Serikali ya Tanzania kuajiri watumishi 44,096 na kupandisha madaraja watumishi 92, 619

Kada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.

Serikali ya Tanzania imesema katika mwaka wa fedha 2021/22 inatarajia kuajiri watumishi wa umma wapya 44,096.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Aprili 22, 2021 Waziri wa Nchi Ofisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilishwa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2021/22.

Amesema kada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.

Amesema Serikali itaajiri watumishi 14,841 wa kada mbalimbali ikiwemo wahadhiri wa vyuo vikuu vyote vya umma nchini pamoja na kada nyingine ambazo haziko kwenye sekta zilizoainishwa awali.

Hata hivyo, amesema watumishi 92,619 wa kada mbalimbali watapandishwa vyeo na watumishi 2,360 watabadilishwa kada katika utumishi.

Amebainisha kuwa maelekezo yatakayotolewa wakati huo ni kuchambua na kuhakiki madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa umma 17,699 yenye thamani ya Sh37.47 bilioni na kuchukua hatua ipasavyo.

Aprili 15, 2021 Serikali ya Tanzania ilieleza matarajio yake ya kuajiri watumishi wapya 44,811 katika mwaka wa fedha 2020/21.

Hayo yalielezwa na aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika wakati akiwasilisha bajeti yake kwa mwaka huo wa fedha.

Alitaja ajira hizo mpya kuwa ni kada ya elimu (13,529), afya (10,467), kilimo, mifugo na uvuvi (2,145) Jeshi la Polisi (2,725), magereza (685), Jeshi la Zimamoto (501), uhamiaji (495) na hospitali za mashirika ya kidini na hiyari (1,262).

Chanzo:
Vipi ajira za Wizara ya nishati,ikiwemo tanesco, TPDC,pura,ewura, wizara ya madini, wizara ya ujenzi, miundombinu na mawasiliano . Wizara ya fedha, bot, tra. Au ajira za huko ni kugawana wakubwa,? Mnakimbilia ualimu kila mara
 
uongo vyuo vyetu vyote ukijumlisha vinatoa graduate 1200 tu wa ualimu kwa mwaka ukipiga kwa miaka 20 nyuma ni elfu 24 tu!! hiyo laki tano umeitoa wapi?
Sekta ya elimu wameajiriwa technicians wa maabara mbalimbali, umeme, civil/architectural, electronics, chemistry/biological etc...

Hivyo na hawa wana soma kozi ambazo sio za elimu ktk vyuo vya ngazi ya veta na technical colleges kama arusha tech, Must, Dit etc

Ina wezekana ndg alikuwa ana zungumzia wadau hao waelimu sababu kuna technical schools pia, shule za kilimo kama kibiti boys kilosa etc...

Ukiwa una toa ufafanuzi basi anza kuuliza kwanza kama amelenga kitu gani...

Mtaani watu hawana ajira tangu 2013... Mpaka sasa 2020 ni miaka saba nq walio pata ajira ni wachache... Kuqnzia ngazi ya certificate, diploma mpaka degree na kuendelea
 
Mashirika yana taratibu zake za Ajira kupitia Sekretarieti ya Ajira.
Nilitaka usema hayo,sekretariet ya ajira, ni bomu litalipuka soon . Ajira zote zirudishwe kwenye wizara husika . Sekretariet huwa haitoi nafasi za juu, ni wahudimu na Ps. Zile nafasi muhimu zinajazwa kihuni
 
Nilitaka usema hayo,sekretariet ya ajira, ni bomu litalipuka soon . Ajira zote zirudishwe kwenye wizara husika . Sekretariet huwa haitoi nafasi za juu, ni wahudimu na Ps. Zile nafasi muhimu zinajazwa kihuni
Sasa huko Wizarani ndio wataacha kuwekana. At least kupitia Sekretarieti kunakuwa na uwazi fulani kidogo.
 
Kada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.

Serikali ya Tanzania imesema katika mwaka wa fedha 2021/22 inatarajia kuajiri watumishi wa umma wapya 44,096.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Aprili 22, 2021 Waziri wa Nchi Ofisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilishwa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2021/22.

Amesema kada ya elimu wataajiri watumishi wapya 10,297, afya 11,215, kilimo 1,383, mifugo 1,250, uvuvi 733, Jeshi la Polisi 1,782, Magereza 843, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji 512 na watumishi wapya wa hospitali za mashirika ya kidini na hiari 1,240.

Amesema Serikali itaajiri watumishi 14,841 wa kada mbalimbali ikiwemo wahadhiri wa vyuo vikuu vyote vya umma nchini pamoja na kada nyingine ambazo haziko kwenye sekta zilizoainishwa awali.

Hata hivyo, amesema watumishi 92,619 wa kada mbalimbali watapandishwa vyeo na watumishi 2,360 watabadilishwa kada katika utumishi.

Amebainisha kuwa maelekezo yatakayotolewa wakati huo ni kuchambua na kuhakiki madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa umma 17,699 yenye thamani ya Sh37.47 bilioni na kuchukua hatua ipasavyo.

Aprili 15, 2021 Serikali ya Tanzania ilieleza matarajio yake ya kuajiri watumishi wapya 44,811 katika mwaka wa fedha 2020/21.

Hayo yalielezwa na aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika wakati akiwasilisha bajeti yake kwa mwaka huo wa fedha.

Alitaja ajira hizo mpya kuwa ni kada ya elimu (13,529), afya (10,467), kilimo, mifugo na uvuvi (2,145) Jeshi la Polisi (2,725), magereza (685), Jeshi la Zimamoto (501), uhamiaji (495) na hospitali za mashirika ya kidini na hiyari (1,262).

