Simulizi: Kisa na Mkasa wa Mauaji ya Jenerali Imran Kombe (Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa-TISS)

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
1698663935703.png
Ni mauaji yaliyogubikwa na simulizi na hisia tofauti juu ya nini hasa kiini cha mauaji ya mkurugenzi mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa nchini (TISS), Luteni Jenerali Imran Kombe aliyeuawa kwa kupigwa risasi Juni 30 mwaka 1996.

Kumekuwepo na nadharia ya ulaji njama (conspiracy theory) kwamba pengine kuna mkono wa mtu katika mauaji hayo yaliyotokea katika Kijiji cha Mailisita Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro na nyingine ni kwamba kweli aliuawa na polisi.

Katika mfululizo wa makala hii, Mwandishi Wetu atakuletea simulizi ya nini hasa kilisababisha mauaji yake, nani walimfyatulia risasi zaidi ya 15, maelezo ya maungamo ya wauaji wake yanasemaje na familia ililipwa fidia ya Shilingi ngapi.

Simulizi hii inaegemea ushahidi uliotolewa mahakamani katika kesi hii na kesi ya madai ya fidia iliyokuwa imefunguliwa na mkewe, Roseleene Kombe dhidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na simulizi zilizogubika mauaji hayo.

Maneno yalisemwa mengi, mojawapo ni hisia kuwa huenda aliuawa kwa sababu ya urafiki wake wa karibu na Agustino Lyatonga Mrema, mgombea urais kwa tiketi ya chama cha NCCR-Mageuzi 1995, lakini kwa kesi ilivyokuwa mahakamani haikuwa sahihi.

Kwa kuwa Kombe alikuwa amepigwa risasi na polisi, licha ya kuripotiwa kuinua mikono yake juu kama ishara ya kujisalimisha kwa watu walioamini ni wezi wa gari, kulikuwa na uvumi kwamba mauaji yake yalikuwa yamepangwa.

Ni kutokana na hisia hizo na moto wa kisiasa juu ya mauaji hayo, Rais wa awamu ya tatu, hayati Benjamin Mkapa aliamua kuunda tume ambayo iliwasilisha ripoti yake 1997 ambayo si wazi, ikisema Serikali haikuwa na mkono katika mauaji hayo.

Tume hiyo iliyokuwa chini ya mwenyekiti, Jaji Damian Lubuva aliyekuwa na Jaji Mussa Kipenka wakati huo akiwa mwanasheria mwandamizi wa Serikali, ilihoji mashahidi 52 na mwaka 1997 ilitoa ripoti kwa Mkapa iliyohitimisha kwamba Serikali haikuwa na mkono wowote katika kifo cha Kombe.

Hadi sasa taarifa ya tume hiyo, kama zilivyo baadhi ya tume zilizoundwa kutafuta ukweli wa jambo ambalo linaibua hisia kali, imekuwa ni siri.

Mwaka 1998, Mbunge wa Temeke Jijini Dar es Salaam, Augustino Mrema aliibua hoja bungeni kuwa kifo cha Kombe kilikuwa sehemu ya mpango wa mauaji uliofanywa na Serikali, ingawa hata hivyo alishindwa kuthibitisha madai hayo. Pamoja na taarifa hiyo ya tume na ushahidi uliotolewa mahakamani kuhusiana na mauaji ya Kombe, bado baadhi ya watu hadi sasa wana hisia tofauti juu ya mauaji hayo na katika makala hii tutakuletea mwanzo mwisho nini kilitokea.

Timu ya makachero ilivyoundwa

Usiku wa Juni 30, 1996 na siku iliyofuata, kulizagaa taarifa za kuuawa kwa kupigwa risasi na Polisi kwa Luteni Jenerali Kombe, aliyewahi kuwa mkurugenzi wa tano wa TISS na taarifa hizo hazikuzagaa kupitia mitandao ya kijamii kama ilivyo sasa.

Wakati huo wala simu za kiganjani (kitochi) zilikuwa hazijawa nyingi, licha ya kwamba zilianza kuingia nchini mwaka 1994, hivyo taarifa zilisambaa kama moto wa kifuu na katika mji wa Moshi, watu walikaa katika makundi wakijadili.

