Sheikh Ponda yuko sahihi

Sheikh Ponda yuko sahihi

nafikiri tufike mahali tupime ukali wa maneno au uwezo wa maneno kwa nadharia tatu moja je kuna sababu gani ambayo ipo nyuma ya hii kauli, maana kila jambo lina sababu hakuna jambo linaloweza kutokea bila sababu, mbili je ni malengo yapi yamezamiliwa katika kauli hiyo na je kama yasipotimizwa ni ninu itakuwa hatima ya hii kauli kama siyo uchochezi, na je hii kauli ina madhara gani kwetu kama taifa.
je wazo zuri ni lipi tugawe mgawanyo wa kazi kutokana na dini na matabaka au tugawe mgawanyo kazi kutokana na taaluma na ujuzi, je shekh ponda amesahau kama serikali haina dini? je anapodai fomu za sensa ziwe na alama au ishara ambayo muislam tajaza dini yake haoni kama tukifanya tutalazimisha na wakristo na wenyewe wadai hivohivo hali kadharika na wale wasiyo na dini na wenyewe hivo na fikiri siyo kila kiwazwacho moyoni lazima kisemwe mdomononi, tuache majungu na propaganda zisizo na msingi tujenge taifa letu
 
juzi Sheikh Ponda Issa ambaye ni katibu wa Jumuiya ya Kutetea Haki za Waislamu alitanabahisha kuwa iwapo serikali haitoweka kipengele cha dini katika fomu za sensa ya mwaka, jumuiya yao itahamasisha Waislamu wasishiriki katika zoezi la sensa.Alisema kuwa nchi hii siyo ya Kikristo lakini INATAWALIWA NA MFUMO KRISTO.

Alisema kutokana na mazoea, Waislamu wanabaguliwa katika mgawanyo wa keki ya taifa khasa upande wa ajira. ofisi na idara za serikali zinaongozwa na Wakristo kwa asilimia kubwa kulinganishwa na waislamu. alitoa mfano wa TRA, NECTA, Wizara ya Eimu, Wizara ya Ujenzi, Afya, Mahakama nk........... kwa mujibu wa Sheikh Ponda, wastani wa ajira ni karibu Wakristo 77% na Waisalmu siyo zaidi ya asilimia 20%. Licha ya hoja inayojengwa kuwa Waislamu hawajasoma lakini akasema waliosoma wapo.

Akatanabahisha kuwa kwa maslahi na umoja wa kitaifa, kupuuza watu ambao ni sehemu ya jamii ktk keki ya taifa ni jambo hatari sana! kwa kuwa wtu wanadai waislamu ni chini ya 20% katika nchi hii, akapendekeza sensa ya mwaka huu kiwekwe kipengele cha dini ili idadi ya watanzania kidini ijulikane. Kwa mujibu wa Sheihk Ponda, anaamini kuwa waislamu ni takriban 64% ya rais wa Tanzania.

"SIYO SAHIHI WATU WENYE IDADI HII KUPUUZWA KATIKA UWIANO WA AJIRA SERIKALINI", alisema Sheikh Ponda.Alitoa mifano wa nchi karibia zote za Ulaya, Marekani, asia pamoja na Afrika, kipengele cha dili kipo kwenye fomu za sensa zao. "Ukisoma country profile au fact file uingiapo katika nchi mbalimbali, utakuta wameandika wastani wa idada ya raia kidini" alisisitiza Ponda. "Mbona mnajifanya kama hamtembei au hamjui kinacho endelea ulimwengunu jamani!" alilalama Ponda.

HOJA YANGU Ndugu znaguni Watanzania, tufike sehemu tuache ukweli udhihiri. kama Waislamu wanalalamika kuwa wanabaguliwa katika ajira labda kutokana na uchache wao, kwa nini suala la dini lisiwekwe wazi? au utakua udini? au uchochezi? au uvunjifu wa amani? kama ni hivyo, mbona karibu 98% ya sensa zote duniani zina kipengele cha dini!? je huko wameuana kutoakana na kipengele hicho? TUBADILIKE!!!

naomba kuwasilisha!

