Shule bora za Serikali, enzi hizo

Shule bora za Serikali, enzi hizo

Kumbuka hata mgawanyo wa wanafunzi waliokuwa wanaenda shule hizo ulikuwa unaenda kimikoa na wilayan, usije ukajiona we kipanga kwa kuchaguliwa kwenda huko wakati wewe umetokea wilaya ya kasulu huko ukamcheka aliyetokea kinondoni ukijilinganisha naye wewe unaweza kuwa wa 250 kwa hapa dar, mgawanyo wa zile nafas ktk wilaya na mikoa ndo ilikuwa chanzo cha baadhi ya watu wenye uwezo mkubwa kutochaguliwa huko kutokana na ushindan mkubwa wa mkoa wake .mf. Dar, na zilikuwa chance kwa washamba kama mtoa mada alipojiona kachaguliwa pale basi anahisi wao ndo walikuwa vipanga nchi nzima kumbe wengi wao walikuwa hovyo na ukitaka kujua angalia hata matokeo ya mwisho yalikuwaje kwa baadh yao
 
Hivi wewe katoto unafikiri JF no kwa watoto hapa watu serious ndio wanakutana ila sikuhizi ninaona mada za kitoto nikawa najiuliza niyale ya mpoto mtumzima kuleta mada za kipuuzi leo nimejidhihorishia kwamba vipo vitoto humu. Moderator inabidi muwafungulie ukumbi wa watoto wote waliozaliwa kuanzia 1990 cause hakuna la maana tunaloweza kuongea nao
 
wengine hizo shule walisoma babu zetu

Ni kweli hizi ni shule kali za enzi zile!!! Naona wengine humu wanajaribu kuzilinganisha na shule kama Loyola na St. Mary's. Wakati huo hiyo Loyola wala St. Mary's hazikuwepo!!!!!

Tiba
 
Ulie leta post hii bado una akili za mgando,elimu sio jina la shule bali elimu ni kwa namna gani imekuwezesha kujitegemea,sasa ww bado na mashule ya zamani daaah kwel hujakuwa
 
Kubalini kataeni yaani uzao wenu nyinyi ni uzao uliopotea. Wenzenu umri wenu mliosoma nao wako vizuri kwa umri wao hata hawahangaiki kuja kupigizana kelele. Nyie mlichezea maisha matokeo yake ndio haya.

mawazo na uandishi wako unaakisi elimu uliyopata
 
Dah nikikumbuka Mkwawa High School (The Big Complex) na kuundua haipo tena nahuzunika sana

That was a place bana....
 
Hahahaha hatare bila kumsahau Mrs Mwang'amba,mr mwabutu,MrsKesy,Miss Msungu,mama semboja jamani nakumbuka enzi za UA,UB,MA,MB,SA,SB,JA,JB

mama sketi mwl sijui nani yule,mama abeid,mama bakari na bajahanuni...!!
 
Anhaaa!....nmekuja kasi sana hapa, ole wako malangali nsingeiona😀😀
...sasa napita!
 
cjapita shule hizo na nna degree ya heshima (Hon.degree) from UDSM.
Hao uliopita nao huko wako wapi?
 
Hizo shule nyingi zilikuwepo wakati wa utawala wa Nyerere wanafunzi wengi tu Tanzania walikuwa na akili lakini nafasi zilikuwa chache sana, na secondary za kulipia nazo zilikuwa chache kupata nafasi ni kazi sana kwa hiyo walipoata nafasi hizo shule siyo kuwa wana akili sana.
 
cjapita shule hizo na nna degree ya heshima (Hon.degree) from UDSM.
Hao uliopita nao huko wako wapi?
Kiukweli waliopita hizo shule wamejaa serikali na wengine ni mafisadi haina maana kuwa waliopita hizo shule ndiyo wana akili sana hapana ni mbeleko tu.
 
Shule zote za Mwanza ulizozitaja tulikuwa tunazipiga gap ile mbaya kwenye mitihani ya Mock! Miaka hiyo ya '90s nakushangaa unapotuita vilaza wakati mlikuwa hamwoni ndani kwenye mitihani!!! Hizo shule sasa hivi zimebaki jina tu hazina lolote la kujivunia sasa hivi! Pamoja na kutosoma shule hizo sasa hivi tunapiga maisha kama kawaida!!
 
Shule zote za Mwanza ulizozitaja tulikuwa tunazipiga gap ile mbaya kwenye mitihani ya Mock! Miaka hiyo ya '90s nakushangaa unapotuita vilaza wakati mlikuwa hamwoni ndani kwenye mitihani!!! Hizo shule sasa hivi zimebaki jina tu hazina lolote la kujivunia sasa hivi! Pamoja na kutosoma shule hizo sasa hivi tunapiga maisha kama kawaida!!
Sijaiona Lake Secondary ya Magadula R.I.P kuna mdogo wangu alikuwa anasoma pale alinisumbua sana miaka ya 90s.
 
Back
Top Bottom