Taarifa hizo zilisema polisi walimuua Kombe kwa kummiminia risasi hata baada ya kushuka kwenye gari na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kujisalimisha, na maiti yake ilipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mawenzi.

Polisi wakati huo walikuwa wanaamini wamemuua mtu waliyekuwa wanaamini ni mwizi mashuhuri wa magari na walikuwa wakitamba kufanikiwa kukamata gari Nissan Patrol namba TZG 50 mali ya D.W Ladwa lililoibwa Jijini Dar es Salaam.

Ni hadi mkuu wa upelelezi (RCO) Mkoa wa Kilimanjaro alipopokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kwa jina la Iwisi Shoo, akimwambia gari walilolikamata si lenyewe na mtu waliyemuua si mwizi, bali ni Kombe, mkuu wa zamani wa TISS.

Hapo ndipo Polisi wenyewe walijikuta wakipata ganzi baada ya kugundua waliyemuua ni Luteni Jenerali mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ambaye alitumikia cheo cha mkurugenzi wa TISS kati ya mwaka 1983 na 1995.

Hapo ndipo mwili wake sasa ukahamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC ili kuhifadhiwa ukisubiri taratibu nyingine za kisheria na mazishi.

Lakini ilikuja kubainika kuwa gari la marehemu namba TZD 8592 aina ya Nissan Patrol lilikuwa likifanana na la Ladwa na siku kadhaa nyuma, polisi Jijini Dar es Salaam, walikuwa wamelikamata na kuliachia baada ya kuridhika silo.

Ingawa Kombe na familia yake ni wenyeji wa Kilimanjaro, wana nyumba jijini Dar es Salaam.

Wakati Polisi wakiendelea na uchunguzi, walipata taarifa fiche zilizowaambia kuwa mwizi aliyeiba gari hilo alikuwa amelipeleka mkoani Kilimanjaro, hivyo ofisi ya RCO Dar es Salaam ikawatuma Polisi wawili kwenda Kilimanjaro.

Makachero hao kwa mujibu wa hukumu ya rufaa namba 8 ya 1998 iliyotolewa na majaji watatu wa mahakama ya Rufani iliyoketi Jijini Arusha na kutoa hukumu yake Machi 16,1992, ni Sajini Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa.

Hukumu hiyo ilitolewa na majaji Lameck Mfalila, Barnabas Samatta na Kahwa Lugakingira kutokana na hukumu ya kifo iliyotolewa Januari 26,1998 na Jaji Buxton Chipeta dhidi ya askari wawili, Koplo Juma Mswa na Konstebo Mataba Matiku.

Kulingana na nyaraka za mahakama ya Rufani, Sajin Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa, waliondoka Jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Kilimanjaro wakiwa na gari lingine la Ladwa likiendeshwa na dereva wake aitwaye Ismail Katembo.

Dereva huyo ndio angetumika pia kulitambua gari la Ladwa lililoibwa na wote watatu waliwasili Moshi Juni 27,1996 na kuripoti Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kilimanjaro na kupokelewa na RCO ambaye aliamua kuwaongezea nguvu.

Hapo wakaongezewa makachero watatu, koplo Elisante Tarimo aliyekuwa mshtakiwa wa pili, Koplo Chediel Elinisafi aliyekuja kuwa mshtakiwa wa nne na Konstebo Mataba Matiku aliyekuwa mshtakiwa wa tano katika kesi hiyo.

Makachero hao walipewa bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) namba N.1270 na risasi 30 ambayo ilibebwa na Mataba Matiku wakati Sajenti Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa kila mmoja alikuwa na bastola yenye risasi nane.

Koplo Elisante Tarimo na Chediel Elinisafi wao hawakuwa na silaha yoyote.

Kwa hiyo timu hiyo ya makachero ikaanza msako wa kulitafuta gari mali ya DW Ladwa aina ya Nissan Patrol lenye namba TZG 50 ambalo lilikuwa likifanana na gari la Luteni Jeneral Kombe TZD 8592 lililokamatwa Jijini Dar es Salaam na kuachiwa.

Siku hiyo ya Juni 30, 1996 kwenye saa 10 alasiri wakiwa katika misheni ya kulisaka gari hilo la Ladwa, wakiwa eneo la kijiji cha Shiri Njoro barabara ya Moshi-Arusha wakati huo wakiwlekea barabara hiyo kuu, mbele waliona gari la Kombe.

