Serikali imeninyang'anya korosho zangu

Serikali imeninyang'anya korosho zangu

Story ya kutunga..hakuna mtu amedhulumiwa korosho zake..kama yupo aende mahakamani
wewe mburula wa lumumba hata korowShow yenyewe huijui unakurupuka kaababako jiwe[emoji196] [emoji90]
 
Wape Notice ya Siku 7 wakigoma kukupa haki yako....Wasomee Al'badir uone kama itamuacha mtu, nakuahidi haitamuacha mtu! Dhulma sio nzuri...
 
Kwani mkuu hakuna pakwenda kushtaki?????
Jalibu kushtaki au tafuta au sambaza taarifa hizi kwenye tv watanzania wengine wasikie.
Kesi ya ngedere ukimpelekea nyani unadhani kuna maajabu yoyote yatatokea! Aliodhulumu serikali, unaenda kuishtaki dola kama nani? Tena usishangae we ndio ukaishia jela pamoja na kwamba ndie mlalamikaji!
 
Aisee so pain, nalia sijui nianzie wapi.

Baada ya kukaa bila ajira niliamua kujiajiri bihashara ikawa ngumu, ikabidi nibadilishe aina ya bihashara, kutokana na ndugu yangu alifanya biashara ya Korosho na ikamlipa nikaamua na mimi kutafuta riziki kupitia korosho.

Sikua na mtaji mbaba mmoja ni family friend alikuwa amestaafu so pensheni alikuwa nayo basi akanionea huruma na kunikopesha milioni kumi(10m).

Basi nkaenda kusini aise wananchi walikuwa na hali mbaya yaani mtu mwenyewe ndo anakuletea au kukuitia korosho, basi nilinunua tena bila kumlazimisha mkulima, bali mkulima ndo anakuomba ununua maana hata pesa ya sukari anakuwa hana.

Serikali walipokuja kuhakiki wakaniuliza kama nina shamba nkawaambia sina, me nimekuja kufanya bihashara kama mtanzania maana ni haki yangu kuishi popote,

Bila huruma wakataifisha korosho zangu, nilizimia baadae nkazinduka, Baba alipopata tarifa naye alizima gafra.

Mzee aliyenisave hela ananidai na serikali imechukua Korosho zangu.

Basi Baba ameamua kumuuzia shamba letu maana hakuna jinsi ya kulipa deni.

Naichukia sana Tanzania, sahivi naisi kujitoa muhanga.
pole sana
 
Kahawa ya mkoa wa Kagera imeishia Uganda Museveni hana shida kwa wajasiliamali wanaojuwa kujiongeza labda usiguse uraisi wake.Waganda wakija Tanzania wakikuta bei ya mkulima ni shs 1,000 wao wako tayari kuongeza ifike TSHS 2,000 au 1,800.pale mpakani Idara ya forodha ya Uganda haijali au hata kuuliza mali hiyo ya kahawa walanguzi wanaitowa wapi? labda ukitoa kahawa kutoka Uganda kuileta Tanzania hapo utaulizwa.Je sisi watanzania tuna weledi zaidi kuliko wenzetu Waganda?
 
Pole sana mdau,nafahamu suala kama hili linaumiza sana esp pale ambapo ulikopa fedha kwa nia ya kupata chochote.
Aidha nakushauri usiichukie Tanzania endelea kujivunia uwepo wa Nchi yako hayo uliyofanyiwa utalipwa na jambo jingine tena.
Kuwa na subira.
 
Pole sana lakini hujatwambia ulikua unanunua kwa kilo bei gani? Je ulijiuliza kwanza kama biashara unayoenda kufanya kisheria inakatiwa lesseni? Ulikua nayo Leseni? Je TIN ya TRA unayo pia?
Hebu tuacheni ungese watanzania wenzangu, hakuna asiyejua sekeseke la korosho mwaka huu lilivyotikisa vyombo vya habari. Mie mwenyewe ilibaki kidogo niwe muhanga wa hilo sakata ila kilichonisaidia ni subira...sikuweka hela mpaka mnada wa kwanza ulipopita nikaona mambo hayaeleweki nikavunga!
Hebu acha kujifanya wazimu kwamba hujui biashara nyingi za vilimo zinaendeshwa kienyeji hapa nchini, unaropoka tu kama vile babu yako alikuwa na TIN namba na leseni ya kulimia kahawa na maharage.
 
