Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,730
- 218,292
.
Sherehe za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar zingali zikiendelea huko visiwani , ambapo sherehe hizo kabambe zimefanyika kwenye Uwanja wa Aman, Gwaride Maalum na Hotoba za viongozi zimesikika .
Jambo kubwa la kufurahisha ni uwepo wa Watanganyika wengi kuliko wakati wowote tangu sherehe hizo zianze kufanyika miaka mingi iliyopita, Taarifa zisizo rasmi zinaeleza kwamba karibu nusu ya waliokuwa uwanjani hapo wametokea Tanganyika na labda viongozi wote wa serikali upande wa Tanganyika walikuwa uwanjani humo Wakiwemo hadi viongozi wa chini kama MA DC na MA RC, si wa sasa wala si wastaafu , Hakika jambo hili linahiraji kupongezwa.
Wafanyabiasha karibu wote wakubwa wa kutoka Tanganyika wameonekana Mjini Unguja , hili jambo ni la kupigiwa mfano.
Natoa pongezi kwa Kamati ya Maandalizi kwa mafanikio haya.