Dereva Ismail Katembo ambaye sasa ni marehemu alitoa sauti ya mshangao akisema gari lililopo mbele yao likitokea barabara ya Arusha-Moshi ndio gari ambalo wanalitafuta, hivyo akaliwashia taa lisimame, lakini dereva hakusimama.

Polisi hao waligeuza gari lao na kuanza kulifukuza gari la Kombe ambalo lilikuwa likifanana kwa rangi na lile na DW Ladwa lililokuwa likitafutwa na wakati wakilifukuza walianza kulishambulia kwa risasi kumlazimisha asimame.

Imran Kombe ni nani

Luteni Jenerali wa JWTZ Imran Kombe, alikuwa mwanajeshi na kachero wa usalama wa Taifa ambapo katika vita Uganda na Tanzania mwaka 1979, aliongoza brigedi ya 201 wakati Tanzania ilipoivamia Uganda kumtoa Nduli Idd Amin.

Mwaka 1980, ndio alipata wadhifa wa Mnadhimu mkuu wa JWTZ na kwa mujibu wa taarifa za mitandao zinaonyesha Desemba 30, mwaka huo, alipandishwa cheo na kuwa meja jenerali na mwaka uliofuata aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenda Hungary.

Mwaka 1983, Kombe aliondoka jeshini akiwa na cheo cha Luteni Jenerali na kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Idara ya Uslama wa Taifa (TISS), nafasi aliyoitumikia hadi 1995 na kustaafu. Aliuawa kwa kushambuliwa kwa risasi Juni 30,1996.

Baada ya mauaji hayo, Jeshi la Polisi liliwatia mbaroni askari watano na raia mmoja, Ismail Katembo ambaye hata hivyo alifariki dunia akiwa gerezani hata kabla ya kesi yao ya mauaji ya kukusudia haijasikilizwa na kutolewa hukumu.

Source: Mwananchi

Fuatilia hapa Sehemu Simulizi: Kisa na Mkasa wa Mauaji ya Jenerali Imran Kombe (Sehemua Ya Pili)

Viongozi na Wanasiasa wengine waliwahi kupigwa risasi
- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

- Utata kifo cha hayati Abeid Karume

- Kifo chenye utata cha Waziri Nicas Mahinda

- TANZIA - John Mwankenja auawa kwa risasi

- Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania

- Dkt. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

- TANZIA - Waziri Salome Mbatia afariki dunia, maswali yaibuka!

- Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA

- Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA

- Maandamano ya CHADEMA: Aqulina Akwilini Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza NIT apigwa risasi na kufariki; Polisi wakiri kuhusika

- Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ashambuliwa kwa risasi na Watu wasiojulikana

- Askari polisi aliyepigwa risasi na majambazi Tanga afariki
 
The same style used to kill
in mysterious circumstances, of Kenya’s then foreign minister Robert Ouko.

His body was discovered by a schoolboy on his walkabout, and when the police arrived it was discovered that not only was the body badly burned but it had bullet holes.

A rumour was put out by someone (silly, obviously) suggesting the minister had committed suicide, in which case he would have shot himself and then set himself on fire, or lit the fire and then shot himself.

Noma sana! Umenikumbusha mbali sana.
 
Ni mauaji yaliyogubikwa na simulizi na hisia tofauti juu ya nini hasa kiini cha mauaji ya mkurugenzi mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa nchini (TISS), Luteni Jenerali Imran Kombe aliyeuawa kwa kupigwa risasi Juni 30 mwaka 1996.

Kumekuwepo na nadharia ya ulaji njama (conspiracy theory) kwamba pengine kuna mkono wa mtu katika mauaji hayo yaliyotokea katika Kijiji cha Mailisita Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro na nyingine ni kwamba kweli aliuawa na polisi.

Katika mfululizo wa makala hii, Mwandishi Wetu atakuletea simulizi ya nini hasa kilisababisha mauaji yake, nani walimfyatulia risasi zaidi ya 15, maelezo ya maungamo ya wauaji wake yanasemaje na familia ililipwa fidia ya Shilingi ngapi.

