Siasa za Mbeya 2005-2010

Siasa za Mbeya 2005-2010

at the end the truth will prevail.

Kwa mara ya kwanza katika hii thread umeandika UKWELI wa asilimia 100.

TUSUBIRI TUONE MAHAKAMA /POLISI WATAAMUA. Ila safari hii mtu lazima aumbulike. Kama ni Mwakalinga au Mwakyembe, mtu lazima avuliwe nguo na atembee UCHI, yes ule uchi wa MNYAMA wa KISIASA.
 
Dr. ni mkweli, Mungu atamsaidia. Mwakalinga ana future nzuri, ni mtu ambaye namfahamu na tuko jirani sana. Kinachoniudhi hapa ni mlango aliopitia Mwakalinga. Otherwise he is a very polite and wise man. Kama angepita njia tofauti , anafaa tu kama ilivyo kwa Dr. Watu wa Kyela hawana tabia ya kujikomba kwa watu wenye hela chafu. Ni watu wanaojiamini kama walivyo. Hivi inakuwaje mtu ambaye amekuwa msitari wa mbele kupinga ufisadi anatumiwa na hao watu waliohujumu maendeleo ya Kyela? Mwakipesile ni kibaraka wa hao wanaomchukia Mwakyembe. Heri Mwakyembe hata kama wanasema hajaleta maendeleo, kuliko mtu ambaye anatumiwa. Please , Please George jiengue na hao watu na nitakupigia debe! Tena utakuwa umeweka Historia kwenye kata ya Katumba Songwe. One word " JIENGUE NA HAO MAFISADI" come clean we will be on your back. Hujachelewa......

Nyumbu,

Sasa unataka Mwakalinga afanye nini?

Ndio maana muda wote Dr. anahangaika kumwunganisha Mwakalinga na Mwakipesile au RA au Lowassa, kwasababu anajua kuna watu kama nyie mtaamini hizo story na kuzidi kueneza.

Kwa taarifa yako tu, Mwakalinga kwa mara ya kwanza aliongea na baadhi ya viongozi wa CCM kuhusu nia yake ya kugombea March 2007. Hiyo ilikuwa kabla ya RICHMOND na pia kabla hata ya Mwakipesile kutangaza kwamba hatagombea. Kama ni mtu wa Kyela na unataka ukweli basi mwulize hata huyo Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ambaye alikuwa mmoja wapo. Huyo Mwenyekiti anamwunga mkono Dr. lakini naamini ni mzee mzima hawezi kuongopa kwenye hili la lini aliambiwa mara ya kwanza. Ukitaka niandikie PM na nitakuambia huo mkutano ulifanyika wapi na nani alikuwepo.

Kwa ujumla ni kwamba Mwakalinga hajatumwa na mtu, hana mawasiliano na akina Lowasa na RA au mafisadi wengine.

Sio siri wapambe wa Mwakipesile sasa wanamuunga mkono Mwakalinga. Hicho kitu ni cha kutegemea maana adui wa adui wako ni rafiki yako na hao watu wako Kyela wala hawahitaji kufuatwa.

Hayo yote wanayoandika IPPMEDIA ni mwendelezo huo huo wa kutumia vyombo vyao ili ionekane Mwakalinga anasaidiwa na akina Lowassa, katumwa na akina Lowassa. Yote hiyo ni kwasababu hawawezi kushindana kwa hoja za maendeleo na wamekimbilia kwenye mambo ya kuzua.

Kwa anayeamini tunayosema anaweza kutuunga mkono, kwa wale wanaoamini ya ya Mwakyembe sawa pia only time will tell kama kweli hayo mnayosema yana ukweli.

Kwa watu wa Kyela wengi wanajua ukweli maana huwezi kusema mtu kapewa mamilioni wakati hata kampeni yake inaendeshwa kwa kujitolea zaidi kuliko pesa. Vijana wanaomsaidia Mwakalinga hata hawana vitendea kazi tofauti na wale wa Mwakyembe ambao wamepewa mpaka pikipiki.
 
Kwenye msafara wa mamba na kenge wapo.

