliachana na utamaduni wakutegemea watu,wakawekeza kwenye mifumo imara inayosimamia kila sekta ndo maana mambo yao mengi yanaenda kwenye mtiririko miaka mingi ata kama viongozi watakua wanabadilika.Hayo mambo yakua na hao unaowaita nguli wakukaa muda mrefu wala sio msaada kwa nchi kama watakua hawajali kuboresha maisha ya wananchi wao.na mifano ipo mingi ,wengi wao wanaishia kua mafisadi.Hao nguli wa urusi wengi ni rafiki zake na putin nasio kwamba kuna chochote cha maana zaidi ya kikundi cha wachache kula mema ya nchi.
Acheni kukaririshwa mambo ya ajabu. Hiyo mifumo nani anaii oparate.
Brother soma historia hakuna Taifa limewahi kuinuka bila kuwa na kiongoza au viongozi shupavu. Hao US, Britain sijui German na wengine. Wapo hapo kwa sababu wapo viongozi shupavu waliwahi kuwapata, wakafanya makubwa. Endeleeni lidanganyana eti mifumo.
Hao wenye mifumo mbona wanacharuana kila mwaka. Si waache hiyo mifumo iwaongoze.
 
Tunae kapitain joji mkuchika nguli wa mifumo ya kimkakati ya taifa..
Nakubaliana na wewe. Tunatakiwa angalau kwa miaka 10 hadi 15 tunakuwa na watu wa aina yake ndani ya Serikali na katika level hizo
 
Hili ni somo ambalo Urusi wamelitumia na likawapa mafanikio makubwa sana hasa ndani ya hii miongo miwili ya Rais Putin.

Ni somo ambalo China sasa wamelichukua na naona linaendelea kuwalipa. Hata jirani zetu Rwanda linawalipa.

Ni somo la kuwapa viongozi Nguli na waandamizi muda wa kutosha kusimamia mipango ya muda mrefu na kupanga mipya. Kwenye sakata linalogonga vichwa mwezi Sasa kati ya Urusi na Ukraine(NATO) Kuna miamba kadhaa upande wa Urusi inasikika mara kwa mara, matharani.

PUTIN.
1.Sergei Lovrov, Waziri wa mambo ya nje.
2. Dmitry Peskov, Msemaji wa Ikulu na na Deputy chief of staff.
3. Anatoly Antonov, Balozi wa Urusi Marekani.
4. Sergei Ivanov, Mkuu wa baraza la usalama.
5.Dmitry Medvedev, Naibu Mwnyekiti baraza la Taifa la usalama.
6. Sergei Shoigu. Waziri wa Ulinzi.

Ndugu zanguni hawa ni miamba wachache ambao nimeona angalau nitolee mfano.
Ukiwaangalia hawa watu kila mtu ni nguli wa eneo fulani na wapo kwenye serikali si chini ya miaka 10.
Miamba wanaweza wakawa wanahama kutoka eneo moja kwenda lingine lakini wapo.
Ukichukua serikali nyingi za sasa hata US ukawapambanisha na hawa Miamba ni kama unawaonea tu aise. Yaani Hawa maimba ni Galaticos.

Putin yupo hapo tangu 2000, amepambana na Bush, Obama na kisiki Trump. Amepitia mikiki mikiki anawajua US and Co in and out. Babu Biden kwake Hana jipya.

Sergei Lavrov yupo foreign ministry tangu 2004. Amepambana na Condi, amepambana na kina Pompeo and Co. Huyu Blinken anamuona mrembo tu aise.Kabla ya hapo alikuwa balozi umoja wa mataifa, anazijua Kona zote, diplomasia imekaa. Miaka 18 kwenye foreign ministry.

Mwamba Peskov yupo Klemrin tangu miaka ya 2006. Ni mwamba kweli kweli kwenye usemaji. Anawajua Westerners inje ndani hawampi kichwa hata kidogo kwenye propaganda aise. Jumlisha mwamba Anatoly Antonov, amewahi kuwa naibu waziri wa Ulinzi na mambo ya nje, Dmitry Medvedev, Sergei Ivanov.N.k.

