Serikali itoe ajira rasmi na kuboresha maslahi ya watumishi wa JKCI-Dar Group

Daktareee

Member
Feb 1, 2022
11
8
. Tuwasalimu kwa jina la muungano wa tanzania.

Ndugu Watanzania awali ya yote tunapenda kutumia fursa hii kuikumbusha serikali ya JMT kutoa ajira rasmi (kuwaingiza watumishi wa hospital wa JKCI-Dar group ktk mfumo rasmi wa ajira za serikali na kuboresha maslahi ya wafanyakazi )

1. Kwanza tunatoa pongezi kwa uongozi wote wa JKCI kwa hatua nzuri na muendelezo wa hospital ya JKCI-Dar group kwa huduma bora na haraka na muelekeo imara wa hospital, kumekua na maboresho na kuongezeka kwa kwa huduma bora mfano kitengo cha dharura (EMD) kuongezeka kwa huduma tabibu za kibingwa mfano clinic za moyo na outreach services, pia kuongezeka kwa madaktar bingwa wa kada zingine mfano gynaecology Ili kuendeleza huduma bora na kasi hii ni vyema serikali ikatoa ajira rasmi ili kupunguza mzigo(burden ) wa kulipa mshara unaotokana mapato ya hospital ili fedha hizo ziweze kuboresha na kusaidia huduma muhimu za hospital kama ununuzi wa vifaa tiba, dawa na kuboresha mazingira ya kazi.

2. Pia ili kutekeleza dira na adhima ya serikali (kama alivoongea waziri wa afya ktk uzinduzi wa hospital hiyo ) ya kuifanya hospital ya jkci-far group kuwa hospital maalum ya magonjwa ya moyo na mishipa ya damu kwa watoto walio chini ya miaka 15 basi serikali haina budi kuchukua jukumu rasmi ya kuwaajiti watumishi hao na kuboresha mazingira ya kazi kwani mpango huo ni wa nchi na sio mpango wa taasisi hivyo serikali ipunguze burden kwa taasisi kwa kulipa mishahara ya wafanyakazi.

3. Upande wa maslahi ya wafanyakazi wa jkci-dar group yapo chini ukilinganisha na wenzao jkci makao makuu, japo ni taasisi moja lakin upande wa maslahi ni tofaut mfano incentives mgao wa bima na malipo ya muda wa kazi wa ziada na shift za usiku malipo ni tofauti na muongozo wa serikali (kauli aliyoitoa Mama SSH ya kuwa malipo yatakua ni 40k kwa 60k kutokana level ya elimu) lakin wafanyakazi wa JKCI-HQ na JKCI -Dar group wanalipwa tofauti hivyo basi ni wajibu wa serikali na taasis kuweka uwiano sawa wa malipo kwa watumishi wote ASAP.

4. Pia kuboresha mazingira ya hospital mfano ni takriban zaid ta miezi mitatu(3) hospital haina Canteen hivyo wagonjwa wanaolazwa , wafanyakazi na clients wengine wanapata sana shida kupata huduma ya chakula.
[mention]Wizara ya Afya Tanzania [/mention] [mention]Jkci [/mention] .
 
Back
Top Bottom