Kila la kheir
 
Engineer,

Nimefuatilia post zako nyingi humu mara nyingi unaegemea upande mmoja na unaelekeza upinzani/mashambulizi moja kwa moja kwa mtu unayemtuhumu na kuwaaminisha wote watakaosoma waamini unaloliandika kuwa ni sawa.

Unalalamikia magazeti ya IPPmedia siyo kweli, siku ya Ijumaa magazeti yote yaliandika kuhusu hili la Mwakyembe siyo Nipashe pekee! Hizi habari hatujazisoma nipashe.

Engineer, kama unakuja humu JF basi jaribu kuvaa ngozi ya kuhabalisha ukweli usije kishabikishabiki na kuelekeza mashambulizi kwa mtu ambaye haumshabikii. Jiulize wote humu tukiwa kama wewe kwenye hii forum patatosha?
 
Ananishangaza huyu Mkuu wa Wilaya ya Kyela, yaani uhai wa mwenzake unatishiwa yeye anasema anaona suala hilo dogo tu na anashangaa watu kumkera kwa kumpigia simu, jamani naye si fisadi wa roho ya mwenzake huyu?
 
Engineer,

Nimefuatilia post zako nyingi humu mara nyingi unaegemea upande mmoja na unaelekeza upinzani/mashambulizi moja kwa moja kwa mtu unayemtuhumu na kuwaaminisha wote watakaosoma waamini unaloliandika kuwa ni sawa.

Unalalamikia magazeti ya IPPmedia siyo kweli, siku ya Ijumaa magazeti yote yaliandika kuhusu hili la Mwakyembe siyo Nipashe pekee! Hizi habari hatujazisoma nipashe.

Engineer, kama unakuja humu JF basi jaribu kuvaa ngozi ya kuhabalisha ukweli usije kishabikishabiki na kuelekeza mashambulizi kwa mtu ambaye haumshabikii. Jiulize wote humu tukiwa kama wewe kwenye hii forum patatosha?

Maggie,
Huyo ndiyo Engineer. Inabidi umzoee. Mbona kuna Malafyale anayesema Mwakalinga alikuwa Arusha na kufungua kikao huko Kyela? Anasema hilo lawezekana kwani kimwili alikuwa Arusha na Kyela KIROHO. Kuna Shalom na yeye na Wazungu wake siku zote ni kumsiliba Mwakalinga.

Engineer HAMPENDI Mwakyeme na hii siyo SIRI. Sifahamu walikosana wapi. Nilishaandika kuwa hata kama ni wewe Maggie ungeligombea Kyela, basi Engineer angelikushangilia. Kila adui wa Mwakyembe ni rafiki wa Eng.

Uandishi wa Engineer ni ki vyake. Vyote anavyoandika ni VYA UKWELI ila siku zote huwa ANAONGEZA CHUMVI. Kila anachosema huwa kinakuja kuthibishwa kuwa ni kweli ila yeye huwa anaongeza ili KUKIREMBA. Kumbuka hata swala la kuteka nyara, aliliandika na watu wakampinga kuwa SI KWELI. Baadaye imekuja kuthibishwa ni kweli na Mwakalinga kaagiza wanasheria wake wawashitaki waliomteka nyara kijana na magazeti atayapandisha kizimbani kwa kuandika "kijana mwenye simu za ERICSSON" alitaka kumuuwa Mwakyembe. Yaani kuwa na simu mbili zenye kupiga picha na kunasa simu basi umekuwa MUUWAJI? Mie hapa nina masimu kibao, basi IPPMEDIA ingelibidi waniite ABDUL NIDAL.
 
Dada,

Habari kwenye magazeti matatu, Nipashe, Majira na Mtanzania yaliandikwa na mwandishi mmoja ambaye yuko Mbeya na ndiye mwandishi wa IPPMEDIA.

Majira na Mtanzania waliandika na Mwandishi maalumu wakti Nipashe ndio walimtaje.

Nimeona nikujulishe hilo kama ulikuwa huna habari.


