Serikali ya Tanzania kuajiri watumishi 44,096 na kupandisha madaraja watumishi 92, 619

Kada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.

Serikali ya Tanzania imesema katika mwaka wa fedha 2021/22 inatarajia kuajiri watumishi wa umma wapya 44,096.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Aprili 22, 2021 Waziri wa Nchi Ofisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilishwa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2021/22.

Amesema kada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.

Amesema Serikali itaajiri watumishi 14,841 wa kada mbalimbali ikiwemo wahadhiri wa vyuo vikuu vyote vya umma nchini pamoja na kada nyingine ambazo haziko kwenye sekta zilizoainishwa awali.

Hata hivyo, amesema watumishi 92,619 wa kada mbalimbali watapandishwa vyeo na watumishi 2,360 watabadilishwa kada katika utumishi.

Amebainisha kuwa maelekezo yatakayotolewa wakati huo ni kuchambua na kuhakiki madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa umma 17,699 yenye thamani ya Sh37.47 bilioni na kuchukua hatua ipasavyo.

Aprili 15, 2021 Serikali ya Tanzania ilieleza matarajio yake ya kuajiri watumishi wapya 44,811 katika mwaka wa fedha 2020/21.

Hayo yalielezwa na aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika wakati akiwasilisha bajeti yake kwa mwaka huo wa fedha.

Alitaja ajira hizo mpya kuwa ni kada ya elimu (13,529), afya (10,467), kilimo, mifugo na uvuvi (2,145) Jeshi la Polisi (2,725), magereza (685), Jeshi la Zimamoto (501), uhamiaji (495) na hospitali za mashirika ya kidini na hiyari (1,262).

Chanzo:
Huyu Waziri toka 2016 mpaka leo Hadithi ni hii hii hakuna jipya hapo
 
Serikali kuajiri kwa wingi wakati huu iko sahihi sababu asilimia kubwa ya miundo mbinu iomeshajengwa hivyo mfanyakazi wa serikali hata akijikopea kagari kake used kataweza kudumu bila shida barabara nyingi nzuri

Kinachotakiwa kwa sasa serikali isiongeze sana miradi mipya iwe kidogo sana imalizie iliyopo ili serikali iwe na extra ya kulipa wafanyayakazi nyongeza nk

Bajeti ya miradi ya maendeleo inabidi ishuke sana hili kila mwananchi anatakiwa kulijua kuwa huwezi kila siuku familia ile pilau hela ukiwa nayo ndogo na wakati huo huo ujenge gorofa!!!
 
uongo vyuo vyetu vyote ukijumlisha vinatoa graduate 1200 tu wa ualimu kwa mwaka ukipiga kwa miaka 20 nyuma ni elfu 24 tu!! hiyo laki tano umeitoa wapi?
Ndugu hivi uko tanzania ya wapi hiyo au bado uko fm6

Udsm Baed tu ni zaidi ya 1000
Bado Bed kama 300
Bado wale wa science Conas 300
Bado coed special need kama 300

Haya Bado branches za udsm Duce na Muce chuo kizima kinatoa degree za education tu

Nenda udom ndio inaongoza kwa udahili utachoka asee hao 1200 ni udom pekee inatema na zaidi,

Hapo sijagusia vyuo vingine vya kati na waajiriwa wengi wanatoka humo.
 
Laah Inaonekana awamu ya tano hii inayoombewa ati iwe na distinguished Legacy haikuajiri hata mtumishi mmoja - likewise haikupandisha daraja mfanyakazi yoyote - Kweli nchi imepata Uhuru wake tena. (Freedom is back baada ya mwendazake kufanya yake)

Ushauri: Wangesubiri subiri watu wasahau sahau kwanza ndipo waanze kumwaga hizi neema.
 
Binafsi sikubaliani na huu mfumo wa ajira wa sasa wa kutegemea ajira za serikali tu.

Serikali iboreshe mazingira watu wengi waajiriwe na sekta binafsi.

Serikali itaajiri hadi lini? Kwa presha ya sasa itabidi kila mwaka serikali ilazimike kuajiri ili kuwaziba watu midomo lakini hii sio njia nzuri ya kutatua tatizo.

Kwa mtindo huu wa kutegemea ajira za serikali na serikali ikawa inaajiri kila mwaka itafika wakati mapato yote na makusanyo yanaishia kwenye kulipana mishahara tu.

