singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 2,153
- 10,849
Damiani ni kijana wa miaka ishirini na mbili, mhitimu wa chuo kikuu cha Tanzania Institute of Accountancy (TIA) akiwa amechukua kozi ya Finance and Accounting in Public Sector (kozi inayohusu maswala ya uhasibu). Mara baada ya Damiani kumaliza masomo yake hakutaka kubaki ndani ya jiji la Dar es Salaam, kwani hakuwa na kazi maalumu ambayo ingemuwezesha kujiingizia kipato ndani ya jiji hilo. Pia maisha ndani ya jiji hilo yalikuwa ghali sana na yalihitaji pesa ili kuweza kuishi.
Hivyo mara baada tu ya kumaliza masomo yake aliamua kurudi nyumbani kwao kijijini mkoani Tanga kwa ajili ya kusikilizia upepo wa ajira. Kwani mwaka ambao alikuwa amemaliza haukuwa kama miaka ya nyuma kwamba ukimaliza tu unasubiri matokeo na kupata ajira. Kinyume chake ni kwamba utasubiri matokeo yatoke na kuomba ajira kwa makampuni ambayo yatakuwa na uhitaji au serikali pale itakapotangaza nafasi za ajira na kuomba. Na kwa kuwa kipindi hicho kulikuwa na wimbi kubwa la vijana ambao walikuwa wahitimu na hawakuwa na ajira mtaani, hivyo ilikuwa ngumu sana kupata ajira. Ilikuwa ni kama kubahatisha tu pale nafasi zinapotoka kwani wengi wa waombaji wana sifa zinazofanana.
Mkuzi ndio kijiji cha kijana Damiani. Kijiji hiki kilikuwa ndani ya wilaya ya Lushoto, kilomita kadhaa kutoka Lushoto mjini. Yaani kama utasafiri kwa gari ni muda wa dakika thelathini mpaka arobaini kufika ndani ya kijiji hicho. Ni moja ya vijiji ambavyo vilikuwa vimezungukwa na misitu na kuwa na mazingira ya kuvutia sana. Yalikuwa ni moja ya mazingira ambayo watalii wengi wa mataifa ya nje na hata watalii wa ndani walikuwa wakipenda kutembelea. Na hiyo yote ni kutokana na hali yake ya hewa ilivyokuwa safi na ya kuvutia.
Basi kijana Damiani ndani ya kijiji cha Mkuzi ndipo alikulia na kujipatia elimu yake ya msingi na sekondari.
Damiani alikuwa kijana mpole, mcheshi, mrefu maji ya kunde, mwenye sura yake ya kuchongoka lakini iliyoumbwa vizuri. Alikuwa ni moja ya vijana walio kuwa na miili mikubwa ya wastani. Damiani alikuwa akiishi na mama yake tu kwani baba yake alikuwa amekwisha kufariki miaka mingi nyuma kipindi akiwa tu na umri wa miaka kumi.
Kurudi kwa Damiani kijijini baada ya kumaliza masomo ilikuwa ni moja ya furaha kubwa sana kwa mama yake kumuona mwanae kurudi ndani ya kijiji hicho, kwani mama huyo alikuwa akimpenda sana mwanae.
“Karibu sana mwanangu,” mama alifurahia sana kwa mwanae kumaliza masomo yake ya ngazi ya juu, na kujihisi kuwa mwanamke aliyefanikiwa kulea kwani watoto wengi ndani ya kijiji hicho hawakufanikiwa kufika ngazi ya juu ya kielimu kama ilivyokuwa kwa Damiani.
“Asante mama, hatimae nimemaliza chuo na nimerudi rasmi,” aliongea Damiani huku akiachia tabasamu. Huku nje watoto wengi walikuwa wakimwangalia na kumshangaa. Hiyo ilikuwa ni kawaida sana kwa vijiji kushangaa watu walio tokea mjini na hata kwa wageni pia.
