Sherehe za Uhuru: Mkapa hakutokea tena

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Dar yaombwa kujitokeza sherehe za Uhuru
Godwin Myovela
Daily News; Saturday,December 06, 2008 @00:03

Wananchi wameombwa kujitokeza kwa wingi katika sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya Uhuru wa Tanganyika zitakazofanyika kwenye Uwanja wa Taifa wa zamani Dar es Salaam, Jumanne ijayo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro, alitoa mwito huo jana, ambapo alisema milango ya Uwanja wa Taifa itakuwa wazi kuanzia saa 12:00 asubuhi, na mgeni katika sherehe hizo atakuwa ni Rais Jakaya Kikwete.

“Nachukua nafasi hii kuwaalikeni mhudhurie kwa wingi kwenye sherehe hizi, ambazo safari hii zitapambwa na gwaride maalumu la majeshi yetu ya ulinzi na usalama, ambayo Rais atapata fursa ya kuyakagua,” alisema.

Aidha, alisema kutakuwa na halaiki iliyoandaliwa na wanafunzi takribani 2,000, ngoma za asili na michezo mingine mbalimbali. Aliwataka pia wamiliki wa vyombo vya usafiri hasa daladala, kuyaelekeza mabasi yao njia ya kwenda Uwanja wa Taifa ili kufanikisha maadhimisho hayo pamoja na kuwawezesha wananchi kushiriki katika tukio hili maalumu na la kihistoria.

Aidha, alitoa mwito kwa viongozi wa madhehebu ya dini, wazee, viongozi wa serikali, wakuu wa idara za serikali, taasisi, mashirika ya umma na viwanda, kuhamasisha waumini wao kuhudhuria kwenye maadhimisho hayo. Tanganyika ilipata Uhuru wake Desemba 9, 1961 kutoka kwa wakoloni wa Uingereza.
 
Last edited by a moderator:
Kesho kutwa tunatimiza miaka 47 toka Tanganyika ilipopata uhuru wake na baadae kuungana na kuwa Tanzania. Hapa kuna watu wenye elimu,ufahamu,ujuzi na kumbu kumbu za kila aina. Naona ni vyema,ukiona inafaa,ukachangia tuna kipi cha kijivunia na unawashauri nini wakuu wetu mpaka hapa tulipofikia? Unapongeza nini na unaona nini kifanyike ili kuboresha uhuru wetu?Wapi parekebiswe?
 
Wakuu,

Happy Indepenence day.Ni miaka Arobaini na saba kamili tangu Tanzania ijipatie uhuru wake. Heshima kubwa ni kwa mashujaa wataifa hili walio hai na waliotangulia mbele ya haki.Wapumzike kwa Amani

Tuakae tuatafakari kama kweli madhmuni ya mashujaa wetu na kile walichopigania kimetimia Au kuna dalili ya kutimia? Tumebakiza miaka mitatu tuadhimishe miaka hamsini ya kuwa huru kibendera.

Kila nikifikiria hivyo nakua na uchungu sana,tujaribu kuwa na mjadala wenye nia ya kusahihisha makosa yetu ili tupige hatua.Hivi leo hii matunda ya uhuru yanamnufaisha kila mtanzania?
 
LEO, Watanzania kote nchini wanaadhimisha miaka 47 tangu taifa letu lipate uhuru Desemba 9, mwaka 1961, kutoka kwenye ukoloni wa Waingereza, uliotanguliwa na ukoloni wa Wajerumani.

Kwetu sisi, heri na fanaka za uhuru tunaousherehekea leo, ni matokeo ya jitihada za wahenga wetu, waliokuwa wa kwanza kutabiri ujio wa wakoloni na hatimaye wakapambana na kumwaga damu kwa manufaa ya vizazi vya leo na vijavyo.

Ni matokeo ya jitihada za mashujaa wa vita ya Maji Maji na wale wote waliopinga ukoloni katika maeneo yao, kina mtemi Mkwawa, Mirambo, Isike, Makunganya, Mangi Meri, Bwana Heri na wengineo ambao damu yao ilikuwa chachu iliyosababisha kupatikana kwa Tanzania huru.