Simulizi hii inaegemea ushahidi uliotolewa mahakamani katika kesi hii na kesi ya madai ya fidia iliyokuwa imefunguliwa na mkewe, Roseleene Kombe dhidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na simulizi zilizogubika mauaji hayo.

Maneno yalisemwa mengi, mojawapo ni hisia kuwa huenda aliuawa kwa sababu ya urafiki wake wa karibu na Agustino Lyatonga Mrema, mgombea urais kwa tiketi ya chama cha NCCR-Mageuzi 1995, lakini kwa kesi ilivyokuwa mahakamani haikuwa sahihi.

Kwa kuwa Kombe alikuwa amepigwa risasi na polisi, licha ya kuripotiwa kuinua mikono yake juu kama ishara ya kujisalimisha kwa watu walioamini ni wezi wa gari, kulikuwa na uvumi kwamba mauaji yake yalikuwa yamepangwa.

Ni kutokana na hisia hizo na moto wa kisiasa juu ya mauaji hayo, Rais wa awamu ya tatu, hayati Benjamin Mkapa aliamua kuunda tume ambayo iliwasilisha ripoti yake 1997 ambayo si wazi, ikisema Serikali haikuwa na mkono katika mauaji hayo.

Tume hiyo iliyokuwa chini ya mwenyekiti, Jaji Damian Lubuva aliyekuwa na Jaji Mussa Kipenka wakati huo akiwa mwanasheria mwandamizi wa Serikali, ilihoji mashahidi 52 na mwaka 1997 ilitoa ripoti kwa Mkapa iliyohitimisha kwamba Serikali haikuwa na mkono wowote katika kifo cha Kombe.

Hadi sasa taarifa ya tume hiyo, kama zilivyo baadhi ya tume zilizoundwa kutafuta ukweli wa jambo ambalo linaibua hisia kali, imekuwa ni siri.

Mwaka 1998, Mbunge wa Temeke Jijini Dar es Salaam, Augustino Mrema aliibua hoja bungeni kuwa kifo cha Kombe kilikuwa sehemu ya mpango wa mauaji uliofanywa na Serikali, ingawa hata hivyo alishindwa kuthibitisha madai hayo. Pamoja na taarifa hiyo ya tume na ushahidi uliotolewa mahakamani kuhusiana na mauaji ya Kombe, bado baadhi ya watu hadi sasa wana hisia tofauti juu ya mauaji hayo na katika makala hii tutakuletea mwanzo mwisho nini kilitokea.

Timu ya makachero ilivyoundwa

Usiku wa Juni 30, 1996 na siku iliyofuata, kulizagaa taarifa za kuuawa kwa kupigwa risasi na Polisi kwa Luteni Jenerali Kombe, aliyewahi kuwa mkurugenzi wa tano wa TISS na taarifa hizo hazikuzagaa kupitia mitandao ya kijamii kama ilivyo sasa.

Wakati huo wala simu za kiganjani (kitochi) zilikuwa hazijawa nyingi, licha ya kwamba zilianza kuingia nchini mwaka 1994, hivyo taarifa zilisambaa kama moto wa kifuu na katika mji wa Moshi, watu walikaa katika makundi wakijadili.

Taarifa hizo zilisema polisi walimuua Kombe kwa kummiminia risasi hata baada ya kushuka kwenye gari na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kujisalimisha, na maiti yake ilipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mawenzi.

Polisi wakati huo walikuwa wanaamini wamemuua mtu waliyekuwa wanaamini ni mwizi mashuhuri wa magari na walikuwa wakitamba kufanikiwa kukamata gari Nissan Patrol namba TZG 50 mali ya D.W Ladwa lililoibwa Jijini Dar es Salaam.

Ni hadi mkuu wa upelelezi (RCO) Mkoa wa Kilimanjaro alipopokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kwa jina la Iwisi Shoo, akimwambia gari walilolikamata si lenyewe na mtu waliyemuua si mwizi, bali ni Kombe, mkuu wa zamani wa TISS.

Hapo ndipo Polisi wenyewe walijikuta wakipata ganzi baada ya kugundua waliyemuua ni Luteni Jenerali mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ambaye alitumikia cheo cha mkurugenzi wa TISS kati ya mwaka 1983 na 1995.