Basi Damiani alikaribishwa vizuri na mama yake katika nyumba yao hiyo ya vyumba vitatu iliyoezekwa kwa mabati, na kwa kuwa Damiani alikuwa na chumba chake tokea akiwa shuleni ndiko mama yake alipeleka begi lake na kukifanyia usafi.
Maisha ya kijana Damiani yanaanza rasmi ndani ya kijiji cha Mkuzi. Licha ya Damiani kuwepo ndani ya kijiji hicho lakini alikuwa na mipango mikubwa sana ya maisha yake hapo mbeleni, kwani alihitaji kuja kuwa mfanya biashara mkubwa sana katika maisha yake na hiyo ilikuwa ndiyo moja ya ndoto yake kubwa. Japo alikuwa amesoma na alikuwa akitarajia kuwajiriwa lakini ajira kwake haikuwa kipaumbele. Ila kipaumbele kwake ilikuwa ni kupata mtaji utakaomwezesha kuanzisha biashara. Hakika alikuwa na safari ndefu sana na hata kwa yeye pia alilijua hilo na hivyo kwa umri aliokuwa nao hakuwa na sababu ya kukatishwa tamaa na mazingira aliokuwemo na aliokulia. Kwani alichokuwa akikiamini katika maisha yake ni juu ya uchapaji kazi kwa bidii na kutokukata tamaa na kuwa na malengo ndiyo nguzo kubwa sana ya kuja kufanikiwa. Hakutaka kabisa kukatishwa tamaa na hali ya maisha yao ya umasikini yaliyopo hapo nyumbani, ila aliamini katika mawazo chanya tu.
Basi hatimae wiki, mwezi na hata miezi ilikatika na matokeo yake yalikuwa yamekwisha kutoka na akiwa amefaulu kwa ufaulu wa daraja la kwanza. Kwake na kwa mama yake ilikuwa ni furaha na faraja kubwa sana, kwani aliamini kupitia ufaulu mkubwa basi angeweza kumrahisishia kupata kazi kwa wepesi zaidi.
Hakutaka kusafiri mpaka Dar es Salaam kwa ajili ya kuomba kazi ilihali kulikuwa na njia rahisi. Alichokifanya yeye ni kutuma maombi kwa kila kampuni ambayo ilikuwa ikitangaza nafasi za ajira kwa njia ya mtandao.
Mwezi wa kwanza uliisha kijana Damiani akiwa amekosa kabisa uelekeo wa ajira kwani ni makampuni zaidi ya matatu ambayo alikuwa ameomba kwa ajili ya kupata ajira lakini amekosa hata wito wa interview (mahojiano ya kiufanisi). Zikiwa zimepita siku kadhaa za kijana Damiani kukata tamaa, hatimae kwenye moja ya kampuni ambayo haikuwa imetoa majibu ilirudisha jibu kwa kijana Damiani kwa ajili ya kuhudhuria interview.
Ilikuwa ni moja ya kampuni iliyokuwa ikipatikana ndani ya jiji la Dar es Salaam, kampuni moja ya usafirishaji iliokuwa na makao yake makuu ndani ya Posta. Kwake Damiani alifurahia kwani aliona tumaini la kupata ajira linaridhisha zaidi. Alimwambia mama yake juu ya taarifa hiyo na mama yake pia alifurahia na kumpa baraka zote mwanae kwa ajili ya kuhudhuria interview hiyo.
Ilikuwa ni siku ya Jumatatu ndiyo siku ambayo kijana Damiani alikuwa ndani ya basi akielekea jijini Dar kwa ajili ya kuhudhuria interview. Alifanya maombi juu ya safari yake hiyo na kusudio lake analoliendea kulifanyia kazi.
