Sheikh Ponda yuko sahihi

Sheikh Ponda yuko sahihi

It doesn't make any sense
....... may be..... lakini huo ulikuwa ni mfano tuu... Ukifikiri watu wote tuko sawa...lakini kuna vitu vinavyomtofautisha mtu mmoja hadi mwingine kama vile majina, kabila ,imani(dini) na hizi tofauti husaidia katika mambo mengine kuweza kufanyika. Tutakuona una akili ajabu kama kama ukienda kufungua duka la nyama ya ngombe katika sehemu ambayo idadi kubwa ya watu kutokana na imani yao hawatumii nyama ya ng'ombe......au ukiwa kama daktari umshauri mgonjwa muislam wako atumie mafuta ya nguruwe ili aweze kupona ugonjwa wake wa ngozi. Kwa kuhitimisha takwimu zinazomtofautisha mtu mmoja na mwingine si za kupuuza..... cha msingi ni kutukiwa katika kuboresha hali fulani....
 
Kuna kitu kimejificha hapo.

Mbona mkiwa mnatoa maelezo Polisi mnaandika sio tu kabila mpaka dini mnabainisha. Kwenye vitabu vya wageni hotelini na nyumba za kulala wageni mbona kunakipengele cha dini na kabila. Kwanini msikiweke hata kwenye sensa zenu.

Nafikiri kiuchumi wanazuia kuona ni misada au misamaha ya kodi kiasi gani wanayopata dini moja dhidi ya zingine na kunufaika kwa namna gani kiuchumi dhidi ya wengine.

Kuna mengi sana . Lakin msingi mkuu ni mipango ya nchi yenu kuweka usawa wa kitabaka na kijamii kwa kupata taarifa sahihi ndani ya sensa.
hivi Barubaru na kusoma kwako unaona madai ya Ponda ni halali? yaani ni sawa na mtu asiye kwenda shule akueleza suala la takwimu, uchumi sayansi nk.
mimi ninaona wewe ungefaa saana kuwa kiongozi wao kuliko huyo Ponda, ndio maana waislamu walio enda shule unawaona wapo kimya kuhusu suala hili.
na Jasusi kasema kipengele cha dini usa hakuna. na zaidi ya hapo mazingira yetu na nchi zingine ni tofauti moja ikiwa elimu na jingine suala la kiuchumi, hivyo basi focus yetu ipo huko.
 
Kuna kitu kimejificha hapo.

Mbona mkiwa mnatoa maelezo Polisi mnaandika sio tu kabila mpaka dini mnabainisha. Kwenye vitabu vya wageni hotelini na nyumba za kulala wageni mbona kunakipengele cha dini na kabila. Kwanini msikiweke hata kwenye sensa zenu.

Nafikiri kiuchumi wanazuia kuona ni misada au misamaha ya kodi kiasi gani wanayopata dini moja dhidi ya zingine na kunufaika kwa namna gani kiuchumi dhidi ya wengine.

Kuna mengi sana . Lakin msingi mkuu ni mipango ya nchi yenu kuweka usawa wa kitabaka na kijamii kwa kupata taarifa sahihi ndani ya sensa.
Mkuu Barubaru, kwa akili yako na elimu yako ya PhD bado unaamini misaada ni njia ya kujiletea maendeleo!
 
The guilty are afraid!
Nchi hii inaenda vibaya, tuna hila nyingi ndiyo maana tunaogopa vivuli vyetu. Malizeni hilo maana na mimi nafikiria kuhamasisha Maandamano kama mtaacha kipengele cha jinsia ambacho kila mtu anajua kinachochoea mfumo dume
 
hawa wenzetu huwa nakuwa na wasiwasi nao juu ya uwezo wao wa kufikiri


inabidi kuwe pia na kipengere cha mvuto(sura)...ili tujue wangapi ni mahandsome/beautifull na wangapi ni ugly,.....argrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrh
 
Narudia kama huna vigezo hupati kazi sio dini wala kabila. Kaangalie NSSF kuanzia mfagizi hadi GM wao ni Muislamu Hr tu hua anaenda kuhiji kila mwaka na hela za wazee wetu na kuna utaratibu wa kubebana dini hiyo na ndo maana mchakato wa Interview iliyopita tulipewa number ila wakatuambia tuandike majina kwenye karatasi ya kujibia..........!