Ntakubaliana na PONDA kwenye suala moja muhimu, nalo ni kuhusu 'dodoso' ya dini ya mtu basi, hayo mengine namwachia mwenyewe. Hili si swali ambalo serikali inatakiwa kujiuliza ama liwepo ama lisiwepo la ni swali la kuwepo kwenye dodo na kukataa litakuwani kosa kubwa sana. Sehemu mbalimbali duniani na mimi binafsi nimewahi kushiriki sensa nikiwa katika nchi moja ya madharibi ni kwamba swali hili linaulizwa. Ila kuna kuwa na option kama mtu haitaji kusema anaachana nalo. Kuna swali kama gender (jinsia) hili ni lazima, ila pia kuna swali la sexual orientation (gay, straight, bisexual) hili ni option - swali hili haswa ndilo lilitakiwa kupingwa na serikali yetu kuuliza kwani sisi hatutambua jinsi mtu anavyofanya mapenzi, sisi tunajua mapnezi ni kati ya mke na mume basi.

Sensa inatakiwa kuwa general purpose na kitendo cha serikali kujimilikisha outcome ya sensa ni worse. Serikali kama mdau inakuwa na maeneo inayotaka kuangalia kwa ajili ya policies zake. Lakini pia serikali kama Authority (Hapa nina maana kuwa wanakusanya kodi na kuzitumia) inatakiwa kuwa broad. Unapokuwa na database ya kila kitu unarahisha maendeleo sana, kwani stakeholders mbalimbali wanaweza kuomba data fulani toka kwenye ofisi ya Takwimu kwa ajili ya shughuli mbalimbali kama research, programme zao n.k.

Serikali haitakiwi kuogopa kuuliza dini ya mtu provided inafanya hivyo for recording purposes and not for political purpose au kwa ajili ya kupendelea kundi lolote lile. Watu wawe na uhuru wa kusema dini zao ni zipi au la. Ule mchezo wa watu wa statistics kukaa chini baada ya sensa na kuanza kuangalia majina kama John, Alex, Anna, Chrisptopher, Ramazani, Frank, Juma, Mwantumu, Havijawa na kuassume dini kutokana na majina umepitwa na wakati. Siku hizi kuna kina Ramazani wakristo , Alex waislam. Why wakae na kuestimate badala ya kuwa na real figures?. Je wapagani wanaoitwa Kulthum au Godwin nao utawaweka wapi?.

Binafsi sioni sababu za msingi za kukataa hoja ya 'dodoso la dini mtu' zaidi ya siasa na kupinga kwa sababu tu aliyeomba ni Sheikh Ponda Isa Ponda na hivyo wawakilishi wa JK kuona kuwa wakikubali basi akina baba askofu watawashambulia na kuhusisha dini ya boss wa nchi na kukubaliwa ombi la Ponda.

Mambo mengine hayahitaji sana analysis bali ni common sense. Kusema kama wanataka idadi wahesabu waumini wao ni irresponsible kwa serikali kwani kama inaweza kutumia kodi kuweka taarifa kwa nini pia isiseme kila dini ihesabu watu wake na kuwapelejka ofisi ya takwimu na hapo sensa itakuw imekamilika?
 
Mimi mwenyewe nataka hicho kipengele cha dini kiwepo kina faida...

Faida zipi hizo na kwa faida kwa dini husika au Watanzania?
Kanisa nalosali tunajua idadi kamili ya Wakristo kwenye parokia yetu, tunajua idadi ya wanakuja Ibadani kila wiki, kwa hiyo tunajua dayosisi ina waumini wangapi na nchi nzima wako wangapi. Waislamu wanashindwa vipi hadi kulazimisha serikali iwasaidie kujua idadi yao? Hawana namna ya kujua Waislamu wako wangapi? Au wanataka kuwatisha wengine tu?
 
juzi Sheikh Ponda Issa ambaye ni katibu wa Jumuiya ya Kutetea Haki za Waislamu alitanabahisha kuwa iwapo serikali haitoweka kipengele cha dini katika fomu za sensa ya mwaka, jumuiya yao itahamasisha Waislamu wasishiriki katika zoezi la sensa.Alisema kuwa nchi hii siyo ya Kikristo lakini INATAWALIWA NA MFUMO KRISTO.

Alisema kutokana na mazoea, Waislamu wanabaguliwa katika mgawanyo wa keki ya taifa khasa upande wa ajira. ofisi na idara za serikali zinaongozwa na Wakristo kwa asilimia kubwa kulinganishwa na waislamu. alitoa mfano wa TRA, NECTA, Wizara ya Eimu, Wizara ya Ujenzi, Afya, Mahakama nk........... kwa mujibu wa Sheikh Ponda, wastani wa ajira ni karibu Wakristo 77% na Waisalmu siyo zaidi ya asilimia 20%. Licha ya hoja inayojengwa kuwa Waislamu hawajasoma lakini akasema waliosoma wapo.