Kutoka Lushoto mpaka ndani ya jiji la Dar ni umbali wa masaa sita mpaka saba. Hivyo Damiani alikuja kufika ndani ya jiji hilo kwenye muda wa saa nane kamili mchana. Siku hiyo alipanga akifika ndani ya jiji hilo kwa kuwa hakuwa na ndugu wa kufikia, alipanga kwenda kwa rafiki yake mmoja aliyekuwa amemuacha ndani ya chuo akiendelea na masomo kwa ajili ya kumuhifadhi mpaka siku inayofuata afanye interview na kisha ageuke kurudi nyumbani.
Basi baada tu ya kushuka ndani ya basi akijisogeza mpaka kwenye daladala zinazoelekea Mbagala na kisha alipanda huku malengo yake aje ashukie Mtongani kwa Azizi Ally kwani hapo ndipo rafiki yake huyo alipokuwa akipatikana kwa kuishi. Barabara haikuwa na foleni sana hivyo hawakuchukua masaa mengi kufika sehemu aliokuwa amekusudia.
Mara baada tu ya kushushwa hatimae alinyoosha moja kwa moja upande wa kushoto wa barabara, huku akipita vichochoro viwili vitatu na kuja kutokelezea mbele ya nyumba moja kubwa iliokuwa na ukuta. Hatimae alisimama nje ya geti la nyumba hiyo huku kama ni mtu aliyekuwa akijishauri agonge ama asigonge. Ila kwa kuwa kilichomleta hapo ni kuonana na rafiki yake na rafiki yake alikuwa akiishi ndani ya nyumba hiyo basi hakuwa na budi ya kugonga geti hilo.
Haikuchukua muda mrefu hatimae alikuwa amefunguliwa na msichana mmoja aliyekuwa amejifunga khanga moja, na alionekana alikuwa akifua kwani alikuwa na mapovu mikononi.
“Karibu,” sauti hiyo nyororo ilimkaribisha ndani huku dada huyo akitangulia mbele na kumuacha kijana Damiani kumsanifu mdada huyo kwa nyuma. Alikuwa ni mlimbwende kweli aliyekuwa amejaliwa umbo zuri haswa la kumvutia kila mwanaume atakayemtia machoni. Alikuwa mrefu wa wastani mwenye rangi yake ya chocolate, alibarikiwa uso wa duara na kwa tathmini za haraka haraka mdada huyo alionekana umri wake haukuwa chini ya miaka ishirini kwenda juu.
“Nimemkuta Elvis??”
“Katoka sema anakuja muda si mrefu. Wewe ndio Damiani??”
“Ndio ni mimi.”
“Okey! Alinipa maelekezo yako kwamba ukifika nikukaribishe ndani,” aliongea msichana huyo huku akimkaribisha Damiani ndani kwani muda wote huo alikuwa amesimama. Damiani alijua lazima huyo mdada atakuwa hawara (mwanamke anayeishi na mwanaume pasipo kuolewa au mpenzi) wake Elvis maana alimjua mngoni huyo songea kwa kupenda warembo hakuwa nyuma na ndiyo maana kabla ya kutoka nyumbani alimtaarifu kuwa atakuja kulala kwake.
Basi mdada huyo alimuongoza Damiani ndani ya nyumba hiyo iliokuwa imepakwa rangi nyeupe mpaka kwenye chumba cha katikati upande kushoto na kisha alimkaribisha ndani. Kilikuwa ni chumba kimoja kikubwa saizi ya kati kilichokuwa kimejaa makorokocho mengi. Damiani alikuwa akikijua chumba hicho sana kwani hata kwa baadhi ya vitu hivyo vilikuwa vyake na ni baada ya yeye kumaliza masomo alimuuzia rafiki yake huyo.
Basi baada ya kukaribishwa dada yule alitoka nje na kuendelea na shughuli yake ya ufuaji huku akimwacha Damiani akimsubiri rafiki yake. Na haikuchukua hata dakika ishirini rafiki yake Elvis aliingia ndani ya nyumba hiyo. Elvis alifurahia sana kumuona Damiani na hata kwa Damiani ilikuwa ni hivyo hivyo. Wote walifurahia kuonana kwa mara nyingine.