Si kwamba mnabaguliwa kama mnavyojiona, ni kwamba mlichelewa shule kwa kukariri vitabu vya dini pekee na kusahau shuleni kuna nini. kUBALINI UKWELI na mfukie mashimo sio kubebana kusiko na misingi. Kama mnataka kujua idadi yenu ni simple kila msikiti ulete waumini wake na kinachobaki ni kujumlisha tu. Hakuna hata haja ya kulalama kwa mambo yasiyo na msingi hasa katika Taifa linalotaka jikomboa kwenye umasikini. Sensa ni kwa ajiri ya kufanya maendeleo kulingana na mgawanyo wa watu (population) sio dini ya mtu na mtu.

Keki gani mnayolalamiaka wakristu wanapewa na nyie kunyimwa? coz mnasemasema tu bila kutaja hasa ni kipi. Shehk mkuu wenu anatembelea STK na hakuna anaejali na haipo popote katika katiba ya Tanzania. Tazama fikra zako usikubali kudanganywa hata kama wew ni mjinga......
 
....... may be..... lakini huo ulikuwa ni mfano tuu... Ukifikiri watu wote tuko sawa...lakini kuna vitu vinavyomtofautisha mtu mmoja hadi mwingine kama vile majina, kabila ,imani(dini) na hizi tofauti husaidia katika mambo mengine kuweza kufanyika. Tutakuona una akili ajabu kama kama ukienda kufungua duka la nyama ya ngombe katika sehemu ambayo idadi kubwa ya watu kutokana na imani yao hawatumii nyama ya ng'ombe......au ukiwa kama daktari umshauri mgonjwa muislam wako atumie mafuta ya nguruwe ili aweze kupona ugonjwa wake wa ngozi. Kwa kuhitimisha takwimu zinazomtofautisha mtu mmoja na mwingine si za kupuuza..... cha msingi ni kutukiwa katika kuboresha hali fulani....

Hayo yote walisha analyse wakubwa wakaona alot of confusions exists unapoingiza swala la udini kwenye mipango ya nchi.kulingana na Sheikh Ponda anadai waislamu wamebaguliwa kwenye mgawanyo wa national cake,ina maana kuwa kwenye ajira za nchi hii waislamu wanawekwa pembeni.Hii siyo sahihi hata kidogo kwani unapoongelea swala la ajira ni kwamba ajira zinatolewa kwa ushindani.mwajiri anataka yule best candidate ndio atapewa kazi.kama ukija kupitia takwimu na kukuta waislamu ni wachache kwenye ajira ya serikali ina maana gani ni kwamba si wazuri katika soko la ajira,yaani hawana ushindani.Kwa vile mwajiri lengo lake ni kupata mtu aliye mzuri ili aje asaidie kutimiza malengo yake, ni lazima atachukua the best candidate bila ya kuangalia other criteria.Huwezi ukaacha watu wazuri kwenye soko ukachukua wabovu eti tu kwa vile ni waislamu.Chukulia wewe una biashara yako ya usafirishaji,unataka kuajiri dereva,wewe ni muislamu wamekuja watu wawili ambao mmoja ni muislamu na mwingine ni mkristo.Katika uchunguzi wako pamoja na interview ulizo wafanyia hawa watu wawili you are certain kuwa yule mkristo ni dereva mzuri kuliko yule muislamu.Na kuna all indications kwamba ukimuajiri huyo muislamu hata kaa muda mrefu kabla hajaibinua hiyo gari.Yule mkristo anautulivu wa hali ya juu na ni mjuzi kwelikweli wa kuendesha magari.Je uta opt kuajiri muislamu mwenzako katika biashara yako kwa sababu tu ni muislamu,bila kujali hasara utakazopata kwenye biashara hiyo ambayo mtaji wake umekopa bank na umeweka nyumba yako kama colateral.

