Sikieni hoja za wazanzibar

Sikieni hoja za wazanzibar

Ni ngumu kwa watanganyika kuwaelewa waz'br kuwa hawataki muungano lakini mtaelewa,action zipo tele za kukufanyeni ili muelewe.
 
Mzee mwanakijiji.hapo nakukosa kidoogo wazanzibati na watanganyika sio watanzania.la pili wazanzibari washazoea kupakwa matope na serekali ya tanganyika.nakupa mfano: kulitokea uhalifu wa makanisa znz.waziri wa ulinzi alikuja moja kwa moja znz na akatangaza kwamba kuna ugaidi znz mbele ya waandishi wa habari ila sasa palipotokea kuripuliwa arusha kule hatujamsikia kusema kuna ugaidi tanganyika.swali langu kwann. Yupo tayari kuwapaka matope wazanzibar ila watanganyika yanayotokea anabana mdomo.jeee haki hii kwelii kwa kuwaharibia jina la wazanzibar ili watali wasije ndio maana yake.mana znz kikubwa wanategemea kipato cha watalii.so amesema vile ili kuwaharibia.inasikitisha sanaa😕
 
Ndugu yangu Nguruvi3, hawa ndugu zetu kuliko kubishana nao heri ubishane na meza! "Mtuache tupumue", ndicho kilio chao huku wametukumbatia kama kupe anavyomganda ng'ombe! Kupe anao uhuru kabisa wa kujiondokea wakati wowote lakini je, huo mlo wa siku utoke wapi? Wakati kamganda ng'ombe kupe hana wasiwasi wa kula, hana wasiwasi wa kuhangaika juani na hana wasi wasi na usalama wake!

Katiba wanayo, Raisi wanaye, bunge wanalo, bendera wanayo na wimbo wa taifa wanao halafu bado wana jeuri ya kudai eti waachiwe wapumue. Ni kama mtu kudai katekwa na kufungiwa huku yuko huru na milango na geti zote ziko wazi...ni kiasi tu cha kuaga lakini wapi! Waache vinono vya bara, thubutu! Hakuna hukumu mbaya kwa kupe kama ile inayotia kufuli milango ya ghala walikozoea kupata lishe bora bila bughdha.
 
Mr nguruvi.ni kweli maneno yako tuachieni tupumuweeeeeeeee jamaniii.mshatutaguna sanaaaaa.fedha zetu mshakula sanaaaaa.lkn nashangaaaa bado mnataka muungano.mnalazimisha muungano kwasabau mtakosa mnachokipata kwetu. Hatutakiii jamaniiii tuacheni tupumuweeeeee
 
Hebu tuellimishane kwa pamoja wanajamvi wote

JokaKuuGHIBUUNondaMzee Mwanakjiji ........ Bongolander Bu'yaka

Mimi nitoe haraka kwenye diva list ya wapenzi wako unaotaka kujadiliana nao!

Mimi sishiriki kwenye mijadala ambayo washiriki wana kinga!

Nataka kusikia mawazo ya kiumbe chochote na naweza ku face off na kiumbe chochote, na wala mimi sio mtaalam wa masuala ya Muungano na wewe sio, maana ungekuwa ndio usingeogopa mawazo wala kujijengea kiota cha kuji protect as if nyinyi ndio mna busara saaana kumbe ni kujenga club ya ma prima donna dhaifu ambao hawawezi kujichanganya bila kulindwa.

Unaalika "wanajamvi wote" halafu unatutajia wapenzi wako watano unaowataka kwenye mjadala. Could not be more ridiculous. Ni vema JF libaki kuwa jamvi huru,
hao wapenzi wako watano watumie pm mkanywe chai pembeni huko!
 
Mimi nitoe haraka kwenye diva list ya wapenzi wako unaotaka kujadiliana nao!

Mimi sishiriki kwenye mijadala ambayo washiriki wana kinga!

Nataka kusikia mawazo ya kiumbe chochote na naweza ku face off na kiumbe chochote, na wala mimi sio mtaalam wa masuala ya Muungano na wewe sio, maana ungekuwa ndio usingeogopa mawazo wala kujijengea kiota cha kuji protect as if nyinyi ndio mna busara saaana kumbe ni kujenga club ya ma prima donna dhaifu ambao hawawezi kujichanganya bila kulindwa.