“Karibu sana HB asiyetaka warembo,” aliongea Elvis akionesha kumtania mwenzie na kwa Damiani kwa kuwa alikuwa ashamzoea rafiki yake huyo kwa matani basi na yeye alicheka.
“Mzee wa totozi, naona shemeji yangu wa awamu hii ni shida.”
“Yaani acha tu mzee toto la toto na isitoshe limedata na ndiyo limenifanya nihangaike siku ya leo.”
“Unahangaishwa na nini sasa??”
“Hahaha lazima kuhangaika. Unajua jana ulivyonicheki unakuja ilikuwa ghafla sana na sikutaka kukwambia naishi na mtoto wa kike. Kwa hiyo unavyoniona hapa kuna msela nimetoka kumpanga ili ukale mbonji kwake ukamilishe mambo yako maana hapa sikuwa na jinsi.”
“Daah! Hapo ndiyo maana nakukubali mshikaji wangu.”
“Hahaha… usijali mzee si unajua hata wewe umenisaidia mara kibao. Hata mavitu haya ni kama ulinipa tu kutokana na bei ile.”
Basi Damiani walichukana na rafiki yake na kutoka eneo hilo kuelekea barabarani na kupanda magari ya kuelekea Rangi Tatu. Walivyofika Mbagala Zakhemu walishuka na kuchukua upande wa kushoto barabara. Umbali wa mita kadhaa hatimae waliingia chochoro ambayo walikuja kuibukia mbele mtaa mwingine, na wakaja kutokea mbele ya kanisa la KKKT na hapo walipinda kushoto tena na kukuta nyumba moja kubwa iliokuwa na geti na kwa nje ilisomeka kwa maandishi ya lodge. Elvis alisukuma mlango na kisha aliingia ndani. Kwa Damiani yeye alikuwa akifatisha tu kuona mwisho wake kwani kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kaletwa lodge.
“Oya mshikaji anakaa hapa, si lodge hapa tena japo ilikuwa lodge. Mwenye nyumba kaamua kuifanya nyumba ya kupangisha,” aliongea Elvis na kumfanya Damiani aelewe. Walipita kwenye vyumba kadhaa na hatimae walisimama nje ya mlango na Elvis aligonga na nusu dakika mlango ilifunguliwa na jamaa mmoja wa makamo mfupi mwenye mwili mkubwa wa kibonge.
“Karibuni.”
Waliingia ndani ya chumba hicho. Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri sana, na pia hata kitanda na samani (furniture) zilizokuwemo humo ndani zilionesha jamaa anayeishi humo ndani hakuwa mnyonge kipesa.
“Oya huyu ni Joshua rafiki yangu sana mwaka wa kwanza hivyo ndiyo utachilia hapa kwake mpaka utakapokamilisha mambo yako,” aliongea Elvis na Joshua alimkaribisha Damiani na Elvis aliaga akaondoka.
Basi siku nyingine iliingia ambayo ni siku Damiani alikuwa akielekea mtaa wa Posta kwa ajili ya kufanya interview. Alikuwa amevaa akapendeza maana kwenye nguo alikuwa nazo na mkopo ulimsaidia sana kipindi akiwa chuo.
Alijisogeza mpaka barabarani ili kusubiri gari ya kwenda stesheni Posta apande. Ila mara baada ya kufika tu kwenye barabara nje kabisa ya supermarket iliyosomeka kwa jina la Kivoni, ilisimama gari moja aina ya Vanguard nyeusi na kioo kilishushwa na akaonekana bwana mmoja wa makamo, makadirio ya miaka 30 kuendelea mweusi alivalia shati jeupe na koti akiwa na miwani. Damiani wakati huo gari hiyo ikisimama alikuwa akiiangalia na hata jamaa huyo alivyoshusha kioo alikuwa pia akimwangalia. Damiani alijikuta akijishtukia na hiyo ni mara baada ya jamaa huyo kumuonesha ishara ya kumuita. Alijithibitishia kama ndio yeye aliyekuwa akiitwa na hapo ndipo alipopiga hatua kulisogelea gari hilo.