Kwahiyo ukiona Urusi anawatoa watu kamasi, moja ya msingi ni huu, kuwa na Nguli, na veterans kwenye maeneo tofauti tofauti ambao wanajua uhuni wote wa dunia hii. Ambao wanajua chocho zote na wanaoweza kupanga Jambo likapangika.
Sisi huku kila baada ya miaka miwili sura mpya, hawajulikani wametoka wapi. Anayejitahidi anakaa miaka mitano na wale wanaodumu ni wale wenye sifa za uchawa, very unproffesionall.

Yaani kwetu ukimuangalia waziri huoni ule uzito kwenye nafasi aliyopo. Huoni kitu Cha maana alichokifanya hapo alipo.
Wizara ukiifanyia tathmini leo haina tofauti na ilivyokuwa 2004. Labda yamebadilika majengo, magari na watu. Huoni Wanaume wa shoka waliokaa pale wanaosimamia vitu vya maana. Ni watu wanakuja wanapiga salary ya waziri wanaondoka, anakuja mwingine anapiga Salary anaondoka.

Ndugu zanguni kwa mtindo huu ni k hatuwezi kupiga hatua.
Nadhani tufike mahali tuweke utaratibu tuwape viongozi waandamizi mda wa kutosha, wapange mipango, watafute wandani wao wa kuwasaidia kusimamia mipango. Miaka mitano ni mda wa kujifunza. Baada ya hapo aangalau wapewe miaka mingine 10 ili sasa wafanye kazi. Tuanze na Chifu, tumpe hadi 2035.

Baada ya miaka hii minne atakuwa amejifunza Sasa baada ya hapo ataanza kupanga na kusimamia mipango ya Inchi na atafafuta watu wa kumsaidia ambao ni nguli na ambao atawaamini kwa mda mrefu atakuwa ameilewa serikali na atakuwa amepata nafasi ya kuwajua vizuri watu wanaomfaa. Hatahadaika na vipara na miwani au skafu za kijani.

Ndugu zanguni hata hapa kwetu somo lipo. Hapo tu Ufipa, CHADEMA imekua taasisi imara kwakuwa yupo mwamba, ameaminiwa na akapewa mda wa kutosha karibia 18 sasa. Amejifunza akazielewaa siasa na sasa za bongo na anawatoa kamasi wanakijani, ameijenga CDM. Sasa ni Taasisi imara kiasi kwamba 2015 Watanzania walitaka kuipa dora. Kama tunaona Urusi mbali tuchukue basi hata hilo somo la hapo Ufipa.

Tunazidiwa akili hadi na Zito jamani. Mkuu wa Chama, Ayatola, mbona ameshaliona mapema hilo, akaazima pale Tehran.
Umeandika unazi na umekurupuka.
 
Punguz kusoma na kusikiliz propaganda za west.
Tafuta habari, soma utajua ukweli ni upi.

Eti russia ilikuwa aichukue ukrain kwa siku mbili tatu, umesikia wapi ujinga huu?

By way wanasema leo na jana walitishia mbwa kiev kapital ili jamaa wakomae kule, kaxi iee rahisi huko donbas, na wamefanikiwa.

Kwanini hawakusimulii hiyo chenga ya mwili?
Mkuu habari za kweli unadhani utazipata wapi? Zile za west unasemaq zinapropaganda,hata za upande wa pili hazikosi propaganda pia,na hiyo ni moja ya principle za vita,hutakiwi kuripoti ukweli unaoendelea kwenye uwanja wa mapambano,warusi wamechinjwa sana Ukraine lakini wao hawezi wakakutangazia wamevipa maagizo vyombo vyao vya habari nini cha kuandika,shusheni jazba ukweli mtaujua baadae.
 
Duh, na wewe unaamini Urusi imerudishwa miaka hamsini nyuma?