Unaalika "wanajamvi wote" halafu unatutajia wapenzi wako watano unaowataka kwenye mjadala. Could not be more ridiculous. Ni vema JF libaki kuwa jamvi huru, hao wapenzi wako watano watumie pm mkanywe chai pembeni huko!


Yaani yote haya kwa sababu tu amekutaka na wewe uone alichoandika! Ungejikalia kimya ungepata hasara gani?

John Legend atakushangaa sana na tantrum yako.

Amandla.....
 
Sikuona mahali pa kujibu kwasababu hoja zako hazina mantiki kwa uchache. Si kila hoja inajibiwa kwasababu nitajibu vipi matusi? Umesema mimi ni mpuuzi sasa hapo nijibu nini. Hata hivyo nakushukuru japo kwa kuandika.

Unaweza kuanzisha thread yako na si lazima nianzishe.
Najua hii nyuzi inawaudhi sana wzn lakini ndiyo habari ya mjini. Ukishaona matusi basi ujue hoja zimegota au kisu kimekula mfupa.

Waziri wa miundo mbinu wa Znz amejitokeza na kusema atalitolea ufafanunuzi suala hili.
Ameona wapi alipokosea, aheri basi kuliko wavurumisha matusi.
Kitu kimoja uelewe, nipo hapa kusimamia ninachokiamini kuwa ni sahihi kwa mtazamo wangu, nitakuambia ninachokusudia si kile unachotaka kusikia.

Lipo la tusi kwa kuambiwa kuwa unakuwa na chuki kwa masuwala ya Zanzibar? Unataka tukupembejee kwa mambo yasiyo na mantiki bali kuendeleza chuki kwa pande mbili sasa kama si upuuzi ni nini? unafikiri upuuzi ni matusi, la si matusi bali ni marejeo ya lugha isiyostahiki kusemwa na Mtanzania dhidi ya Mtanzania mwegine.
Nimesema uanzishe thread nyengine kwani wewe ni expert juu ya kuikashifu Zanzibar na elewa maadam tuna uhuru wa kutowa mawazo yetu tutakujibu kwa jinsi ile ile unayokuja nayo. Lete mjadala wa kujenga ili tujenge!
 
Lipo la tusi kwa kuambiwa kuwa unakuwa na chuki kwa masuwala ya Zanzibar? Unataka tukupembejee kwa mambo yasiyo na mantiki bali kuendeleza chuki kwa pande mbili sasa kama si upuuzi ni nini? unafikiri upuuzi ni matusi, la si matusi bali ni marejeo ya lugha isiyostahiki kusemwa na Mtanzania dhidi ya Mtanzania mwegine.
Nimesema uanzishe thread nyengine kwani wewe ni expert juu ya kuikashifu Zanzibar na elewa maadam tuna uhuru wa kutowa mawazo yetu tutakujibu kwa jinsi ile ile unayokuja nayo. Lete mjadala wa kujenga ili tujenge!
Mkiambiwa ukweli mtu ana chuki. Leo Mzaninzibar anakubali kuitwa Mtanzania!! ama kweli mumeshikwa pabaya.
Tupeni nafasi tupumue
 
Yaani yote haya kwa sababu tu amekutaka na wewe uone alichoandika! Ungejikalia kimya ungepata hasara gani?

Hasara ya ku compromise on a principle, principle of open-sourced forum, na kushindwa kutumia nafasi hiyo kufikisha ujumbe, kwamba, kualika "wanajamvi wote" kwenye mjadala halafu unatutajia majina matano ya unaowapenda ndio waje wachangie ni unafiki, moja, la pili, hasara ya kupunguza wigo wa mawazo yanayoweza kuletwa jamvini kuhusu Muungano kwa kualika wapenzi wako wachache.

Kubalini mawazo ya kila mtu, msiogope, msialikane wenyewe wenyewe, JF ibaki kuwa open forum, sio kugeuzwa clubby chat room ya wanaodhani kwamba wao ndio wakualikana tuje tudumishe fikra zao wao. Yani yeye au nyinyi muandike, sisi tusome, then "tujikalie kimya!" Ethos and legacy ya Mwalimu J. Nyerere kwa Watanzania, mpaka leo.

