Wakuu heshima kwenu,
Mkuu Jasusi kagusia kidogo sensa ya mwaka 1967 ngoja niwawekee kwa faida ya mjadala.
Takwimu ya dini
[hariri] Sensa ya 1967
Takwimu ya
dini nchini Tanzania kwa sasa haipatikani kwa sababu maswali kuhusu dini yaliondolewa na serikali katika sensa baada ya mwaka
1967. Sensa ile ya tarehe
27 Agosti ilihesabu wafuasi wa dini za jadi kuwa 34.3%, Wakristo 33.5% na Waislamu 31.4%, mbali na wengineo 0.8%.[SUP]
[1][/SUP]
[hariri] Namba zenye athira ya kisiasa
Tangu mwaka ule swali la takwimu ya kidini Tanzania limejadiliwa sana inaonekana ni swali lenye uzito wa kisiasa pamoja na upande wake wa kitaalamu.
Kwa miaka mingi makadirio ya kawaida yalikuwa Watanzania ni theluthi 1 wafuasi wa dini za jadi, theluthi 1 Waislamu na theluthi 1 Wakristo.[SUP]
[2][/SUP]
Lakini ni wazi ya kwamba dadi ya wafuasi wa dini za jadi imeendelea kupungua. Baadhi ya viongozi na wanaelimu-jamii wanakadiria kwamba jumuia za
Kikristo na
Kiislamu zipo sawa tu kwa ukubwa, zote huhesabiwa kiasi cha asilimia 30 hadi 40 kwa idadi ya wakazi, na waliosalia ni waumini wa
imani zingine,
dini za jadi, na wale wasio na
dini kabisa.
Lakini wataalamu wengine wanasema uwiano huo unashikiliwa kisiasa kwa sababu uhusiano kati ya Wakristo na Waislamu ni jambo la siasa ya taifa kwa hiyo makadirio yanaelekea kutaja uwiano sawa kati ya pande hizi mbili.[SUP]
[3][/SUP]
[hariri] Mifano ya makadirio mbalimbali
Kwa hiyo namba zote kuhusu takwimu ya dini nchini Tanzania ni makadirio tu hakuna namba za kutegemea. Vyanzo vinavyotaja namba vinatofautiana sana mara nyingi kufuatana dini ya wahariri.
- "World Christian Encyclopedia" (toleo la pili, Oxford 2001) imekadiria kwa mwaka 2000 Wakristo kuwa 50.4 % (Wakatoliki 24.7%, Waprotestanti mbalimbali 16.5%, Waanglikana 7.9%, wasio na madhehebu maalumu 3.5%, madhehebu huru 1.9%, madhehebu yasiyokubali imani ya msingi ya Wakristo wengine wote 0.1%, wenye kufuata madhehebu mawili kwa wakati mmoja 4.2%), Waislamu 31.8%, wafuasi wa dini za jadi 16.1% na wengineo 1.8%. Pia imetabiria kwa mwaka 2025 uwiano kuwa 56.1, 32.8, 8.9 na 2.1%, na kwamba kufikia mwaka 2050 Wakristo na Waislamu watakuwa karibu 65 na 35% kati ya wakazi wa nchi.
- Takwimu zinazoonyeshwa na Waislamu hudai kundi kubwa la Watanzania kuwa Waislamu wakiwa na asilimia 50 - 60 za watu wa nchi [SUP][5][/SUP]
- Kuna shirika za Kiislamu zinazotabiri Tanzania itakuwa nchi ya Waislamu wengi mnamo mwaka 2020 [SUP][6][/SUP]
Pande zote zinarejea takwimu za kuongezeka za watu katika maeneo fulani wakiongeza makadirio yao juu ya matokeo kwenye namba za kidini.
Source; wikipedia.