kasyabone tall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2009
- 254
- 63
injinia japo bado ninaendelea na utafiti na mzee imbombongafu amesema anasubiri sasa inabini nifanye kazi kweli kweli japo ninakusanya data kwa njia ya interview sijafikia kwenye conlusion lakini nikapata wazo nafikiri ni la maana zaidi.Kaka Lole,
Mimi naweza kukusanya mtaa mzima kama hilo pambano litapangwa. Mtu lazima atolewe knock-out siku hiyo.
Hata mimi hawa wakubwa wamenichosha na hizi kelele zao kupitia magazetini. Wakipatanishwa wanashikana mikono, kesho yake wanaanza kugombana tena.
hapa wazee tukiangalia vita vyao athari kubwa ni kwa wanakyela. huyu mwakyembe akuchaguliwa na miti ni watu. na sisi vijana wa kyela tumekuwa wapole mno, na wengi wao hawashiriki hata kupiga kura. lakini tukiacha haya mambo yaendelee na tabia za mbunge zinaonekana zina matatizo. watakao kuja kuumia ni watoto wetu na wajukuu wetu. kwa kuwa viongozi wetu wote hakuna vijana. mimi ninashangaa kama darasa la pili anashika udiwani wakati injinia upo hapo. hapa kuna haja ya kutumia ujana wetu tuikamate kyela.
HIvi huyu mwakyembe mnamuogopa sana? kusubili mpaka uchaguzi ndio kumshughulikia mtu hii imetuumiza sana.( kumbuka enzi za mwakipesile). na uongo kwa hawa wabunge wetu imekuwa ni jadi wakiamini kuwa watu wa kyela hajui lolote.
sasa kuna umuhimu wa ku organize mkutano wa vijana wa kyela na huyu mbunge atueleze kwa kirefu nini kinafanyika. lakini pia asutwe kwa tabia zake mbaya. pia lazima tuwe na vipaumbele sisi kama vijana ili kila mbunge tumwambie tunataka ufanye hiki na kile.hapa tutakuwa tumewashika, la sivyo watakuwa wanatuchezea kama mpira wa kona. kama organisation itakwenda vizuri ni suala la kuwasiliana kwenda ofisini kwa mbunge(kama mnaogopa mimi nitawawakilisha) tumuandikie barua na kumwita. ni vizuri ikawa mwenzi wa kumi na mbili wakati vijana wengi wanakuwepo hapo. lakini ili tuwe na nguvu za kuwaendesha watu hawa ni lazima tujiandikishe kwa wingi na tukipiga kura basi kuwe na effect inayoonekana. hii inawezekana, pia kuongea na vijana ambao wanahitimu vyuo vikuu waje wagombee hata udiwani. hapa hakuna mchezo. vijana wajenge kyela yao kwa manufaa ya watoto na wajukuu wao. hapo injinia kama utaweza kuorganize maana wewe ndio upo hapo na unaweza kukutana na vijana wengi sana tuwasiliane. na wengine ambao mnaaunga mkono hili ebu tuweke network. hii ndio njia pekee ya kuwashughulikia watu hawa. tutamwambia aje, akigoma kuja huyo mbunge sisi tutaunganisha nguvu ya kumuondoa. hawezi kugoma. hapo tumseme waziwazi kama sio kumsuta aache kuhisi kila mwanakyela atakayempinga basi anauhusiano na mafisadi. ajue wanataka mabadiliko, hii vita ya mafisadi isimpe kiburi na kuamini atashinda hata bila ya kuleta maendeleo. hata kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mjiandikishe na muweke viongozi wenye dira. hapa tutaikamata kyela na kuindeleza.
Last edited: