Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Wachina wasio jua kiingereza wako competent kwwnte careers zao. Wachina wanao jifunza kiingereza basi wanaongea fluently.. wanao jifunza kifaransa fluently even kiswahili wakijifunza wanaongea kama wamatumbi. Elimu ya bongo mangu mangu tuu
Mkuu umewahi soma kichina?
Approach yao ya kufundisha lugha ni vitu tofauti na sisi.
Wachina wanajua kufundisha aisee.
Ukikaa nao miezi 6 utajua kichina tu.
Wako practical oriented hawakaririshi.
Sisi tunakaririsha tense, grammer nk.
 
Leo nimetembelea shule moja ya Kata nikashuhudia kituko cha mwaka kutoka kwa mwalimu mmoja shuleni hapo.

Mwalimu huyo amehitimu Chuo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) hivi karibuni na akaajiriwa moja kwa moja kufundisha katika shule hiyo ya Kata.

Wakati akiendelea kufundisha nilimsikia akiwauliza wanafunzi swali hili: WHERE DOES IT LOCATED?

Inaonekana ni mwalimu wa somo la Jiographia, hivyo alikuwa akiwauliza wanafunzi wake wamtajie location ya kitu fulani kwenye ramani.

Jamani, hapa ndipo shule za kata zilipotufikisha. Ikiwa mhitimu wa Chuo Kikuu anaongea kiingereza kibovu kama hiki, tena mbele ya wanafunzi,mnategemea wanafunzi anaowafundisha watapata maarifa gani kutoka kwake?

Chukulia huyu ni mwalimu wa Kidato Cha Kwanza, wanafunzi wake wanaoambiwa kila siku "SPEAK ENGLISH" wataiga kiingereza gani kutoka kwake? Si ndio atawapoteza kabisa?

Ikiwa walimu hawajui kiingereza unategemea nini kutoka kwa wanafunzi wao? Haya ndio madhara ya serikali yetu kuchanganya elimu na siasa. Tumekwisha hasa!!
Ndilo tatizo la kuajiri bila usahili🤣🤣🤣🪑
 
Hii lugha imeshatushinda kabisa. Mi kuna mwalim nilimsikia anasema 'You there stand up' akiwaamuru wanafunzi flani waliokuwa wanachanja mbio kutoroka shule
 
Kama wewe ni mwanaume uweke huu Uzi wako Kwa kiingereza!! Otherwise huna jipya
 
Tena Nina uhakika katika watumishi wa serikali wenye angalau kuelewa kiingereza ni walimu wa sekondari!! Njoo huku jeshini uone,njoo wizara ya kilimo ,afya ,mifugo uone
 
Mkuu umewahi soma kichina?
Approach yao ya kufundisha lugha ni vitu tofauti na sisi.
Wachina wanajua kufundisha aisee.
Ukikaa nao miezi 6 utajua kichina tu.
Wako practical oriented hawakaririshi.
Sisi tunakaririsha tense, grammer nk.
Umeongea vizuri mimi nilijifunza kijapani rafiki yangu kichina ila kwa kumuuliza tuu amehifunza vitu gani nilijikuta naweza maneno mengi ya kichina
Shei she
 
Tena Nina uhakika katika watumishi wa serikali wenye angalau kuelewa kiingereza ni walimu wa sekondari!! Njoo huku jeshini uone,njoo wizara ya kilimo ,afya ,mifugo uone
Wanajua kingereza cha kuandika. Unatakiwa utambue kingereza kina nguzo kuu nne.
1. Speaking skill
2. writing skill
3. listerning skill
4. Reading skill
Sasa mtaala wa Tanzania umeshindwa ku intergrate those skills.
Mtaala unazingatia writing skill na hizo zingine ni bla bla walau reading skill.
Dk 40 za kipindi cha kingereza TZ umfundishe mwanf.
Kusoma., kuandika, kusikiliza na kuongea. Atambue sauti za maneno, muundo wa neno, kuliambisha, kupata maneno mengine.
Alijue neno ktk tenses, asome sentense, aunde sentense, aigize sentese, asikilize.
Asome habari na kutambua matumizi ya vocabilary na maana zake.
Ajue part of speech, ajue kwa ujumla grammer yote.
Aweze kusikiliza habari kisha aifupishe, aitafsiri aisimulie nk.
Vipindi ni 192 au 194 humo kuna sikukuu, ugonjwa, ukaguzi, michezo, wageni, seminar, incompetency, uvivu na mambo mengi yasioeleweka.
Isitoshe mtoto wa miaka 7 drs la 3 asome masomo 6 nayo yana mlolongo wa vitu kibao kama hapo juu.
Ni mwalimu gani wa kayumba anaweza kumuwezesha mwanafunzi wa TZ awe fluent speaker.
NECTA wanapima skills kizamani sana, yani ni wasomi wasioenda na wakati au wanahofia upimaji wa kisasa unatumia gharama kubwa nao hawana zana bora za upimaji.
Wizara nayo imeshindwa kutekeleza mahitaji wa msingi ya utekelezaji wa kisasa wa mtaala hasa lugha.
Tukirudi kwenye hoja yako, kimsingi hizo sekta zingine training yao ni tofauti na walimu. Mwalimu wa sekondari comm skill ni jambo linalotiliwa mkazo na anafanya presentation nying chuoni na TP. Anatumia hio lugha kufundishia.
Shida inakuja je msingi wa huyo mwalimu upoje ? Ukizingatia katoka kayumba s/m.
Wapo walio vizuri na wasio vizuri.
TZ hakuna pa kuiongelea lugha ya kingereza hasa kama sio mwalimu au mkufunzi wa chuo. Hivyo si rahisi kuiongea.
 
Back
Top Bottom