John Legend anatoka Magharibi, asingeshangaa, wao wanapokuwa na jambo la kuwa addressed hawana ethos za "kujikalia kimya," wanaheshimu sana passionate advocacy of principle, nasimamia open forum, untrammeled sea of discussions, kwenye forum ya kuchocheana kuchangia asingeweza kumwambia mtu "jikalie kimya."

Mngepata hasara gani kujialika kwa pm?
 
Hee ndugu yangu hawa ni wafanyakazi.
Mmiliki wa meli ni zanzibar.

Ukiwa rubani wa Qatar au Emirate wewe humiliki ndege, ni mfanyakazi tu.
Wenye meli ndio watoke watuambie nini kilitokea.

Habari za Polisi kutafuta mzigo zaidi ndani ya meli ya Zanzibar zimeandikwa kumbe!! sasa waziri alipowashukia waandishi wa Habari wa Tanzania bara alikuwa na maana gani. Kuwa mbara basi ni kosa kuandika habari za bangi la Zanzibar!!

Yeye alitakiwa atoke aeleze meli hiyo iliyokuwa na bendera ya znz na iliyosajiliwa na ZMA kwa ushirikiano na Philatex ambayo JMT haijui kimetokea nini.

Hao mabaharia hawakubeba bendera kwa hiari yao, ilikuwa ni lazima waweke bendera. Nani alitoa bendera ni Philatex, kwa kibali cha nani -ZMA, inayowakilisha serikali gani SMZ.

Kuna uhusiano kati ya SMZ na JMT jibu ni ndio, lakini kwa hili la shughuli za majini jibu ni hapana.

Sasa kama unadhani hakuna mznz mbona waziri Mwakyembe ameingilia kati, mbona waziri wa miundo mbinu wa zanzibar amelizungumzia kwa kigugumizi bila kulaani.

Si lazima wawepo wznz kinachoangaliwa ni usajili na mmiliki ambaye ni SMZ. Hili zigo la biashara msilikatae, mtakuja kukataa waziri wenu siku mkijiunga na Oganization of Islamic conference(OIC) kama hali ikitengemaa

Mkuu mimi simjui mmiliki wa meli wewe kama unamjua basi nitajie inaonekana unajua mambo mengi ya zanzibar
 
Mkiambiwa ukweli mtu ana chuki. Leo Mzaninzibar anakubali kuitwa Mtanzania!! ama kweli mumeshikwa pabaya.
Tupeni nafasi tupumue

Hahaha1 Nguruvi3 hujapatapo kunichekesha kama leo. Eti leo unakariri maneno ya watani wako "Tupeni nafasi tupumue". Nyie endeleeni kutungangania tu mtavaa shuka kama sisi tarabu tayari mnacheza!
 
Mkuu Nguruvi3, unakuwa kama hujui kupenda!, Mke ukimpenda, unamhudumia kama jukumu lako ikiwemo kumlisha, kumvisha, kumtunza na kumpendezesha, na sio hayo tuu, kwa sababu una mpenda, unampa kila anachokita, hata kama wewe hukipendi!, mfano anapenda ubuyu, utamletea hata kama wewe huupendi!.

Hiyo faini ya dola 500,000 ni hela tuu ya kununulia ubuyu na wanja na vipondozi, mwache mama aitie kwenye kijaluba chake! na endelea kumhudumia!.
Kuna watu humu hawajui kupenda!, mimi nakumbuka enzi zangu za ujana, wakati huo mishahara ilikipiwa dirishani, niliwahi kuhonga bahasha nzima za mshahara wote, ile nimetoka tuu dirishani, nikakabidhi bahasha yote vile vile ilivyo mpaka na coins zake, kwa ka binti fulani cheupe kalichokuwa ndio kwanza kameajiriwa!.

Leo mnalalamikia mke Zanzibar baada ya miaka 49 ya ndoa!, tena kipindi hiki tunapopanga kusheherekea Diamond Jubilee! April 26 mwakani!. Mke nitaendelea kumhudumia, kudumisha ndoa!.
Pasco.