 
Mkuu Barubaru, kwa akili yako na elimu yako ya PhD bado unaamini misaada ni njia ya kujiletea maendeleo!

Kumbuka kujitegemea sio kujitenga. Misaada ni sehemu au chachu ya kuharakisha maendeleo kama misaada hiyo itatumika vizuri kwa ajili ya makusudia yaliyokusudiwa.

Ukitaka kuliona hilo naomba upitie bajeti zenu za miaka mitatu kipengele cha misamaha yakodi kwa taasisi na NGO za kidini utaliona hilo.

Nakuomba upitie jedwali zima kisha utaliona na kukubaliana na mimi.
 
Sensa ya mwaka 1967 ilionyesha kuna wakristo wangapi, waislamu wangapi, na wapagani wangapi. Tunaweza kuanzia hapo. Mambo ya kuhesabu watu kwa dini zao hayana tija katika serikali ambayo haina dini.

Kenya baada ya kuuana kwa ukabila,wameweka kwenye katiba yao makabila yote na dini zote na kuweka kipenegele kinachozuia mahala popote pa ajira za serikali kuwa na idadi ya kabila moja zaidi ya robo tatu
 
Nafikiri imefika wakati kila mtu mwenye akili timamu kukemea hii non sense na hawa akina ponda. Mimi nishangaa serikali kwa nini inamfumbia macho mrundi huyu. Mna agenda gani na mrundi huyu? Hivi waislamu mnataka tuamini maneno anayosema ponda mnakubaliana nayo???????? Unajua kuna mambo mtu mzima anaongea unajiuliza alimaliza kunyonya lini maana kama ameanza angalau kutembea hawezi kuwa na akili hizi. Hivi kujua waislamu wako wangapi kwenye sensa inatusaidia nini? Wanaotetea wazo hili watuambie na sisi tujue!!!!!! Ponda anajua maana ya sensa? Moja ya kazi ya data za sensa ni kujua namna ya kugawa raslimali za nchi kwa usawa. Je idadi ya waislamu inatusaidiaje hapa? au kwenye elimu, afya, miundo mbinu n.k. Kuna huduma za waislamu peke yao na wakristo peke yao? Au kuna agenda ya siri kuhusiana na suala la Ponda? Kwani Zanzibar walitumia kigezo cha katiba wakachoma makanisa, kwa mtindo huo anataka kutumia kigezo cha sensa achome makanisa huku bara. This time we are fed up, kama akileta huo ujanja wake hatutavumilia. Wakristo tumevumilia sana vitendo hivi vya kijinga. Tumechoka, enough is enough.
Suala la ajira, aliyekuwa katika Wizara hiyo kwa muda mrefu (Hawa Ghasia) alikuwa mkristo? Rais wa nchi hii ambaye ndiye mwajiri mkuu ni mkristo? Makamu wa Rais ni Mkristo? Acheni majungu na kuunga mkono mawazo ya watu wajinga. Natamani kujua elimu ya Ponda maana sitaki hata kumwita sheikh kwani naamini sheikh ni mtu mwadilifu, mcha Mungu si mtu mhuni anayetamani kuona watu wakimwaga damu kwa mambo ambayo hayana tija kwa nchi yetu. Mgawanyo wa ajira unafanywa kwa kutumia dini? Haya mambo gani ya ajabu haya? Kwa hiyo kama umesoma sana dini ya kiislamu hata kama huna qualification upewe ajira? Hivi ambao wasimamia ajira wote ni wakristo?
Nafikiri ifike mahali waislamu wakatae watu kama Ponda kwani wanafika mahali wanawadhalilisha waislamu ambao mimi ninaamini ni watu wenye akili safi na wanaofahamu ukweli wa kila jambo.
 