Aiseee, nchi yetu hii tuna matatizo kwelikweli na ufahamu wa mambo yalivyo ya wananchi wetu. Hili ni tatizo kubwa sana, na hatuwezi kuendelea tukiwa na watu wa kiwango hiki cha kukosa ufahamu.
Mpaka hapo tumeiahaendelea maendeleo gani unataka? Kilaq kaya Ina choo chake,waqtu wanamwamko wa kuwapeleka watoto shule,ufaulu umeongezeka mashuleni,sasa wewe unataka nini? au unataka turushe rocket yenye satellite kwenda anga za juu ndo uamini kwamba sisi watanzania tumeendelea?
 
Urusi ndio nchi yenye mafanikio zaidi duniani? GDP yake ni ngapi? GDP per capita ni ngapi? HDI yake ipoje? wnanchi wake wana furaha kiasi gani?
acha upumbavu, mkitaka kuongozwa n madikteta nendeni Burundi au Uganda hapo
NANI ALIYEKWAMBIA KUWA NA GDP KUBWA NDIO MAFANIKIO?,HATA DADA SAMIA ATAKUFA ATAKUACHA MJINGA,
 
Mpaka hapo tumeiahaendelea maendeleo gani unataka? Kilaq kaya Ina choo chake,waqtu wanamwamko wa kuwapeleka watoto shule,ufaulu umeongezeka mashuleni,sasa wewe unataka nini? au unataka turushe rocket yenye satellite kwenda anga za juu ndo uamini kwamba sisi watanzania tumeendelea?
EeeenHeee Heeee!

Na wewe umetokea sayari gani, au makazi yako ni pangoni pasipofikiwa na mwanga wala sauti?

Hata uandishi wenyewe ni wa shida, takwimu unazoweka kama ushahidi ni takataka!

Kwa hiyo kiwango cha elimu yako ndiyo tukichukue kama kielelezo cha maendeleo ya nchi yako uliyonayo kichwani mwako?
 
Kama viongozi wa Urusi unadhani wanauwezo mkubwa wa kuongoza na kutoa maamuzi mazuri kuliko hawa wa kwetu,basi wasingeingia mkenge wa kuivamia Ukraine,uvamizi ambao umepelekea nchi za magharibi kuiwekea Urusi vikwazo vya uchumi ambavyo vimeirudisha Urusi miaka 50 nyuma kimaendeleo.
KAbla ya hi vita uliwahi kujua sarafu ya Urusi inaitwaje? Anyway, kila mtu na fikra zake; i think nchi kama India sasa hivi zinatajirika sana kupitia hu mgogoro, mafuta ya Urusi mengi yanauzwa India kwa bei rahisi halafu India ana process then tunakuja kuuziwa sisi; hebu pia prot graph ya thamani ya pesa ya Urusi ilivyokua kabla ya vita na wakati hu wa vita; mkuu, vita ni biashara. For your information, USA anapenda hi vita iendelee ili baadae aje afanye biashara kubwa sana na Ukraine, zile silaha na pesa hatoi bure, hakunaga kitu cha namna hiyo kwenye hi sayari inayoitwa DUNIA
 
Hili ni somo ambalo Urusi wamelitumia na likawapa mafanikio makubwa sana hasa ndani ya hii miongo miwili ya Rais Putin.

Ni somo ambalo China sasa wamelichukua na naona linaendelea kuwalipa. Hata jirani zetu Rwanda linawalipa.

Ni somo la kuwapa viongozi Nguli na waandamizi muda wa kutosha kusimamia mipango ya muda mrefu na kupanga mipya. Kwenye sakata linalogonga vichwa mwezi Sasa kati ya Urusi na Ukraine(NATO) Kuna miamba kadhaa upande wa Urusi inasikika mara kwa mara, matharani.

PUTIN.
1.Sergei Lovrov, Waziri wa mambo ya nje.
2. Dmitry Peskov, Msemaji wa Ikulu na na Deputy chief of staff.
3. Anatoly Antonov, Balozi wa Urusi Marekani.
4. Sergei Ivanov, Mkuu wa baraza la usalama.
5.Dmitry Medvedev, Naibu Mwnyekiti baraza la Taifa la usalama.
6. Sergei Shoigu. Waziri wa Ulinzi.

