Siasa za Mbeya 2005-2010

Siasa za Mbeya 2005-2010

Mto Songwe unatajwa katika kuweza kuinua kipato cha wakaazi wa Jimbo la Songwe iwapo mto huo utatumika katika kilimo cha umwagiliaji. Hata hivyo mto huo ambao unamwaga maji yake katika Ziwa Rukwa una umuhimu kwa nchi mbili, Tanzania na Malawi. Kwani unamwaga maji yake ndani ya Ziwa Malawi/Nyasa vilevile.

Kabla ya kuendelea kujadili hili kuna memba yoyote mwenye ufahamu wa mto huu, unaanzia wapi?

Iwapo una manufaa kwa nchi mbili, je kuna mpango wowote wa kuwa na kamisheni ya pamoja kati ya Tz na Malawi ili kuona kuwa mto huo unatumika kwa faida ya wananchi wa pande zote mbili pasipo kuwepo na ugomvi?

Kibunango,

Hiyo makala imenifungua kichwa. Mimi nilikuwa najua mto Songwe unaanzia huko mlimani na kuishia lake Nyasa, kumbe upande mwingine unaishia lake Rukwa?

Hapo imenichanganya zaidi, naomba wenye ujuzi na hayo maeneo tuelemisheni. Je mto Songwe unaanzia wapi na kuishia wapi?

Kule Malawi wakati wa Banda kulikuwa na kilimo cha kumwagilia maji, sisi Watanzania mpakani tukashindwa hata kuiga na badala yake tulikuwa tunaenda kule kuhemea chakula.

Inasikitisha kwamba huwa hatujifunzi kutokana na mafanikio ya mtu mwingine labda ndio maana tunaweka fitina badala ya kujifunza ili nasi tufanye yaliyo bora zaidi.
 
Kibunango,

... naomba wenye ujuzi na hayo maeneo tuelemisheni. Je mto Songwe unaanzia wapi na kuishia wapi?

nilipokuwa primary nilikuwa naishi kilomita 1 kutoka mto songwe ulipo. mpaka leo sijui unaanzia wapi lakin najua unamwaga maji yake ziwa nyasa. kijij nilichokuwa naishi mto huo ulikuwa unaact kama mpaka kat ya tz na malaw
mto huo ambao hauna kingo kama za mto kiwira unaletaga shida sana unapofurika miez ya 4 au 5 maana maji yake yanasambaa kwenye vijij vya jiran
 
.... ukimuuliza mwakipesile kwa nini unawachukuia hawa wezako hana jibu ukiwauliza wasomi hawa watakuambia kwanini ameteuliwa u RC na kuwekwa mbeya ....

kama hawa jamaa hawaelewani kweli hiv hakuna wa kuwapatanisha?
anaweza kuwa mbunge yeyote wa maeneo yale au mkuu wa mkoa wa mkoa jirani au kiongoz wa kitaifa.

siku akiwapatanisha inaweza kuwa habari kwenye vyombo vya habari na aliyewapatanisha anaweza pata credits ktk siasa. wanasiasa wetu hawaoni hii opportunity? cv inaweza kua
 
nilipokuwa primary nilikuwa naishi kilomita 1 kutoka mto songwe ulipo. mpaka leo sijui unaanzia wapi lakin najua unamwaga maji yake ziwa nyasa. kijij nilichokuwa naishi mto huo ulikuwa unaact kama mpaka kat ya tz na malaw
mto huo ambao hauna kingo kama za mto kiwira unaletaga shida sana unapofurika miez ya 4 au 5 maana maji yake yanasambaa kwenye vijij vya jiran

Mwakatojofu,

Wewe unaweza kuwa jirani yangu. Mimi nimekulia meter kama 100 toka huo mto. Nilikuwa bingwa wa kupiga mbizi kwenye huo mto.

Ila ndugu yangu mbona Mbeya hakuna akina Mwakatojofu? Sisi Mbeya wote ni majitu kwahiyo tunajiita Mwaitojofu au Mwalitojofu.

