Maelezo yako yamejaa chuki mpaka unashindwa kufikiri vizuri na ukaishia kujikanganya. Unasema Waislam hawakusoma na wanaishia kunywa kahawa vijiweni lakini ukakiri kuwa Rais wa Nchi na Makamu wake ni waislamu, je una maana hao hawakuenda shule? Ni product ya vijiwe vya kahawa? Au hujui kuwa Dr Gharib Bilal ni Engineer wa Nuclear Energy pekee hapa nchini ( one of the most cumbersome Mathematical subject in existence) ila serkali inashindwa kumtumia kutokana na mfumo mbovu uliopo. Au una maana Judge Chande hana elimu? Kina Proffesor Lipumba na Maprofessa na Ma Drs wote wa Kiislamu waliotapakaa nchi nzima hawakusoma bali ni watu wa Madrassa na Vijiwe vya kahawa? Unasema Waislamu wanajilipua ovyo duniani, hivi ina maana wewe hukusoma na wala hujui historia ya watu wanaojilipua duniani au ni chuki zako dhidi ya Uislamu ndio zimekutia upofu? Tulia nikupe darasa, Wenye Historia kubwa ya kujilipua duniani ni Wajapani, wanajilipua kwa staili ya KAMIKAZE (Kamikaze Bombers) wanajilipua ili kuua watu wengi zaidi na kuteketeza mali au zana kubwa zaidi, hao wako kwenye orodha ya mashujaa wa nchi hiyo mpaka leo, na Japan ikivamiwa tena kivita mtawasikia tena, Kisha kuna HARAKIRI, hawa hujipasua matumbo hadi kufa kwa kutumia Upanga wa Samurai, ikiwa ni kuonesha kutubu kwa kushindwa majukumu au anaposhindwa kujiokoa kwa maadui. Je hao ni Waislamu? Hapa Tz kuna Waislamu wangapi waliojilipua kwa njia hiyo? Hivi wewe na akili zako, na wenzako wenye fikra Kama zako mnaona vijiwe vya kahawa ndio tatizo, ila Mabaa ya Pombe na wanaokunywa pombe mpaka wakajinyea hao ndio barabara? Mbona Mwl Nyerere alipenda sana kucheza bao na wazee wenzake kwenye hivyo vijiwe vya Kahawa? Alikuwa mpumbavu?
hongera<MGUNGA MIBA: wasipoelewa tena hawa walaf wa NYAMAFU cjui wataelewa lini!