Siasa, unafiki na usanii: Ufaulu wa kidato cha nne mwaka 2023 umejificha ndani ya divisheni 4

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,836
18,250
Ndugu watanzania, tuamke kumekucha! Tuamke tupiganie haki yetu ya msingi ya kupewa elimu bora na sio bora elimu. Leo wakati katibu mtendaji wa NECTA anawasilisha matokeo nimemsikiliza kwa makini sana. Amedai eti ufaulu wa mwaka 2023 umepanda kwa 0.87% ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2022.

Baada ya kusikiliza matokeo yaliyowasilishwa, nimeingia kwenye mtandao kujiridhisha kama alichosema katibu kinaakisi kupanda ufaulu au la. Nimegundua serikali imejificha kwenye kichaka cha siasa ndio maana kila siku mambo yanaenda ovyo lakini watanzania hawajali. Wamekaa kimya kama mabubu kana kwamba kila kitu kiko sawa.

Serikali inaficha uovu wake wa kuua elimu ya watanzania kwenye siasa za majitaka. Zamani NECTA walikuwa hawatoi matokeo ya jumla na ya kipuuzi kama haya wanayotoa sasa. Walilazmishwa kubadili mfumo kisiasa ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Kwa mfano, siku za nyuma wanafunzi walikuwa wanachaguliwa kuingia kidato cha kwanza kwa kuangalia jumla ya alama ambazo kila mwanafunzi amepata.

Kipindi hicho nafasi za sekondari zilikuwa chache, hivyo ushindani ulikuwa mkubwa. Pia mitihani ilikuwa migumu sana. Kwa mfano, kwa upande wa shule za msingi kulikuwa na mkusanyiko wa masomo matatu tu yaani Lugha, Hisabati na Maarifa, na kila somo lilichukua jumla ya alama 50. Hivyo, jumla ya alama za juu ilikuwa 150.

Haikuwa ajabu mwanafunzi kupata alama 145 akakosa nafasi ya kwenda sekondari. Siku hizi utakuta mwanafunzi kapata alama 11 lakini anachaguliwa kwenda sekondari kwa kisingizio cha kwamba amepata wastani wa D! Hii ni nchi ya ajabu sana. Ndio maana serikali imefanya kila njia kuongeza mafumbo kwenye elimu ili kuficha udhaifu wa kushuka kwa kiwango cha elimu na ufaulu katika nchi hii.

Nikirejea kwenye hoja yangu ya msingi, ukiangalia matokeo ya shule za serikali (shule za kata) ambazo NECTA inasema ufaulu wake umepanda, ni ubatili mtupu. Nimejaribu kuchukua shule chache kama mfano. Hebu tazama hiki kichekesho, ucheke uongeze siku za kuishi:
1706198739953.png

1706198801813.png
1706198852822.png
1706199059019.png

Ukihesabu idadi ya wanafunzi walioangukia kwenye ufaulu wa daraja la nne ni zaidi ya 95% ya wanafunzi wote nchi nzima. Kumbe ufauulu ulioongezeka ni wa divisheni foo! Sote tunafahamu kuwa ufaulu wa divisheni foo hauna maana yoyote. Mwanafunzi aliyepata divisheni foo hastahili hata kupewa cheti. Akafanyie nini hicho cheti? Hakina maana yoyote ile.

Hivi serikali sikivu ya CCM mnamdanganya nani na haya matokeo yenu ya mchongo ambayo kila mwaka ufaulu wake unapanda? Haya ndiyo maajabu ya serikali hii ya kusadikika iliyojaa hadaa, usanii na unafiki kila mahali.
Pia soma: Wanne kati ya watano kidato cha pili Temeke wapata daraja la nne na sifuri
 

Attachments

  • 1706198912594.png
    1706198912594.png
    5.4 KB · Views: 4
  • 1706199018141.png
    1706199018141.png
    5.4 KB · Views: 4
This is just sad..at least kungekuwa na vyuo vya ufundi hao wa form four wangeenda huko..most of their fates are already sealed at a young age
Kabisa mkuu. Tukumbuke watoto hawa wengi ni under age (miaka 15, 16 na 17). Serikali ndio inahusika kuua future yao halafu wanaturudishia sisi wazazi tuwapeleke wapi? Serikali hii ina mambo ya kipumbavu sijapata kuona.
 
Ndugu watanzania, tuamke kumekucha! Tuamke tupiganie haki yetu ya msingi ya kupewa elimu bora na sio bora elimu. Leo wakati katibu mtendaji wa NECTA anawasilisha matokeo nimemsikiliza kwa makini sana. Amedai eti ufaulu wa mwaka 2023 umepanda kwa 0.87% ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2022.

Baada ya kusikiliza matokeo yaliyowasilishwa, nimeingia kwenye mtandao kujiridhisha kama alichosema katibu kinaakisi kupanda ufaulu au la. Nimegundua serikali imejificha kwenye kichaka cha siasa ndio maana kila siku mambo yanaenda ovyo lakini watanzania hawajali. Wamekaa kimya kama mabubu kana kwamba kila kitu kiko sawa.