Kuhusu hawa waheshimiwa kupatanishwa mbona imefanywa mara nyingi? Hata kamati ya Kinana iliwapatanisha na wakaombana na msamaha, lakini kabla hata wino kwenye hayo makubaliano yao haujaisha, wakaanza kulimana vijembe.

Labda atokee bundi hapo 2010, wakati wao njiwa wanagombana, anakamata wote wawili na kuwafanya kitoweo.
 
Lakini mimi nina shida kubwa hapa, nilikuwa nikiishi Mbeya wakati Mkuu wa Mkoa akiwa Maj Gen Makame. Gen Makame aliweza kufanya lolote awezalo juu ya Mbeya na still wanambeya walimshangilia. Ni kipindi hichohicho Mwenyekiti wa Mkoa wa Mbeya alikuwa akitoka Ushirika(kitongoji kati ya Kiwira na Kyela).Na kilikuwa ni kipindi kofia mbili, katibu wa mkoa(CCM) akitokea Tanga(sahamani katibu huyo kwa sasa ni marehemu na jina limenitoka). Mbona hatukuweza kusikia longolongo zozote?

Ikumbukwe kuwa ni wakati au enzi hizo ambapo Mbeya Hotel ilivamiwa na hotel za watu binafsi, na ni kipindi hichohicho jumba la sinema opposite na Posta kuu ya Mbeya ilipogeuzwa kuwa jumba la kutangaza Injili. Na ni kipindi hicho hicho boogie disco ilipopigwa marufuku Mbeya. Sioni lolote katika mada hii kuhusu Gen Makame jinsi alivyoweza kuwafunga mdomo wanyakyusa! Ama kwa uwa kuwa alikuwa ni Mjeshi na amehusu Mtwara?

Tafadhalini sana nina omba tujiepushe na ukabila na udini, kwani hivyo sio sehemu ya maendeleo ya TZ kwa Ujumla. Iwapo Mkuu wa Mkoa wa sasa anapinga maendeleo ni vema kuweka bayana kuwa mkuu huyo ameweka mguu katika suala hili ama ile ambalo lina lengo la kuendeleza Mkoa huo!

Mimi binafsi hapa nilipo nje ya TZ, napokutana na watu wapendao kwenda TZ huwa nawaambia wasite kwenda Mbeya kuona comet, kule Mbozi, the highest road peak in Tz barabara ya kwenda Chunya, Daraja la Mungu Kiwira(Mshike adabu zenu na Mkapa, kwani yeye ana tengeneza umeme tu). Matofali ya Mungu(Lutengano karibu na shule ya Viziwi), Mlima Rungwe(wa tatu kwa urefu Tz) Milima ya Livingstone, lake Nyasa(sasa ni malawi...wanyakyusa wa Kyela mmelalal mno) Mfumo wa Kichifu, kilimo cha iriki,chai na kahawa.. na mambo tele..

Kwa wale waliokuwa Lutengano 1985-7,tuwasiliane
 
Ila ndugu yangu mbona Mbeya hakuna akina Mwakatojofu? Sisi Mbeya wote ni majitu kwahiyo tunajiita Mwaitojofu au Mwalitojofu.

kenyewe ni kadogodogo. sio 'giant'. nafikiri itakuwa right kukaita 'katojofu'

Kuhusu hawa waheshimiwa kupatanishwa mbona imefanywa mara nyingi? Hata kamati ya Kinana iliwapatanisha na wakaombana na msamaha, lakini kabla hata wino kwenye hayo makubaliano yao haujaisha, wakaanza kulimana vijembe.

dk. amejipatia sifa kubwa kote tz kwa kuongoza ile kamat ambayo kusema kweli iliifanyia mema nchi. uswahilin kote na kwingineko tulikuwa tunajua wakubwa wote wanalindana hasa kwa mambo ya ovyo. matokeo ya ile kamat yalipotoka na sis tukashuhudia pitia tv bos wa pili kwa ukubwa akiondoka kwenye kit tukajua ala! kumbe kuna wengine wako na sie!