Chanzo: MWANANCHI
Tena hawa wakiajiriwa inakuwa ni chanzo cha mapato ya serikali kupitia kodi.
 
uongo vyuo vyetu vyote ukijumlisha vinatoa graduate 1200 tu wa ualimu kwa mwaka ukipiga kwa miaka 20 nyuma ni elfu 24 tu!! hiyo laki tano umeitoa wapi?
we
uongo vyuo vyetu vyote ukijumlisha vinatoa graduate 1200 tu wa ualimu kwa mwaka ukipiga kwa miaka 20 nyuma ni elfu 24 tu!! hiyo laki tano umeitoa wapi?
wewe ndo muongo, nimemaliza UDSM 2015 namba yangu 01366 surname yangu inaanza na M , rafiki yangu surname yake A inaanza reg no yake ni 00730 sasa mwenye surname inayoanza na na Z atakuwa na reg no ngapi? Mahaba yakizid hupunguza uwezo wa kufiri, hicho ni chuo kimoja tu je hapa nchini kuna vyuo vingapi?
 
Huu ni mpango wa kuharibu legacy ya magufuli
Kwamba watu wasiajiriwe, wasipandishwe madaraja na kulipwa malimbikizo ya mishahara ili kulinda legacy ya mtu?
After all, nani hapendi kutengeneza legacy yake?
Kiongozi yeyote hata ngazi ya kijiji & kitongoji lazima uwe na followers.
Utawapataje kama siyo kwa kutenda yanayostahili kutendwa kwa wakati?
 
Serikali kuajiri kwa wingi wakati huu iko sahihi sababu asilimia kubwa ya miundo mbinu iomeshajengwa hivyo mfanyakazi wa serikali hata akijikopea kagari kake used kataweza kudumu bila shida barabara nyingi nzuri

Kinachotakiwa kwa sasa serikali isiongeze sana miradi mipya iwe kidogo sana imalizie iliyopo ili serikali iwe na extra ya kulipa wafanyayakazi nyongeza nk

Bajeti ya miradi ya maendeleo inabidi ishuke sana hili kila mwananchi anatakiwa kulijua kuwa huwezi kila siuku familia ile pilau hela ukiwa nayo ndogo na wakati huo huo ujenge gorofa!!!
Unarudi nyuma au unarudi kinyume kinyume?! Unamsaliti mwendazake kwa kumbusuuu?!!
 
Huu ni mpango wa kuharibu legacy ya magufuli

Waganga na walozi nao warudishe vile vibao vyao vya kutangaza amali zao mabarabarani na mitaani. Mwendazake aliwaharabia ajira zao pale alipo hamasisha kumtegemea Mungu kwanza.

Na watapiga fedha wakiongezea kwenye matangazo yao kuwa wana dawa ya kinga ya jini funika legacy kutoka Anjuan.
 
Binafsi sikubaliani na huu mfumo wa ajira wa sasa wa kutegemea ajira za serikali tu.

Serikali iboreshe mazingira watu wengi waajiriwe na sekta binafsi.

Serikali itaajiri hadi lini? Kwa presha ya sasa itabidi kila mwaka serikali ilazimike kuajiri ili kuwaziba watu midomo lakini hii sio njia nzuri ya kutatua tatizo.

Kwa mtindo huu wa kutegemea ajira za serikali na serikali ikawa inaajiri kila mwaka itafika wakati mapato yote na makusanyo yanaishia kwenye kulipana mishahara tu.

Serikali kwanza irekebishe mifumo, isambaze pesa sekta binafsi. Pili ipitie upya muundo wa watumishi wake. Unaenda shule za mjini waalimu 80, shule za vijijini waalimu 2.

Kabla ya kufikiria kuajiri, kwanza pitia miundo upya, boresha mazingira ya hao watumishi waliopo watafanya kazi kwa morali, mfano mwalimu leo analipwa 720,000. Unataka utajiri mwalimu mwingine, wakati hiyo hela ya mwalimu mpya ukiboresha mazingira kwa mwalimu aliepo ukamlipa 1M ama 1.1M, huyu atakua moralized sana na atafanya kazi hata ya waalimu 2.

Tuboreshe sekta binafsi kwanza, pili tuboreshe maslahi ya watumishi tulionao kabla ya kufikiria kuajiri wapya.
Mh. Hakimu unaweza kutuambia kuwa...
Je, watu waliosomea ualimu wanaweza kuajiriwa katika sekta gani binafsi tofauti na shule za binafsi licha ya kuwa waajiri katika shule hizi wanawasimanga walimu wahanga wa ajira? Na ni kwa kiwango gani sekta binafsi inaweza kutoa ajira kwa walimu?...
Je, ni maeneo gani mtu aliyesomea ualimu yaani MWALIMU anaweza kujiajiri tofauti na kufundisha?
.
ANGALIZO: Hadhi ya walimu iheshimiwe kwani kuna watu walioshiba hadi kusahau wengine hawakawii kuwaambia walimu kuwa wasitegemee serikali iwaajiri kwani kuna fursa nyingi za kujiajiri hata kuokota chupa za plastic, vyuma chakavu, n.k kuwa nazo ni fursa tosha ambazo mwalimu anaweza kuzitumia kujiingizia kipato!
Narudia hayo ni maneno/mawazo ya watu walioshiba na kuwasahau wenye njaa!
 
Back
Top Bottom