Hapo ndipo mwili wake sasa ukahamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC ili kuhifadhiwa ukisubiri taratibu nyingine za kisheria na mazishi.

Lakini ilikuja kubainika kuwa gari la marehemu namba TZD 8592 aina ya Nissan Patrol lilikuwa likifanana na la Ladwa na siku kadhaa nyuma, polisi Jijini Dar es Salaam, walikuwa wamelikamata na kuliachia baada ya kuridhika silo.

Ingawa Kombe na familia yake ni wenyeji wa Kilimanjaro, wana nyumba jijini Dar es Salaam.

Wakati Polisi wakiendelea na uchunguzi, walipata taarifa fiche zilizowaambia kuwa mwizi aliyeiba gari hilo alikuwa amelipeleka mkoani Kilimanjaro, hivyo ofisi ya RCO Dar es Salaam ikawatuma Polisi wawili kwenda Kilimanjaro.

Makachero hao kwa mujibu wa hukumu ya rufaa namba 8 ya 1998 iliyotolewa na majaji watatu wa mahakama ya Rufani iliyoketi Jijini Arusha na kutoa hukumu yake Machi 16,1992, ni Sajini Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa.

Hukumu hiyo ilitolewa na majaji Lameck Mfalila, Barnabas Samatta na Kahwa Lugakingira kutokana na hukumu ya kifo iliyotolewa Januari 26,1998 na Jaji Buxton Chipeta dhidi ya askari wawili, Koplo Juma Mswa na Konstebo Mataba Matiku.

Kulingana na nyaraka za mahakama ya Rufani, Sajin Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa, waliondoka Jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Kilimanjaro wakiwa na gari lingine la Ladwa likiendeshwa na dereva wake aitwaye Ismail Katembo.

Dereva huyo ndio angetumika pia kulitambua gari la Ladwa lililoibwa na wote watatu waliwasili Moshi Juni 27,1996 na kuripoti Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kilimanjaro na kupokelewa na RCO ambaye aliamua kuwaongezea nguvu.

Hapo wakaongezewa makachero watatu, koplo Elisante Tarimo aliyekuwa mshtakiwa wa pili, Koplo Chediel Elinisafi aliyekuja kuwa mshtakiwa wa nne na Konstebo Mataba Matiku aliyekuwa mshtakiwa wa tano katika kesi hiyo.

Makachero hao walipewa bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) namba N.1270 na risasi 30 ambayo ilibebwa na Mataba Matiku wakati Sajenti Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa kila mmoja alikuwa na bastola yenye risasi nane.

Koplo Elisante Tarimo na Chediel Elinisafi wao hawakuwa na silaha yoyote.

Kwa hiyo timu hiyo ya makachero ikaanza msako wa kulitafuta gari mali ya DW Ladwa aina ya Nissan Patrol lenye namba TZG 50 ambalo lilikuwa likifanana na gari la Luteni Jeneral Kombe TZD 8592 lililokamatwa Jijini Dar es Salaam na kuachiwa.

Siku hiyo ya Juni 30, 1996 kwenye saa 10 alasiri wakiwa katika misheni ya kulisaka gari hilo la Ladwa, wakiwa eneo la kijiji cha Shiri Njoro barabara ya Moshi-Arusha wakati huo wakiwlekea barabara hiyo kuu, mbele waliona gari la Kombe.

Dereva Ismail Katembo ambaye sasa ni marehemu alitoa sauti ya mshangao akisema gari lililopo mbele yao likitokea barabara ya Arusha-Moshi ndio gari ambalo wanalitafuta, hivyo akaliwashia taa lisimame, lakini dereva hakusimama.

Polisi hao waligeuza gari lao na kuanza kulifukuza gari la Kombe ambalo lilikuwa likifanana kwa rangi na lile na DW Ladwa lililokuwa likitafutwa na wakati wakilifukuza walianza kulishambulia kwa risasi kumlazimisha asimame.

Imran Kombe ni nani

Luteni Jenerali wa JWTZ Imran Kombe, alikuwa mwanajeshi na kachero wa usalama wa Taifa ambapo katika vita Uganda na Tanzania mwaka 1979, aliongoza brigedi ya 201 wakati Tanzania ilipoivamia Uganda kumtoa Nduli Idd Amin.

