engineer wa majungu ya ukweli mkuu,wanakyela wamesha mstukia kuwa ni mamluki katumwa na mafisadi na kapewa minoti kufa mtu.......
Asante Sikonge,Mhandisi,
Na heshima zote lazima nikuambie kuwa Shalom na Masanilo ni watu wawili tofauti. Shalom ni Mnyakyusa na Masanilo ni Msukuma. Mengine yote nawaachieni wenyewe ila nilitaka kukusaidia kwa hilo tu.
Jile habari yako hapo juu imenichekesha sana kwa kweli;sidhani kama "Engineer"kapewa hela yeyote na mafisadi maana angekuwa nazo lzm angekuja pale kijiweni kwetu Kyerucu kula bata na rafiki zake akina Kenne,Malwilo na Kambi!
Namtetea kwa hilo,hajapewa hela lkn huwa anajaziwa pikipiki yake mafuta ili awe anazunguka vijijini hasa kule Ipinda,Kasumulu,Ntaba,Butangali,Njisi,Matema,Kafundo,Mwaya na Kajunjumele kuona wana Kyela wanamuongelea vipi Mbunge wao!
"Engineer" njoo kesho hapa Baling'enyo tupate kubadilishana mawazo hasa nikimaliza safari ya kutoka kijijini kwetu Ilopa;jana nilikuona pale kibandani kwa Madaraka nahisi ulikuwa unaongea na kaka Maneno!
Lolah,
Naona umeandika maneno ya KISWAHILI hapa ila nafikiri wakati unaandika, ULIKUWA UKIWAZA KINYAKYUSA. Mie sikukuelewa kabisa, ila Mnyakyusa mwenzio Masanilo kakuelewa haswaa hadi kajisahau kaandika Kikwenu.
Uwe unaandika Kiswahili hata ki-maana na siyo kuandika kikwenu hapa.
dah pole sana ndugu yangu kumbe unanaukabila pia? mimi sina kabila ndugu mimi ni mtanzania tu sio mnyakyusa wala mpare,
Ningelikuwa na UKABILA si ningelikuwa kwenye mambo ya Tabora na Sikonge huko? Ila nipo hapa nikimkoma nyani wa Kinyakyusa. Sasa unaniita mie Mkabila, zinakutosha kweli wewe? Au neno FIKIRI limeondolewa kwenye ubongo wako?
NB: Masanilo, wahi Sikonge sasa mkuu maana haya Matonga kwa sasa yapo kibao. Pia Mahama na Nfulu ndiyo zimeiva kwa wingi. Ntalantu nazo msituni kwa wingi sana. Mapera na Mapapai yameisha na twajiandaa kwa Maembe mwezi ujao mwishoni. Ahhhh, maembe wewe acha. Asali aka "wuki" ndiyo kwa saana. Chai ya asali umeshakunywa mkuu? Ngoja nimalise maana Lorah atasema "si mkabila huyu?"
Huyo kijana angekuwa mtoto wa maskini, mpaka sasa angekuwa anasota rumande bila kosa.
Mbunge unaanza kuwatungia wananchi wako makosa makubwa kama hayo? Mbunge inatakiwa uwe unatetea wanyonge na wala sio kuwazulia wanyonge makosa ambayo hayapo.
Mbona uchaguzi uko mbali? Tunataka tuwapige chini wababaishaji.
Uchunguzi wa awali tishio la kuuawa Mwakyembe wakamilika
Na Thobias Mwanakatwe
9th September 2009
![]()
Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limekamilisha uchunguzi wa awali wa tukio la vurugu za kutaka kuuawa kwa kisu kwa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, wakati akiwahutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Advocate Nyombi, akizungumza na waandishi wa habari jana ofisi kwake, alisema Mkuu wa Upelelezi Mkoa, (RCO) Athuman Diwani, ambaye alimtuma kwenda kuchunguza tukio hilo amesharudi na sasa anayapitia majalada husika kulingana na ushahidi uliotolewa na watu waliohojiwa.
"RCO amerudi na hivi sasa anayapitia majalada husika ili kuona kama kuna makosa yoyote ya jinai yaliyotendekea na ni nani hasa waliohusika na jinai hizo ili mwisho wa siku hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao," alisema Nyombi na kuongeza kuwa kazi hiyo ikikamilika taarifa rasmi itatolewa.
Alisema polisi wamelazimika kufanya uchunguzi wa tukio hilo kwa kina kufuatia, Collins Abwene Mwakalinga, kufungua jalada katika Kituo cha Polisi cha Kyela akilalamika kuwa ndugu yake, Daniel Mwakalinga, alitekwa Septemba mosi mwaka huu wakati wa mkutano wa hadhara wa mbunge wa huyo.
Awali ilielezwa kuwa katika tukio hilo ambalo limeleta mjadala mkubwa ndani na nje ya nchi, Dk. Mwakyembe wakati akihutubia mkutano wa hadhara kwa wananchi wa kijiji cha Tenende wilayani Kyela, ghafla walifika vijana wawili kwenye mkutano huo.
Vijana hao mmoja alidaiwa kuwa na kisu na mwingine akiwa na kinasa sauti ingawa haikuelezwa lengo lao ni nini, taarifa zilieleza kuwa walitumwa kwa ajili ya kutaka kumdhuru mbunge huyo.
Mbunge huyo wakati akiendelea kuwahutubia wananchi hao huku akiwa hajui nini kinaendelea, wasaidizi wake waliwashtukia vijana hao wawili na kumkamata mmoja wao huku mwingine alifanikiwa kuwakimbia.
Wakati wasaidizi wa Dk. Mwakyembe wakiwa katika harakati za kumkimbiza aliangusha kisu alichokuwa amekificha kwenye shati lake kwa ndani.
Maafisa wa Polisi Wilaya ya Kyela waliozungumza na Nipashe kwa kuomba majina yao yasiandikwe gazetini walieleza kuwa kijana aliyekamatwa na kukutwa na kinasa sauti pamoja na simu ya kisasa aina ya Sonny Erickson anajulikana kwa jina la Daniel Mwakalinga ambaye ni mkazi wa Kyela mjini.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Abdallah Kihato, akizungumza na Nipashe kwa simu baada ya tukio hilo alithibitisha kukamatwa kwa kijana huyo aliyekuwa na mwenzake aliyetoroka na kudondosha kisu na kwamba alikuwa akihojiwa.
Tangu kutokea kwa tukio hilo wananchi wa mji wa Kyela na vitongoji vyake wamekuwa wakitega masikio kutaka kujua nini polisi watabaini katika uchunguzi wao, hasa kutokana na mara nyingi uchunguzi wa polisi kuchukua muda mrefu kukamilika kama wa tukio la mauaji ya kijana mmoja Lucas Mwaipopo.
Mwaipopo alidaiwa kuuawa na polisi mjini humo na uchunguzi wake hadi sasa umekuwa kimya.
Mwanakatwe unatia huruma ndugu yetu. Karibu ukweli wote utajulikana, endelea kuwalaumu polisi wa Kyela. Uchunguzi huu umefanywa na RCO. Wajanja wa mjini tunajua wamegundua nini, siku hiyo nitalewa kimpumu ile mbaya. Wamefulia kweli kweli!
Hili nalo tunatakiwa kulijua? walevi wa chimpumu ovyo kabisa
Na wewe ****** siku hiyo sijui uso wako utaficha wapi? Mijitu mingine kama Masanilo ina wivu wa kijinga.
Hapo RPC haongelei tena mauaji bali utekaji nyara.
Malafyale,
Siku wakitoa taarifa tu nitakutafuta nikupe beer Barimonye, pesa ya siku moja nitaipata tu hata kama itakuwa kwa kuuza kokoa mbichi.
Eti Engineer wa majungu ha haa haaaa!!! For Kyela Breaking News - Engineer is the man! Itabidi munipe mji tu au kata ila isiwe Ikolo maana kule wasanii wengi sana pia kuna mbunge mteka vijana, sitaki waniue miye!
Sikonge/Engineer:
Mbona hamjibu maswali? Tunauliza, mworozeshe yale aliyoweza Mwakyembe, na yale aliyoshindwa. Kisha mtuonyeshe yale atakayoweza Mwakalinga.
Sisi wana Kyela tunataka maendeleo, si tu ya Kyela bali ya nchi nzima. Leteni data hapa, ni kipi kinamsukuma Mwakalinga kuwania ubunge? Ni yepi atayafanya kuliko Mwakyembe? Na yepi aliyoshindwa
Mwakyembe?. Maana tukijua hilo we will not give a damn to Mwakyembe and we will all go to Mwakalinga or any other aspirant. Jibu swali hili tuanzie hapo.....