Hivyo mara baada tu ya kumaliza masomo yake aliamua kurudi nyumbani kwao kijijini mkoani Tanga kwa ajili ya kusikilizia upepo wa ajira. Kwani mwaka ambao alikuwa amemaliza haukuwa kama miaka ya nyuma kwamba ukimaliza tu unasubiri matokeo na kupata ajira. Kinyume chake ni kwamba utasubiri matokeo yatoke na kuomba ajira kwa makampuni ambayo yatakuwa na uhitaji au serikali pale itakapotangaza nafasi za ajira na kuomba. Na kwa kuwa kipindi hicho kulikuwa na wimbi kubwa la vijana ambao walikuwa wahitimu na hawakuwa na ajira mtaani, hivyo ilikuwa ngumu sana kupata ajira. Ilikuwa ni kama kubahatisha tu pale nafasi zinapotoka kwani wengi wa waombaji wana sifa zinazofanana.
Mkuzi ndio kijiji cha kijana Damiani. Kijiji hiki kilikuwa ndani ya wilaya ya Lushoto, kilomita kadhaa kutoka Lushoto mjini. Yaani kama utasafiri kwa gari ni muda wa dakika thelathini mpaka arobaini kufika ndani ya kijiji hicho. Ni moja ya vijiji ambavyo vilikuwa vimezungukwa na misitu na kuwa na mazingira ya kuvutia sana. Yalikuwa ni moja ya mazingira ambayo watalii wengi wa mataifa ya nje na hata watalii wa ndani walikuwa wakipenda kutembelea. Na hiyo yote ni kutokana na hali yake ya hewa ilivyokuwa safi na ya kuvutia.
Basi kijana Damiani ndani ya kijiji cha Mkuzi ndipo alikulia na kujipatia elimu yake ya msingi na sekondari.
Damiani alikuwa kijana mpole, mcheshi, mrefu maji ya kunde, mwenye sura yake ya kuchongoka lakini iliyoumbwa vizuri. Alikuwa ni moja ya vijana walio kuwa na miili mikubwa ya wastani. Damiani alikuwa akiishi na mama yake tu kwani baba yake alikuwa amekwisha kufariki miaka mingi nyuma kipindi akiwa tu na umri wa miaka kumi.
Kurudi kwa Damiani kijijini baada ya kumaliza masomo ilikuwa ni moja ya furaha kubwa sana kwa mama yake kumuona mwanae kurudi ndani ya kijiji hicho, kwani mama huyo alikuwa akimpenda sana mwanae.
“Karibu sana mwanangu,” mama alifurahia sana kwa mwanae kumaliza masomo yake ya ngazi ya juu, na kujihisi kuwa mwanamke aliyefanikiwa kulea kwani watoto wengi ndani ya kijiji hicho hawakufanikiwa kufika ngazi ya juu ya kielimu kama ilivyokuwa kwa Damiani.
“Asante mama, hatimae nimemaliza chuo na nimerudi rasmi,” aliongea Damiani huku akiachia tabasamu. Huku nje watoto wengi walikuwa wakimwangalia na kumshangaa. Hiyo ilikuwa ni kawaida sana kwa vijiji kushangaa watu walio tokea mjini na hata kwa wageni pia.
Basi Damiani alikaribishwa vizuri na mama yake katika nyumba yao hiyo ya vyumba vitatu iliyoezekwa kwa mabati, na kwa kuwa Damiani alikuwa na chumba chake tokea akiwa shuleni ndiko mama yake alipeleka begi lake na kukifanyia usafi.