juzi Sheikh Ponda Issa ambaye ni katibu wa Jumuiya ya Kutetea Haki za Waislamu alitanabahisha kuwa iwapo serikali haitoweka kipengele cha dini katika fomu za sensa ya mwaka, jumuiya yao itahamasisha Waislamu wasishiriki katika zoezi la sensa.Alisema kuwa nchi hii siyo ya Kikristo lakini INATAWALIWA NA MFUMO KRISTO. alisema kutokana na mazoea, Waislamu wanabaguliwa katika mgawanyo wa keki ya taifa khasa upande wa ajira. ofisi na idara za serikali zinaongozwa na Wakristo kwa asilimia kubwa kulinganishwa na waislamu. alitoa mfano wa TRA, NECTA, Wizara ya Eimu, Wizara ya Ujenzi, Afya, Mahakama nk........... kwa mujibu wa Sheikh Ponda, wastani wa ajira ni karibu Wakristo 77% na Waisalmu siyo zaidi ya asilimia 20%. Licha ya hoja inayojengwa kuwa Waislamu hawajasoma lakini akasema waliosoma wapo. akatanabahisha kuwa kwa maslahi na umoja wa kitaifa, kupuuza watu ambao ni sehemu ya jamii ktk keki ya taifa ni jambo hatari sana! kwa kuwa wtu wanadai waislamu ni chini ya 20% katika nchi hii, akapendekeza sensa ya mwaka huu kiwekwe kipengele cha dini ili idadi ya watanzania kidini ijulikane. Kwa mujibu wa Sheihk Ponda, anaamini kuwa waislamu ni takriban 64% ya rais wa Tanzania. "SIYO SAHIHI WATU WENYE IDADI HII KUPUUZWA KATIKA UWIANO WA AJIRA SERIKALINI", alisema Sheikh Ponda.Alitoa mifano wa nchi karibia zote za Ulaya, Marekani, asia pamoja na Afrika, kipengele cha dili kipo kwenye fomu za sensa zao. "Ukisoma country profile au fact file uingiapo katika nchi mbalimbali, utakuta wameandika wastani wa idada ya raia kidini" alisisitiza Ponda. "Mbona mnajifanya kama hamtembei au hamjui kinacho endelea ulimwengunu jamani!" alilalama Ponda.HOJA YANGUNdugu znaguni Watanzania, tufike sehemu tuache ukweli udhihiri. kama Waislamu wanalalamika kuwa wanabaguliwa katika ajira labda kutokana na uchache wao, kwa nini suala la dini lisiwekwe wazi? au utakua udini? au uchochezi? au uvunjifu wa amani? kama ni hivyo, mbona karibu 98% ya sensa zote duniani zina kipengele cha dini!? je huko wameuana kutoakana na kipengele hicho? TUBADILIKE!!!!!!!!naomba kuwasilisha!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Sasa ndio nimeamini baba wa taifa hili hayati Jullius Kambarage Nyerere aliondoka na Tanzania yake.Mwalimu alishalikemea hili mara nyingi awezavyo na matunda yake tumeyaona,Ila sasa huku tunakoelekea hakika tutalia.Hivi tukianza kuangalia vigezo vya dini ktk mgawanyiko wa kazi vipi kwa wale raia wasiokuwa na dini haki zao zitakuwa wapi?Wahenga walinena"Ndondondo sio chururu"tunaanza kidogo kidogo kuingiza udini ktk masuala ambayao sio ipo siku tutalia sbb haitoishia hapo mpaka vizazi vyetu vijavyo vitaathirika.
 
mbona nyie wagala mnaogopa sana hiki kipengele? Kuna nini kimejificha?
wala hatuogopi sema tumeshafikilia mbele zaidi na tunaona madhara yatakayojitokeza tukianza kuweka udini tatizo uwa hamfikilii mbele zaidi ndo mana hata mtawala wenu akuwaza kuwajengea shule mana akujua kama baadaye itakuja kuwa na umuhimu ila mtawala wetu aliona hivyo.

mimi nadhani wangewawekea kipengele cha elimu kwamba waislam wangapi wana elimu na wangapi hawana ili muweze kujikomboa kwenye elimu dunia na kupata vyeo ambavyo sisi mnaona tunapendelewa.

