Siasa za mbeya ndo zilivyo, ukabila ndo msingi mkuu, hata hivyo mmesahau kuwa mtanzania ni gazeti la fisadi rostam, mnategemema liandike lolote zuri kuhusu mwandosya?
HUO NI MRADI WA MWAKIPESILE NA MULLA KULA FEDHA YA EPA
Steven wa BOT hawezi hata kushinda uchaguzi wa uenyekiti wa kijiji cha Mwakaleli! Wengi tunamfahamu hapa Mbeya, ni mdebwedo kama Tom Mwang'onda na hafahamiki kiasi hicho hata kama magazeti ya Rostam yataendelea kumwandika kila siku. Tatizo la Mkoa wa Mbeya ni ushamba na ulimbukeni wa watu wa Mbeya.
Watu wa Mbeya hawana aibu, wanatumiwa na watu walio nje ya mkoa kukomoana wao wenyewe! Ujinga huu huwezi kuuona Kilimanjaro au Mwanza, ni ujinga maalum wa watu wa Mbeya! Tom Mwang'onda alichochewa na akina Lowassa kumg'oa Mpesya, akaishia yeye mwenyewe kung'oka meno pamoja na baba yake kumalizia ushushushu wake wote na fedha ya EPA kwenye uchaguzi huo!
Tom Mwang'onda huyo huyo akachochewa na akina Rostam, Lowassa na Makamba kumg'oa Mwandosya kwenye NEC, akaishia tena kung'oka meno mengi zaidi pamoja na kusaidiwa na vyombo vya dola, Mkuu wa Mkoa, Wakuu wote wa Wilaya, Makamba, watendaji wote wa CCM na baba yake! Sasa, akina Rostam, Lowassa, Makamba na Kingunge wameona Tom hafai, atafutwe mtu mwingine wa kutumwa.
Kama kawaida yake, korokoroni wao Mbeya - Mwakipesile, akamtafuta Steven na anamwandaa ati kupambana na Mwandosya! Mwakipesile si mjinga, anajua kuwa Steven hawezi! Lakini anajua kuwa huo ni mradi wa kula fedha ya EPA! Steven ni mradi wa Mwakipesile na Mulla kutafuna vizuri fedha ya EPA aliyonayo Rostam. Hata mimi nimekaa mkao wa kula kumshabikia Steven ili nipate mgao wangu wa EPA! Hii Bongoland bwana!
Mimi nina taarifa kuwa hata Dk. Mwakyembe katafutiwa mtu wa kupambana naye! Mtu mwenyewe ni dereva wa malori anaitwa Elias Mwanjala! Huo ni mradi mwingine wa Mwakipesile wa kula hela ya EPA. Wabunge wengine machachari Zambi, Dk. Siame na Victor Mwambalaswa ati nao wametafutiwa wagombea.
YOTE HII NI MIRADI YA KINA MWAKIPESILE NA JANGILI MULLA KULA FEDHA YA EPA!
HUO NI MRADI WA MWAKIPESILE NA MULLA KULA FEDHA YA EPA
Watu wa Mbeya hawana aibu, wanatumiwa na watu walio nje ya mkoa kukomoana wao wenyewe! Ujinga huu huwezi kuuona Kilimanjaro au Mwanza, ni ujinga maalum wa watu wa Mbeya! Tom Mwang'onda alichochewa na akina Lowassa kumg'oa Mpesya, akaishia yeye mwenyewe kung'oka meno pamoja na baba yake kumalizia ushushushu wake wote na fedha ya EPA kwenye uchaguzi huo!
Na huko Rungwe mke wa Prof Mwakyusa anachukua magari ya afya pale hospitali ya wilaya kwa shughuri zake binafsi na watumishi wanamwachia tu, bila kumkatalia.Namtafuta sana kijana Mmanyi Malang'ombe ajitokeze kwa chama chochote cha upinzani amshe upya mkoa wetu kuziba ombwe la uongozi waliloliacha akina Elly Anangisye na Mwakitwange tukimwacha mnafiki wa Nyerere,Mzee Mwakangale.Kwa kweli watu wa Mbeya watabidi waamke waache ujinga wa kutumiwa, wafanye vitu vya maendeleo..Maendeleo hatatokani na majungu nakutupiana matope. Miaka mitatu ya Mh Mwakipesile mzaliwa wa mbeya imezaa nini? Acheni siasa fanyeni kazi.
Mhh Elias Mwanjala kwenye ubunge? mhh haya wee siasa inachezewa sasa naona! twendeni tu tutafika kama mambo yenyewe ndiyo hayo? Elias Mwanjala alitumiwa na Dk.Mwakyembe kwasababu ya pesa aliyonayo kushawishi wananchi wa kyela kumpigia kura Mwakyembe lakini kama ameona hiyo ni nafasi tosha inayomfanya kujidai anauwezo wa kumuondoa Dk.Mwakyembe pale tusubiri tuone! yetu macho na masikio!!
hivi wala ndizi wenzetu......mbeya na ujanja wote huo hawana website!!
Mkuu Ogah,
Nikisema unatutukana nitakuwa nimekosea? Kwi kwi kwi!!!
Taarifa nilizonazo ni kwamba DED yule mwanamke ndiye aliyekuwa mratibu wa mradi huo.Bahati nzuri amehamishwa na nafasi yake imechukuliwa na Senyagwa kwa sasa hivi wacha tusubiri kusikia yanayofuatia.Kinyamana,
Ni kweli Bw. Mwanjala anajiandaa kuwa mgombea; nilipokuwa likizo mwaka jana nilikutana naye Kyela na katika mazungumzo aliniambia kwamba ana mpango huo ... na tayari malori yake huwa yanashusha bidhaa katika kata mbali mbali from time to time ... and you guessed it right, alikuwa anapewa msukumo na Lowassa pamoja na Mwakipesile ... sijui sasa hivi hali ikoje.
Swala la kugombea sio msukumom ni demokrasia inayoweza kuja kwa njia mbalimbali hivyo so far nakubaliana na mtu yeyote anaefanya maandalizi yake mapema.Taarifa nilizonazo ni kwamba DED yule mwanamke ndiye aliyekuwa mratibu wa mradi huo.Bahati nzuri amehamishwa na nafasi yake imechukuliwa na Senyagwa kwa sasa hivi wacha tusubiri kusikia yanayofuatia.
Taratibu mzee katika uringo wa demokrasia hakuna kutishana tumpe moyo kijana mwenzetu