Ndugu yangu,Enginner,
Kazi za mbunge ni
Kipimo cha ufanisi wa mbunge wakati wa muhula wake sharti kiendane na kazi zake kama inavyotajwa hapo juu.
- Kutunga sheria;
- Kuisimamia serikali; na
- Kuwakilisha wananchi.
Ni makosa kwa wananchi kudhani mbunge anatakiwa kujenga shule, vituo vya afya, barabara, visima vya maji na kadhalika. shughuli hizi pamoja na nyinginezo zianzofanana na hizo ni wajibu wa serikali. Lakini iwapo serikali itakuwa imetekwa na mafisadi haiwezi kuwa na rasilimali za kutosha kugharimia shughuli za maendeleo kwa ajili ya manufaa ya wananchi. Kyela haina shule, barabara, vituo vya afya au miundombinu ya huduma nyingine, ambavyo ni hafifu, basi kelele za Mbunge wenu Mwakyembe dhidi ya mafisadi ndio mahali pake; anaisimamia serikali ipasavyo. Shukuruni Mwenyezi Mungu kwa maana mnaye mbunge mahili anayefanya kazi zake kwa ipaswavyo.
Mtu yeyote anayejinadi kujendga visima vya maji, kujenga barabara, kununulia watoto sare za shule na kadhalika sharti atambulike kuwa ni mtu asiyefaa kuwa mbunge, kwa sabau, ama hana uelewa na kazi za mbunge au ni malaghai. Je, Kyela mnataka kulaghaiwa?
Ni juu yenu kusuka au kunyoa!
wakhtanabahu
Kama kazi za mbunge ni hizo tu unazozisema wewe, basi hatuhitaji kuwa na wabunge wa majimbo. Tuanzishe wabunge wa kuchaguliwa kufuatana na kura za chama kama zinavyofanya baadhi ya nchi.
Pesa nyingi sasa ziko kwenye halmashauri ya wilaya na hata mipango mingi ya maendeleo inaamuliwa huko na sijui kwa kazi za mbunge kama ulivyoandika, nini wajibu wa mbunge kwenye halmashauri ya wilaya yake?
Nakuhakikishia, kazi ya mbunge ni zaidi ya ulizozitaja. Maendeleo sehemu kubwa kwasasa hayaletwi na serikali peke yake. Sehemu kubwa wananchi wanachangia na Mbunge hapo ni kiungo muhimu mno.