hivi leo tukisema wakristu wawasomeshe watoto wao kwenye shule zao na waislam wafanye hivyo patatosha kweli? na kila dini watibiwe kwenye hospital zao.

ikumbukwe nchi yetu haina udini na tukianza kufanya hivyo tunaukaribisha udini ambao sio mzuri, tafuteni njia sahihi ya kupata vyeo kama mnavyotaka lakini si kwa mabafu.
 
juzi Sheikh Ponda Issa ambaye ni katibu wa Jumuiya ya Kutetea Haki za Waislamu alitanabahisha kuwa iwapo serikali haitoweka kipengele cha dini katika fomu za sensa ya mwaka, jumuiya yao itahamasisha Waislamu wasishiriki katika zoezi la sensa.Alisema kuwa nchi hii siyo ya Kikristo lakini INATAWALIWA NA MFUMO KRISTO. alisema kutokana na mazoea, Waislamu wanabaguliwa katika mgawanyo wa keki ya taifa khasa upande wa ajira. ofisi na idara za serikali zinaongozwa na Wakristo kwa asilimia kubwa kulinganishwa na waislamu. alitoa mfano wa TRA, NECTA, Wizara ya Eimu, Wizara ya Ujenzi, Afya, Mahakama nk........... kwa mujibu wa Sheikh Ponda, wastani wa ajira ni karibu Wakristo 77% na Waisalmu siyo zaidi ya asilimia 20%. Licha ya hoja inayojengwa kuwa Waislamu hawajasoma lakini akasema waliosoma wapo. akatanabahisha kuwa kwa maslahi na umoja wa kitaifa, kupuuza watu ambao ni sehemu ya jamii ktk keki ya taifa ni jambo hatari sana! kwa kuwa wtu wanadai waislamu ni chini ya 20% katika nchi hii, akapendekeza sensa ya mwaka huu kiwekwe kipengele cha dini ili idadi ya watanzania kidini ijulikane. Kwa mujibu wa Sheihk Ponda, anaamini kuwa waislamu ni takriban 64% ya rais wa Tanzania. "SIYO SAHIHI WATU WENYE IDADI HII KUPUUZWA KATIKA UWIANO WA AJIRA SERIKALINI", alisema Sheikh Ponda.Alitoa mifano wa nchi karibia zote za Ulaya, Marekani, asia pamoja na Afrika, kipengele cha dili kipo kwenye fomu za sensa zao. "Ukisoma country profile au fact file uingiapo katika nchi mbalimbali, utakuta wameandika wastani wa idada ya raia kidini" alisisitiza Ponda. "Mbona mnajifanya kama hamtembei au hamjui kinacho endelea ulimwengunu jamani!" alilalama Ponda.HOJA YANGUNdugu znaguni Watanzania, tufike sehemu tuache ukweli udhihiri. kama Waislamu wanalalamika kuwa wanabaguliwa katika ajira labda kutokana na uchache wao, kwa nini suala la dini lisiwekwe wazi? au utakua udini? au uchochezi? au uvunjifu wa amani? kama ni hivyo, mbona karibu 98% ya sensa zote duniani zina kipengele cha dini!? je huko wameuana kutoakana na kipengele hicho? TUBADILIKE!!!!!!!!naomba kuwasilisha!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Sasa ndio nimeamini baba wa taifa hili hayati Jullius Kambarage Nyerere aliondoka na Tanzania yake.Mwalimu alishalikemea hili mara nyingi awezavyo na matunda yake tumeyaona,Ila sasa huku tunakoelekea hakika tutalia.Hivi tukianza kuangalia vigezo vya dini ktk mgawanyiko wa kazi vipi kwa wale raia wasiokuwa na dini haki zao zitakuwa wapi?Wahenga walinena"Ndondondo sio chururu"tunaanza kidogo kidogo kuingiza udini ktk masuala ambayao sio ipo siku tutalia sbb haitoishia hapo mpaka vizazi vyetu vijavyo vitaathirika.Hatuwezi kuendesha nchi kidini(Ukristo na Uislam)
 