Serikali inaficha uovu wake wa kuua elimu ya watanzania kwenye siasa za majitaka. Zamani NECTA walikuwa hawatoi matokeo ya jumla na ya kipuuzi kama haya wanayotoa sasa. Walilazmishwa kubadili mfumo kisiasa ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Kwa mfano, siku za nyuma wanafunzi walikuwa wanachaguliwa kuingia kidato cha kwanza kwa kuangalia jumla ya alama ambazo kila mwanafunzi amepata.

Kipindi hicho nafasi za sekondari zilikuwa chache, hivyo ushindani ulikuwa mkubwa. Pia mitihani ilikuwa migumu sana. Kwa mfano, kwa upande wa shule za msingi kulikuwa na mkusanyiko wa masomo matatu tu yaani Lugha, Hisabati na Maarifa, na kila somo lilichukua jumla ya alama 50. Hivyo, jumla ya alama za juu ilikuwa 150.

Haikuwa ajabu mwanafunzi kupata alama 145 akakosa nafasi ya kwenda sekondari. Siku hizi utakuta mwanafunzi kapata alama 11 lakini anachaguliwa kwenda sekondari kwa kisingizio cha kwamba amepata wastani wa D! Hii ni nchi ya ajabu sana. Ndio maana serikali imefanya kila njia kuongeza mafumbo kwenye elimu ili kuficha udhaifu wa kushuka kwa kiwango cha elimu na ufaulu katika nchi hii.

Nikirejea kwenye hoja yangu ya msingi, ukiangalia matokeo ya shule za serikali (shule za kata) ambazo NECTA inasema ufaulu wake umepanda, ni ubatili mtupu. Nimejaribu kuchukua shule chache kama mfano. Hebu tazama hiki kichekesho, ucheke uongeze siku za kuishi:
View attachment 2882622
View attachment 2882624View attachment 2882625View attachment 2882628
Ukihesabu idadi ya wanafunzi walioangukia kwenye ufaulu wa daraja la nne ni zaidi ya 95% ya wanafunzi wote nchi nzima. Kumbe ufauulu ulioongezeka ni wa divisheni foo! Sote tunafahamu kuwa ufaulu wa divisheni foo hauna maana yoyote. Mwanafunzi aliyepata divisheni foo hastahili hata kupewa cheti. Akafanyie nini hicho cheti? Hakina maana yoyote ile.

Hivi serikali sikivu ya CCM mnamdanganya nani na haya matokeo yenu ya mchongo ambayo kila mwaka ufaulu wake unapanda? Haya ndiyo maajabu ya serikali hii ya kusadikika iliyojaa hadaa, usanii na unafiki kila mahali.
Ahsante kwa kuliongelea hili swala,wakati naangalia haya matokeo nilimwambia jamaa yangu hawa serekali wanamdanganya nani,kuna shule ina fo 230 bila zero,ikabidi tucheke tu
 
Ulitaka wengi wapate Divisheni One???? Sijakuelewa..
Hiyo ni Statistical Distribution table.. ambayo ni Normal hapo

S4213 MARIAN BOYS' SECONDARY SCHOOL​


DIVISION PERFORMANCE SUMMARY


S4213 MARIAN BOYS' SECONDARY SCHOOL



DIVISION PERFORMANCE SUMMARY


SEX
I
II
III
IV
0
F​
0​
0​
0​
0​
0​
M​
96​
0​
0​
0​
0​
T​
96​
0​
0​
0​
0​


S0248 MARIAN GIRLS' SECONDARY SCHOOL​


DIVISION PERFORMANCE SUMMARY

SEX
I
II
III
IV
0

F​
64​
17​
0​
0​
0​

M​
0​
0​
0​
0​
0​

T​
64​
17​
0​
0​
0​
 

S4213 MARIAN BOYS' SECONDARY SCHOOL​


DIVISION PERFORMANCE SUMMARY


S4213 MARIAN BOYS' SECONDARY SCHOOL



DIVISION PERFORMANCE SUMMARY

SEX
I
II
III
IV
0
F​
0​
0​
0​
0​
0​
M​
96​
0​
0​
0​
0​
T​
96​
0​
0​
0​
0​
Khaa! Mambo si ndio haya sasa. Hadi raha! Hivi serikali inakwama wapi kuboresha shule za kata?
 
Wewe Mzazi mtoto wako amefeli.. unailaumu Serikali...
Weww ulichukua hatua gani kumsaidia huyo mtoto tokea akiwa Form one.. mfdno Kukaa nae na kummsisitiza kuhusu elimu; kumnunulia Vitabu vya ziada; Kumtafutia remedial class
Unabaki kulia lia tu Serikali impe mtoto wako Ufaulu
 
Back
Top Bottom