Maisha ya kijana Damiani yanaanza rasmi ndani ya kijiji cha Mkuzi. Licha ya Damiani kuwepo ndani ya kijiji hicho lakini alikuwa na mipango mikubwa sana ya maisha yake hapo mbeleni, kwani alihitaji kuja kuwa mfanya biashara mkubwa sana katika maisha yake na hiyo ilikuwa ndiyo moja ya ndoto yake kubwa. Japo alikuwa amesoma na alikuwa akitarajia kuwajiriwa lakini ajira kwake haikuwa kipaumbele. Ila kipaumbele kwake ilikuwa ni kupata mtaji utakaomwezesha kuanzisha biashara. Hakika alikuwa na safari ndefu sana na hata kwa yeye pia alilijua hilo na hivyo kwa umri aliokuwa nao hakuwa na sababu ya kukatishwa tamaa na mazingira aliokuwemo na aliokulia. Kwani alichokuwa akikiamini katika maisha yake ni juu ya uchapaji kazi kwa bidii na kutokukata tamaa na kuwa na malengo ndiyo nguzo kubwa sana ya kuja kufanikiwa. Hakutaka kabisa kukatishwa tamaa na hali ya maisha yao ya umasikini yaliyopo hapo nyumbani, ila aliamini katika mawazo chanya tu.
Basi hatimae wiki, mwezi na hata miezi ilikatika na matokeo yake yalikuwa yamekwisha kutoka na akiwa amefaulu kwa ufaulu wa daraja la kwanza. Kwake na kwa mama yake ilikuwa ni furaha na faraja kubwa sana, kwani aliamini kupitia ufaulu mkubwa basi angeweza kumrahisishia kupata kazi kwa wepesi zaidi.
Hakutaka kusafiri mpaka Dar es Salaam kwa ajili ya kuomba kazi ilihali kulikuwa na njia rahisi. Alichokifanya yeye ni kutuma maombi kwa kila kampuni ambayo ilikuwa ikitangaza nafasi za ajira kwa njia ya mtandao.
Mwezi wa kwanza uliisha kijana Damiani akiwa amekosa kabisa uelekeo wa ajira kwani ni makampuni zaidi ya matatu ambayo alikuwa ameomba kwa ajili ya kupata ajira lakini amekosa hata wito wa interview (mahojiano ya kiufanisi). Zikiwa zimepita siku kadhaa za kijana Damiani kukata tamaa, hatimae kwenye moja ya kampuni ambayo haikuwa imetoa majibu ilirudisha jibu kwa kijana Damiani kwa ajili ya kuhudhuria interview.
Ilikuwa ni moja ya kampuni iliyokuwa ikipatikana ndani ya jiji la Dar es Salaam, kampuni moja ya usafirishaji iliokuwa na makao yake makuu ndani ya Posta. Kwake Damiani alifurahia kwani aliona tumaini la kupata ajira linaridhisha zaidi. Alimwambia mama yake juu ya taarifa hiyo na mama yake pia alifurahia na kumpa baraka zote mwanae kwa ajili ya kuhudhuria interview hiyo.
Ilikuwa ni siku ya Jumatatu ndiyo siku ambayo kijana Damiani alikuwa ndani ya basi akielekea jijini Dar kwa ajili ya kuhudhuria interview. Alifanya maombi juu ya safari yake hiyo na kusudio lake analoliendea kulifanyia kazi.
Kutoka Lushoto mpaka ndani ya jiji la Dar ni umbali wa masaa sita mpaka saba. Hivyo Damiani alikuja kufika ndani ya jiji hilo kwenye muda wa saa nane kamili mchana. Siku hiyo alipanga akifika ndani ya jiji hilo kwa kuwa hakuwa na ndugu wa kufikia, alipanga kwenda kwa rafiki yake mmoja aliyekuwa amemuacha ndani ya chuo akiendelea na masomo kwa ajili ya kumuhifadhi mpaka siku inayofuata afanye interview na kisha ageuke kurudi nyumbani.