Mwaka 1980, ndio alipata wadhifa wa Mnadhimu mkuu wa JWTZ na kwa mujibu wa taarifa za mitandao zinaonyesha Desemba 30, mwaka huo, alipandishwa cheo na kuwa meja jenerali na mwaka uliofuata aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenda Hungary.

Mwaka 1983, Kombe aliondoka jeshini akiwa na cheo cha Luteni Jenerali na kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Idara ya Uslama wa Taifa (TISS), nafasi aliyoitumikia hadi 1995 na kustaafu. Aliuawa kwa kushambuliwa kwa risasi Juni 30,1996.

Baada ya mauaji hayo, Jeshi la Polisi liliwatia mbaroni askari watano na raia mmoja, Ismail Katembo ambaye hata hivyo alifariki dunia akiwa gerezani hata kabla ya kesi yao ya mauaji ya kukusudia haijasikilizwa na kutolewa hukumu.

Fuatilia hapa Kesho.............
Picha sio ya Kombe ni ya Robert Manumba!tuwekee picha ya Kombe
 
Ni mauaji yaliyogubikwa na simulizi na hisia tofauti juu ya nini hasa kiini cha mauaji ya mkurugenzi mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa nchini (TISS), Luteni Jenerali Imran Kombe aliyeuawa kwa kupigwa risasi Juni 30 mwaka 1996.

Kumekuwepo na nadharia ya ulaji njama (conspiracy theory) kwamba pengine kuna mkono wa mtu katika mauaji hayo yaliyotokea katika Kijiji cha Mailisita Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro na nyingine ni kwamba kweli aliuawa na polisi.

Katika mfululizo wa makala hii, Mwandishi Wetu atakuletea simulizi ya nini hasa kilisababisha mauaji yake, nani walimfyatulia risasi zaidi ya 15, maelezo ya maungamo ya wauaji wake yanasemaje na familia ililipwa fidia ya Shilingi ngapi.

Simulizi hii inaegemea ushahidi uliotolewa mahakamani katika kesi hii na kesi ya madai ya fidia iliyokuwa imefunguliwa na mkewe, Roseleene Kombe dhidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na simulizi zilizogubika mauaji hayo.

Maneno yalisemwa mengi, mojawapo ni hisia kuwa huenda aliuawa kwa sababu ya urafiki wake wa karibu na Agustino Lyatonga Mrema, mgombea urais kwa tiketi ya chama cha NCCR-Mageuzi 1995, lakini kwa kesi ilivyokuwa mahakamani haikuwa sahihi.

Kwa kuwa Kombe alikuwa amepigwa risasi na polisi, licha ya kuripotiwa kuinua mikono yake juu kama ishara ya kujisalimisha kwa watu walioamini ni wezi wa gari, kulikuwa na uvumi kwamba mauaji yake yalikuwa yamepangwa.

Ni kutokana na hisia hizo na moto wa kisiasa juu ya mauaji hayo, Rais wa awamu ya tatu, hayati Benjamin Mkapa aliamua kuunda tume ambayo iliwasilisha ripoti yake 1997 ambayo si wazi, ikisema Serikali haikuwa na mkono katika mauaji hayo.

Tume hiyo iliyokuwa chini ya mwenyekiti, Jaji Damian Lubuva aliyekuwa na Jaji Mussa Kipenka wakati huo akiwa mwanasheria mwandamizi wa Serikali, ilihoji mashahidi 52 na mwaka 1997 ilitoa ripoti kwa Mkapa iliyohitimisha kwamba Serikali haikuwa na mkono wowote katika kifo cha Kombe.

Hadi sasa taarifa ya tume hiyo, kama zilivyo baadhi ya tume zilizoundwa kutafuta ukweli wa jambo ambalo linaibua hisia kali, imekuwa ni siri.

Mwaka 1998, Mbunge wa Temeke Jijini Dar es Salaam, Augustino Mrema aliibua hoja bungeni kuwa kifo cha Kombe kilikuwa sehemu ya mpango wa mauaji uliofanywa na Serikali, ingawa hata hivyo alishindwa kuthibitisha madai hayo. Pamoja na taarifa hiyo ya tume na ushahidi uliotolewa mahakamani kuhusiana na mauaji ya Kombe, bado baadhi ya watu hadi sasa wana hisia tofauti juu ya mauaji hayo na katika makala hii tutakuletea mwanzo mwisho nini kilitokea.

