DOKEZO Watumishi Ajira Mpya (Sikonge na Rombo) hatujalipwa Fedha za Kujikimu, tunapigwa danadana

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Sisi watumishi ajira mpya kutoka maeneo tofauti tumeshirikiana kuandika andiko hili kuhusu malipo ya fedha za kujikimu ambayo yamekuwa kizungumkuti kwetu, lengo ni mamlaka zipate kujua kinachoendelea na tuweze kusaidiwa.

SIKONGE, TABORA
Tunaomba Wanahabari mtusaidie kupaza sauti kuhusu hili jambo, sisi ajira mpya katika Wilaya ya Sikonge, Kada ya Ualimu Msingi, tangu mwezi wa sita hela ya kujikimu hatujaipata.

Mpaka leo (Septemba 27, 2023) bado hatujalipwa ili hali hela hiyo unatakiwa kulipwa kabla ya kuanza kazi na huu mwezi wa tatu tangu tumeanza kazi.

Malipo haya tunatakiwa kulipwa zile wiki mbili za mwanzo unapopewa muda wa kujiandaa kabla ya kuanza kazi rasmi, kuna gharama flani ya kuanzia maisha.

Tumejaribu kufuatilia tunaambiwa fedha zimeshafika lakini ukiulizia unaambiwa tuwape muda, Mkurugenzi yeye tulimbana wiki iliyopita akasema fedha zimeshafika kwa idara, tuwaulize huko.

ROMBO, KILIMANJARO
Upande mwingine Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro pia tuna changamoto ya kutolipwa fedha za kujikimu.

Sisi Walimu tuliajiriwa Juni 2023 lakini mpaka leo hatujapata malipo hayo, tumeshadai muda mrefu lakini tunabaki njia panda, tupo na wenzetu Madaktari, Wauguzi wa kike pamoja na sisi Walimu.

Mwaka jana na mwaka juzi wenzetu walipata changamoto kama hiyohiyo, ilifikia hatua hadi wakaandamana ndio wakapata haki yao.

Safari hii (2023) hali inaendelea vilevile, tulitakiwa kupata ndani ya wiki mbili za kwanza lakini mpaka leo, Halmashauri za wenzetu huku Kilimanjaro tumesikia wameshapata lakini sisi tu ndio bado na tunasikia hela zimeshatoka TAMISEMI.

Kama zimetoka TAMISEMI, kwa nini hawatupi malipo yetu? Ukiuliza kwa Mkurugenzi (Godwin Chacha) hatoi ushirikiano mzuri, kila wiki tunaenda ofisini kwake lakini hakuna kinachopatika cha maana.

Pia soma

= Waziri Mchengerwa aagiza Fedha za Kujikimu za Ajira Mpya zilipwe kabla 30 Oktoba, 2023
= Waziri Mchengerwa njoo Halmashari ya Ngara Watumishi Wapya hatujalipwa Fedha za Kujikimu
 
Sisi watumishi ajira mpya kutoka maeneo tofauti tumeshirikiana kuandika andiko hili kuhusu malipo ya fedha za kujikimu ambayo yamekuwa kizungumkuti kwetu, lengo ni mamlaka zipate kujua kinachoendelea na tuweze kusaidiwa.

SIKONGE, TABORA
Tunaomba Wanahabari mtusaidie kupaza sauti kuhusu hili jambo, sisi ajira mpya katika Wilaya ya Sikonge, Kada ya Ualimu Msingi, tangu mwezi wa sita hela ya kujikimu hatujaipata.

Mpaka leo (Septemba 27, 2023) bado hatujalipwa ili hali hela hiyo unatakiwa kulipwa kabla ya kuanza kazi na huu mwezi wa tatu tangu tumeanza kazi.

Malipo haya tunatakiwa kulipwa zile wiki mbili za mwanzo unapopewa muda wa kujiandaa kabla ya kuanza kazi rasmi, kuna gharama flani ya kuanzia maisha.

Tumejaribu kufuatilia tunaambiwa fedha zimeshafika lakini ukiulizia unaambiwa tuwape muda, Mkurugenzi yeye tulimbana wiki iliyopita akasema fedha zimeshafika kwa idara, tuwaulize huko.

ROMBO, KILIMANJARO
Upande mwingine Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro pia tuna changamoto ya kutolipwa fedha za kujikimu.

Sisi Walimu tuliajiriwa Juni 2023 lakini mpaka leo hatujapata malipo hayo, tumeshadai muda mrefu lakini tunabaki njia panda, tupo na wenzetu Madaktari, Wauguzi wa kike pamoja na sisi Walimu.

Mwaka jana na mwaka juzi wenzetu walipata changamoto kama hiyohiyo, ilifikia hatua hadi wakaandamana ndio wakapata haki yao.

Safari hii (2023) hali inaendelea vilevile, tulitakiwa kupata ndani ya wiki mbili za kwanza lakini mpaka leo, Halmashauri za wenzetu huku Kilimanjaro tumesikia wameshapata lakini sisi tu ndio bado na tunasikia hela zimeshatoka TAMISEMI.

Kama zimetoka TAMISEMI, kwa nini hawatupi malipo yetu? Ukiuliza kwa Mkurugenzi (Godwin Chacha) hatoi ushirikiano mzuri, kila wiki tunaenda ofisini kwake lakini hakuna kinachopatika cha maana.
Aisee serikali haiwasiliani hivi ndugu ajira mpya.Fanya mawasiliano sahihi hii sio nzuri kwenu.
 