Basi baada tu ya kushuka ndani ya basi akijisogeza mpaka kwenye daladala zinazoelekea Mbagala na kisha alipanda huku malengo yake aje ashukie Mtongani kwa Azizi Ally kwani hapo ndipo rafiki yake huyo alipokuwa akipatikana kwa kuishi. Barabara haikuwa na foleni sana hivyo hawakuchukua masaa mengi kufika sehemu aliokuwa amekusudia.
Mara baada tu ya kushushwa hatimae alinyoosha moja kwa moja upande wa kushoto wa barabara, huku akipita vichochoro viwili vitatu na kuja kutokelezea mbele ya nyumba moja kubwa iliokuwa na ukuta. Hatimae alisimama nje ya geti la nyumba hiyo huku kama ni mtu aliyekuwa akijishauri agonge ama asigonge. Ila kwa kuwa kilichomleta hapo ni kuonana na rafiki yake na rafiki yake alikuwa akiishi ndani ya nyumba hiyo basi hakuwa na budi ya kugonga geti hilo.
Haikuchukua muda mrefu hatimae alikuwa amefunguliwa na msichana mmoja aliyekuwa amejifunga khanga moja, na alionekana alikuwa akifua kwani alikuwa na mapovu mikononi.
“Karibu,” sauti hiyo nyororo ilimkaribisha ndani huku dada huyo akitangulia mbele na kumuacha kijana Damiani kumsanifu mdada huyo kwa nyuma. Alikuwa ni mlimbwende kweli aliyekuwa amejaliwa umbo zuri haswa la kumvutia kila mwanaume atakayemtia machoni. Alikuwa mrefu wa wastani mwenye rangi yake ya chocolate, alibarikiwa uso wa duara na kwa tathmini za haraka haraka mdada huyo alionekana umri wake haukuwa chini ya miaka ishirini kwenda juu.
“Nimemkuta Elvis??”
“Katoka sema anakuja muda si mrefu. Wewe ndio Damiani??”
“Ndio ni mimi.”
“Okey! Alinipa maelekezo yako kwamba ukifika nikukaribishe ndani,” aliongea msichana huyo huku akimkaribisha Damiani ndani kwani muda wote huo alikuwa amesimama. Damiani alijua lazima huyo mdada atakuwa hawara (mwanamke anayeishi na mwanaume pasipo kuolewa au mpenzi) wake Elvis maana alimjua mngoni huyo songea kwa kupenda warembo hakuwa nyuma na ndiyo maana kabla ya kutoka nyumbani alimtaarifu kuwa atakuja kulala kwake.
Basi mdada huyo alimuongoza Damiani ndani ya nyumba hiyo iliokuwa imepakwa rangi nyeupe mpaka kwenye chumba cha katikati upande kushoto na kisha alimkaribisha ndani. Kilikuwa ni chumba kimoja kikubwa saizi ya kati kilichokuwa kimejaa makorokocho mengi. Damiani alikuwa akikijua chumba hicho sana kwani hata kwa baadhi ya vitu hivyo vilikuwa vyake na ni baada ya yeye kumaliza masomo alimuuzia rafiki yake huyo.
Basi baada ya kukaribishwa dada yule alitoka nje na kuendelea na shughuli yake ya ufuaji huku akimwacha Damiani akimsubiri rafiki yake. Na haikuchukua hata dakika ishirini rafiki yake Elvis aliingia ndani ya nyumba hiyo. Elvis alifurahia sana kumuona Damiani na hata kwa Damiani ilikuwa ni hivyo hivyo. Wote walifurahia kuonana kwa mara nyingine.
“Karibu sana HB asiyetaka warembo,” aliongea Elvis akionesha kumtania mwenzie na kwa Damiani kwa kuwa alikuwa ashamzoea rafiki yake huyo kwa matani basi na yeye alicheka.