Si wanaume wote wanaoowa kwa mapenzi lakini wapo wanaowa kwa tamaa. Kwa bahati mbaya si Wazanzibari wake wa wa Tanganyika hatukuolewa kwa mapenzi kwa sababu kwanza mwanamme mwenyewe si mstaarabu, ana choyo na hata familia yake yote ni matapeli, wanafisadiana wenyewe kwa wenyewe na makatili bado wako kwenye miaka ya ujahilia ya kuamini vitendo vya mauwaji na ushirikina.
Pasco, unajidai tu lakini Nguruvi ndie sampuli ya waume zetu Wazanzibari. Kinapotokea kitu kidogo basi mume yuko tayari kumkana mke na ikitajwa pesa basi haraka anatangaza cheo chake. Mume wetu kwa bahati mbaya yeywe mwenyewe ni ombaomba lakini hujisifu kuwa anatuhudumia. Atamuhudumia nani iwapo nae ana mabwana zake anaowategemea? Tumechoka na uke huu lakini mume ----- kasikia kuwa kwetu kuna urithi hivyo anatungangania. Janadume hili limefika mpaka kwa wajomba kuomba urithi wetu bila ya hata kutuambia sisi wake zake. Halafu unasema mapenzi, toka lini iwapo ndani ya familia yako hamna neno hilo, bali lipo ubinafsi tu.
 
Well said mkuu. Nianze na ulipomalizia, wengi hapa jamvini tumeshatoa ushauri wa namna Zanzibar wanavyoweza kuwa na mamlaka kamili. Wazanzibar wamekataa na kufuata njia zile zile wanazolaumu.

Njia ya pili ni kura ya maoni, lakini nayo kwa kujua inaweza kuzaa wasichokitaka hawaitilii mkazo.
Mkazo upo katika masilhai yao kwa lugha yao ni muungano wa mkataba. Tanganyika haihitaji mkataba na Zanzibar!
wa nini?Kwakuelewa wanaihitaji Tanganyika sasa wanakuja na mlango wa mkataba.

Ushahidi kutotaka kuvunja muungano umetolewa na vinara wa wao akina Jusa na Moyo. Kwamba, kuwepo na passport ya Tanzania-Tanganyika, Tanzania-Zanzibar baada ya kuona rasimu na ujio wa Tanganyika.

Rasimu imeondoa utegemezi kama ajira na ardhi n.k huku ikiweka wazi sheria ya pande moja itatumika pande nyingine kama kibano cha ubaguzi wao.

Haitawezekana kukaa na Tanganyika na kutoa masharti wanayotoa sasa. Ili kuweza kuendelea kunufaika na fursa zilizopo ndio wamekuja na kituko cha passport wakitaka mafao yao watumie neno Tanzania kama ambavyo wanalipiwa ada za ZMA wakati wanasafirisha bangi. Hili tumeling'amua na ni ushahidi wa wao kun ng'ang'ania muungano!

Maana ya kufanya mambo watakavyo ni kwasababu hakuna Tanganyika.Mathalan wanatumia umeme wa JMT bila malipo kwasababu nani awaulize, hata kama hawana mchango, si wana jina?
Wanasajili meli za bangi kwa ada za JMT nani awaulize hata kama wana bendera yao na wimbo wao wa taifa.

Tanganyika ikirudi hakutakuwa katika upuuzi wa kuendeshwa na watu milioni 1.2 tena lakini tano wakiwa wanaishi Tanganyika.

Kwa msingi huo akina Nape tuwaeleze wazi kuhusu wizi na hujuma dhidi ya taifa na kwamba sasa tunataka Tanganyika. Kama hilo halitafanyika kwa amani ninatabiri hali mbaya sana siku za mbeleni hasa kwa wazanzibar kwasababu Mtanganyika hatavumilia tena kodi yake itumike kusafirisha bangi za nchi nyingine.