Ndugu zanguni hawa ni miamba wachache ambao nimeona angalau nitolee mfano.
Ukiwaangalia hawa watu kila mtu ni nguli wa eneo fulani na wapo kwenye serikali si chini ya miaka 10.
Miamba wanaweza wakawa wanahama kutoka eneo moja kwenda lingine lakini wapo.
Ukichukua serikali nyingi za sasa hata US ukawapambanisha na hawa Miamba ni kama unawaonea tu aise. Yaani Hawa maimba ni Galaticos.

Putin yupo hapo tangu 2000, amepambana na Bush, Obama na kisiki Trump. Amepitia mikiki mikiki anawajua US and Co in and out. Babu Biden kwake Hana jipya.

Sergei Lavrov yupo foreign ministry tangu 2004. Amepambana na Condi, amepambana na kina Pompeo and Co. Huyu Blinken anamuona mrembo tu aise.Kabla ya hapo alikuwa balozi umoja wa mataifa, anazijua Kona zote, diplomasia imekaa. Miaka 18 kwenye foreign ministry.

Mwamba Peskov yupo Klemrin tangu miaka ya 2006. Ni mwamba kweli kweli kwenye usemaji. Anawajua Westerners inje ndani hawampi kichwa hata kidogo kwenye propaganda aise. Jumlisha mwamba Anatoly Antonov, amewahi kuwa naibu waziri wa Ulinzi na mambo ya nje, Dmitry Medvedev, Sergei Ivanov.N.k.

Kwahiyo ukiona Urusi anawatoa watu kamasi, moja ya msingi ni huu, kuwa na Nguli, na veterans kwenye maeneo tofauti tofauti ambao wanajua uhuni wote wa dunia hii. Ambao wanajua chocho zote na wanaoweza kupanga Jambo likapangika.
Sisi huku kila baada ya miaka miwili sura mpya, hawajulikani wametoka wapi. Anayejitahidi anakaa miaka mitano na wale wanaodumu ni wale wenye sifa za uchawa, very unproffesionall.

Yaani kwetu ukimuangalia waziri huoni ule uzito kwenye nafasi aliyopo. Huoni kitu Cha maana alichokifanya hapo alipo.
Wizara ukiifanyia tathmini leo haina tofauti na ilivyokuwa 2004. Labda yamebadilika majengo, magari na watu. Huoni Wanaume wa shoka waliokaa pale wanaosimamia vitu vya maana. Ni watu wanakuja wanapiga salary ya waziri wanaondoka, anakuja mwingine anapiga Salary anaondoka.

Ndugu zanguni kwa mtindo huu ni k hatuwezi kupiga hatua.
Nadhani tufike mahali tuweke utaratibu tuwape viongozi waandamizi mda wa kutosha, wapange mipango, watafute wandani wao wa kuwasaidia kusimamia mipango. Miaka mitano ni mda wa kujifunza. Baada ya hapo aangalau wapewe miaka mingine 10 ili sasa wafanye kazi. Tuanze na Chifu, tumpe hadi 2035.

Baada ya miaka hii minne atakuwa amejifunza Sasa baada ya hapo ataanza kupanga na kusimamia mipango ya Inchi na atafafuta watu wa kumsaidia ambao ni nguli na ambao atawaamini kwa mda mrefu atakuwa ameilewa serikali na atakuwa amepata nafasi ya kuwajua vizuri watu wanaomfaa. Hatahadaika na vipara na miwani au skafu za kijani.

Ndugu zanguni hata hapa kwetu somo lipo. Hapo tu Ufipa, CHADEMA imekua taasisi imara kwakuwa yupo mwamba, ameaminiwa na akapewa mda wa kutosha karibia 18 sasa. Amejifunza akazielewaa siasa na sasa za bongo na anawatoa kamasi wanakijani, ameijenga CDM. Sasa ni Taasisi imara kiasi kwamba 2015 Watanzania walitaka kuipa dora. Kama tunaona Urusi mbali tuchukue basi hata hilo somo la hapo Ufipa.

