Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 1,914
- 6,029
Leo tarehe 25/01/2024 Baraza la Mitihani Tanzania, litatangaza matokeo ya mtihani Kidato cha nne iliyofanyika mwaka jana.
Matokeo hayo yatatangazwa majira ya Saa 5:00 asubuhi kupitia youtube account ya Necta.
Matokeo hayo utayapata hapa punde tu baada ya kutangazwa.
=======
Katibu Mtendaji Mkuu wa NECTA, Dkt. Said Mohamed, Akitangaza matokeo ya kidato cha nne, amesema kuwa
Ufaulu umepanda hadi kufikia asilimia 86.78 ukilinganisha na mwaka 2022 ufaulu wa watahininiwa umeongezeka kwa asilimia 0.87 ambapo idadi kubwa ya wasichana wamefaulu huku wavulana wakifaulu vizuri zaidi katika masomo yao.
Baraza la mitihani limefuta matokeo ya watahiniwa 102 waliofanya udanganyifu na 5 walioandika matusi.
Ufaulu kwa somo la Basic Mathematics umeendelea kuwa chini ya wastani kwa mwaka 2023 kama ilivyokuwa mwaka 2022. Hata hivyo, ufaulu wake umeendelea kuimarika mwaka huu na kufikia asilimia 25.42 kutoka asilimia 20.08 ya mwaka 2022.
Baraza limezuia matokeo ya watahiniwa 376 ambao hawakufanya sehemu kubwa ya mitihani kutokana na ugonjwa, wamepewa fursa ya kurudia mitihani.
Matokeo hayo yatatangazwa majira ya Saa 5:00 asubuhi kupitia youtube account ya Necta.
Matokeo hayo utayapata hapa punde tu baada ya kutangazwa.
=======
Katibu Mtendaji Mkuu wa NECTA, Dkt. Said Mohamed, Akitangaza matokeo ya kidato cha nne, amesema kuwa
Ufaulu umepanda hadi kufikia asilimia 86.78 ukilinganisha na mwaka 2022 ufaulu wa watahininiwa umeongezeka kwa asilimia 0.87 ambapo idadi kubwa ya wasichana wamefaulu huku wavulana wakifaulu vizuri zaidi katika masomo yao.
Baraza la mitihani limefuta matokeo ya watahiniwa 102 waliofanya udanganyifu na 5 walioandika matusi.
Ufaulu kwa somo la Basic Mathematics umeendelea kuwa chini ya wastani kwa mwaka 2023 kama ilivyokuwa mwaka 2022. Hata hivyo, ufaulu wake umeendelea kuimarika mwaka huu na kufikia asilimia 25.42 kutoka asilimia 20.08 ya mwaka 2022.
Baraza limezuia matokeo ya watahiniwa 376 ambao hawakufanya sehemu kubwa ya mitihani kutokana na ugonjwa, wamepewa fursa ya kurudia mitihani.