Serikali kwanza irekebishe mifumo, isambaze pesa sekta binafsi. Pili ipitie upya muundo wa watumishi wake. Unaenda shule za mjini waalimu 80, shule za vijijini waalimu 2.

Kabla ya kufikiria kuajiri, kwanza pitia miundo upya, boresha mazingira ya hao watumishi waliopo watafanya kazi kwa morali, mfano mwalimu leo analipwa 720,000. Unataka utajiri mwalimu mwingine, wakati hiyo hela ya mwalimu mpya ukiboresha mazingira kwa mwalimu aliepo ukamlipa 1M ama 1.1M, huyu atakua moralized sana na atafanya kazi hata ya waalimu 2.

Tuboreshesekta binafsi kwanza, pili tuboreshe maslahi ya watumishi tulionao kabla ya kufikiria kuajiri wapya.
Iboreshwe uku ikitoa ajira ndio formula
 
Ndugu hivi uko tanzania ya wapi hiyo au bado uko fm6

Udsm Baed tu ni zaidi ya 1000
Bado Bed kama 300
Bado wale wa science Conas 300
Bado coed special need kama 300

Haya Bado branches za udsm Duce na Muce chuo kizima kinatoa degree za education tu

Nenda udom ndio inaongoza kwa udahili utachoka asee hao 1200 ni udom pekee inatema na zaidi,

Hapo sijagusia vyuo vingine.
Miaka 5 bila ajira wahitimu laki tano maana yake kila mwaka wahitimu laki moja wa ualimu.
 
Huu ni mpango wa kuharibu legacy ya magufuli
Dah cjui unawaza nn ndugu..kwa hio serikali isifanye chochote ..maaana kwa mtazamo wako wakiajir itakua wanataka kuharaib legacy ya magu hata wakijenga miundo mbinu bhc itakua wanataka kuharib legacy ..kwa maana hio nchi isifanye jambo lolote la kimaendeleo ili tuzid kumkumbuka huyo magu
 
Binafsi sikubaliani na huu mfumo wa ajira wa sasa wa kutegemea ajira za serikali tu.

Serikali iboreshe mazingira watu wengi waajiriwe na sekta binafsi.

Serikali itaajiri hadi lini? Kwa presha ya sasa itabidi kila mwaka serikali ilazimike kuajiri ili kuwaziba watu midomo lakini hii sio njia nzuri ya kutatua tatizo.

Kwa mtindo huu wa kutegemea ajira za serikali na serikali ikawa inaajiri kila mwaka itafika wakati mapato yote na makusanyo yanaishia kwenye kulipana mishahara tu.

Serikali kwanza irekebishe mifumo, isambaze pesa sekta binafsi. Pili ipitie upya muundo wa watumishi wake. Unaenda shule za mjini waalimu 80, shule za vijijini waalimu 2.

Kabla ya kufikiria kuajiri, kwanza pitia miundo upya, boresha mazingira ya hao watumishi waliopo watafanya kazi kwa morali, mfano mwalimu leo analipwa 720,000. Unataka utajiri mwalimu mwingine, wakati hiyo hela ya mwalimu mpya ukiboresha mazingira kwa mwalimu aliepo ukamlipa 1M ama 1.1M, huyu atakua moralized sana na atafanya kazi hata ya waalimu 2.

Tuboreshe sekta binafsi kwanza, pili tuboreshe maslahi ya watumishi tulionao kabla ya kufikiria kuajiri wapya.
Mkuu huoni wakiajiriwa hawa automatic sekta binafsi nayo inaneemeka?

Chukulia mfano average wanalipwa laki 5 kwa mwezi, hizo ni kama Bilioni 20 kwa mwezi zinaenda kwenye mabeki, maduka ya nguo, vyakula, viatu, vocha etc.

Sekta binafsi pia inaweza kukua kukiwa na mzunguko wa pesa, mtu hawezi kuja kuwekeza ikiwa purchasing power ni ndogo.
 
Ndugu hivi uko tanzania ya wapi hiyo au bado uko fm6

Udsm Baed tu ni zaidi ya 1000
Bado Bed kama 300
Bado wale wa science Conas 300
Bado coed special need kama 300

Haya Bado branches za udsm Duce na Muce chuo kizima kinatoa degree za education tu

Nenda udom ndio inaongoza kwa udahili utachoka asee hao 1200 ni udom pekee inatema na zaidi,

Hapo sijagusia vyuo vingine vya kati na waajiriwa wengi wanatoka humo.
Huyo ni mpiga propaganda achananae.
 
Back
Top Bottom