“Mzee wa totozi, naona shemeji yangu wa awamu hii ni shida.”
“Yaani acha tu mzee toto la toto na isitoshe limedata na ndiyo limenifanya nihangaike siku ya leo.”
“Unahangaishwa na nini sasa??”
“Hahaha lazima kuhangaika. Unajua jana ulivyonicheki unakuja ilikuwa ghafla sana na sikutaka kukwambia naishi na mtoto wa kike. Kwa hiyo unavyoniona hapa kuna msela nimetoka kumpanga ili ukale mbonji kwake ukamilishe mambo yako maana hapa sikuwa na jinsi.”
“Daah! Hapo ndiyo maana nakukubali mshikaji wangu.”
“Hahaha… usijali mzee si unajua hata wewe umenisaidia mara kibao. Hata mavitu haya ni kama ulinipa tu kutokana na bei ile.”
Basi Damiani walichukana na rafiki yake na kutoka eneo hilo kuelekea barabarani na kupanda magari ya kuelekea Rangi Tatu. Walivyofika Mbagala Zakhemu walishuka na kuchukua upande wa kushoto barabara. Umbali wa mita kadhaa hatimae waliingia chochoro ambayo walikuja kuibukia mbele mtaa mwingine, na wakaja kutokea mbele ya kanisa la KKKT na hapo walipinda kushoto tena na kukuta nyumba moja kubwa iliokuwa na geti na kwa nje ilisomeka kwa maandishi ya lodge. Elvis alisukuma mlango na kisha aliingia ndani. Kwa Damiani yeye alikuwa akifatisha tu kuona mwisho wake kwani kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kaletwa lodge.
“Oya mshikaji anakaa hapa, si lodge hapa tena japo ilikuwa lodge. Mwenye nyumba kaamua kuifanya nyumba ya kupangisha,” aliongea Elvis na kumfanya Damiani aelewe. Walipita kwenye vyumba kadhaa na hatimae walisimama nje ya mlango na Elvis aligonga na nusu dakika mlango ilifunguliwa na jamaa mmoja wa makamo mfupi mwenye mwili mkubwa wa kibonge.
“Karibuni.”
Waliingia ndani ya chumba hicho. Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri sana, na pia hata kitanda na samani (furniture) zilizokuwemo humo ndani zilionesha jamaa anayeishi humo ndani hakuwa mnyonge kipesa.
“Oya huyu ni Joshua rafiki yangu sana mwaka wa kwanza hivyo ndiyo utachilia hapa kwake mpaka utakapokamilisha mambo yako,” aliongea Elvis na Joshua alimkaribisha Damiani na Elvis aliaga akaondoka.
Basi siku nyingine iliingia ambayo ni siku Damiani alikuwa akielekea mtaa wa Posta kwa ajili ya kufanya interview. Alikuwa amevaa akapendeza maana kwenye nguo alikuwa nazo na mkopo ulimsaidia sana kipindi akiwa chuo.
Alijisogeza mpaka barabarani ili kusubiri gari ya kwenda stesheni Posta apande. Ila mara baada ya kufika tu kwenye barabara nje kabisa ya supermarket iliyosomeka kwa jina la Kivoni, ilisimama gari moja aina ya Vanguard nyeusi na kioo kilishushwa na akaonekana bwana mmoja wa makamo, makadirio ya miaka 30 kuendelea mweusi alivalia shati jeupe na koti akiwa na miwani. Damiani wakati huo gari hiyo ikisimama alikuwa akiiangalia na hata jamaa huyo alivyoshusha kioo alikuwa pia akimwangalia. Damiani alijikuta akijishtukia na hiyo ni mara baada ya jamaa huyo kumuonesha ishara ya kumuita. Alijithibitishia kama ndio yeye aliyekuwa akiitwa na hapo ndipo alipopiga hatua kulisogelea gari hilo.