Ni matokeo ya juhudi za waasisi wetu wa chama cha siasa cha wakati huo ‘Tanganyika National Union (TANU)', kilichopigania uhuru kwa amani na mafanikio, chini ya uongozi, wa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere – Baba wa Taifa huru la Tanzania.

Tunapokumbuka na kuthamini mchango wa wale wote waliotimiza wajibu wao wakati huo, tuamini kuwa nasi tunaweza kuutumia wajibu huo kama funzo, katika kukabiliana na changamoto za leo na kesho ili taifa letu lisitopee kwenye utumwa.

Ikumbukwe kuwa taifa letu mara baada ya kupata uhuru lilikuwa na ndoto kuu tatu, nazo ni kutokomeza ujinga, umaskini na maradhi – kutimia kwa ndoto zote hizi kwa pamoja kungetufanya kuwa taifa lililoendelea na linalojitegemea.

Tunakiri kuwa taifa tulilonalo leo si lile la wakati wa uhuru, ni dhahiri kuwa tumepiga hatua, kijamii, kiuchumi na kisiasa – amani, umoja na mshikamano, ni vielelezo vya baadhi ya mafanikio ambayo taifa limepata na kuyadumisha tangu uhuru.

Hata hivyo, hatua tuliyopiga kimaendeleo kama taifa haiwiani hata kidogo na uhuru wetu wa miaka 47, maendeleo yetu yamekuwa ya kusuasua, kwa kiasi kikubwa tumeshindwa kuutumia uhuru wetu kupunguza umaskini.

Ieleweke kuwa sisi ni moja ya nchi 10 zilizo maskini kabisa duniani, kwa kipimo cha kimataifa cha umaskini, asilimia 57.8, sawa na watu milioni 20.2, wanaishi chini ya dola moja ya Marekani kwa siku, na asilimia 89.9, sawa na watu milioni 31.5, wanaishi chini ya dola mbili za Marekani kwa siku.

Kutokana na kasi yetu ndogo ya maendeleo, tafiti zinakadiria kwamba kwa kasi ya sasa ya ukuaji wa uchumi kwa asilimia sita kwa mwaka, italichukua taifa miaka 18 zaidi kuweza kuwanyanyua wananchi kutoka kwenye wastani wa kipato cha chini ya dola moja za Marekani kwa siku hadi kufikia dola mbili za Marekani kwa siku.

Tungependa Watanzania waelewe kuwa kama hawatachukua hatua za makusudi katika kuchochea uwajibikaji na ufanisi, hata baada ya miaka hiyo 18, bado watakuwa ni maskini, kwani hata wakipata uwezo wa kuishi chini ya dola mbili kwa siku, karibu sawa na shilingi elfu mbili, hawataweza kujikimu kikamilifu.

Tunaamini kuwa ili ndoto ya uhuru iweze kutimia, kuna haja ya msingi ya kuutazama upya mfumo wetu wa utawala, kujua ni kwanini umeshindwa kutupatia maendeleo ya haraka licha kuwa na rasilimali za kutosha na uhuru wa miaka 47.

Tanzania huru yenye maendeleo na inayojitegemea inawezekana, kila mtu atimize wajibu wake.
 
LEO, Watanzania kote nchini wanaadhimisha miaka 47 tangu taifa letu lipate uhuru Desemba 9, mwaka 1961, kutoka kwenye ukoloni wa Waingereza, uliotanguliwa na ukoloni wa Wajerumani.

Kwetu sisi, heri na fanaka za uhuru tunaousherehekea leo, ni matokeo ya jitihada za wahenga wetu, waliokuwa wa kwanza kutabiri ujio wa wakoloni na hatimaye wakapambana na kumwaga damu kwa manufaa ya vizazi vya leo na vijavyo.

Ni matokeo ya jitihada za mashujaa wa vita ya Maji Maji na wale wote waliopinga ukoloni katika maeneo yao, kina mtemi Mkwawa, Mirambo, Isike, Makunganya, Mangi Meri, Bwana Heri na wengineo ambao damu yao ilikuwa chachu iliyosababisha kupatikana kwa Tanzania huru.

Ni matokeo ya juhudi za waasisi wetu wa chama cha siasa cha wakati huo ‘Tanganyika National Union (TANU)’, kilichopigania uhuru kwa amani na mafanikio, chini ya uongozi, wa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere – Baba wa Taifa huru la Tanzania.

