Arusha: Polisi wawakamata Waliohusika na Mauaji ya Dereva wa magari ya Watalii Omari Msamo

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
1711465988752.png
Machi 20, 2024 Jeshi la Polisi lilitoa taarifa kuhusiana na kifo cha Omary Saimon Msamo kilichotokea huko Wilayani Karatu Mkoa wa Arusha Machi 16, 2024.

Tulieleza kutokana na mazingira yaliyokuwa yamezunguka tukio hilo ilitubidi kushirikisha wataalam mbalimbali wakiwepo wachunguzi wa matukio ya vifo. Timu hiyo katika uchunguzi wake ilibaini kifo chake hakikuwa cha kawaida bali ni Mauaji. Baada ya kubaini hivyo ilichunguza nani aliyefanya mauaji hayo na kwa malengo au madhumuni gani. Hivyo kwa kutumia uchunguzi wa kisayansi waliweza kubaini waliohusika na mauaji hayo na malengo yao yalikuwa ni kumpora Omary Saimon Masamo chochote kile watakacho mkuta akiwa nacho.
Waliohusika na mauaji hayo tayari wamekamatwa na wamekutwa wakiwa na simu ya marehemu ila fedha walizompora kiasi cha Shilingi 200,000/= walikuwa wameshagawana na kuzitumia. Waliweza kumpora baada ya kumpiga kisogoni na kudondoka chini.

Waliokamatwa ni Anthony Paskali ambaye anajulikana kwa jina maarufu Lulu na Emmanuel Godwin Jeseph anayejulikana kwa jina maarufu la Emma wote wakiwa ni wakazi wa Karatu. Taratibu zilizobaki za kiuchunguzi zinakamilishwa ili hatua nyingine za kisheria ziweze kufuata.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa tahadhari kwa baadhi ya watu kuacha kueneza taarifa za uwongo, chuki na uzushi dhidi ya mtu mwingine au taasisi kwa ajili ya malengo yao binafsi kwani kwakufanya hivyo watakuwa wanaukaribisha mkono wa sheria uweze kuwafikia na kuchukuliwa hatua.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania

1711466753375.png

Picha: Omary Saimon Msamo enzi za uhai wake

 
Sarakasi zinaendelea.

Alisikika mzalendo mmoja akisema kesi ya nyani ameuziwa panya.
 
Alouziwa cm ya marehemu ndo kabeba msala wote cm used za bongo mbaya sana
 
Hivyo kwa kutumia uchunguzi wa kisayansi waliweza kubaini waliohusika na mauaji hayo na malengo yao yalikuwa ni kumpora Omary Saimon Masamo chochote kile watakacho mkuta akiwa nacho.

Sikuwahi kufahamu kwamba jeshi letu limeshafikia pazuri kiasi hiki kwenye masuala ya uchunguzi wa kisayansi.

Kwamba tunaweza kuuchunguza mwili wa marehemu na ukatueleza ni nani aliemuua?

Basi tuendelee kuimba jina lake.
 
Yule dada wa kibaha mpaka leo kimya, wale wauwaji waliomfuta kanisani. Yule mama kule Moro Mwajuma nani aliuwawa nyumbani kwake 2022 mpaka leo kimya.
 
Jeshi la Polisi linaendelea kutoa tahadhari kwa baadhi ya watu kuacha kueneza taarifa za uwongo, chuki na uzushi dhidi ya mtu mwingine au taasisi kwa ajili ya malengo yao binafsi kwani kwakufanya hivyo watakuwa wanaukaribisha mkono wa sheria uweze kuwafikia na kuchukuliwa hatua.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania
Mbona matukio mengine ya shambulizi hamjitokezi kuyaandikia hivi?
 
Sikuwahi kufahamu kwamba jeshi letu limeshafikia pazuri kiasi hiki kwenye masuala ya uchunguzi wa kisayansi.

Kwamba tunaweza kuuchunguza mwili wa marehemu na ukatueleza ni nani aliemuua?

Basi tuendelee kuimba jina lake.
Hakuna kitu hapo. Polisi tangu wavuruge ushahidi wa kesi ya mauaji ya dadangu sina hamu nao. Hakuna jeshi poyoyo kama hili la polisi. Yaani ushahidi waliopeleka mahakamani ulikuwa wa kipumbavu shauri ya rushwa! Hata wakili aliyewekwa utafikri ni wakili wa ngumbaru anauliza maswali ya layman. Eti tukashirikisha wataalam wa mauaji! Hopeless!
 
Jeshi la Polisi linaendelea kutoa tahadhari kwa baadhi ya watu kuacha kueneza taarifa za uwongo, chuki na uzushi dhidi ya mtu mwingine au taasisi kwa ajili ya malengo yao binafsi kwani kwakufanya hivyo watakuwa wanaukaribisha mkono wa sheria uweze kuwafikia na kuchukuliwa hatua.
Kwa hiyo kumbe raia kwenye haya matukio ya mauaji wawe wanawasingizia polisi ili uchunguzi ufanyike haraka na kwa kina? Bila polisi kutajwa kwamba wamehusika wasingeshughulika la hili!
 
Back
Top Bottom