Ninacho kiona kwa huyu Sheikh na wengine wenye mtazamo kama wake ni kutaka kila kitu cha dini yake kifanywe na serikali, mfano, wanasema Mahakama ya Kaadhi ni sehemu ya ibada yao lakini igharamikiwe na serikali, hivi inaingia akilini serikali igharamie ibada ya dini? mara uongozi uwe wa kuachiana, wa dini hi kipindi hiki na kipindi kingine dini nyingine, sasa hapa kuna mtego wanataka kuutega, issue hapa wanataka kujua Waislam wako wangapi? mi sidhani kama ni hii ni kazi ya serikali, hi ni kazi ya masheikh kama yeye, conduct your own Censor ili mjue mko wangapi? Ninahakika kama Kadinari Pengo anataka kujua kuna wakatoriki wangapi hapa nchini, ni yeye kuwasiliana na maaskofu wake ambao nao watashuka kwa mapadre then atajua tu wako wangapi, hali kadhalika Anglican, Lutheran Walokole kwa madheebu yao the same, hivi nyie waislam mnashindwa nini kufjua idadi yenu hadi serikali iwafanyie?

Kigezo kwamba dini zingine zinafanyaje nadhani si issue, kuna serikali humu duniani zina sheria ya kuruhusu mashoga, je na siye tu copy toka kwao? kuna nchi waislam hawaruhusiwi kuvaa Hijabu, tukopi na hiyo pia? Hebu tuwe realistic na masuala common na muhimu kwa nchi yetu, umasikini ni mkubwa sana Tanzania ambao kimsingi haungalii dini ya mtu, tuwekeze nguvu zetu huko, mlitaka rais mwislam, naye mmempata then mnakuja na story nyingine, ninahakika mkikubaliwa hili na la Kaadhi, kesho mtasema kuhiji Makka ni ibada, serikali iwagharamikie.

Haaaahaaaa! Unachosema sawa kabisa mkuu. Kuna watu hapa watadai nauli za kwenda makka maana wakirisitu wanawafanyia dhulma. Kuna vichwa vina very low thinking ability. Wanafikiria mambo magumu kama nimarahisi sana
 
Hivi nyinyi ndugu zetu mnafanya kazi kweli jamani mnapaa wapi muda wakueneza fitna kama hizi jamani jamanai du ,mimi nimewachoka sana hivi vitu ni muhimu mbona nikutoa ushauri tuu kwanini mtumie nguvu hivi eti hawatakubali kuhesabiwa du? Kwanini usishauri wewe sijui shehe mbina ni jambo zuri kwanini muanze kuweka vizuizi potelea mbali mhesabiwe msihesabiwe watakaohesabiwa poa ,nawachukia sana,na sijui hawa watu wenye elimu akhera huwaza kwakutumia nini mbona ni jambo rahisi na ungetoa kama ushauri ungeheshimika sana,
 
sasa ndio nimeamini baba wa taifa hili hayati jullius kambarage nyerere aliondoka na tanzania yake.mwalimu alishalikemea hili mara nyingi awezavyo na matunda yake tumeyaona,ila sasa huku tunakoelekea hakika tutalia.hivi tukianza kuangalia vigezo vya dini ktk mgawanyiko wa kazi vipi kwa wale raia wasiokuwa na dini haki zao zitakuwa wapi?wahenga walinena"ndondondo sio chururu"tunaanza kidogo kidogo kuingiza udini ktk masuala ambayao sio ipo siku tutalia sbb haitoishia hapo mpaka vizazi vyetu vijavyo vitaathirika.hatuwezi kuendesha nchi kidini(ukristo na uislam)

kwa nini mnaogopa kipengele hiki? Mna lenu jambo!
 
Wakuu heshima kwenu,

Mkuu Jasusi kagusia kidogo sensa ya mwaka 1967 ngoja niwawekee kwa faida ya mjadala.