Na hii ni wake up call kuwa lazima sasa tuamue, tumejitahidi lakini haiwezekani.
Inapofikia wanataka makao makuu ya JMT yahamie kwa watu laki tano bila kujali sababu za kijiografia, uchumi na siasa hapo hakuna la ziada bali kuachana nao. Hatujui wanadai nini hasa ! hatuwezi kuishi namna hiyo, tuvunje jahazi

Unajuwa ni kitu cha kushangaza sana kuona watu na akilizao wanazungumza mambo bila ya kufikiri.
1. Ni nani alieiondowa Tanganyika hata sasa mtwambie sisi kuwa mnataka Tanganyika yenu? Tanganyika yenu mliitowa wenyewe kwa kutaka sifa na kukubali kuchezewa akili na mtu mmoja tu, Nyerere. Angalau sisi tulitiwa katika muungano kwa nguvu ya silaha na tukawa hatuna la kusema , lakini Watanganyika mliitowa Tanganyika nyie wenyewe kwa akili ya mtu mmoja. Sasa alieitowa hayupo lakini mjukuu wake yupo. Ni Nape,basi mwambieni yeye sio sisi akupeni Tanganyika yenu, kwetu sisi ni sawa tu Zanzibar yetu ipo naitaendelea kuwepo hata hapo mtapoweza kumshinda mzuka wa Nyerere.
2. Mbona tunapofanya jitihada ya kuirudisha Tanganyika yenu mnaungana kutupiga vita? Tulifanya 1984, tukakutengenezeeni njia miaka ya 90 mkafikia hata kuunda G55 mkakubali kuzimwa. Ikaja rasimu ya Katiba na tukaichana hadharani na kutaka swala la muungano lijadiliwe mkawabatiza watu UAMSHO (Awareness sasa inakuwa mbaya). Baada ya rasimu kuambiwa serikali tatu ili Tanganyika iwepo mnaruka kimanga eti gharama, lakini mnapoteza pesa kutaka umoja ambao hamtakiwi EAC.
Nionavyo mimi sisi Wazanzibari tusiwe wagomvi wenu bali tuungane ili kuhakikisha kuwa Tanganyika yenu mnairejesha. Hili la Zanzibar itakuwaje lisikupeni hofu kwani angalau mtakuwa hamna mzigo. Tuwachieni mje kutembea na kupata watoto wa Kiarabu baada ya kwisha kutajirika na gesi na mafuta!
 
N akutumia bendera ya JMT kufungia tani za bangi nalo linahitaji Tanganyika irudi? Kwanini wasifungie na bendera ya znz ambayo imepugiwa kelele sana kuwa ipo na inagfanya kazi. Real! Kwanini BAYAZA imuathiri mtu wa matombo Morogoro?

Mzee naona kama tayari umesha data... Harakati za ukombozi wa Zanzibar hakuna aneweza kuziziwia tena. Mimi nataka unune mpaka upasuke, na huo unga sasa itabidi wauziyane wenyewe kwa wenyewe hapo Tanganyika...
 
Ndugu yangu Nguruvi3, hawa ndugu zetu kuliko kubishana nao heri ubishane na meza! "Mtuache tupumue", ndicho kilio chao huku wametukumbatia kama kupe anavyomganda ng'ombe! Kupe anao uhuru kabisa wa kujiondokea wakati wowote lakini je, huo mlo wa siku utoke wapi? Wakati kamganda ng'ombe kupe hana wasiwasi wa kula, hana wasiwasi wa kuhangaika juani na hana wasi wasi na usalama wake!

Katiba wanayo, Raisi wanaye, bunge wanalo, bendera wanayo na wimbo wa taifa wanao halafu bado wana jeuri ya kudai eti waachiwe wapumue. Ni kama mtu kudai katekwa na kufungiwa huku yuko huru na milango na geti zote ziko wazi...ni kiasi tu cha kuaga lakini wapi! Waache vinono vya bara, thubutu! Hakuna hukumu mbaya kwa kupe kama ile inayotia kufuli milango ya ghala walikozoea kupata lishe bora bila bughdha.
Mkuu Mag3 , uongo ukirudiwa mara nyingi hugeuka kuwa ukweli. Ndugu zetu wa zanzibar kwa kujua au kutokujua wamezusha maneno mengi yasiyo na ukweli. Hawa unaowaona mtandaoni ni ''elite''sijui mvua samaki inakuwaje.