Akatanabahisha kuwa kwa maslahi na umoja wa kitaifa, kupuuza watu ambao ni sehemu ya jamii ktk keki ya taifa ni jambo hatari sana! kwa kuwa wtu wanadai waislamu ni chini ya 20% katika nchi hii, akapendekeza sensa ya mwaka huu kiwekwe kipengele cha dini ili idadi ya watanzania kidini ijulikane. Kwa mujibu wa Sheihk Ponda, anaamini kuwa waislamu ni takriban 64% ya rais wa Tanzania.

"SIYO SAHIHI WATU WENYE IDADI HII KUPUUZWA KATIKA UWIANO WA AJIRA SERIKALINI", alisema Sheikh Ponda.Alitoa mifano wa nchi karibia zote za Ulaya, Marekani, asia pamoja na Afrika, kipengele cha dili kipo kwenye fomu za sensa zao. "Ukisoma country profile au fact file uingiapo katika nchi mbalimbali, utakuta wameandika wastani wa idada ya raia kidini" alisisitiza Ponda. "Mbona mnajifanya kama hamtembei au hamjui kinacho endelea ulimwengunu jamani!" alilalama Ponda.

HOJA YANGU Ndugu znaguni Watanzania, tufike sehemu tuache ukweli udhihiri. kama Waislamu wanalalamika kuwa wanabaguliwa katika ajira labda kutokana na uchache wao, kwa nini suala la dini lisiwekwe wazi? au utakua udini? au uchochezi? au uvunjifu wa amani? kama ni hivyo, mbona karibu 98% ya sensa zote duniani zina kipengele cha dini!? je huko wameuana kutoakana na kipengele hicho? TUBADILIKE!!!

naomba kuwasilisha!


UKO SAHIHI KABISA .....sioni jambo la ajabu kuwepo kwa kipengele cha dini kwenye sensa ni kupata tarakimu tu
 
The study of the United States Bureau of Democracy, Human Rights, and Labor for 2009 suggests that 62% of the population of Tanzania isChristian, 35% is Muslim, and 3% are members of other religious group
The Christian population of Tanzania is mostly composed of Roman Catholics,Lutherans and Anglicans, Pentecostals, Seventh-day Adventists, members of The Church of Jesus Christ of Latter-day Saints (Mormons), and Jehovah's Witnesse

Islam is, as of 2007, the religion in Tanzania with 40% of the population of the mainland (Tanganyika) and more than 99% of the population on the island ofZanzibar being Muslim
soma zaidi Wikipedia
fanya random sampling ya idadi ya wanaomaliza form 4, 6 na wanaoingia
vyuo utaona asilimia 70 ni wakristo na 30 ni waislamu na wasio na dini.
bado tu huamini? mnalala mnangangania usawa wa kielimu na kikazi wapi na wapi.



Hapo kwenye RED
Ndo utuambie sasa umepata wapi takwimu hizi ikiwa sensa yetu haina kipengele cha dini??? kama co hearsay zanazolenga kuiaminisha jamii ya Watanzania kuwa dini flani ni wengi kuliko wengine?? Pia uwiano wa kielimu hautoshi kuhitimisha kuwa dini flani ni wengi kwakuwa tatizo la elimu kwa waislamu hapa TZ ni lakihistoria!!
Wajua kuwa Rwanda Watutsi ni wachache kuliko Wahutu lakini ndio waliosoma na wanaohodhi nafasi nyingi serikalini kuliko wenzao ambao ndio wengi?? Na kwanini ukitembelea coutry profiles za nchi kibao utakuta wameweka idadi ya watu kwa dini zao? Wanazitoa wapi?
Kwakuwa sisi kama Tanzania tulikubaliana kutokujumuisha kupengele cha dini kwenye sensa yetu wacha twende hivyo hivyo lakini Maoni yake yana Mashiko
 
Unataka kutuambia kuwa kama waislam watakuwa wengi itabidi watengewe ardhi kubwa kwa ajili ya makaburi kwa kuwa waislam watakuwa wanakufa sana au?!
Sikuwa na maana ya waislam pekee..... nilimaananisha kwa dini zote kwani kila dini inautaratibu wake wa baada ya muumini wao kufariki.....wengine wanazika miili... wengine wanachoma moto nk. hoja kuu ilikuwa ni kuwa na takwimu ili kuweza kufanya mipango/maamuzi
 
Waswahili bana, yaani dini za wakoloni zimewatawala sana. Watu watauana tu kwa sababu ya kuwatetea Mungu Allah, Mungu wa Israel, Mungu Papa, Mungu Anglican...ilhali hata hivyo vitabu vya Mungu hao haviwataji kabisa waswahili hawa!