Tunazidiwa akili hadi na Zito jamani. Mkuu wa Chama, Ayatola, mbona ameshaliona mapema hilo, akaazima pale Tehran.
Kambarage alijaribu huo ungangari matokeo yake Nchi ilidondokea kwenye umaskini wa kutumia majani kufulia nguo huo ubabe unaousifia miaka mi2 ijayo utaona kitakachotokea URUSI ktk uchumi na Utawala.
Dunia ya leo ubabe Aina ya urusi au Korea kaskazini haulipi Tena.
 
Sio lazima Hawa manguli wawe ni marais. Hujaipata concept yake. Kuhusu rais Samia kupewa muda mrefu wa kutawala naikataa
Mlitamani kayafa apewe muda wa kutawala bila kikomo na mpumbavu mmoja kiongozi wa mhili ulionajisiwa akaapa eti apende asipende atalazimishwa !!
Leo woteee makanyanga mmoja kalala mazima mwingine hajulikani kalala au kasimama
Mungu kaamua ugomvi.
 
Russia hakuna uzalendo wowote Russia inatawaliwa na kikundi kidogo cha mafisadi wakiongozwa na Putin.Hawataki kuachia madaraka wanajua wakiondoka tu Takukuru ya Urusi inao

Hao wote uliwataja mali zao za mabilioni na pesa mabilioni zimekuwa frozen nchi za Magharibi

Vikwazo wamewekewa wao na familia zao
Ile vita sio Kuwa anapigana na Ukraine la.Yeye kavamia Ukraine kisa aliota kuwa kuna siku Ukraine watakuja mvamia.Hivi mtu unaota tu halafu unaenda fanya uharibifu kama ule Ukraine kweli? Mtu hajakuvamia .Ukraine jeshi ni la wananchi wanapigania nchi yao na wana support ya wananchi wakati Urusi Jeshi linampigania Putin abaki madarakani halina support ya wananchi.Wanampigania mtu mmoja na kikundi cha mafisadi wenzie ma Oligarchs


Alichofanya Urusi kinatakiwa kulaaniwa na kila binadamu mwenye akili timamu si cha kufanya kwenye dunia ya kistaarabu ya sasa
 
Russia hakuna uzalendo wowote Russia inatawaliwa na kikundi kidogo cha mafisadi wakiongozwa na Putin.Hawataki kuachia madaraka wanajua wakiondoka tu Takukuru ya Urusi inao

Hao wote uliwataja mali zao za mabilioni na pesa mabilioni zimekuwa frozen nchi za Magharibi

Vikwazo wamewekewa wao na familia zao
Ile vita sio Kuwa anapigana na Ukraine la.Yeye kavamia Ukraine kisa aliota kuwa kuna siku Ukraine watakuja mvamia.Hivi mtu unaota tu halafu unaenda fanya uharibifu kama ule Ukraine kweli? Mtu hajakuvamia .Ukraine jeshi ni la wananchi wanapigania nchi yao na wana support ya wananchi wakati Urusi Jeshi linampigania Putin abaki madarakani halina support ya wananchi.Wanampigania mtu mmoja na kikundi cha mafisadi wenzie ma Oligarchs


Alichofanya Urusi kinatakiwa kulaaniwa na kila binadamu mwenye akili timamu si cha kufanya kwenye dunia ya kistaarabu ya sasa
Bora madikteta wa live live kabisa kuliko hawa viongozi tunaosema ni wa demokrasia kumbe ni vibaraka tu wa wamagharibi
 