Mshahara ndio haki yako kwa sababu umeufanyia kazi hiyo ya kujikimu ni hisani tu kwahiyo usikomae sana mwalimu chapa kazi.
 
Wakuu mimi ndio kiranja mkuu huku kuzimu yote yaliyosemwa sio kweli. Narudia tena ni uwongo mtupu.

Kunyweni bia sana imbeni na fanyeni ibada kujifurahisha mwili. Huku hakuna mambo ya duniani kwa hiyo fanyeni mpaka mzeekee.

Huku ni kuzuri ila sio kama duniani. Kuna shida na karaha kuliko duniani. Sio sehemu ya kufikiria kuja ukiwa na nguvu. Ni bora ukae gerezani kuliko kuzimu huku haina vitu vya duniani.
 
Mimi mwenyewe hapa nasubiria, Wewe DED halmashauri ya Karatu, fanya mpango ajira mpya tupate hela yetu ya kujikimu, haraka sana.
 
Sisi watumishi ajira mpya kutoka maeneo tofauti tumeshirikiana kuandika andiko hili kuhusu malipo ya fedha za kujikimu ambayo yamekuwa kizungumkuti kwetu, lengo ni mamlaka zipate kujua kinachoendelea na tuweze kusaidiwa.

SIKONGE, TABORA
Tunaomba Wanahabari mtusaidie kupaza sauti kuhusu hili jambo, sisi ajira mpya katika Wilaya ya Sikonge, Kada ya Ualimu Msingi, tangu mwezi wa sita hela ya kujikimu hatujaipata.

Mpaka leo (Septemba 27, 2023) bado hatujalipwa ili hali hela hiyo unatakiwa kulipwa kabla ya kuanza kazi na huu mwezi wa tatu tangu tumeanza kazi.

Malipo haya tunatakiwa kulipwa zile wiki mbili za mwanzo unapopewa muda wa kujiandaa kabla ya kuanza kazi rasmi, kuna gharama flani ya kuanzia maisha.

Tumejaribu kufuatilia tunaambiwa fedha zimeshafika lakini ukiulizia unaambiwa tuwape muda, Mkurugenzi yeye tulimbana wiki iliyopita akasema fedha zimeshafika kwa idara, tuwaulize huko.

ROMBO, KILIMANJARO
Upande mwingine Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro pia tuna changamoto ya kutolipwa fedha za kujikimu.

Sisi Walimu tuliajiriwa Juni 2023 lakini mpaka leo hatujapata malipo hayo, tumeshadai muda mrefu lakini tunabaki njia panda, tupo na wenzetu Madaktari, Wauguzi wa kike pamoja na sisi Walimu.

Mwaka jana na mwaka juzi wenzetu walipata changamoto kama hiyohiyo, ilifikia hatua hadi wakaandamana ndio wakapata haki yao.

Safari hii (2023) hali inaendelea vilevile, tulitakiwa kupata ndani ya wiki mbili za kwanza lakini mpaka leo, Halmashauri za wenzetu huku Kilimanjaro tumesikia wameshapata lakini sisi tu ndio bado na tunasikia hela zimeshatoka TAMISEMI.

Kama zimetoka TAMISEMI, kwa nini hawatupi malipo yetu? Ukiuliza kwa Mkurugenzi (Godwin Chacha) hatoi ushirikiano mzuri, kila wiki tunaenda ofisini kwake lakini hakuna kinachopatika cha maana.
Upo Sikonge sehemu gani??
Embuu njoo hapa madukani tusemezane kidogo.
 
Hizi halmashauri kuna madude mengi sana kwa maana serikali kuu haioni huu upumbavu unaofanywa na wakurugenzi na watendaji wapumbavu wenzie
 
Mtazoea tu...maadai ya fedha ya serikalini huchukua muda. Cha msingi mshahara umeingia (una check number) Hilo ndio la maana. Hiyo hela ya kununua subwoofer,Azam decoder, flat tv inchi 32 na kunywia bia mtaipata ila muwe wastaarabu maana mnatukana sana kwenye makundi yenu ya Whatsapp (alafu mko katika kipindi Cha majaribio ya mwaka mmoja) mmeshasahau mmesota miaka mingi bila ajira.
 
Mtazoea tu...maadai ya fedha ya serikalini huchukua muda. Cha msingi mshahara umeingia (una check number) Hilo ndio la maana. Hiyo hela ya kununua subwoofer,Azam decoder, flat tv inchi 32 na kunywia bia mtaipata ila muwe wastaarabu maana mnatukana sana kwenye makundi yenu ya Whatsapp (alafu mko katika kipindi Cha majaribio ya mwaka mmoja) mmeshasahau mmesota miaka mingi bila ajira.
Siyo hisani, watoe hela, wao mbona maposho yao ya kisiasa huko hayachelewi, afu haya masuala ya mazoea siyo mazuri, watoe hela kwa wakati.
 
Na hata mkipewa hiyo hela ya kujikimu mtapewa pungufu na matazamio yenu.
 
Hizi habari zifike katavi, Bahi, Itilima, ileje, tandahimba, Songea, Muheza...
Walipeni vijana pesa yao kabla Hakujaharibika, Muongozo ulitoka kuanzi ter 21-August, na kiasi kinajulikana
 
Back
Top Bottom