Tunapokumbuka na kuthamini mchango wa wale wote waliotimiza wajibu wao wakati huo, tuamini kuwa nasi tunaweza kuutumia wajibu huo kama funzo, katika kukabiliana na changamoto za leo na kesho ili taifa letu lisitopee kwenye utumwa.

Ikumbukwe kuwa taifa letu mara baada ya kupata uhuru lilikuwa na ndoto kuu tatu, nazo ni kutokomeza ujinga, umaskini na maradhi – kutimia kwa ndoto zote hizi kwa pamoja kungetufanya kuwa taifa lililoendelea na linalojitegemea.

Tunakiri kuwa taifa tulilonalo leo si lile la wakati wa uhuru, ni dhahiri kuwa tumepiga hatua, kijamii, kiuchumi na kisiasa – amani, umoja na mshikamano, ni vielelezo vya baadhi ya mafanikio ambayo taifa limepata na kuyadumisha tangu uhuru.

Hata hivyo, hatua tuliyopiga kimaendeleo kama taifa haiwiani hata kidogo na uhuru wetu wa miaka 47, maendeleo yetu yamekuwa ya kusuasua, kwa kiasi kikubwa tumeshindwa kuutumia uhuru wetu kupunguza umaskini.

Ieleweke kuwa sisi ni moja ya nchi 10 zilizo maskini kabisa duniani, kwa kipimo cha kimataifa cha umaskini, asilimia 57.8, sawa na watu milioni 20.2, wanaishi chini ya dola moja ya Marekani kwa siku, na asilimia 89.9, sawa na watu milioni 31.5, wanaishi chini ya dola mbili za Marekani kwa siku.

Kutokana na kasi yetu ndogo ya maendeleo, tafiti zinakadiria kwamba kwa kasi ya sasa ya ukuaji wa uchumi kwa asilimia sita kwa mwaka, italichukua taifa miaka 18 zaidi kuweza kuwanyanyua wananchi kutoka kwenye wastani wa kipato cha chini ya dola moja za Marekani kwa siku hadi kufikia dola mbili za Marekani kwa siku.

Tungependa Watanzania waelewe kuwa kama hawatachukua hatua za makusudi katika kuchochea uwajibikaji na ufanisi, hata baada ya miaka hiyo 18, bado watakuwa ni maskini, kwani hata wakipata uwezo wa kuishi chini ya dola mbili kwa siku, karibu sawa na shilingi elfu mbili, hawataweza kujikimu kikamilifu.

Tunaamini kuwa ili ndoto ya uhuru iweze kutimia, kuna haja ya msingi ya kuutazama upya mfumo wetu wa utawala, kujua ni kwanini umeshindwa kutupatia maendeleo ya haraka licha kuwa na rasilimali za kutosha na uhuru wa miaka 47.

Tanzania huru yenye maendeleo na inayojitegemea inawezekana, kila mtu atimize wajibu wake.

Uhuru ulipatikana sio kwa juhudi za wanasiasa wetu. Nchi zilizotutawala ziliona hakuna tena umuhimu wa kushikilia makoloni.
 
Uhuru ulipatikana sio kwa juhudi za wanasiasa wetu. Nchi zilizotutawala ziliona hakuna tena umuhimu wa kushikilia makoloni.

Nchi zilizotutawala zilitaka sana kuendelea kututawala, kuhamisha raslimali zetu kwenda kwao nk. Wanasiasa wetu walisimama kidete kupigania Uhuru kwa maslahi ya Taifa. Barani Afrika na kwingineko, wakoloni walitaka kuendelea kung'ang'ania kama kupe anavyong'ang'ania mwili wa ng'ombe. Wananchi walipigana na wengine kupoteza maisha, hadi wakafanikiwa kuwaondoa kupe wale!

Ni dhahiri, tangu nchi zilipojikomboa wakoloni wamekuwa hawalali usingizi wakitafuta mbinu za kurudi kwenye makoloni yao wakikumbuka jinsi walivyokuwa wakinufaika na kufaidi raslimali. Kwa sababu hiyo, ni dhahiri wameishaanza kurudi tena kwenye makoloni kwa mgongo wa 'utandawizi'.

