Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

ni kweli kabisa mkuu. ni hatari kwa mwalimu kama huyu kuwafundisha watoto wa form 1 maana watakariri makosa haya na kwenda nayo hadi chuo kikuu. ndio maana kuna baadhi wasomi wa chuo kikuu humu wanaotetea uchapiaji wa kikanyaboya kama huu ama kwa kujua au kutokujua. ikifikia msomi wa chuo kikuu anafanya obvious BLUNDER kama hii halafu anatetewa na wasomi wenzake ujue kwamba kuna tatizo kubwa katika elimu yetu kwa ujumla.

nilikuuliza swali kuhusu hiki kiingereza ulichotumia hapa.... naona umechumpa ..na unachagua ya kujibu sio... au na haya ya "kufanya OBVIOUS BLUNDER" uliyasikia kwa mwalimu wa shule ya kata... BADO NAHITAJI MAJIBU NDUGU... MAANA HIYO SENTENSI HAPOOO.. USINIKWEPE JAMAA
 
English sio tatizo sio mother language yetu ni lugha ya kufundishia tuu.si busara kuzarau chuo eti kisa aliesoma hapo kakosea lugha. Nchi hii inahitaji nguvu kazi zetu na tuondoe uvivu wa kufikiri ili maendeleo yapatikane na si kwa hili mkuu haujajenga hapo umebomoa. Tuwahurumie walimu na kero zao still wanafundisha.tusiwabeze walimu aisee.
 
nilikuuliza swali kuhusu hiki kiingereza ulichotumia hapa.... naona umechumpa ..na unachagua ya kujibu sio... au na haya ya "kufanya OBVIOUS BLUNDER" uliyasikia kwa mwalimu wa shule ya kata... BADO NAHITAJI MAJIBU NDUGU... MAANA HIYO SENTENSI HAPOOO.. USINIKWEPE JAMAA

kwani wewe unaona nimekosea wapi? nisahihishe basi. hayo maneno "OBVIOUS BLUNDER" sijayasikia kwa mwalimu bali ni maneno yangu niliyoyatumia katika moja ya majibu yangu wakati natetea hoja hii. kwani na yenyewe unaona hayakaa sawa kisarufi au vipi mkuu? je, unataka nikueleweshi nini kuhusiana na maneno haya?
 
Ujinga kwa Mwaafrika ni ndani ya genes.

Hauna dawa.

huu ni uwongo wa hali ya juu
ww sema baadhi ya waafrika kwasababu sio wote.
Hakuna ujinga ambao hauna dawa nakaata hiyo.dawa ya ujinga wowote ni elimu.
 
kwani wewe unaona nimekosea wapi? nisahihishe basi. hayo maneno "OBVIOUS BLUNDER" sijayasikia kwa mwalimu bali ni maneno yangu niliyoyatumia katika moja ya majibu yangu wakati natetea hoja hii. kwani na yenyewe unaona hayakaa sawa kisarufi au vipi mkuu? je, unataka nikueleweshi nini kuhusiana na maneno haya?

isome hiyo sentensi yako mara mbilimbili..then jaribu kuuliza watu wawili watatu then naomba kesho uje unipe majibu kama hiyo sentensi iko sawa...
i can assure you..bora hata huyo mwalimu uliyemuanzishia thread ya kejeli humu..
TUNATOA BORITI KWA WENZETU...
 

Attachments

  • 1429824727620.jpg
    1429824727620.jpg
    72.7 KB · Views: 150
Hivi ni kweli haya ni MAAJABU???

Hata mimi nashangaa! Basi kuna maajabu mengi sana duniani. Cha msingi sentensi ilieleweka ana maanisha nini, hta waingereza wenyewe wanakosea structure sembuse mtanzania!!
 
Wakifundisha kiswahili wanaonekana kama wanaongea kichina, kiingereza ndio kabisa, mi naona saivi tuanze kutumia kila sehemu na kilugha chake labda haya ya maajabu ya mleta mada yatakwisha. Kuna vitu vya kushangaa na kuwa maajabu sio hiki. mleta mada HUNA AKILI. Unaacha kushangaa kwanini Serikali ya SISIHEMU imeleta ugumu wa maisha we unashangaa yasiyokuhusu. SHENZI KABISA.
 
Leo nimetembelea shule moja ya Kata nikashuhudia kituko cha mwaka kutoka kwa mwalimu mmoja shuleni hapo.

Mwalimu huyo amehitimu Chuo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) hivi karibuni na akaajiriwa moja kwa moja kufundisha katika shule hiyo ya Kata. Wakati akiendelea kufundisha nilimsikia akiwauliza wanafunzi swali hili: WHERE DOES IT LOCATED? Inaonekana ni mwalimu wa somo la Jiographia, hivyo alikuwa akiwauliza wanafunzi wake wamtajie location ya kitu fulani kwenye ramani.

Jamani, hapa ndipo shule za kata zilipotufikisha. Ikiwa mhitimu wa Chuo Kikuu anaongea kiingereza kibovu kama hiki, tena mbele ya wanafunzi,mnategemea wanafunzi anaowafundisha watapata maarifa gani kutoka kwake? Chukulia huyu ni mwalimu wa Kidato Cha Kwanza, wanafunzi wake wanaoambiwa kila siku "SPEAK ENGLISH" wataiga kiingereza gani kutoka kwake? Si ndio atawapoteza kabisa?

Ikiwa walimu hawajui kiingereza unategemea nini kutoka kwa wanafunzi wao? Haya ndio madhara ya serikali yetu kuchanganya elimu na siasa. Tumekwisha hasa!!

:israel:

Upuuzi mtupu, kwani yeye alikuwa anasoma kingereza UDSM? Hata hicho kiswahili chenyewe huwa tunakosea...! grammar ni tatizo dogo katika lugha, hasa kwa lugha ngeni. Acha porojo....! Wewe ukikutana na native english speaker utaonekana unaongea utoko pia. Just different level of fluency (usinikosoe na mimi, mwenzio nimejitahidi hapo).
 
Leo nimetembelea shule moja ya Kata nikashuhudia kituko cha mwaka kutoka kwa mwalimu mmoja shuleni hapo.

Mwalimu huyo amehitimu Chuo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) hivi karibuni na akaajiriwa moja kwa moja kufundisha katika shule hiyo ya Kata. Wakati akiendelea kufundisha nilimsikia akiwauliza wanafunzi swali hili: WHERE DOES IT LOCATED? Inaonekana ni mwalimu wa somo la Jiographia, hivyo alikuwa akiwauliza wanafunzi wake wamtajie location ya kitu fulani kwenye ramani.

Jamani, hapa ndipo shule za kata zilipotufikisha. Ikiwa mhitimu wa Chuo Kikuu anaongea kiingereza kibovu kama hiki, tena mbele ya wanafunzi,mnategemea wanafunzi anaowafundisha watapata maarifa gani kutoka kwake? Chukulia huyu ni mwalimu wa Kidato Cha Kwanza, wanafunzi wake wanaoambiwa kila siku "SPEAK ENGLISH" wataiga kiingereza gani kutoka kwake? Si ndio atawapoteza kabisa?

Ikiwa walimu hawajui kiingereza unategemea nini kutoka kwa wanafunzi wao? Haya ndio madhara ya serikali yetu kuchanganya elimu na siasa. Tumekwisha hasa!!

:israel:

Sijawahi ona uzi dhaifu kama huu tangu nijiunge JF zaidi ya miaka 6 iliyopita, hivi uwezo wa kutafakari mambo umekuwa chini kiasi hiki? yani mtu kukosea sentensi fupi kama hiyo inakuwa mada? How could you draw conclusion about UDSM graduates kwa hiyo small grammatical error? Hapo mtu kakosea lugha ngeni, je akikosea kiswahili si itakuwa breaking news? Hili nalo janga
 
nilikuuliza swali kuhusu hiki kiingereza ulichotumia hapa.... naona umechumpa ..na unachagua ya kujibu sio... au na haya ya "kufanya OBVIOUS BLUNDER" uliyasikia kwa mwalimu wa shule ya kata... BADO NAHITAJI MAJIBU NDUGU... MAANA HIYO SENTENSI HAPOOO.. USINIKWEPE JAMAA

Na kama angekua mzalendo wa kweli nilitegemea angethubutu hata kumuita huyo mwalimu na kumwambia pale pale ili hasiendelee kulisha hilo "zao" hicho inachoita blunder. Matokeo yake amekuja kukurupukia humu. Amethubutu mpaka kunena yakua "Nyerere" ndiye aliyeanza kuvuruga mfumo wa elimu hapa Tanzania. Sijui hapo hawali kabla tulikua vizuri vipi.?
 
Kawaida ya watanzania ni kushughulika na matawi na majani mnaacha kushughulikia chanzo ulemavu wa mtu kama huyo una historia ya kimchakato mfumo mzima wa elimu na sera na mipango umetoa mazao kama yanayosemwa juu ya huyo mwalimu mbofoaji ukianza kulishughulikia tatizo lake utarudi mpaka pale kozi za crush (kuparaza) programs zilipoanza zilizotoa waalimu walioitwa wa UPE(Ualimu Pasipo Elimu)alafu utapelekwa kwenye sera ya elimu na mtaala mbovu wa elimu alafu vitabu holela ambavyo ithibati yake ni ya kuparaza tu usitegemee kupata elimu yenye elimu kama mifumo yako ni ya kuparaza tu.ukiona hayo yanatokea hakuibuka over a night ni process ndivyo tulivyofika hapa.
 
Back
Top Bottom