Asanteee! Like!
 
tunaonewa tunaonewa jamani y dont you do something about it...yani full lawama mkiambiwa changisheni hela mjenge shule mnalalama mkiambiwa changisheni mjenge chuo lawama mkiambiwa mjitolee kufundisha hizo shule zenu lawama mkiambiwa mchange mjenge hospitali lawama mkiambiwa mnunue hisa mfungue benki zenu lawama...

lakini hao wakristo mnaowalaum kila kukicha wanafanya vitu vyote hivo wenyewe....wanajenga shule zao wenyewe, makanisa yao wenyewe, vyuo vyao wenyewe, hospitali zao wenyewe, wana mabenki yao wenyewe yani sijui utaanzia wapi kulinganisha maendeleo ya waislam na wakristo.


mkoa unaongoza kwa shule ni k`njaro asilimia kubwa zinamilikiwa na makanisa na nyingine wamejenga wao..sote tunajua maendeleo ya watu wa huko kielimu....ukiangalia maeneo ya upareni(kwenye uislam wengi) hakuna maendeleo kama ule upande wa wachaga ambao wengi ni wakristo, pamoja na hiyo miradi yao mingi haina ubaguzi kabisa...

yani dini ya uislam imekua ni dini ya kulalama dailly....mbona matajiri wengi hapa dar ni waislam..?? kwanini wasiwekeze kwenye taaluma ili iwasaidieni ?? ukweli ni kwamba idadi ya wanafunzi wa dini hzi mbili hailingani...hata userious wa wazazi juu ya kuwekeza elim dunia kwa watoto wao ni mdogo sana, pamoja na hvo miundombinu hamna ya kutosha...kubalini mpo nyuma ili muweze kuweka mikakati ya kwenda mbele na sio kila siku malalamiko.
 
aliokuambia kanda ya ziwa wote ni wagala ni nani? Kumbuka huko kuna watu wanaofuata dini za asili kwa idadi kubwa tu.

Kwa mtazamo wangu mimi, yeyote ambaye si wa dini yangu huyo ni kafiri tu, kutazama majina ni kitu kinachotu-mislead. Nilishangaa sana wakati wa uchaguzi 2010, BBC Jumamosi moja walitaka kuongea na Mkurugenzi wa NEC Rajab Kiravu, akawajibu kwa wakati ule alikuwa Kanisani, asingweza kujibu chochote .
 
nilikua pakistani.... jamaa mmoja akawa anasifia jinsi walivyozaana na kuwa na influence kwa nambaz huku akijilinganisha na india na bangladesh

wahindia pia walizaaana kweli....

Ndio utajiri wa watu maskini na wajinga wajinga....
 
kama Sheikh wangu ponda kasema hivyo basi na mimi sihesabiwi mpaka kipengele cha dini kiwekwe mbona wao waisilamu hawaogopi kipengele cha dini iweje nyie wakiristo munaogopa ? na sisi waisilamu hatutoshiriki hio sensa yenu jihesabuni wenyewe
 
Ponda yuko sahihi na serikali umewadanganya watanzania kuwa hili ni suala la kimataifa hamna kipengele cha dini na kwanini wanakataa kuna nini nyuma ya pazia, hii inatupelekea tuamini serikaali iliona mfumo krito bado inatumiwa na wachache kupangiwa mambo yake
 
ha haa haaa nimecheka hizi takwimu kwa taarifa yako asilimia kubwa ya Wasukuma kanda ya ziwa Shinyanga, Mwanza, na Mara, hawana dini..hata Iringa Wakinga hawana dini.
Kwangu hata wasio na dini nao ni Waislamu, maana maisha wanayoishi yanakaribia Uislamu zaidi ingawa wengi wao ukiwauliza wao ni dini gani au kama hawana dini; watakujibu wao ni Wakristo!
Kuhusu watu wengi Kanda ya Ziwa na Wakinga hawana dini msubiri Sikonge, Lunyungu, Balantanda na Ukolokwitanga watakupa jibu.
 
The study of the United StatesBureau of Democracy, Human Rights, and Labor for 2009 suggests that 62% of the population of Tanzania isChristian, 35% is Muslim, and 3% are members of other religious group
The Christian population of Tanzania is mostly composed of
Roman Catholics,Lutherans and Anglicans, Pentecostals, Seventh-day Adventists, members of The Church of Jesus Christ of Latter-day Saints (Mormons), and Jehovah's Witnesse

Islam is, as of 2007, the religion in Tanzania with 40% of the population of the mainland (Tanganyika) and more than 99% of the population on the island ofZanzibar being Muslim
soma zaidi Wikipedia
fanya random sampling ya idadi ya wanaomaliza form 4, 6 na wanaoingia
vyuo utaona asilimia 70 ni wakristo na 30 ni waislamu na wasio na dini.
bado tu huamini? mnalala mnangangania usawa wa kielimu na kikazi wapi na wapi.