Tukumbuke pia kwamba baada ya Uhuru wazungu waliihama nchi, ilikuwa nadra kuona sura ya mzungu mitaani. Walibaki wchache waliojitolea kusaidia na kulitumikia Taifa letu - akina Bryceson, Leader Sterling, Babra Johanneson, Joan Wicken, maburuda ..... nk. Mwenyezi Mungu awarehemu waliotangulia mbele ya haki na awabariki wanasiasa wote waliopigania Uhuru wa nchi yetu!
 

:eek:

9th.December, tunasherehekea uhuru wa Tanganyika 1961,

12th.January, Zanzibar husherehekea mapinduzi ya 1964

Nyie mnaosherehekea uhuru wa TANZANIA, mmeutoa wapi, lini na kwa nani?
 
Miaka 47 ya Uhuru...

1. Je ni uhuru upi ambao Watanganyika [Tanzania Bara] tunajivunia katika miaka yote hiyo?

2. Je bado tuna wakoloni humu nchini?

3. Mwelekeo wa Tanzania kwa ujumla, je ni wa kujivunia na je kila kitu ambacho Watanzania 'TUNAFAIDIKA NACHO' ni matunda ya Uhuru.

Kwangu mimi Binafsi leo ni siku ya majonzi, kusherehekea kuadhimisha miaka 47 ya Maisha Bora kwa 'Elite Few' kwa gharama ya jasho la wengine!!!!

Hapana!
 
Nchi zilizotutawala zilitaka sana kuendelea kututawala, kuhamisha raslimali zetu kwenda kwao nk. Wanasiasa wetu walisimama kidete kupigania Uhuru kwa maslahi ya Taifa. Barani Afrika na kwingineko, wakoloni walitaka kuendelea kung'ang'ania kama kupe anavyong'ang'ania mwili wa ng'ombe. Wananchi walipigana na wengine kupoteza maisha, hadi wakafanikiwa kuwaondoa kupe wale!

Ni dhahiri, tangu nchi zilipojikomboa wakoloni wamekuwa hawalali usingizi wakitafuta mbinu za kurudi kwenye makoloni yao wakikumbuka jinsi walivyokuwa wakinufaika na kufaidi raslimali. Kwa sababu hiyo, ni dhahiri wameishaanza kurudi tena kwenye makoloni kwa mgongo wa 'utandawizi'.

Tukumbuke pia kwamba baada ya Uhuru wazungu waliihama nchi, ilikuwa nadra kuona sura ya mzungu mitaani. Walibaki wchache waliojitolea kusaidia na kulitumikia Taifa letu - akina Bryceson, Leader Sterling, Babra Johanneson, Joan Wicken, maburuda ..... nk. Mwenyezi Mungu awarehemu waliotangulia mbele ya haki na awabariki wanasiasa wote waliopigania Uhuru wa nchi yetu!

Blah Blah:

Nchi za Afrika mashariki zilikuwa ni last frontier katika kutawaliwa na zikapata uhuru mapema na kuna nchi moja kama Ethiopia haikutawaliwa kabisa.

Tanganyika inapata uhuru ilikuwa na ma-settler chini ya 20,000. Na wakati wanaondoka kulikuwa na watu wengi bado hawaelewi mzungu anafananaje.

Ukiondoa watu wa Arumeru. Hakuna walionyang'anywa mashamba yao au mifugo yao kama ilivyotokea Africa kusini au Zimbwabwe.

Hivyo basi ukoloni uliokuwepo Tanganyika ulikuwa ni wa kijiografia tu kuwa eneo fulani liko chini ya himaya ya nchi fulani. Na kujivunia kuhusu kupigania uhuru ni siasa tu na ndio maana uhuru wenye hatuupi thamani.
 
Nchi zilizotutawala zilitaka sana kuendelea kututawala, kuhamisha raslimali zetu kwenda kwao nk. Wanasiasa wetu walisimama kidete kupigania Uhuru kwa maslahi ya Taifa. Barani Afrika na kwingineko, wakoloni walitaka kuendelea kung'ang'ania kama kupe anavyong'ang'ania mwili wa ng'ombe.