Takwimu ya dini[h=3][hariri] Sensa ya 1967[/h]Takwimu ya dini nchini Tanzania kwa sasa haipatikani kwa sababu maswali kuhusu dini yaliondolewa na serikali katika sensa baada ya mwaka 1967. Sensa ile ya tarehe 27 Agosti ilihesabu wafuasi wa dini za jadi kuwa 34.3%, Wakristo 33.5% na Waislamu 31.4%, mbali na wengineo 0.8%.[SUP][1][/SUP]
[h=3][hariri] Namba zenye athira ya kisiasa[/h]Tangu mwaka ule swali la takwimu ya kidini Tanzania limejadiliwa sana inaonekana ni swali lenye uzito wa kisiasa pamoja na upande wake wa kitaalamu.
Kwa miaka mingi makadirio ya kawaida yalikuwa Watanzania ni theluthi 1 wafuasi wa dini za jadi, theluthi 1 Waislamu na theluthi 1 Wakristo.[SUP][2][/SUP]
Lakini ni wazi ya kwamba dadi ya wafuasi wa dini za jadi imeendelea kupungua. Baadhi ya viongozi na wanaelimu-jamii wanakadiria kwamba jumuia za Kikristo na Kiislamu zipo sawa tu kwa ukubwa, zote huhesabiwa kiasi cha asilimia 30 hadi 40 kwa idadi ya wakazi, na waliosalia ni waumini wa imani zingine, dini za jadi, na wale wasio na dini kabisa.
Lakini wataalamu wengine wanasema uwiano huo unashikiliwa kisiasa kwa sababu uhusiano kati ya Wakristo na Waislamu ni jambo la siasa ya taifa kwa hiyo makadirio yanaelekea kutaja uwiano sawa kati ya pande hizi mbili.[SUP][3][/SUP]
[h=3][hariri] Mifano ya makadirio mbalimbali[/h]Kwa hiyo namba zote kuhusu takwimu ya dini nchini Tanzania ni makadirio tu hakuna namba za kutegemea. Vyanzo vinavyotaja namba vinatofautiana sana mara nyingi kufuatana dini ya wahariri.

  • "World Christian Encyclopedia" (toleo la pili, Oxford 2001) imekadiria kwa mwaka 2000 Wakristo kuwa 50.4 % (Wakatoliki 24.7%, Waprotestanti mbalimbali 16.5%, Waanglikana 7.9%, wasio na madhehebu maalumu 3.5%, madhehebu huru 1.9%, madhehebu yasiyokubali imani ya msingi ya Wakristo wengine wote 0.1%, wenye kufuata madhehebu mawili kwa wakati mmoja 4.2%), Waislamu 31.8%, wafuasi wa dini za jadi 16.1% na wengineo 1.8%. Pia imetabiria kwa mwaka 2025 uwiano kuwa 56.1, 32.8, 8.9 na 2.1%, na kwamba kufikia mwaka 2050 Wakristo na Waislamu watakuwa karibu 65 na 35% kati ya wakazi wa nchi.


  • Takwimu zinazoonyeshwa na Waislamu hudai kundi kubwa la Watanzania kuwa Waislamu wakiwa na asilimia 50 - 60 za watu wa nchi [SUP][5][/SUP]

  • Kuna shirika za Kiislamu zinazotabiri Tanzania itakuwa nchi ya Waislamu wengi mnamo mwaka 2020 [SUP][6][/SUP]
Pande zote zinarejea takwimu za kuongezeka za watu katika maeneo fulani wakiongeza makadirio yao juu ya matokeo kwenye namba za kidini.

Source; wikipedia.
 
Kusema kweli kuna umuhimu kwa kipengele cha dini kuongezwa kwenye zoezi zima la sensa ya wa TZ

Mimi sijui ni wadudu gani wapo ndani ya baadhi ya viongozi wa kiislamu, nashauri kipengele cha elimu kiwe moja ya vipaumbele vya mtu kupewa ushehe. Tena wasome kama mapadre miaka saba on philosophy and tiology. Pengine huenda wakaanza kuongea point. mara oo tupo wachache, mara oo tunaonewa , mara oo hatujaajiriwa...Mbona wakristu hawalalamiki kwenye biashara wapo wachache?? Si wanaona gap na kutafaklari kwa kina kuwa wengi walikuwa kwenye elimu zaidi.