Timu ya makachero ilivyoundwa

Usiku wa Juni 30, 1996 na siku iliyofuata, kulizagaa taarifa za kuuawa kwa kupigwa risasi na Polisi kwa Luteni Jenerali Kombe, aliyewahi kuwa mkurugenzi wa tano wa TISS na taarifa hizo hazikuzagaa kupitia mitandao ya kijamii kama ilivyo sasa.

Wakati huo wala simu za kiganjani (kitochi) zilikuwa hazijawa nyingi, licha ya kwamba zilianza kuingia nchini mwaka 1994, hivyo taarifa zilisambaa kama moto wa kifuu na katika mji wa Moshi, watu walikaa katika makundi wakijadili.

Taarifa hizo zilisema polisi walimuua Kombe kwa kummiminia risasi hata baada ya kushuka kwenye gari na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kujisalimisha, na maiti yake ilipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mawenzi.

Polisi wakati huo walikuwa wanaamini wamemuua mtu waliyekuwa wanaamini ni mwizi mashuhuri wa magari na walikuwa wakitamba kufanikiwa kukamata gari Nissan Patrol namba TZG 50 mali ya D.W Ladwa lililoibwa Jijini Dar es Salaam.

Ni hadi mkuu wa upelelezi (RCO) Mkoa wa Kilimanjaro alipopokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kwa jina la Iwisi Shoo, akimwambia gari walilolikamata si lenyewe na mtu waliyemuua si mwizi, bali ni Kombe, mkuu wa zamani wa TISS.

Hapo ndipo Polisi wenyewe walijikuta wakipata ganzi baada ya kugundua waliyemuua ni Luteni Jenerali mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ambaye alitumikia cheo cha mkurugenzi wa TISS kati ya mwaka 1983 na 1995.

Hapo ndipo mwili wake sasa ukahamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC ili kuhifadhiwa ukisubiri taratibu nyingine za kisheria na mazishi.

Lakini ilikuja kubainika kuwa gari la marehemu namba TZD 8592 aina ya Nissan Patrol lilikuwa likifanana na la Ladwa na siku kadhaa nyuma, polisi Jijini Dar es Salaam, walikuwa wamelikamata na kuliachia baada ya kuridhika silo.

Ingawa Kombe na familia yake ni wenyeji wa Kilimanjaro, wana nyumba jijini Dar es Salaam.

Wakati Polisi wakiendelea na uchunguzi, walipata taarifa fiche zilizowaambia kuwa mwizi aliyeiba gari hilo alikuwa amelipeleka mkoani Kilimanjaro, hivyo ofisi ya RCO Dar es Salaam ikawatuma Polisi wawili kwenda Kilimanjaro.

Makachero hao kwa mujibu wa hukumu ya rufaa namba 8 ya 1998 iliyotolewa na majaji watatu wa mahakama ya Rufani iliyoketi Jijini Arusha na kutoa hukumu yake Machi 16,1992, ni Sajini Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa.

Hukumu hiyo ilitolewa na majaji Lameck Mfalila, Barnabas Samatta na Kahwa Lugakingira kutokana na hukumu ya kifo iliyotolewa Januari 26,1998 na Jaji Buxton Chipeta dhidi ya askari wawili, Koplo Juma Mswa na Konstebo Mataba Matiku.

Kulingana na nyaraka za mahakama ya Rufani, Sajin Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa, waliondoka Jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Kilimanjaro wakiwa na gari lingine la Ladwa likiendeshwa na dereva wake aitwaye Ismail Katembo.

Dereva huyo ndio angetumika pia kulitambua gari la Ladwa lililoibwa na wote watatu waliwasili Moshi Juni 27,1996 na kuripoti Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kilimanjaro na kupokelewa na RCO ambaye aliamua kuwaongezea nguvu.