Kinachofanyika hapa ni kuweka uongo wazi halafu kumuonyesha Mtanganyika wapi amegezwa ng'ombe wa maziwa huku akitukanwa kwa kila aina ya tusi. Tanganyika imejitoa ili kuleta Utanzania kwa manufaa ya wananchi. Haina maana kuwa Tanganyika inaihitaji znz, la hasha ni kujitoa katika spirit ya Uafrika.

Tanganyika a.k.a Tanzania imevumilia sana katika katika muungano. Wakati sasa umefika Tanganyika iwe na shughuli zake kuliko kushughulikia mambo kama bangi za serikali ya nchi nyingine kwa gharama zake.
Unaposikia Barubaru ambaye ni msomi na mchumi anadai misaada igawanywe nusu bila kudai madeni yagawanywe hapo kuna tatizo.

Ni tatizo hilo tunaliona katika kila sehemu ya muungano huu. Wazanzibar ambao ni 1.2 milioni na ambao 500,000 wanaishi Tanganyika na kuongeza strain katika social service huku wakifaidika na fursa za muungano hawana sababu ya kututukana.

Watanganyika wafikirie kama umuhimu wa muungano upo kwa kuzingatia haya machache.

1. Gharama za kuendesha serikali ya JMT inabebwa na Mtanganyika 100%
2. Gharama za huduma za jamii kama elimu na afya zinalipiwa na Mtanganyika 100%
3. Gharama za ulinzi na usalama zinalipiwa na Mtanganyika 100%
4. Huduma za SMZ zinachangiwa na Mtanganyika hata kama hana mafao kama hili la Usajili wa ZMA kule IMO
n.k

Ushahidi wa Mtanganyika kukabidhiwa zigo la kuendesha mambo ya muungano upo kwa aina nyingi.
Mathalan, katika taasisi na NGO zote za Zanzibar na wazanzibar wote hakuna anayeongelea gharama za uendeshaji wa serikali ya muungano hata hiyo inayoshauriwa ya serikali 3.

Uamsho, BAKAZA, Kamati ya maridhiano zote zimejikita katika hoja za mafao kwa znz kwa kuelewa kuwa Tanganyika ndio muungano na hakuna wa kuiongelea.

Leo wznz wamedai kupewa uwakilishi katika tume ya warioba kwa silimia 50,gharama za tume akibeba Mtanganyika

Wanataka bunge la katiba liwe na wajumbe asilimia 50 gharama akitupiwa Mtanganyika
Wanadai mgawanyo wa madaraka uwe 50% bila kusema wanchangia nini katika suala hilo
Wametaka rais achaguliwa kwa zamu ikiwa na maana ya 50% bila kusema anahudumiwa na gharama zipi, na sasa wanadai makao mamkuu yahamishiwe znz sababu ambayo sipendi kuijadili ikizingatia ni ya kipuuzi, kitoto na iliyotolewa na profesa kabisa kutoka znz.

Katika kamati zote hizo, hakuna hata siku moja, narudia hakuna hata siku moja kumekuwa na ushauri wa namna gani shughuli za muungano zigharamiwe.

Hakuna kamati iliyokuja na pendekezo la shughuli za uchumi ikiwemo madeni.
Kamati zote hizo zimejikita katika kutafuta uwakilishi sawa, vyeo na marupu rupu bila kusema yanagharamiwaje na nani na kwa utaratibu gani wakijua mzigo huo ataubeba Mtanganyika.

Huu ndio mwendelezo wa mambo kama ya kutoa mishahara kwenda kusaidia SMZ, kulipia umeme bure kwasababu hawataki kulipa tu na hakuna wa kuwafanya lolote, na hivi karibuni kulipia vyombo vyao vinavyojishughulisha na shughuli za biashara kama ya bangi hata kama havina mafao kwa Mtanganyika

Tukiangalia kwa undani, Mtanganyika anaumia sana katika muungano bila kuwa na mafao.
Ni kwa msingi huo tunashauri serikali ya Tanganyika ipewe utambulisho rasmi(ipo) ili ishughulikiea matatizo na maendeleo yake bila kuwabughadhi wazanzibar.