lakin kama anaendekeza magomv na RC ndo itakuwaje?
inabid ajishushe. kuna mtu nimemsoma humu anasema mbunge akiwa serious na kaz yake sio rahis kuathiriwa na RC. tumeshaona wabunge wa upinzan.
kaz aliyofanya na sifa alizopata hazitoshi. so long he is alive he will have to do more than what he has done

[/QUOTE]
 
kama hawa jamaa hawaelewani kweli hiv hakuna wa kuwapatanisha?
anaweza kuwa mbunge yeyote wa maeneo yale au mkuu wa mkoa wa mkoa jirani au kiongoz wa kitaifa.

siku akiwapatanisha inaweza kuwa habari kwenye vyombo vya habari na aliyewapatanisha anaweza pata credits ktk siasa. wanasiasa wetu hawaoni hii opportunity? cv inaweza kua

Mwe Mulobwike.

Unajua tatizo letu sisi, ni kuwa hatuna professionalism, unajua ifike wakati tujue kuwa hata kama si marafiki, tuna lengo moja yaani kuiendeleza either ofisi au mkoa au taasisi yoyote ile tunayoifanyia kazi. Tukikubali hivyo personal issues hazitaingilia ufanyaji kazi wetu. Yaani kama hawa viongozi wanashindwa kufanya kazi kwa sababu hawapatani ni immaturity. Wakae chini, wapange priorities za mmaendeleo na wafanye kazi. Hakuna mtu anayepatana na kila mtu ofisini kwake.
 
Lakini mimi nina shida kubwa hapa, nilikuwa nikiishi Mbeya wakati Mkuu wa Mkoa akiwa Maj Gen Makame. Gen Makame aliweza kufanya lolote awezalo juu ya Mbeya na still wanambeya walimshangilia. Ni kipindi hichohicho Mwenyekiti wa Mkoa wa Mbeya alikuwa akitoka Ushirika(kitongoji kati ya Kiwira na Kyela).Na kilikuwa ni kipindi kofia mbili, katibu wa mkoa(CCM) akitokea Tanga(sahamani katibu huyo kwa sasa ni marehemu na jina limenitoka). Mbona hatukuweza kusikia longolongo zozote?

Ikumbukwe kuwa ni wakati au enzi hizo ambapo Mbeya Hotel ilivamiwa na hotel za watu binafsi, na ni kipindi hichohicho jumba la sinema opposite na Posta kuu ya Mbeya ilipogeuzwa kuwa jumba la kutangaza Injili. Na ni kipindi hicho hicho boogie disco ilipopigwa marufuku Mbeya. Sioni lolote katika mada hii kuhusu Gen Makame jinsi alivyoweza kuwafunga mdomo wanyakyusa! Ama kwa uwa kuwa alikuwa ni Mjeshi na amehusu Mtwara?

Tafadhalini sana nina omba tujiepushe na ukabila na udini, kwani hivyo sio sehemu ya maendeleo ya TZ kwa Ujumla. Iwapo Mkuu wa Mkoa wa sasa anapinga maendeleo ni vema kuweka bayana kuwa mkuu huyo ameweka mguu katika suala hili ama ile ambalo lina lengo la kuendeleza Mkoa huo!

Mimi binafsi hapa nilipo nje ya TZ, napokutana na watu wapendao kwenda TZ huwa nawaambia wasite kwenda Mbeya kuona comet, kule Mbozi, the highest road peak in Tz barabara ya kwenda Chunya, Daraja la Mungu Kiwira(Mshike adabu zenu na Mkapa, kwani yeye ana tengeneza umeme tu). Matofali ya Mungu(Lutengano karibu na shule ya Viziwi), Mlima Rungwe(wa tatu kwa urefu Tz) Milima ya Livingstone, lake Nyasa(sasa ni malawi...wanyakyusa wa Kyela mmelalal mno) Mfumo wa Kichifu, kilimo cha iriki,chai na kahawa.. na mambo tele..