Hapo wakaongezewa makachero watatu, koplo Elisante Tarimo aliyekuwa mshtakiwa wa pili, Koplo Chediel Elinisafi aliyekuja kuwa mshtakiwa wa nne na Konstebo Mataba Matiku aliyekuwa mshtakiwa wa tano katika kesi hiyo.

Makachero hao walipewa bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) namba N.1270 na risasi 30 ambayo ilibebwa na Mataba Matiku wakati Sajenti Thomson Mensah na Koplo Juma Mswa kila mmoja alikuwa na bastola yenye risasi nane.

Koplo Elisante Tarimo na Chediel Elinisafi wao hawakuwa na silaha yoyote.

Kwa hiyo timu hiyo ya makachero ikaanza msako wa kulitafuta gari mali ya DW Ladwa aina ya Nissan Patrol lenye namba TZG 50 ambalo lilikuwa likifanana na gari la Luteni Jeneral Kombe TZD 8592 lililokamatwa Jijini Dar es Salaam na kuachiwa.

Siku hiyo ya Juni 30, 1996 kwenye saa 10 alasiri wakiwa katika misheni ya kulisaka gari hilo la Ladwa, wakiwa eneo la kijiji cha Shiri Njoro barabara ya Moshi-Arusha wakati huo wakiwlekea barabara hiyo kuu, mbele waliona gari la Kombe.

Dereva Ismail Katembo ambaye sasa ni marehemu alitoa sauti ya mshangao akisema gari lililopo mbele yao likitokea barabara ya Arusha-Moshi ndio gari ambalo wanalitafuta, hivyo akaliwashia taa lisimame, lakini dereva hakusimama.

Polisi hao waligeuza gari lao na kuanza kulifukuza gari la Kombe ambalo lilikuwa likifanana kwa rangi na lile na DW Ladwa lililokuwa likitafutwa na wakati wakilifukuza walianza kulishambulia kwa risasi kumlazimisha asimame.

Imran Kombe ni nani

Luteni Jenerali wa JWTZ Imran Kombe, alikuwa mwanajeshi na kachero wa usalama wa Taifa ambapo katika vita Uganda na Tanzania mwaka 1979, aliongoza brigedi ya 201 wakati Tanzania ilipoivamia Uganda kumtoa Nduli Idd Amin.

Mwaka 1980, ndio alipata wadhifa wa Mnadhimu mkuu wa JWTZ na kwa mujibu wa taarifa za mitandao zinaonyesha Desemba 30, mwaka huo, alipandishwa cheo na kuwa meja jenerali na mwaka uliofuata aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenda Hungary.

Mwaka 1983, Kombe aliondoka jeshini akiwa na cheo cha Luteni Jenerali na kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Idara ya Uslama wa Taifa (TISS), nafasi aliyoitumikia hadi 1995 na kustaafu. Aliuawa kwa kushambuliwa kwa risasi Juni 30,1996.

Baada ya mauaji hayo, Jeshi la Polisi liliwatia mbaroni askari watano na raia mmoja, Ismail Katembo ambaye hata hivyo alifariki dunia akiwa gerezani hata kabla ya kesi yao ya mauaji ya kukusudia haijasikilizwa na kutolewa hukumu.

Fuatilia hapa Kesho.............
IMmeamua kuileta wakati huu sio!!?

sawa tutasoma,kwani wastaafu wa sasa wapo salama!!?

"Hakuaminika juu ya taarifa fulani japo alinyoosha mikono juu vyuma vilipenya"Tumia akili
 
Juni 30; 996.

Mei 21, 1996:
AJALI YA MELI YA MV BUKOBA, watu takriban 1500 wapoteza maisha

Ilisemekana kuwa ilikuwa ni ajali ya kwanza kubwa duniani kuwahi kutokea kwenye maji ya MAZIWA

TETSI ZA KISAYANSI:
Inasemekana kuwa Meli huwa haiwezi kupata ajali na kubinuka tumbo juu. NI kama ndege huwa haiwezi kupata ajali halafu iakbinuka tumbo juu. Kwa hiyo ukiona ndege au meli imepata ajali na kubinuka tumbo juu, ujue kuna nguvu ya ziada nje ya ajali ambayo imetumika kuifanya ikae tumbo juu
MV BUKOBA ILIZAMA KWA KUBINUKA TUMBO JUU!
 
Back
Top Bottom