Engineer,

Nimefuatilia post zako nyingi humu mara nyingi unaegemea upande mmoja na unaelekeza upinzani/mashambulizi moja kwa moja kwa mtu unayemtuhumu na kuwaaminisha wote watakaosoma waamini unaloliandika kuwa ni sawa.

Unalalamikia magazeti ya IPPmedia siyo kweli, siku ya Ijumaa magazeti yote yaliandika kuhusu hili la Mwakyembe siyo Nipashe pekee! Hizi habari hatujazisoma nipashe.

Engineer, kama unakuja humu JF basi jaribu kuvaa ngozi ya kuhabalisha ukweli usije kishabikishabiki na kuelekeza mashambulizi kwa mtu ambaye haumshabikii. Jiulize wote humu tukiwa kama wewe kwenye hii forum patatosha?
 
Ananishangaza huyu Mkuu wa Wilaya ya Kyela, yaani uhai wa mwenzake unatishiwa yeye anasema anaona suala hilo dogo tu na anashangaa watu kumkera kwa kumpigia simu, jamani naye si fisadi wa roho ya mwenzake huyu?

Kwasababu yeye anajua yale ambayo wewe huyajui. Anajua hakukuwa na jaribio lolote la kutaka kumwua mbunge na badala yakke ni siasa za mwaka 2010 na ndio maana akasema hivyo.

Tunasubiri kwa hamu report ya polisi ili ukweli wote ujulikane.
 
Kwasababu yeye anajua yale ambayo wewe huyajui. Anajua hakukuwa na jaribio lolote la kutaka kumwua mbunge na badala yakke ni siasa za mwaka 2010 na ndio maana akasema hivyo.

Tunasubiri kwa hamu report ya polisi ili ukweli wote ujulikane.

Engineer,

Ripoti gani unasubiri!! Ile ya ajari kwa Mh. juzi ampapo walisema Mh. alikuwa amelala fofofo kabla ya ajari yake ndo unasubiri tena ripoti!! Nchi hii kweli kuna ripoti!! haya wewe subiri.
 
Engineer wa majungu!

Kuwa mtu mzima kidogo basi, stop lamenting and crying like a little high school girl.....wengine sisi tunakujua wewe kama ni kishoka tu huna mbele wala nyuma...uko kama saa mbovu, either utakuwa mbele ya muda ama nyuma.

Masanilo,

Ningekujua unaishi wapi basi nisingeumiza kichwa changu.

Lakini ukweli unabaki kuwa ukweli, mtu mzima hatishwi ny'au, sasa huyo Mwakyembe wenu kama anapika habari ambazo hazipo basi ni mtu wa hatari sana.

Anateka nyara wapiga kura wake huku akiwaomba wamsaidie 2010, nani atampa kura?

Anataka kuharalisha uongo na kuingilia utalaamu wa police, lakini watu wa Kyela sasa watajua uongo wake wa kila siku anaoimba.

Iweje kijana mdogo apenyeze kisu kikubwa kwenye mkutano na asipigwe na wapambe?

Unampeleka nyumbani kwako kumdhalilisha kana kwamba yeye ndiye police sasa.

Mwakyembe hana jipya, ameshindwa kuliendeleza jimbo lake na huku anatapatapa tu.
 
Huyo Mwakalinga kama anakubalika Mbeya kwa nini asigombee jimbo jingine? Vp pale Mbeya mjini nyie wapambe wake hauziki? Muuzeni Mby mjini pale mwageni laptop Mwanjelwa pale. Tumechoka hizi kambi hizi Mwakalinga kuwa makini na hawa wapambe wako watakulostisha wengine ndo hapo hapo wanategemea kupata laptop. Kuwa makini mkuu unaweza jikuta unafulia.
 
Huyo Mwakalinga kama anakubalika Mbeya kwa nini asigombee jimbo jingine? Vp pale Mbeya mjini nyie wapambe wake hauziki? Muuzeni Mby mjini pale mwageni laptop Mwanjelwa pale. Tumechoka hizi kambi hizi Mwakalinga kuwa makini na hawa wapambe wako watakulostisha wengine ndo hapo hapo wanategemea kupata laptop. Kuwa makini mkuu unaweza jikuta unafulia.