Kwahiyo njia nzuri ni serikali kuchukua korosho zao? Kama wana vikundi nina uhakika wamewekeana utaratibu wa kushughulikiana ikiwemo namna ya kulipa na ukishindwa kulipwa wanakuchukulia hatua gani? Hilo la tumbaku usinibishie nina ishi kwenye jamii ya wakulima wa tumbaku, middle ni wengi sana.
labda nikuulize kwenye tumbaku ukibainika umeuza mtumba/bello kimagendo (kwa mfanyabiashara) hatua gani huchukuliwa

kwenye tumbaku yapo sana ila si halali, hii imepelekea mtu wa kati kutajirika huku wakulima wakibaki wakilipiana madeni na hali mbaya

tumbaku haitambui mkulima mwenye tumbaku huku hajachukua pembejeo na hii imepelekea mwaka jana chama cha msingi katavi kufanya tathimini walio zalisha kuliko walivyo chukua

Narudia tena kukwambia hakuna sehemu mtu wa kati katika korosho tumbaku anapo ruhusiwa sema tunaishi kimazoea

Tumbaku wanauza kwa namba, baada ya mjumbe kupeleka majina ya watu na uzalishaji wao. huyo mtu wa kati anapata wapi namba na kiasi cha uzalishaji(kama sio dili)
 
Nenda mahakamani acha ufala. Wewe kma unsushahidi wa kutosha kuwa wamekunyanganya nenda kwashtaki na iyokesi watakuja wengi kibao yu watawaunga mkono. Tafta ushahidi maana wao watajitetea kuwa leta ushahidi kuwa ulinyanganywa na kiasi gani. Ila wakishaconfarm kuwa ulinyanganywa kweli lazima kesi uwashinde
 
Uko sahihi mkuu na nakubaliana na wewe, lakini tusitumie fursa kuwakandamiza wakulima wanyonge..ni kweli serikali kuna sehemu inakosea kama vile kuchelewa kupeleka fedha kwa ajili ya kununua mazao kwa wakati jambo ambalo mkulima mdogo hawezi kuvumilia kusubiri. Mtoa uzi alichofanya hapa ni kutafuta huruma ya wana jf na ameipata bila kuangalia wakulima wangapi wameumia kwa kumpelekea korosho zao hata kama walikuwa hawapendi.
Chief, mimi naamini kwamba kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake. Tusilazimishe kukomoana kwa kuwa tu mtu ana mtaji wake na tumeshajua kuwa amegomesha kutetea maslahi yetu. Kamba ya hao walivyokuwa Wakulima ilikuwa haiwaruhusu kungojea fedha za msimu, kwa maana nyingine hata wewe "Kama" una nafasi nzuri kifedha na upo kijijini bado kuna mkulima angeweza kuja kwako mkapatana na akaweka bond mavuno yake yote ya mwaka kabla ya msimu wa kununua. Ni hali duni ya Wakulima ndiyo imeruhusu wawepo wachuuzi hawa ambao mimi naona hakukuwa na ulazima wa kufanyia haya. Pesa amekula mkulima kwa hiari yake, leo tunataifisha mali ya mchuuzi, kesho tunasema tunaondoa umaskini...
Labda
 
  • Thanks
Reactions: BRN
hayo mahindi wanakopeshwa pembejeo

hayo mahindi yako chini ya ushirika.

unaleta mifano usiyo na mfanano, leta tumbaku, pamba alafu utwambie lini umewahi ona mtu akanunua marobota na marobota ama mitumba ya tumbaku kwenda kuuza kama mahindi
Kwa taarifa yako wakulima wa korosho huuza kiasi kidogo sana chini ya robo ya korosho zao zote kwa hao wanunuzi wadogowadogo ili wapate hela ya kujikimu wakati wakisubiri mnunuzi mkuu yaani vyama vya ushirika. Hapa hakuna athari yoyote kwa mkulima na chama chake cha ushirika. Lakini zaidi ni kwamba hata baadhi ya hao wakulima wenyewe wametapeliwa na serikali kwa madai kwamba korosho waliyouza ni nyingi kuliko uwezo wa mashamba yao. Hakuna shaka serikali hii imedhulumu watu haki zao kwenye hili sakata la korosho.
 
