Zanzibar ilijitoa katika sheria za Jamhuri ya muungano ya usafiri wa majini ya mwaka 2003 na kuunda sheria yake ya bahari na usafiri ya mwaka 2006 na kuanzisha chombo chao, Zanzibar Maritime authority((ZMA) 2006.
ZMA haijaandikishwa na shirika la International Maritime organization(IMO) isipokuwa kupitia Jamhuri ya muungano wa Tanzania(JMT) ambayo inalipa ada za usajili. JMT haipati mapato kutoka ZMA au biashara zinazotokana.
Meli ilizosajili Zanzibar ni 400 kupitia wakala wake aiyeko Dubai kampuni ya Philatex. Mapato yatokanayo huingia SMZ na JMT haipati chochote isipokuwa jukumu la kulipa ada kwa chombo huru na chenye mamlaka kamili cha SMZ
Mwezi June meli zilizosajiliwa na Zanzibar zilikiuka vikwazo vya UN kwa kusafirisha mizigo ya Iran na kuiweka JMT katika wakati mgumu ikiwa ni pamoja na kuwekewa vikwazo vya uchumi.
Wiki hii meli yenye tani 30 zenye thamani ya bilioni milioni 125 zikiwa zimesajiliwa na ZMA chombo cha SMZ imekamatwa huko Italia. Hiyo ni sehemu tu ya meli mbovu ambazo zimesajiliwa. Umoja wa Ulaya (EU) umeiweka Tanzania katika nchi zenye vyombo hatari vya majini na vinavyohitaji ukaguzi.(Siyo SMZ ni JMT).
Ikumbukwe SMZ ilishajitoa kuhusu masuala ya usafiri wa majini tangu mwaka 2006 na kuwa na mamlaka kamili
Nguruvi3 kati ya watu walio na akili mbovu as far as Zanzibar concerns mmojawapo ni wewe na kujionyesha hivyo ni jinsi unavyochukuwa muda na pumba kuandika itokeapo jambo kuhusu Zanzibar. Sasa hapa unakusudia nini kutaka kuikana Zanzibar juu ya utanzania eti ina sheria yake juu ya suala la meli. Sasa ulitaka kuwepo na bendera tofauti? Kwani hili si kati ja mambo ambayo nyie hamtaki yafanyike? Hata katika harakati za sasa hivi za katiba hiyo ndiyohamu ya Wazanzibari kuwa na bendera yao na utawala wao wa mambo ya nje.Hili likifanyika ingesaidia sana kuondowa hili suwala kla kupakana matope. Kinyume cha hivyo mabaya yanayofanywa na upande mmoja yatakuwa yanawahusu pia na upande wa pili.
Jana waziri wa mawasiliano na miundo mbinu wa SMZ Rashid Seif suleiman amevilaumu vyombo vya habari vya Tanzania BARA kuhusu kuandika habari hizo.
http://www.habarileo.co.tz/index.ph...meli-zilizosajili-zanzibar-zaichafua-tanzania na
http://www.dailynews.co.tz/index.php/local-news/22134-katiba-still-a-thorny-issue
Waziri wa SMZ haoni tatizo la kusafirisha mzigo wa bangi lilivyoichafua JMT ambayo Zanzibar ilishajitoa katika sheria na kuanzisha ZMA ila anaona tatizo habari hizo kuandikwa
Waziri Mwakyembe wa JMT ameingilia kati kufuatilia kadhia hiyo kwasababu Tanzania ndiyo yenye bendera na usajili wa IMO (Siyo meli) inakabliwa na kibano cha kimataifa kama ilivyokuwa kwa meli za Iran.
Gharama za ZMA kule IMO zinalipwa na JMT na waziri anatumia muda na gharama za JMT kuzuia uharibifu wa meli
yenye mzigo wa Bangi ya SMZ.
Unaona jinsi chuki zako zinavyokupotowa? Eti ni mzigo wa bangi wa nani?
Waziri huyo wa miundo mbinu wa SMZ alikaririwa na gazeti jana akisema faini inayotokana na kukiuka mkataba kati ya wenye meli na SMZ ambayo ni dollar 500,000 italipwa kwa SMZ(Siyo JMT)
Kumbuka hapo juu ulishasisitiza utengano wa SMZ na JMT lakini unapata karaha linapokuja suwala la mafao. uliona kichefuchefu kwa kuharibiwa jina, aisee unahangaika, hutulii!
Nilidhani waziri wa SMZ alitakiwa aeleze nini kimetokea hadi mzigo wa bangi tani 30 ukamatwe kwa jina la nchi ya Tanzania (Siyo Zanzibar)huku tukifahamu mapato yatokanyo na shughuli za meli hizo ikiwa ni pamoja na faini tarajiwa ni ya SMZ.
Ninajiuliza:
1. Kama Zanzibar ilishajitoa na kuanzisha ZMA kwanini meli zake hazisajiliwi na SMZ tukijua wana bendera yao
Tupeni uhuru wa kuipeperusha na hapo hatutakukereni wala nyie hamtatukera.
2. Kwanini kodi ya JMT ambayo ni ya Mtanganyika itumike kuhudumia shughuli za SM
Hili unalijuwa wewe tu kwani hata ikitumika unajuwa maana ya Tanzania wewe? Ukijuwa maana ya Tanzania usingejiuliza swala la kipuuzi kama hili.
3.Kwanini waziri Mwakyembe ashughulikie suala hili ambalo si la muungan
Kama kafanya hivyo basi ni kimbelembele chenu cha kufanya kila kitu nyie ndio wenye mamlaka! Kuanzia sasa acha kulaumu Wazanzibari na badala yake laumu sheria na muundo wa utelezaji wa Tanzania.
4. Je waziri Mh Suleiman wa SMZ anajua madhara yatakayomkumba Mtanganyika kutokana na biashara ya SMZ ambayo haimhusu kwa namna yoyote?
Mtanganyika ni nani ndugu yangu? Kuna Mtanzania na Mzanzibari na ingekuwa busara kuuliza madhara kwa Mtanzania kama yanavyoletwa na mauwaji ya maalbino na usafirishaji wa madawa kupitia JNIA. Watanzania wote wanapata madhara kwa tendo lolote baya!
5. Kuna tatizo gani vyombo vya habari kuandika kuhusu kakamatwa kwa mzigo wa biashara wa meli zilizosajiliwa na ZMA ambacho ni chombo halali cha SMZ? Vyombo vya habari vimekosea nini na wapi?
Kwa upande wangu nahisi tatizo linakuja pale panapopigiwa baragumu dhidi ya upande mmoja na kujitowa katika makosa ya ujumla. Yes meli imeandikishwa Tanzania basi iwe hivyo kuwa meli imeandikishwa Tanzania Zanzibar na kila mmoja atajuwa kuwa imeandikishwa wapi. Lakini hilila kujifanya kuwa eti limetokea kwasababu meli imeandikishwa Zanzibar si sahihi. Kuna kesi nyingi tu amazo vyombo vya upande mmoja hufanya madudu lakini haisemwi kuwa upande wa pili hauhusiki. Uandishi wenye mtizamo kama wako si sahihi hata kidogo
Hebu tuellimishane kwa pamoja wanajamvi wote
JokaKuu GHIBUU Nonda Mzee Mwanakjiji Mchambuzi Jasusi EMT Ngongo platozoom Barubaru Zitto Mnyika Ritz chama Mkirua Zinedine AshaDii gfsonwin The Bigshow Kimweri Fundi Mchundo Bongolander
Ahsanteni