Nilipo Blue.

ndio maana zinatakiwa zipatikane takwimu sahihi sio za assumptions. Waislam wameliona hilo kwa kina sana na sasa wanataka kipengele cha dini kiwemo ndani ya karatasi zenu za sensa ila kujijua na kujisahihisha kama itawezekana na kuondokana na hii tarbia yya kukisia.

Lakin msingi mkubwa ni mipango ya nchi kwani vipengele kama jinsia, dini , elimu na ulemavu ni muhimu sana katika kupanga maendeleo ya nchi.

Sioni sababu kwanini wenzenu wanakataa. sijui wana ajenda gani hao.
 
Nilipo Blue.

ndio maana zinatakiwa zipatikane takwimu sahihi sio za assumptions. Waislam wameliona hilo kwa kina sana na sasa wanataka kipengele cha dini kiwemo ndani ya karatasi zenu za sensa ila kujijua na kujisahihisha kama itawezekana na kuondokana na hii tarbia yya kukisia.

Lakin msingi mkubwa ni mipango ya nchi kwani vipengele kama jinsia, dini , elimu na ulemavu ni muhimu sana katika kupanga maendeleo ya nchi.

Sioni sababu kwanini wenzenu wanakataa. sijui wana ajenda gani hao.

Barubaru maendeleo ya nchi yanapangwa kwa kuangalia dini?
kama mnataka kujua mko wangapi jihesabuni wenyewe kama wakristo wanavofanya ktk jumuia,parokia,usharika nk... waziri wa fedha anavosoma bajeti huwa anasema bejti hii ni ya waislamu na hii ni ya wakristo au inamlenga kila Mtanzania?
 
Faida zipi hizo na kwa faida kwa dini husika au Watanzania?
Kanisa nalosali tunajua idadi kamili ya Wakristo kwenye parokia yetu, tunajua idadi ya wanakuja Ibadani kila wiki, kwa hiyo tunajua dayosisi ina waumini wangapi na nchi nzima wako wangapi. Waislamu wanashindwa vipi hadi kulazimisha serikali iwasaidie kujua idadi yao? Hawana namna ya kujua Waislamu wako wangapi? Au wanataka kuwatisha wengine tu?

Siku zote tunasema kwenda skuli sio KUELIMIKA. hivi hata wewe kweli utajiita Great thinker kwa hayo ulioandika.

Nakushauri huko Tanzania kuna mabalozi wa nyumba kumi siku hizi wanaitwa wajumbe wa mashina,wenyeviti wa vitongoji na vijiji, Village exec officers, Ward Exec Oddicers. Sasa kama kila mtu anajua idadi ya watu ndani ya familia yake, na kila mjumbe anajua idadi ya kaya katika eneo lake. kwanini wasiunganisha hisabu hizo zote na kujua idadi ya watu na NCHI IKAAMUA KUFANYA SENSA.

Nafikiri ukijibu suala hilo utakuwa na kujua nini maana ya sensa.

Fikiri kabla kuandika

 
Mfumo kristo ndio unaotawala nchi hii mtake msitake. Kwenye vyumba vya hoteli utakuta biblia! Kwa nini kusiwekwe korani? Kwenye vyombo vya usafiri kunapigwa kanda za injili kwa nini kusipigwe kaswida?
 
Sheikh Ponda unatisha,uko juu,angalia unavyojadiliwa.Mimi na wenzangu wengi tumetega sikio ukisema tususie nije nione mtu anakanyaga kwangu eti kunihesabu,nitamtoa nduki
 
Alonena ni suala zuri sana. vipengele muhimu va kuzingatiwa katika sensa ni pamoja na Umri, Dini, jinsia, hali za watu (ulemavu n.k) kwa ajili ya mipango ya nchi kwa maendeleo na ustawi wa jamii.

Ni vizuri kulijadili kwa kina kwa mustakabali bora wa nchi yenu katika mipango ya baadae.

Kuna ya maana sana ya kujadili, si udini. Udini ni sera ya watu wasio na elimu na wasio na hoja na wasiojua sababu za umasikini Tanzania, ukitaka kuwajua jaribu kuangalia hoja katika thread hii.
 
Back
Top Bottom