zanzibar ilijitoa katika sheria za jamhuri ya muungano ya usafiri wa majini ya mwaka 2003 na kuunda sheria yake ya bahari na usafiri ya mwaka 2006 na kuanzisha chombo chao, zanzibar maritime authority((zma) 2006.
Zma haijaandikishwa na shirika la international maritime organization(imo) isipokuwa kupitia jamhuri ya muungano wa tanzania(jmt) ambayo inalipa ada za usajili. Jmt haipati mapato kutoka zma au biashara zinazotokana.
Meli ilizosajili zanzibar ni 400 kupitia wakala wake aiyeko dubai kampuni ya philatex. Mapato yatokanayo huingia smz na jmt haipati chochote isipokuwa jukumu la kulipa ada kwa chombo huru na chenye mamlaka kamili cha smz
mwezi june meli zilizosajiliwa na zanzibar zilikiuka vikwazo vya un kwa kusafirisha mizigo ya iran na kuiweka jmt katika wakati mgumu ikiwa ni pamoja na kuwekewa vikwazo vya uchumi.
iran haijawekewa vikwazo na un kusafirisha mafuta yake, imewekewa vikwazo vya kuhusu technologia ya neuclea . Ni marekani na washirika wake ndio walio weka vikwazo vya mafuta, lakini china india turkey na wengineo wana nunua mafuta kutoka iran. Sisi kwa vile ni omba omba basi tunawaogopa wafadhiliwetu hivyo kukubali shindikizo lao kufutia leseni meli hizo
wiki hii meli yenye tani 30 zenye thamani ya bilioni milioni 125 zikiwa zimesajiliwa na zma chombo cha smz imekamatwa huko italia. Hiyo ni sehemu tu ya meli mbovu ambazo zimesajiliwa. Umoja wa ulaya (eu) umeiweka tanzania katika nchi zenye vyombo hatari vya majini na vinavyohitaji ukaguzi.(siyo smz ni jmt).
dubai ndiko kuna agent ambaye anafanya ukaguzi na usajili wa meli zote za tanzania/zanzibar. Dubai ni sehemu ambayo ina viwango vya kimataifa na meli hiyo ni kiwango.
Kupakia kwa bangi au gongo si tatizo la meli..au walo sajili meli..bali ni tatizo la bandari husika ya nchi ilipo toka na kupakia meli hiyo. Huo mzigo si wa wenye meli na wao hawahusiki. Juzi agnes mwasongo nani sijui yule mrembo mwenye wowo kubwa alikamatwa akiwa south afrika airpprt na alipanda ndege ya south afrika na kama umewahi kusafiri sio kazi ya kaptain kusachi mizigo iliomo humo
ndio maana kuna kampuni kama swiss port na airport authority wanao cheki mizigo
na meli ni hivo hio...kaptai wa meli hatazami kila container linalo pakiwa hio ni kazi ya bandari na polisi wa nchi ile inapo pakiwa mzigo...
ikumbukwe smz ilishajitoa kuhusu masuala ya usafiri wa majini tangu mwaka 2006 na kuwa na mamlaka kamili
jana waziri wa mawasiliano na miundo mbinu wa smz rashid seif suleiman amevilaumu vyombo vya habari vya tanzania bara kuhusu kuandika habari hizo.
http://www.habarileo.co.tz/index.ph...meli-zilizosajili-zanzibar-zaichafua-tanzania na
http://www.dailynews.co.tz/index.php/local-news/22134-katiba-still-a-thorny-issue
waziri wa smz haoni tatizo la kusafirisha mzigo wa bangi lilivyoichafua jmt ambayo zanzibar ilishajitoa katika sheria na kuanzisha zma ila anaona tatizo habari hizo kuandikwa
vyombo vya habari vinafanya kazi ya wivu inapo tokea kitu kutoka zanzibar..huwa havipendi kuona zanzibar ina mipango ya kuongeza mapato..hivo wali ripoti kwa wivu, uchoyo na husda..ndio maana waziri akasema hivyo.
Kupakiwa bangi kwenye meli si tatizo la usajili wa meli ..ni sawa na mbwana matumla na kaniki walokamatwa wakitapanda ndege ya eithopia wakitokea burundi ..jeee ile ndege iliyo wachukua kutoka burundi na unga wao nayo ina matatizo ?//
waziri mwakyembe wa jmt ameingilia kati kufuatilia kadhia hiyo kwasababu tanzania ndiyo yenye bendera na usajili wa imo (siyo meli) inakabliwa na kibano cha kimataifa kama ilivyokuwa kwa meli za iran.
Gharama za zma kule imo zinalipwa na jmt na waziri anatumia muda na gharama za jmt kuzuia uharibifu wa meli yenye mzigo wa bangi ya smz.
bendera ni muungano na zanzibar ni muungano hio ni yetu wote siyo kwa matumizi ya tanganyika pekee yake
waziri huyo wa miundo mbinu wa smz alikaririwa na gazeti jana akisema faini inayotokana na kukiuka mkataba kati ya wenye meli na smz ambayo ni dollar 500,000 italipwa kwa smz(siyo jmt)
nilidhani waziri wa smz alitakiwa aeleze nini kimetokea hadi mzigo wa bangi tani 30 ukamatwe kwa jina la nchi ya tanzania (siyo zanzibar)huku tukifahamu mapato yatokanyo na shughuli za meli hizo ikiwa ni pamoja na faini tarajiwa ni ya smz.
hiyi ni biashara ya zanzibar ndani ya muungano...hayakuhusu
ninajiuliza:
1. Kama zanzibar ilishajitoa na kuanzisha zma kwanini meli zake hazisajiliwi na smz tukijua wana bendera yao
bendera ya tanzania ni ya pamoja sio ya tanganyika pekee. Ikiwa znz wanahitajio la kuitumia watatumia.. Na kama tanganyika inaposaini mikataba kwa niaba ya tanganyika kuweka bendera hio..
2. Kwanini kodi ya jmt ambayo ni ya mtanganyika itumike kuhudumia shughuli za smz
kodi gani ya mtanganyika ? Mtanganyika ndie anakula kodi ya zanzibar, visa, airport charges, simu , posta, vat, custom duty, zote za upande wa zanzibar wanazila tanganyika
3.kwanini waziri mwakyembe ashughulikie suala hili ambalo si la muungano
sio lazima kweli akae e kimya , hapo sawa...kuna wauza unga wengi tanganyika awashughulikie
4. Je waziri mh suleiman wa smz anajua madhara yatakayomkumba mtanganyika kutokana na biashara ya smz ambayo haimhusu kwa namna yoyote?
ndio faida ya muungano...kustahamiliana ..kama hutaki vunjeni..kwa ni na anaushikilia uwepo
5. Kuna tatizo gani vyombo vya habari kuandika kuhusu kakamatwa kwa mzigo wa biashara wa meli zilizosajiliwa na zma ambacho ni chombo halali cha smz? Vyombo vya habari vimekosea nini na wapi?
hakuna tatizo ila ubaya upo unapo potosha na ama unapokua na chuki..na sehemu ambayo umeungana nayo hapo ndio kuna tatizo
hebu tuellimishane kwa pamoja wanajamvi wote
jokakuu ghibuu nonda mzee mwanakjiji mchambuzi jasusi emt ngongo platozoom barubaru zitto mnyika ritz chama mkirua zinedine ashadii gfsonwin the bigshow kimweri fundi mchundo bongolander
ahsanteni