Ingawa sikubaliani na mchakato wa katiba kuanzia mwanzo na hadi sasa, labda niseme ukiisoma rasimu utaona jinsi gani tume ilivyojitahidi kuhakikisha kuwa masilahi ya pande zote yanalindwa.
Kupitia hilo masilahi ya Tanganyika yanalindwa kwa kiasi kikubwa sana kuliko ilivyo sasa.

Kwanini Mtanganyika anapaswa kuunga mkono mapendekezo.
Itapunguza gharama inazotoa Tanganyika katika muungano, itafungua fursa za Watanganyika kunufaika na rasilimali za nchi yao. Mfano, hakuna sababu Tanganyika ilipie wanafunzi 1000 wa znz na kuwanyima Watanganyika fursa za elimu ya juu ambazo baba zao wanalipia kodi kwa ukamilifu.

Hakuna sababu mkulima wa kidatu alipie umeme kwa znz ambayo haitaki kulipa tu.
Hakuna sababu za ardhi ya Tanganyika kuwa shamba la bibi huku tukiwa na 'wahamiaji halali-haram'

Tanganyika itapata utambulisho wake, na kuanzia hapo tutajua nini cha kufanya.
Kwasasa ni kuwazindua watanganyika kuhusu kuitetea nchi yao.
 
Mzee naona kama tayari umesha data... Harakati za ukombozi wa Zanzibar hakuna aneweza kuziziwia tena. Mimi nataka unune mpaka upasuke, na huo unga sasa itabidi wauziyane wenyewe kwa wenyewe hapo Tanganyika...
Hakika mimi nipo katika rekodi ya kuunga mkono harakati za znz kujikomboa. Nimewahi kuwahsuri mara nyingi sana. Tatizo ni wzn kuwa waoga na sijui wanaogopa nini. Znz inaweza kuwa kama Luxembourg, Mauritius, Dubai n.k. Znz inaweza kuwa na neema kama ile ya nyakati za sultan na utumwa.
Znz inawekana nje ya muungano, hakuna anayeweza kuifuta historia yake na znz itasimama yenyewe.

Huu upuuzi wa muungano wa mkataba au serikali 3 haupaswi kupigiwa upatu na mzanzibar mwenye akili.
Kinachotakiwa n kufanya haya
1. Kususia tume ya Warioba na kuzuia wajumbe wake au kujitoa
2. Kususia bunge la katiba
3. Kumrudisha makamu wa rais aliyepatikana kwa uzanzibar wake
4. Kuzuia wabunge wasije Dodoma
5. Kujadili kujitoa ndani ya BLW kama ilivyokuwa kwa mafuta na gesi, baraza la mitihani na ZMA n.k
6. Kuwarudisha wafanyakazi wote wa SMZ kutoka bara
7. Kuzuia wanafunzi kuchukua mikopo ya bara na kuja kusoma huku bara
8. Kuwashawishi wafanyabiashara kuondoka na kurudi kuwekeza znz
9. Kunzisha balozi zao kama walivyoanzisha wakala wa Philatex

Hadi hapo muungano utakuwa umekufa na harakati za kuiokomboa znz zitakuwa zimetimia.

Kama hawaweza kutumia fursa hiyo wakabaki na upuuzi wa mkataba ambao mzee amekwama nao chumbe, wakaleta hoja za kugawana vyeo bila gharama na kudai kisicho chao basi wajiandae kuwa chini ya kivuli mwanana cha Tanganyika kama mkoa. Hakuna njia ya mkato ni ima kunyoa au kusuka, ukombozi utabaki kuwa ndoto na simuliz mwanana. period.
 
