Mkuu
Nguruvi3 Hivi kama muungano usingekuwapo unadhani malalamishi ya kuchafuliwa kwa tanganyika na nchi ya zanzibar, na sio Tanzania kama unavyoandika ingetokea?
Nb tanzania ni pamoja na tanganyika na zanzibar yenyewe. Na kama jibu nila unadhani ni nani wa kulaumiwa? Walioasisi Muungano au wanaondeleza muungano?
Hapa kuna issue ya muungano watu wanachanganya. Hili si suala la muungano.
Hoja ni hii niweke kwa urahisi zaidi.
Mwaka 2003 Zanzibar wanajitoa katika usafiri wa majini wa JMT na kutokuwa sehemu ya JMT kwa suala hilo. Walifanya hivyo kupitia BLW bila kuishirikisha JMT na wala hawakuwa na mawasiliano zaidi ya kuondoka kama walivyofanya katika katiba mara nyingi.
Mwaka 2006 wakaanzisha chombo chao cha ZMA akinachosajili meli. Hadi sasa wanasajili meli 400 kupitia Philatec bila kushirikisha serikali ya JMT
June 2013 meli zilizosajiliwa na Zanzibar kupitia ZMA na Philatec zaonekane zikiisaidia IraN kinyume na vikwazo vya UN. JMT yapokea barua za onyo kutokana hjambo isilolijua.
Mwaka 2013 Sept meli yakamatwa ikiwa na bangi tani 30. Imesajiliwa na ZMA na Philatec kama taasisi za SMZ. Picha na habari za zagaa duniani kuhusu JMT.
Waziri wa miundo mbinu ajitokeza kulaumu vyombo vya habari vya Tanzania bara kuweka habari hii wazi kwa wananchi. Amezea kulaani au kueleza ushiriki wa znz katika zigo hili la aibu
Waziri Mwakyembe wa JMT aingilia kati kutoa ufafanunuzi wa jambo lisilo la JMT ambalo znz imeshajitoa.
Tangau mwaka 2003 ada za usafiri wa majini zinalipwa na JMT wakati znz imeshajitoa na kuwa na chombo chake bila kuishirikisha JMT. Udanganyifu wa juu kabisa.
Sasa tunataka tuelezwe uhusiano wa
1.Jumuiya ya kimataifa na JMT kuhusu zigo la bangi. Wapi na kwanini tuhusishwe
2. Kwanini znz itumie bendera ya JMT waliokataa kuwa sehemu yake mwaka 2003
3. Kwanini waziri wa JMT ashughulikie mambo yasiyo mhusu
4. Kwanini waziri alaani vyombo vya habari kwa habari za dunia na si bangi
5. Kuna uhusiano gani wa vyombo vya habari vya bara na zigo la bangi, kwanini isiwe vyombo vya habari vya Italia.
6. Kwanini JMT ilipe ada IMO kwa chombo ZMA kisicho na masilahi na JMT na ibebe lawama na kashfa zinazotokana na chombo kilichoikana JMT
Ukishaelewa hapo utaona suala la muungano halina mantiki zaidi ya mantiki ya ''hujuma'' kutojali na kushiriki kwa mgongo wa