Tutafute chanzo halisi..
 
Wakuu heshima kwenu,

Mkuu Jasusi kagusia kidogo sensa ya mwaka 1967 ngoja niwawekee kwa faida ya mjadala.


Takwimu ya dini[hariri] Sensa ya 1967

Takwimu ya dini nchini Tanzania kwa sasa haipatikani kwa sababu maswali kuhusu dini yaliondolewa na serikali katika sensa baada ya mwaka 1967. Sensa ile ya tarehe 27 Agosti ilihesabu wafuasi wa dini za jadi kuwa 34.3%, Wakristo 33.5% na Waislamu 31.4%, mbali na wengineo 0.8%.[SUP][1][/SUP]
[hariri] Namba zenye athira ya kisiasa

Tangu mwaka ule swali la takwimu ya kidini Tanzania limejadiliwa sana inaonekana ni swali lenye uzito wa kisiasa pamoja na upande wake wa kitaalamu.
Kwa miaka mingi makadirio ya kawaida yalikuwa Watanzania ni theluthi 1 wafuasi wa dini za jadi, theluthi 1 Waislamu na theluthi 1 Wakristo.[SUP][2][/SUP]
Lakini ni wazi ya kwamba dadi ya wafuasi wa dini za jadi imeendelea kupungua. Baadhi ya viongozi na wanaelimu-jamii wanakadiria kwamba jumuia za Kikristo na Kiislamu zipo sawa tu kwa ukubwa, zote huhesabiwa kiasi cha asilimia 30 hadi 40 kwa idadi ya wakazi, na waliosalia ni waumini wa imani zingine, dini za jadi, na wale wasio na dini kabisa.
Lakini wataalamu wengine wanasema uwiano huo unashikiliwa kisiasa kwa sababu uhusiano kati ya Wakristo na Waislamu ni jambo la siasa ya taifa kwa hiyo makadirio yanaelekea kutaja uwiano sawa kati ya pande hizi mbili.[SUP][3][/SUP]
[hariri] Mifano ya makadirio mbalimbali

Kwa hiyo namba zote kuhusu takwimu ya dini nchini Tanzania ni makadirio tu hakuna namba za kutegemea. Vyanzo vinavyotaja namba vinatofautiana sana mara nyingi kufuatana dini ya wahariri.

  • "World Christian Encyclopedia" (toleo la pili, Oxford 2001) imekadiria kwa mwaka 2000 Wakristo kuwa 50.4 % (Wakatoliki 24.7%, Waprotestanti mbalimbali 16.5%, Waanglikana 7.9%, wasio na madhehebu maalumu 3.5%, madhehebu huru 1.9%, madhehebu yasiyokubali imani ya msingi ya Wakristo wengine wote 0.1%, wenye kufuata madhehebu mawili kwa wakati mmoja 4.2%), Waislamu 31.8%, wafuasi wa dini za jadi 16.1% na wengineo 1.8%. Pia imetabiria kwa mwaka 2025 uwiano kuwa 56.1, 32.8, 8.9 na 2.1%, na kwamba kufikia mwaka 2050 Wakristo na Waislamu watakuwa karibu 65 na 35% kati ya wakazi wa nchi.


  • Takwimu zinazoonyeshwa na Waislamu hudai kundi kubwa la Watanzania kuwa Waislamu wakiwa na asilimia 50 - 60 za watu wa nchi [SUP][5][/SUP]

  • Kuna shirika za Kiislamu zinazotabiri Tanzania itakuwa nchi ya Waislamu wengi mnamo mwaka 2020 [SUP][6][/SUP]
Pande zote zinarejea takwimu za kuongezeka za watu katika maeneo fulani wakiongeza makadirio yao juu ya matokeo kwenye namba za kidini.

Source; wikipedia.
 
Back
Top Bottom