KAbla ya hi vita uliwahi kujua sarafu ya Urusi inaitwaje? Anyway, kila mtu na fikra zake; i think nchi kama India sasa hivi zinatajirika sana kupitia hu mgogoro, mafuta ya Urusi mengi yanauzwa India kwa bei rahisi halafu India ana process then tunakuja kuuziwa sisi; hebu pia prot graph ya thamani ya pesa ya Urusi ilivyokua kabla ya vita na wakati hu wa vita; mkuu, vita ni biashara. For your information, USA anapenda hi vita iendelee ili baadae aje afanye biashara kubwa sana na Ukraine, zile silaha na pesa hatoi bure, hakunaga kitu cha namna hiyo kwenye hi sayari inayoitwa DUNIA
Kukua kwa thamani ya fedha siyo kiashiria pekee cha uchumi kukua,nchi nyingi bado zinauziwa mafuta na Urusi kama vile India uliyoitolea mfano,lakini zipo kwenye mchakato wa kidumu wa kuachana na mafuta na gesi ya Urusi,unajua Urusi walipoivamia nchi ya Georgia hawakuwekewa vikwazo vya uchumi na nchi yoyote,so wakajisahau wakadhani kuivamia Ukraine itakuwa ni jambo rahisi la wiki mbili hivi basi,wauondoe madarakani utawala wA Zelensky na kuacha mtu wanayemtaka wao akiendelea kutawala,lakini wamekutana na hali tofauti,walipojaribu kuiteka Kiev walipata upinzani mkali ambao iliwapelekea kuyarudisha majeshi yao nyuma na kuendelea vita kwenye mikoa yenye bandari,huku vikwazo vya uchumi vikiwakalia kooni,sasa hivi huko kwao Hali si shwari,kama una nugu huko anaweza kukusimulia,manaake vyombo vya habari mmevikataa mnasema vinatangaza propaganda za magharibi.
 
Kukua kwa thamani ya fedha siyo kiashiria pekee cha uchumi kukua,nchi nyingi bado zinauziwa mafuta na Urusi kama vile India uliyoitolea mfano,lakini zipo kwenye mchakato wa kidumu wa kuachana na mafuta na gesi ya Urusi,unajua Urusi walipoivamia nchi ya Georgia hawakuwekewa vikwazo vya uchumi na nchi yoyote,so wakajisahau wakadhani kuivamia Ukraine itakuwa ni jambo rahisi la wiki mbili hivi basi,wauondoe madarakani utawala wA Zelensky na kuacha mtu wanayemtaka wao akiendelea kutawala,lakini wamekutana na hali tofauti,walipojaribu kuiteka Kiev walipata upinzani mkali ambao iliwapelekea kuyarudisha majeshi yao nyuma na kuendelea vita kwenye mikoa yenye bandari,huku vikwazo vya uchumi vikiwakalia kooni,sasa hivi huko kwao Hali si shwari,kama una nugu huko anaweza kukusimulia,manaake vyombo vya habari mmevikataa mnasema vinatangaza propaganda za magharibi.
Nadhani tuna source tofauti tofauti sana za inform; ninacho kijua mimi ni kwamba hata USA na baraza lao wanajiuliza kwanini jamaa haichukui Kiev? Kwanini pia hapigi reli, vyanzo vya umeme? Kaviacha tu why? Kwanini hapigi hata jengo la bunge ilihali halina ulinzi kiviile? Why? hayo ni maswali ambayo Ulaya na USA wanajiuliza. Umesema Urusi hakujua kama angepambana na vikwazo? Kaka, kabla hawajarusha bomu hukuziona ziara za Putin kwa rafiki zake China, Cuba na kule Venezuela? Unadhani kwanini wakati anaivamia Georgia kama unavyo sema hakufanya hivyo? Mkuu, CIA, M16, KGB wamekua wanapelelezana miaka na miaka, sio leo, wanajuana siri zao nyingi sana; hata hili la vikwazo walijua hao KGB and this is why Putin alisema mapema kabla hajaanza vita kwamba yeyote atakae rusha risasi kwenda kwake atakipata; hizo statement zilitoka kabla; baada sasa ya kuanza vita, rais wa USA alitamka hadharani kwamba USA na NATO hawata peleka majeshi kule, kwa kufanya hivyo ni kukaribisha vita ya dunia. Statement hizo hazikutoka tu ghafla, wale ni wazungu mkuu, wanapigana wenyewe kwa wenyewe, wana akili, wanafanya utafiti sana kabla ya kushambuliana. Usinambie kwamba kitendo cha Putin kutaka kuuza gesi na mafuta yake kwa pesa ya Urusi kilitokea tu ghafla, they knew it even before. Hushangai hata mataifa ya Kiarabu ambayo ni marafiki wakubwa wa USA ni kama wapo upande wa Urusi?
 
Back
Top Bottom