Kwa wale waliokuwa Lutengano 1985-7,tuwasiliane


Nilipokuwa National Service Makame alikuwa Kamanda kikosi, Mafanikio yake yanatokana na Charisma aliyo nayo, hata jeshini alikuwa anaelewana vizuri Karibu na askari wa ngazi zote. Anaproject aina fulani ya relaxation, nadhani vijana mnaita being cool, hivyo ukifanya nae kazi unachapa kazi bila kinyongo. ( I may be biased remember I was a kuruta then)
 
Nilipokuwa National Service Makame alikuwa Kamanda kikosi, Mafanikio yake yanatokana na Charisma aliyo nayo, hata jeshini alikuwa anaelewana vizuri Karibu na askari wa ngazi zote. Anaproject aina fulani ya relaxation, nadhani vijana mnaita being cool, hivyo ukifanya nae kazi unachapa kazi bila kinyongo. ( I may be biased remember I was a kuruta then)
Indeed, lakini katika social life ya Jiji la Mbeya, Afande wako alichemka vibaya
 
  • Mmoja adakwa akiwa na kisu, mwingine kinasa sauti
  • DC asema yaelekea alidhamiria kumdhuru mbunge huyo
Na Thobias Mwanakatwe
4th September 2009


Mwakye%282%29.jpg


Mikakati ya kutaka kuwanyamazisha wabunge wanaopiga vita vya ufisadi nchini, imezidi kushika kasi baada ya Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe, kunusurika kuuawa kwa kuchomwa kisu.

Tukio hilo lilitokea juzi wakati Dk. Mwakyembe akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Kijiji cha Tenende wilayani Kyela.

Hatua hiyo imekuja miezi minne tangu mbunge huyo anusurike kifo kingine baada ya kupata ajali mbaya ya gari mkoani Iringa, Mei mwaka huu, wakati akirejea Dar es Salaam kutoka Mbeya.

Wakati Dk. Mwakyembe akihutubia wananchi hao juzi, ghafla walifika vijana wawili, mmoja akiwa na kisu na mwingine akiwa na kinasa sauti.

Ingawa haikufahamika lengo lao, lakini taarifa zinadai walitumwa kwa ajili ya kutaka kumdhuru mbunge huyo.

Akiwa anahutubia wananchi, Dk. Mwakyembe bila kujua kilichokuwa kinaendelea, wasaidizi wake waliwashtukia vijana hao ndipo walipomkamata mmoja wao.

Baada ya kukamatwa kijana huyo, mwenzake aliamua kutimua mbio na katika harakati za kumkimbiza, alidondosha kisu alichokuwa ameficha ndani ya shati lake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Advocate Nyombi, alithibitisha kukamatwa kwa kijana mmoja ambaye hata hivyo hakumtaja jina na kwamba taarifa zaidi atazitoa baada ya kukamilisha uchunguzi.

Hata hivyo, baadhi ya maafisa wa polisi Wilaya ya Kyela waliozungumza na kuomba kutotajwa, walisema kijana aliyekamatwa anaitwa Daniel Mwakalinga, mkazi wa Kyela mjini, alikutwa na kinasa sauti na simu ya kisasa aina ya Erickson.

"Unajua suala hili bado lina utata kidogo, kwa hiyo nimemtuma Mkuu wa Upelelezi Mkoa (RCO) ili akafanye uchunguzi na akishamaliza kazi zake nitatoa taarifa rasmi, lakini yule kijana aliyekamatwa anashikiliwa na polisi wa Kituo Kikuu cha Wilaya ya Kyela," alisema Nyombi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Abdallah Kihato, alithibitisha kukamatwa kwa kijana huyo na kwamba, mwenzake alifanikiwa kukimbia na kudondosha kisu na kwamba, anaendelea kuhojiwa na polisi.

