Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,456
- 34,266
Zanzibar ilijitoa katika sheria za Jamhuri ya muungano ya usafiri wa majini ya mwaka 2003 na kuunda sheria yake ya bahari na usafiri ya mwaka 2006 na kuanzisha chombo chao, Zanzibar Maritime authority((ZMA) 2006.
ZMA haijaandikishwa na shirika la International Maritime organization(IMO) isipokuwa kupitia Jamhuri ya muungano wa Tanzania(JMT) ambayo inalipa ada za usajili. JMT haipati mapato kutoka ZMA au biashara zinazotokana.
Meli ilizosajili Zanzibar ni 400 kupitia wakala wake aiyeko Dubai kampuni ya Philatex. Mapato yatokanayo huingia SMZ na JMT haipati chochote isipokuwa jukumu la kulipa ada kwa chombo huru na chenye mamlaka kamili cha SMZ
Mwezi June meli zilizosajiliwa na Zanzibar zilikiuka vikwazo vya UN kwa kusafirisha mizigo ya Iran na kuiweka JMT katika wakati mgumu ikiwa ni pamoja na kuwekewa vikwazo vya uchumi.
Wiki hii meli yenye tani 30 zenye thamani ya bilioni milioni 125 zikiwa zimesajiliwa na ZMA chombo cha SMZ imekamatwa huko Italia. Hiyo ni sehemu tu ya meli mbovu ambazo zimesajiliwa. Umoja wa Ulaya (EU) umeiweka Tanzania katika nchi zenye vyombo hatari vya majini na vinavyohitaji ukaguzi.(Siyo SMZ ni JMT).
Ikumbukwe SMZ ilishajitoa kuhusu masuala ya usafiri wa majini tangu mwaka 2006 na kuwa na mamlaka kamili
Jana waziri wa mawasiliano na miundo mbinu wa SMZ Rashid Seif suleiman amevilaumu vyombo vya habari vya Tanzania BARA kuhusu kuandika habari hizo. http://www.habarileo.co.tz/index.ph...meli-zilizosajili-zanzibar-zaichafua-tanzania na http://www.dailynews.co.tz/index.php/local-news/22134-katiba-still-a-thorny-issue
Waziri wa SMZ haoni tatizo la kusafirisha mzigo wa bangi lilivyoichafua JMT ambayo Zanzibar ilishajitoa katika sheria na kuanzisha ZMA ila anaona tatizo habari hizo kuandikwa
Waziri Mwakyembe wa JMT ameingilia kati kufuatilia kadhia hiyo kwasababu Tanzania ndiyo yenye bendera na usajili wa IMO (Siyo meli) inakabliwa na kibano cha kimataifa kama ilivyokuwa kwa meli za Iran.
Gharama za ZMA kule IMO zinalipwa na JMT na waziri anatumia muda na gharama za JMT kuzuia uharibifu wa meli yenye mzigo wa Bangi ya SMZ.
Waziri huyo wa miundo mbinu wa SMZ alikaririwa na gazeti jana akisema faini inayotokana na kukiuka mkataba kati ya wenye meli na SMZ ambayo ni dollar 500,000 italipwa kwa SMZ(Siyo JMT)
Nilidhani waziri wa SMZ alitakiwa aeleze nini kimetokea hadi mzigo wa bangi tani 30 ukamatwe kwa jina la nchi ya Tanzania (Siyo Zanzibar)huku tukifahamu mapato yatokanyo na shughuli za meli hizo ikiwa ni pamoja na faini tarajiwa ni ya SMZ.
Ninajiuliza:
1. Kama Zanzibar ilishajitoa na kuanzisha ZMA kwanini meli zake hazisajiliwi na SMZ tukijua wana bendera yao
2. Kwanini kodi ya JMT ambayo ni ya Mtanganyika itumike kuhudumia shughuli za SMZ
3.Kwanini waziri Mwakyembe ashughulikie suala hili ambalo si la muungano
4. Je waziri Mh Suleiman wa SMZ anajua madhara yatakayomkumba Mtanganyika kutokana na biashara ya SMZ ambayo haimhusu kwa namna yoyote?
5. Kuna tatizo gani vyombo vya habari kuandika kuhusu kakamatwa kwa mzigo wa biashara wa meli zilizosajiliwa na ZMA ambacho ni chombo halali cha SMZ? Vyombo vya habari vimekosea nini na wapi?
