Ninacho kiona kwa huyu Sheikh na wengine wenye mtazamo kama wake ni kutaka kila kitu cha dini yake kifanywe na serikali, mfano, wanasema Mahakama ya Kaadhi ni sehemu ya ibada yao lakini igharamikiwe na serikali, hivi inaingia akilini serikali igharamie ibada ya dini? mara uongozi uwe wa kuachiana, wa dini hi kipindi hiki na kipindi kingine dini nyingine, sasa hapa kuna mtego wanataka kuutega, issue hapa wanataka kujua Waislam wako wangapi? mi sidhani kama ni hii ni kazi ya serikali, hi ni kazi ya masheikh kama yeye, conduct your own Censor ili mjue mko wangapi? Ninahakika kama Kadinari Pengo anataka kujua kuna wakatoriki wangapi hapa nchini, ni yeye kuwasiliana na maaskofu wake ambao nao watashuka kwa mapadre then atajua tu wako wangapi, hali kadhalika Anglican, Lutheran Walokole kwa madheebu yao the same, hivi nyie waislam mnashindwa nini kufjua idadi yenu hadi serikali iwafanyie?
Kigezo kwamba dini zingine zinafanyaje nadhani si issue, kuna serikali humu duniani zina sheria ya kuruhusu mashoga, je na siye tu copy toka kwao? kuna nchi waislam hawaruhusiwi kuvaa Hijabu, tukopi na hiyo pia? Hebu tuwe realistic na masuala common na muhimu kwa nchi yetu, umasikini ni mkubwa sana Tanzania ambao kimsingi haungalii dini ya mtu, tuwekeze nguvu zetu huko, mlitaka rais mwislam, naye mmempata then mnakuja na story nyingine, ninahakika mkikubaliwa hili na la Kaadhi, kesho mtasema kuhiji Makka ni ibada, serikali iwagharamikie.