Kihato ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kyela, alisema tukio la kukamatwa kwa kijana huyo na mwenzake aliyekimbia, limemletea usumbufu mkubwa hasa kutokana na viongozi kupiga simu kila wakati kuuliza kinachoendelea.

"Nimefanyakazi wilaya nyingi, hili suala lililotokea ni la kawaida tu, lakini ninavyokwambia simu ambazo nimepigiwa na wakubwa kwa maana ya viongozi wa serikali na Jeshi la Polisi Makao Makuu hadi nimechoka wakati naliona ni dogo," alisema Kihato.

Akuzungumza na gazeti hili, mmoja wa wasaidizi wa mbunge huyo, Emmanuel Mwamlinge, alisema kijana aliyedondosha kisu wakati akikimbizwa alionyesha wazi dhamira mbaya ya kutaka kumdhuru Dk. Mwakyembe kutokana na kitendo chake cha kukimbia baada ya kushtukiwa na wananchi.

"Tulivyowashtukia wale vijana wawili hatukutaka kuonyesha vurugu zozote maana wananchi waliokuwepo kwenye mkutano huo wangeweza kuacha kumsikiliza mbunge na kuanza kuwashambulia," alisema Mwamlinge na kuongeza:

"Tulichokifanya ni kuwasogeza pembeni mwa mkutano, lakini ghafla mmoja wa vijana hao alikimbia ndipo akadondosha kisu wakati tukimkimbiza, lakini mwenzake tukamdhibiti."

Mwamlinge alisema kijana waliyekamatwa baadaye walimwingiza kwenye gari na kumpeleka Kituo cha Polisi Kyela Mjini na kumkuta na simu mbili za kunasia sauti, picha na alipotakiwa kueleza uhusiano wake na aliyekimbia alikataa.

Hata hivyo, taarifa ambazo Nipashe ilizipata jana saa 12:15 mchana, zilieleza kuwa kijana aliyekuwa akishikiliwa na polisi aliachiwa huru kutokana na shinikizo kutoka kwa baadhi ya viongozi.

Kwa upande wake, Dk. Mwakyembe akielezea mkasa huo, alisema wakati kijana huyo na mwenzake aliyekimbia wanakamatwa hakujua kilichokuwa kinaendelea hadi baada ya mkutano kumalizika.

Kufuatia tukio hilo, wananchi wa mji wa Kyela wamekuwa wakijikusanya katika makundi kujadili suala hilo, huku wengine wakidai kuwa wanaomwandama mbunge wao ni wale ambao wapo kwenye mtandao wa kisiasa ulioundwa na mafisadi wanaopanga njama za kutaka kumuua Dk. Mwakyembe.

Katika mfululizo wa ziara yake jimboni, Dk. Mwakyembe amekuwa akiwaleza wapiga kura wake kuwa mafisadi wametenga Sh. milioni 400 kumwangamiza kwa kumuua au kumdhoofisha kisiasa na umeundwa mtandano maalum wa kufanya kazi hiyo.

Dk. Mwakyembe alianza kuandamwa na watu wanaodaiwa kuwa ni mafisadi baada ya kuwasilisha taarifa ya Kamati Teule ya Bunge Kuchunguza Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura iliyotoa ushindi Kampuni ya Richmond Development.

Matokeo ya taarifa hiyo, ilisababisha serikali kuvunjwa baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Ibrahim Msabaha, kujiuzulu baada ya kuhusishwa kwenye kashfa hiyo.
 
Hii stori mbona haijakaa vizuri. Yaani ukitaka kumuuwa mwanasiasa humuvizii kimya kimya nyumbani kwake au hotelini bali unamufuata kwenye mukutano wa hadhara ambapo kutakuwa na mamia au ma-alufu ya watu ambao wamekuja kumusikiliza huyo mwanasiasa. Ili iweje? Kama habari hizo ni kweli basi mimi nasema kuwa huyo muuwaji amepungukiwa na akili! Badala ya kumupeleka jela, mupelekeni kwenye hosipitali ya vichaa!

It doesn’t even pass the smell test, let alone any detailed scrutiny of the events that “really” took place at the meeting that is supported by more than a single media source. Reporters in Tanzania can easily be bought and it does to require a lot of cash to do it, in case you don’t already know this. It is a widely accepted thesis that for a little cash, some Tanzanian newspaper reporters can and are often used to lavish glory and praise on their paymasters who are usually politicians that are seeking to promote a particular point of view for political gain of course. But more often than not, reporters are used to demonize and destroy their paymasters’ political opponents. I hope you are not as naïve as to realize for the very first time that these troubling developments have crept into the Tanzanian political landscape.

If you are good at connecting dots (there won’t be a prize for getting it right🙂 you will undoubtedly reach the conclusion that I personally came to, that is to say, the Dear Dr. and his Kyela entourage and disciples are getting desperate and this is only September 2009, God help us come September 2010!. Until this event, I was a strong supporter of the good Dr. but he is beginning to show a dark and vicious side will put him in a bad light in the public eye, political hero or not. Tanzanians voters of this and future generation will not be easily fooled by political stunts so don’t underestimate our intelligence.

But I also have to confess; if it’s any consolation to the Dear Dr, I am not from Kyela so I won’t be given the opportunity to express my disgust at the ballot box for their politics but I am deeply troubled nonetheless as a human being and a Tanzanian. That’s why I have decided to use this forum to speak up now while I can and you should do the same. The mantra that “desperate times call for desperate and drastic measures” certainly applies here in spectacular fashion. Pretty sad!
 
nakumbuka mengi alisha waasa wapiganaji kuwa mafisadi hawa wananguvu kubwa ya fedha na ushawishi na kwamba wanaweza kukuangamiza hata ukiwa nje ya nchi kwani wana mtandao.Matukio haya kwa mwakyembe ni kielelezo tosha,we unadhani Iringa ilipotokea ajari au Kyela ni mbali kiasi hicho kwa mafisadi?Thubutuuuuuu............usimjeruhi mbogo atakuua inabidi kuua kabisa(Hawa majeruhi Lowasa,Rostam,Karamagi watatumaliza tukiwaacha waendelee na ushawishi wao serikalini na kutumia umasikini wa wanakyela kuangamiza wapambanaji akiwemo dr.mwakyembe)
 
nakumbuka mengi alisha waasa wapiganaji kuwa mafisadi hawa wananguvu kubwa ya fedha na ushawishi na kwamba wanaweza kukuangamiza hata ukiwa nje ya nchi kwani wana mtandao.Matukio haya kwa mwakyembe ni kielelezo tosha,we unadhani Iringa ilipotokea ajari au Kyela ni mbali kiasi hicho kwa mafisadi?Thubutuuuuuu............usimjeruhi mbogo atakuua inabidi kuua kabisa(Hawa majeruhi Lowasa,Rostam,Karamagi watatumaliza tukiwaacha waendelee na ushawishi wao serikalini na kutumia umasikini wa wanakyela kuangamiza wapambanaji akiwemo dr.mwakyembe)

Na wewe acha kamba.

Kuwa na simu mbili za Ericsson zenye kunasa sauti na kupiga picha siyo big deal kwa dunia hii. Sasa angelikutwa na Iphone au Blackberry?

Ukitaka kumuuwa mtu siku hizi huhitaji kutumia kisu. Inatosha kumpa Zombe type visenti kidogo na umekwisha. Polisi wanafanya kazi hiyo safi kabisa na wanakukingia kifua. Kwa sasa anatembea na Waandishi wa IPPMEDIA kibao na ilisemwa tangu mwanzo.

Kwa ni siri kuwa Mwakyembe kaolea uchagani? Huko ukweni si ndiyo familia ya Mengi? Mwamba ngoma ndugu yangu, huvutia kwake......

Halafu jina la kijana aliyekuwa na simu mbili za Ericsson linaleta utata sana. Walau ingelikuwa Sony-Ericsson ningeliona ni simu ya kisasa. Mie nilifikiri Ericsson wameshakufa na kuamua kufunga ndoa na Sony? Hii miandishi OVYOOO KABISAAA..

Halafu kukutwa na KISU si kuwa umekuwa muuwaji. Huyu jamaa anaweza kuwa alikimbia kwa kuogopa kipigo kutoka kwa vijana wa CCM wanaofahamika kwa kibano chao cha nguvu. Wakati POLISI wanasema tunaendelea na uchunguzi, wao tayari wameshamhukumu? Ningelikuwa mie ningeliwashtaki kwa kunipakazia kuwa NILITAKA KUMUUWA Mwakyembe.

na Mwakyembe mwenyewe, wewe mwanasheria mzima unakuwa kama Mtei? Ukibanwa useme aliyepewa hizo milioni 400 ili kukumaliza, utaonyesha? Watu wamevurunda wenyewe na sasa kipindi cha malipo kinakaribia mtu anaanza kutafuta kisingizio. Nani alikuambia utowe AHADI kibao kama Muungwana? Mwakani utaubeba msalaba wa ahadi HEWA.
 
Kazi ipo!

Sikonge naomba wimbo wa Mayasa- Marijani Rajabu, kama unao kwenye archives zako.

Waachieni polisi wafanye kazi yao! visu na mapanga ya nini kwenye mikutano! hahahahaha
 
Kazi ipo!

Sikonge naomba wimbo wa Mayasa- Marijani Rajabu, kama unao kwenye archieves zako.

Waachieni polisi wafanye kazi yao! visu na mapanga ya nini kwenye mikutano! hahahahaha

Masa,
Hapo tupo pamoja. tusubiri POLISI wafanye kazi yao na si Mwandishi uchwara kuanza kuwahukumu vijana kwa hisia zake potofu.

Wimbo wa Mayasa, ohh my God. Nipe muda baada ya Weekend ntaanza kukutafutia. Tatizo hii miziki imekuwa too much na hadi nasahau kuwa ninayo. Ntaomba univumilie kidogo kwani sina uhakika kama ninayo au laah. Vinginevyo nitautafuta ni site gani upo na nikuelekeze ukadownload.
 
Sikonge,

Hii habari mimi niliituma moderators wa JF wakasema ni majungu.

Ni kwamba huyo kijana alikamatwa akiwa ana record mkutano wa mbunge kwa kutumia simu. Baada ya hapo wakamfungia kwenye gari, kisha wakampeleka nyumbani kwa mbunge Ikolo na kuanza kumpekua, wakamnyang'anya simu, wakasoma sms zote.

Walimkamata saa nane mchana lakini wakamfikisha polisi saa mbili usiku wakati huo tayari jeshi la polisi limeshaanza kumtafuta.

Walipoona balaa wakazua case ya kwamba alikuwa na mwenzake ambaye alikuwa na kisu na walitaka kumdhuru mbunge. Polisi hata wamejua kisu kilinunuliwa wapi mjini. Ni yale yale ya ajali ya Iringa na kusingizia kugongwa na lori kwa nyuma.

Kwa taarifa za chini chini, RCO na kundi lake wameshathibitisha kwamba ni uwongo mtupu na sasa wanaandaa taarifa ambayo kila mtu anaisubiri kwa hamu maana kuna mtu atafungwa safari hii.

Huwezi kumteka kijana na ukampeleka nyumbani kwako na kumtesa masaa sita wakati hiyo kazi ni ya polisi, tena polisi wenyewe wako sio mbali na hapo mkutano ulipokuwa unafanyika. Hayo yote yanafanywa mbunge anashiriki, mtu ambaye inatakiwa aongoze kwa kulinda sheria.

Nipashe hawataji muda kwasababu haiingii akilini umkamate mtu aliyetaka kumuua mbunge saa nane na umfikishe polisi saa tatu usiku.

Wengine hapa tumetulia na uwongo huu utaumbuliwa mno. Someni na nipashe ya leo muone waliyoyaandika. Ni magazeti ya Mengi yanatumiwa vibaya na watu ambao wanataka wabaki madarakani kwa njia zote. Kila mtu anasubiri RPC wa Mbeya anonge.
 
Masa,
Hapo tupo pamoja. tusubiri POLISI wafanye kazi yao na si Mwandishi uchwara kuanza kuwahukumu vijana kwa hisia zake potofu.

Wimbo wa Mayasa, ohh my God. Nipe muda baada ya Weekend ntaanza kukutafutia. Tatizo hii miziki imekuwa too much na hadi nasahau kuwa ninayo. Ntaomba univumilie kidogo kwani sina uhakika kama ninayo au laah. Vinginevyo nitautafuta ni site gani upo na nikuelekeze ukadownload.

Natanguliza shukrani ndugu yangu!

Nitakupa story baadaye kuhusiana na Mayasa niliyekuwa naye Jeshini. Mkuu nimechoka na siasa za bongo hasa ukizingatia yaliyotokea week inayoisha hii.

Kila laheri

Masa
 
Asubuhi nimesikia kwenye uchambuzi Danny Mwakalinga sijui inakuwaje hapo Masa na Sikonge?
 
Sikonge,

Hii habari mimi niliituma moderators wa JF wakasema ni majungu.

Ni kwamba huyo kijana alikamatwa akiwa ana record mkutano wa mbunge kwa kutumia simu. Baada ya hapo wakamfungia kwenye gari, kisha wakampeleka nyumbani kwa mbunge Ikolo na kuanza kumpekua, wakamnyang'anya simu, wakasoma sms zote.

Walimkamata saa nane mchana lakini wakamfikisha polisi saa mbili usiku wakati huo tayari jeshi la polisi limeshaanza kumtafuta.

Walipoona balaa wakazua case ya kwamba alikuwa na mwenzake ambaye alikuwa na kisu na walitaka kumdhuru mbunge. Polisi hata wamejua kisu kilinunuliwa wapi mjini. Ni yale yale ya ajali ya Iringa na kusingizia kugongwa na lori kwa nyuma.

Kwa taarifa za chini chini, RCO na kundi lake wameshathibitisha kwamba ni uwongo mtupu na sasa wanaandaa taarifa ambayo kila mtu anaisubiri kwa hamu maana kuna mtu atafungwa safari hii.

Huwezi kumteka kijana na ukampeleka nyumbani kwako na kumtesa masaa sita wakati hiyo kazi ni ya polisi, tena polisi wenyewe wako sio mbali na hapo mkutano ulipokuwa unafanyika. Hayo yote yanafanywa mbunge anashiriki, mtu ambaye inatakiwa aongoze kwa kulinda sheria.

Nipashe hawataji muda kwasababu haiingii akilini umkamate mtu aliyetaka kumuua mbunge saa nane na umfikishe polisi saa tatu usiku.

Wengine hapa tumetulia na uwongo huu utaumbuliwa mno. Someni na nipashe ya leo muone waliyoyaandika. Ni magazeti ya Mengi yanatumiwa vibaya na watu ambao wanataka wabaki madarakani kwa njia zote. Kila mtu anasubiri RPC wa Mbeya anonge.

Engineer wa majungu!

Kuwa mtu mzima kidogo basi, stop lamenting and crying like a little high school girl.....wengine sisi tunakujua wewe kama ni kishoka tu huna mbele wala nyuma...uko kama saa mbovu, either utakuwa mbele ya muda ama nyuma.
 
Back
Top Bottom