Hebu tuellimishane kwa pamoja wanajamvi wote
JokaKuu GHIBUU Nonda Mzee Mwanakjiji Mchambuzi Jasusi EMT Ngongo platozoom Barubaru Zitto Mnyika Ritz chama Mkirua Zinedine AshaDii gfsonwin The Bigshow Kimweri Fundi Mchundo Bongolander Bu'yaka
Ahsanteni
ZMA haijaandikishwa na shirika la International Maritime organization(IMO) isipokuwa kupitia Jamhuri ya muungano wa Tanzania(JMT) ambayo inalipa ada za usajili. JMT haipati mapato kutoka ZMA au biashara zinazotokana.
Meli ilizosajili Zanzibar ni 400 kupitia wakala wake aiyeko Dubai kampuni ya Philatex. Mapato yatokanayo huingia SMZ na JMT haipati chochote isipokuwa jukumu la kulipa ada kwa chombo huru na chenye mamlaka kamili cha SMZ
Mwezi June meli zilizosajiliwa na Zanzibar zilikiuka vikwazo vya UN kwa kusafirisha mizigo ya Iran na kuiweka JMT katika wakati mgumu ikiwa ni pamoja na kuwekewa vikwazo vya uchumi.
Wiki hii meli yenye tani 30 zenye thamani ya bilioni milioni 125 zikiwa zimesajiliwa na ZMA chombo cha SMZ imekamatwa huko Italia. Hiyo ni sehemu tu ya meli mbovu ambazo zimesajiliwa. Umoja wa Ulaya (EU) umeiweka Tanzania katika nchi zenye vyombo hatari vya majini na vinavyohitaji ukaguzi.(Siyo SMZ ni JMT).
Ikumbukwe SMZ ilishajitoa kuhusu masuala ya usafiri wa majini tangu mwaka 2006 na kuwa na mamlaka kamili
Jana waziri wa mawasiliano na miundo mbinu wa SMZ Rashid Seif suleiman amevilaumu vyombo vya habari vya Tanzania BARA kuhusu kuandika habari hizo. http://www.habarileo.co.tz/index.ph...meli-zilizosajili-zanzibar-zaichafua-tanzania na http://www.dailynews.co.tz/index.php/local-news/22134-katiba-still-a-thorny-issue
Waziri wa SMZ haoni tatizo la kusafirisha mzigo wa bangi lilivyoichafua JMT ambayo Zanzibar ilishajitoa katika sheria na kuanzisha ZMA ila anaona tatizo habari hizo kuandikwa
Waziri Mwakyembe wa JMT ameingilia kati kufuatilia kadhia hiyo kwasababu Tanzania ndiyo yenye bendera na usajili wa IMO (Siyo meli) inakabliwa na kibano cha kimataifa kama ilivyokuwa kwa meli za Iran.
Gharama za ZMA kule IMO zinalipwa na JMT na waziri anatumia muda na gharama za JMT kuzuia uharibifu wa meli yenye mzigo wa Bangi ya SMZ.
Waziri huyo wa miundo mbinu wa SMZ alikaririwa na gazeti jana akisema faini inayotokana na kukiuka mkataba kati ya wenye meli na SMZ ambayo ni dollar 500,000 italipwa kwa SMZ(Siyo JMT)
Nilidhani waziri wa SMZ alitakiwa aeleze nini kimetokea hadi mzigo wa bangi tani 30 ukamatwe kwa jina la nchi ya Tanzania (Siyo Zanzibar)huku tukifahamu mapato yatokanyo na shughuli za meli hizo ikiwa ni pamoja na faini tarajiwa ni ya SMZ.
Ninajiuliza:
1. Kama Zanzibar ilishajitoa na kuanzisha ZMA kwanini meli zake hazisajiliwi na SMZ tukijua wana bendera yao
2. Kwanini kodi ya JMT ambayo ni ya Mtanganyika itumike kuhudumia shughuli za SMZ
3.Kwanini waziri Mwakyembe ashughulikie suala hili ambalo si la muungano
4. Je waziri Mh Suleiman wa SMZ anajua madhara yatakayomkumba Mtanganyika kutokana na biashara ya SMZ ambayo haimhusu kwa namna yoyote?
5. Kuna tatizo gani vyombo vya habari kuandika kuhusu kakamatwa kwa mzigo wa biashara wa meli zilizosajiliwa na ZMA ambacho ni chombo halali cha SMZ? Vyombo vya habari vimekosea nini na wapi?
Hebu tuellimishane kwa pamoja wanajamvi wote
JokaKuu GHIBUU Nonda Mzee Mwanakjiji Mchambuzi Jasusi EMT Ngongo platozoom Barubaru Zitto Mnyika Ritz chama Mkirua Zinedine AshaDii gfsonwin The Bigshow Kimweri Fundi Mchundo Bongolander Bu'yaka
Ahsanteni
Last edited by a moderator: