Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Kuwa mwalimu haimaanishi kuwa hutofanya mistake wakati wa kuelezea kitu, walimu wa Uganda wenyewe wameaibika kwa kufeli kwa kiasi kikubwa mtihani waliopewa na baraza la mitihani la nchi hiyo.
 
We ni mzee wa matukio Jana majambazi leo umeibukia Shule za kata
 
Wachina na wajerumani wenye maendeleo makubwa wanajua Kiingereza ?, pili ushasema ni mwl. wa Geography si kosa lake Tatu ww kwa siku Kiswahili lugha yako unachapia mara ngapi ? Nne ; watoto wenu mlokuwa mnawepeleka Kusoma Uganda na Kenya miaka michache ilopita mbona hamuwapeleki baada ya kuona watoto wanaendelea kuwa vilaza Tano Rekebisha ulitaka Mwl. aseme vp.

Bayebe;
Ka mimi ni weye nisingali tetea uozo huu. Tatizo si shule za kata, ni za muhimu kuliko chochote ila, ka zingesubirisha kwa miaka 4 tu, na miaka hiyo ikawa kuwaanda waalim, shule za kata zingelikuwa za kuigwa mfano.
Tulikurupuka, tukubali tusikubali, tulikurupuka. Shule zimeanzishwa hakuna man power ulitegemea nini?? Waalim wawili shule nzima, au waalimu 4 wote arts, juzi kati ndo wameanzisha waalim wa voda fasta kufundisha Science! Gosh!
hao waliopita hapo kati bila waalim wa Science tuseme watarudishwa shuleni au??
Mambo yetu ni kukurupuka, tukidhani watatuelewa huko huko mbele kwa mbele. Nasema Sii hivyo. Nioneshe BRN ya elimu
 
cha kufanya ni kuufumua mfumo mzima wa utawala na kuweka utawala mpya ifikapo Oktoba kwa kuwa wao ndio waliotufikisha hapa. wamedunisha elimu yetu kwa makusudi kwa kuwa watoto wao wanasoma ulaya na marekani wakati watoto wa wakulima wanarudikwa kama ng'ombe kwenye shule za kata zinazotoa elimu duni kwa watoto wetu. jiandikisheni kwa wingi na mjitokeze kupiga kura ili tuufutilie mbali utawala huu wa kishetani kutoka ardhi ya Tanzania.

Mkuu you need enough "time" to rethink and reposition yourself. Naishia hapa, na ubarikiwe kwa hoja zako.
 
Tumetoka mbali hata hivyo, mpaka kufikia miaka 50 ya Uhuru na muungano. Si eti Dada faizafox
 

Attachments

  • 1429814665395.jpg
    1429814665395.jpg
    27.9 KB · Views: 208
Last edited by a moderator:
kwanza kabisa Kiingereza sio lugha yetu Mama, pili mwalimu kutojua lugha vizuri sio kwamba hajui kufundisha, tatu kiingereza sio majibu kwamba ukiandika au kukijua vizuri (fluent) ndo umemaliza kila kitu, mie nimeshuhudi mwalimu mmoja kutoka congo alikuwa anafundisha geography na mathematics ikiwa hajui kiswahili wala kiingereza yeye ni french tu..pia nmeshuhudia mwalimu mchina anafundisha physics na math ikiwa yeye hajui kiswahili wala kiingereza ila wanafunzi wanaelewa vizuri.....over
 
Niliwahi kumsikia mwingine akifundisha F2 geography akasema hivi: the earth rotate in its own axis. It go, it go, it stops. Wakati anasema hivyo na yeye anajizungusha.

Hahahahahahahahaha! For true, it is job!
 
Nachukia mim. Cjui tatizo ni hiki kizazi cha wabishi? Kwa nn inakuwa ni ngumu mtz kukubali kosa ambalo laonekana wazi? HIVI, NI KWELI NINYI NI WALIMU WENY HADHI YA CHUO KIKUU, ndo mnatetea huu uozo ambao mtoa mada ameukosoa??? Hamuoni kuwa hilo ni janga kuu kuelekea kweny ushindani wa soko la ajira na EAC??? Au hivyo vyeti vyenu ni natokeo ya kulala na mwalimu ili upewe majibu??? KAMA TUNAKWENDA NWENDO HUO, BASI TWAENDA KINYUME NYUME TUKIDHANI TWASONGA MBELE. Tusubiri kuwa watumwa tena kama longi!
 
Tumetoka mbali hata hivyo, mpaka kufikia miaka 50 ya Uhuru na muungano. Si eti Dada faizafox[/QUOTE
Ndio sawa na kifundisha Divinity halafu unawauliza wanafunzi "Who betrayed Yesu?"
 
Last edited by a moderator:
ni hatari kama mtu mzima unajipinda kuandika uzi kama huu huku ukiamini anaeongea kiingereza vizuri ndie msomi shame on you
 
Watanzania tunaongea saaaana na tunajua saaana kukosoa na kulaumu. Unaposema waafrika wajinga umechukua hatua gani kuufuta ujinga kama wewe ni mwerevu? Unafikiri lugha ni ujuzi? Jifunze kwa Wajapani Wachina na Wakorea hata Warusi....
Tafakari Chukua Hatua.
nge nge
hakielimu
 
Nachukia mim. Cjui tatizo ni hiki kizazi cha wabishi? Kwa nn inakuwa ni ngumu mtz kukubali kosa ambalo laonekana wazi? HIVI, NI KWELI NINYI NI WALIMU WENY HADHI YA CHUO KIKUU, ndo mnatetea huu uozo ambao mtoa mada ameukosoa??? Hamuoni kuwa hilo ni janga kuu kuelekea kweny ushindani wa soko la ajira na EAC??? Au hivyo vyeti vyenu ni natokeo ya kulala na mwalimu ili upewe majibu??? KAMA TUNAKWENDA NWENDO HUO, BASI TWAENDA KINYUME NYUME TUKIDHANI TWASONGA MBELE. Tusubiri kuwa watumwa tena kama longi!

Unasubiri Kuwa Mtumwa Wakati Tayari Ni Mtumwa Wa Mwingereza. Kiingereza Si Elimu, Ni Lugha. Hivi kiingereza unachokiona wewe kuwa ndo elimu hujui kuwa kilikuwa na wazungumzaji wachache kama kisukuma kabla ya 1800's? unataka kunambia ulimwengu haukuelimika kwa kutojua kiingereza? kipindi cha Roman Empire, Kilatin kilikuwa lugha inayofahamika zaid duniani, leo kiko wapi? kuna sababu nyingi za kupotea kwa lugha, je kiingereza kikipotea dunia itakuwa mazuzu kwa kukikosa? Think Big.
 
....hoja yako imetugusa wengi...tunahisi umemtumia huyo mwalimu kutusema siye. So vumilia haya mashambulizi
 
we unafiki uache, kila tukio unalishuhudia wewe, mara magaidi mara kareti embu kwenda zako huko
 
ni hatari kama mtu mzima unajipinda kuandika uzi kama huu huku ukiamini anaeongea kiingereza vizuri ndie msomi shame on you

elewa kinachoongelewa hapa kwanza. usikurupuke kama kuku (mtetea) anayetafuta kiota cha kutagia. mwalimu ni kioo cha mwanafunzi: ikiwa walimu wataachiwa wawafundishe watoto wetu kingereza kanyaboya hujui kuwa wataakisi makosa hayo na kuyaendeleza kizazi na kizazi? hii ni kama seli ya kansa ambayo huanza kama seli moja na hatimaye kujigawanya na kutapakaa mwili mzima. mfumo wa elimu yetu unachezewa na wanasiasa uchwara. wakati wa kuchukua hatua kurekebisha haya makosa ni sasa. usisubiri mpaka watoto wetu waharibiwe kielimu ndipo uingie barabarani kudai elimu bora kwa walalahoi. chukua hatua sasa kabla mambo hayajaharibika zaidi.
 
Back
Top Bottom