No mkuu unakosea sana. Aliyeshujaa wa Tanzania si Mwakyembe?
Kwa nini Mwakyembe asiende huko kugombea? Au hata aende kwao Rungwe kugombea sasa. Vingnevyo ningelitamani sana awe mbunge wa kuteuliwa (wa TAIFA) maana siyo siri jamaa ni msomi mzuri na ana uwezo wa kufanya mambo makubwa sana. Ila kudeal na Wakulima hilo si lake.
Mwakymbe wee rudi bunge la East Africa ukanoane kichwa na wasomi kutoka nchi majirani zetu.
 
Sio siri wapambe wa Mwakipesile sasa wanamuunga mkono Mwakalinga.

Hawa ndo wanao mfanya Mwakalinga aonekane nae anapigiwa chapuo na mafisadi maana Mwakipesile huwezi mtenganisha au kuunganisha dot na mafisadi. Akifanikiwa kuwakwepa hawa atakuwa msafi lakini kwa sasa mmmmh! na wakianza kutumbukiza visenti amekwisha...
 
Hebu tusemzane tena. Kuna mtu anaweza eleza yepi Dr kashindwa, na yepi kafanikiwa. Na vipi Bro. George atayamaliza? Naamini badala ya kumshambulia George, au Mwakyembe tufanye tathmin ya aliyepo madarakani kwanza, tuangalie jinsi GAM anavyoweza kuyapiku au hata kuyaendeleza. Hapo tutaisaidia Kyela kuangukia siasa za chuki. Letu wote hapa ni moja: iwe Mwakyembe au George au hata huyo aliyepoteza mvuto: Mwakipesile. Tatizo la Mwakipesile ni kuwaadhibu wazazi wake na watoto wake wa Kyela kwa chuki binafsi na Mwakyembe. Na hili ndo tunataka kulipambanua kabla hatujasema George au Mwakyembe ....
 
Engineer,

Ripoti gani unasubiri!! Ile ya ajari kwa Mh. juzi ampapo walisema Mh. alikuwa amelala fofofo kabla ya ajari yake ndo unasubiri tena ripoti!! Nchi hii kweli kuna ripoti!! haya wewe subiri.
Wenzako wanasubiri report ya uchunguzi kwamba kijana alitaka kumwua Mwakyembe kwa kisu. Kwa taarifa nilizo nazo report tayari iko hapa ofisni kwa iko IGP na kisha itarudishwa Mbeya kusomwa.
 
Dada,

Habari kwenye magazeti matatu, Nipashe, Majira na Mtanzania yaliandikwa na mwandishi mmoja ambaye yuko Mbeya na ndiye mwandishi wa IPPMEDIA.

Majira na Mtanzania waliandika na Mwandishi maalumu wakti Nipashe ndio walimtaje.

Nimeona nikujulishe hilo kama ulikuwa huna habari.
mbeya nzima kuna mwaandishi wa habari mmoja tu....
 
mbeya nzima kuna mwaandishi wa habari mmoja tu....

Yale ya kule Tarime kwani Mara yote ilikuwa na mwandishi mmoja tu?

Wanafiki utawajua tu, kwenye mambo ya CHADEMA walikuwa wa kwanza kusema habari imeandikwa na mwandishi mmoja, kwa ya Mwakalinga wanaleta maswali.
 
Daahh.........sasa nyie mashemeji sijui hata tuwasaidieje
 
Yale ya kule Tarime kwani Mara yote ilikuwa na mwandishi mmoja tu?

Wanafiki utawajua tu, kwenye mambo ya CHADEMA walikuwa wa kwanza kusema habari imeandikwa na mwandishi mmoja, kwa ya Mwakalinga wanaleta maswali.
engineer wacha jazba unatakiwa kuzoea kutumia ushawishi wa hoja, kama uwezi kutoa ushawishi wa hoja utawezaje kumpigia mtu wako kampeni...

dili na mwakyembe kwanza, maana yake chadema ni vijana huwawezi....
 
Back
Top Bottom