Lakini kwa sasa mbona sisi ndo tupo mstari wa mbele kuhakikisha ya kwamba rasilimali za Taifa hazitumiki kwa maslahi ya Taifa? Ni sisi pia ambao tumekuwa tumewang'ang'ania kama kupe hao ambao walikuwa watawala wetu na kuwahamasisha waje kuhamisha hizo rasilimali!!!

Kupewa uhuru na mzungu ili uje kutawaliwa na 'mkoloni' Mtanganyika ni the worst form of colonialism on earth.

Mabadiliko ya Kweli katika kila ngazi ndio yatakayotutoa kutoka katika hii 'Bottomless Pit!'
 
Lakini kwa sasa mbona sisi ndo tupo mstari wa mbele kuhakikisha ya kwamba rasilimali za Taifa hazitumiki kwa maslahi ya Taifa? Ni sisi pia ambao tumekuwa tumewang'ang'ania kama kupe hao ambao walikuwa watawala wetu na kuwahamasisha waje kuhamisha hizo rasilimali!!!

Kupewa uhuru na mzungu ili uje kutawaliwa na 'mkoloni' Mtanganyika ni the worst form of colonialism on earth.

Mabadiliko ya Kweli katika kila ngazi ndio yatakayotutoa kutoka katika hii 'Bottomless Pit!'

Uhuru katika mazingira ambamo raia hawawezi kupata huduma za kiserikali ni sawa na kutokuwapo uhuru.
 
Naona miaka 47 baadaye bado hatujawa na msamiati makini wa kuzungumzia huu (au huo) UHURU. Tulipewa UHURU? Kwani tuliuomba?

Kama tulipigania UHURU, basi labda Desemba 9 1961 tulinyakua UHURU? Rais wa Kwanza wa Kenya (Jomo Kenyatta) alitumia msamiati huo wa kunyakua UHURU.

Tulipata uhuru? Kupata hapa kuna maana gani?

Desemba 9 1961 tulifikia UHURU? Kwani tulikuwa bado kufikia hali ya kuwa HURU au tulinyimwa tu UHURU kabla ya hapo?

Tunao bado UHURU? Kama ukiisha ni nini kitabadilika? Unaweza kwisha?

Mimi napendelea zaidi msamiati wa kutwaa UHURU. Tuliutwaa UHURU wetu Desemba 9 1961. Tulikuwa nao siku zote, lakini ulikuwa unakaliwa na watu wengine. Tarehe hiyo ilipofika, tuliutwaa.
 
Napendekeza Mramba na Yona wapewe nafasi uwanja mkuu wa taifa watueleze matunda ya uhuru. Wao wenzetu ndiyo walionufaika na matunda ya uhuru wa Tanganyika mpaka wanaweza kujidhamini wao wenyewe kwa nyumba yenye thamani ya bilioni 2 na ushee. Sisi wengine tupo bado kwenye machungu tukitafuta uhuru wetu wa kiuchumi uliopokwa na Bwana Mramba, Yona na mafisadi wenzao.
 
Uhuru hatukuutwaa/pata/pewa/nyakua 1961 maana bado Malkia alikuwa ndio Mkuu wa Nchi yetu na Nyerere alikuwa ni mwakilishi wake!
 
Rais Mstaafu Mkapa hajahudhuria Sherehe za Uhuru.

May be yupo nje ya nchi au mgonjwa.
 
FYI: Muungwana wakati anapokea madaraka toka kwa Mjasililiamali aliachiwa Mercedes Benz mpya Limosine. Naona sasa anatumia BMW.
 
Mpaka sasa, ITV wanaonekana kwa Quality nzuri kuliko TBC1 na StarTv. Quality ya matangazo ya TBC1 (ambapo ndipo Channel 10 wamechukua matangazo) si nzuri. Inaelekea camera zimewekwa eneo lisilo zuri kabisa.

StarTv naona nao wameshindwa ku-control lights
 
JK kasalimiana na waliokaa Jukwaani baada ya kupigiwa mizinga 21 pamoja na wimbo wa taifa kuimbwa lakini kilichowafurahisha wengi ni yeye kusalimiana na Mama Salma Kikwete.

Gwaride linaanza
 
Back
Top Bottom