Unajuwa ni kitu cha kushangaza sana kuona watu na akilizao wanazungumza mambo bila ya kufikiri.
1. Ni nani alieiondowa Tanganyika hata sasa mtwambie sisi kuwa mnataka Tanganyika yenu? Tanganyika yenu mliitowa wenyewe kwa kutaka sifa na kukubali kuchezewa akili na mtu mmoja tu, Nyerere. Angalau sisi tulitiwa katika muungano kwa nguvu ya silaha na tukawa hatuna la kusema , lakini Watanganyika mliitowa Tanganyika nyie wenyewe kwa akili ya mtu mmoja. Sasa alieitowa hayupo lakini mjukuu wake yupo. Ni Nape,basi mwambieni yeye sio sisi akupeni Tanganyika yenu, kwetu sisi ni sawa tu Zanzibar yetu ipo naitaendelea kuwepo hata hapo mtapoweza kumshinda mzuka wa Nyerere.
2. Mbona tunapofanya jitihada ya kuirudisha Tanganyika yenu mnaungana kutupiga vita? Tulifanya 1984, tukakutengenezeeni njia miaka ya 90 mkafikia hata kuunda G55 mkakubali kuzimwa. Ikaja rasimu ya Katiba na tukaichana hadharani na kutaka swala la muungano lijadiliwe mkawabatiza watu UAMSHO (Awareness sasa inakuwa mbaya). Baada ya rasimu kuambiwa serikali tatu ili Tanganyika iwepo mnaruka kimanga eti gharama, lakini mnapoteza pesa kutaka umoja ambao hamtakiwi EAC.
Nionavyo mimi sisi Wazanzibari tusiwe wagomvi wenu bali tuungane ili kuhakikisha kuwa Tanganyika yenu mnairejesha. Hili la Zanzibar itakuwaje lisikupeni hofu kwani angalau mtakuwa hamna mzigo. Tuwachieni mje kutembea na kupata watoto wa Kiarabu baada ya kwisha kutajirika na gesi na mafuta!
Hapana hakuna sababu za mzanzibar kulilia Tanganyika. Tanganyika ndio Tanzania kwasababu nchi ni gharama si jina. Ninyi mna serikali yenu kitu gani kinawashughulisha na Tanganyika?

Manchotakiwa kufanya ni kuhakikisha kuwa serikali yenu inafanya kazi kama mnavyotarajia. Hamna sababu za kuomba ulinzi na usalama wala kudai usawa katika muungao. Mbona mumevunja katiba ya JMT mara nyingi na hakuna anayewasemsha. Mathalan, mlipondoa mafuta na gesi nani amewasema kwa hillo. Mlipounda baraza lenu la mitihani ili watoto wasifeli nani amewauliza kuhusu hilo. Mlipounda ZMA na sas akusafirisha marobota ya nagi nani amewauliza kama mngetumia bendera yenu ambayo mliliia kwa nguvu sana. Sijui inafanya kazi gani hadi kufungia bangi bendera isiyowahusu maana mlijiyoa SUMATRA ya JMT.

Sijui Tanganyika inawakaza nini kiasi cha kuacha kushughulikia mambo yenu.
Ngojeni baada ya muda mtakuwa huru kabisa hata sisi tupo katika jitihada za kuaindaa tena Tanganyika amabyo ipo kwa kila aina ya ushahidi. Hilo si tatizo lenu ni tatizo letu tuachieni wenyewe.
 
Mkuu mimi simjui mmiliki wa meli wewe kama unamjua basi nitajie inaonekana unajua mambo mengi ya zanzibar
Meli imesajiliwa na SMZ kupitia ZMA na Philatex. Hawa wanajua mmiliki ni nani.
Waziri wa miundo mbinu alipaswa kuwaambia wanadamu wa dunia hii nani mmiliki wa meli, alichokifanya ni kuwananga waandishi wa habari wa TANZANIA BARA kana kwamba kuandika bangi ni kosa la jinai tena likifanywa na Mtanganyika.

Kamuulize waziri wako mmiliki ni nani? Lazima anajua maana alikuwa anachukua mapato.
Sina hakika kama mamapto hayo yalimsaaidia mshona nayavu za samaki.
 


Yaani yote haya kwa sababu tu amekutaka na wewe uone alichoandika! Ungejikalia kimya ungepata hasara gani?

John Legend atakushangaa sana na tantrum yako.

Amandla.....
Fundi , nilipoacha kumtaja ilikuwa gubu, nilipomtaja imekuwa kuwa gubu. sijui huyu bwana anatataka nini. Hajazuiwa kuchangia wala kulazimishwa. Nadhani ni kumu ignore tu ii kumsaidia avae nguo alizovua.
 
Back
Top Bottom