Aisee so pain, nalia sijui nianzie wapi.

Baada ya kukaa bila ajira niliamua kujiajiri bihashara ikawa ngumu, ikabidi nibadilishe aina ya bihashara, kutokana na ndugu yangu alifanya biashara ya Korosho na ikamlipa nikaamua na mimi kutafuta riziki kupitia korosho.

Sikua na mtaji mbaba mmoja ni family friend alikuwa amestaafu so pensheni alikuwa nayo basi akanionea huruma na kunikopesha milioni kumi(10m).

Basi nkaenda kusini aise wananchi walikuwa na hali mbaya yaani mtu mwenyewe ndo anakuletea au kukuitia korosho, basi nilinunua tena bila kumlazimisha mkulima, bali mkulima ndo anakuomba ununua maana hata pesa ya sukari anakuwa hana.

Serikali walipokuja kuhakiki wakaniuliza kama nina shamba nkawaambia sina, me nimekuja kufanya bihashara kama mtanzania maana ni haki yangu kuishi popote,

Bila huruma wakataifisha korosho zangu, nilizimia baadae nkazinduka, Baba alipopata tarifa naye alizima gafra.

Mzee aliyenisave hela ananidai na serikali imechukua Korosho zangu.

Basi Baba ameamua kumuuzia shamba letu maana hakuna jinsi ya kulipa deni.

Naichukia sana Tanzania, sahivi naisi kujitoa muhanga.
Serikali imesahau kabisa issue kuna chain katika biashara, wanaamini katika kumiliki shamba,
 
wewe ulikuwa unawatapeli wakulima, ulikuwa unakitapeli chama kilicho mpa mkulima pembejeo

eti nikaweka m10, unajua pembejeo za kustawisha iyo korosho zilipo toka.

ko ulipo taka didimiza chama cha ushirika unaona ulikuwa sawa
Unaongea kinadharia zaidi, sio lazima mkulima.akope pembejeo kwenye chama cha ushirika, na hata akikopa hachukui mkopo unaozidi thamani ya mazao yake.

Hivyo anaweza kuamua kuwa sehemu ya mavuno apeleke ushirika na sehemu nyingine auze kwa cash ili aweze kukidhi mahitaji ya kifamilia hasa ukizingatia.kuwa kwenye chama inachukua muda kupata malipo.

Wakulima hapaswi kulazimishwa kupeleka mazao yote ushirika anaweza kushindwa hata kuhudumia familia
 
Uko sahihi mkuu na nakubaliana na wewe, lakini tusitumie fursa kuwakandamiza wakulima wanyonge..ni kweli serikali kuna sehemu inakosea kama vile kuchelewa kupeleka fedha kwa ajili ya kununua mazao kwa wakati jambo ambalo mkulima mdogo hawezi kuvumilia kusubiri. Mtoa uzi alichofanya hapa ni kutafuta huruma ya wana jf na ameipata bila kuangalia wakulima wangapi wameumia kwa kumpelekea korosho zao hata kama walikuwa hawapendi.
Kufanya biashara na mtu japo hupendi sio kigezo kuwa umedhulumiwa, nimeshawahi kuuza gari kwa bei ya chini kwa sababu ya dharura zangu na kutaka kwangu na kwa hiyo alienunua hakuwa amenidhulumu
 
Unaongea kinadharia zaidi, sio lazima mkulima.akope pembejeo kwenye chama cha ushirika, na hata akikopa hachukui mkopo unaozidi thamani ya mazao yake.

Hivyo anaweza kuamua kuwa sehemu ya mavuno apeleke ushirika na sehemu nyingine auze kwa cash ili aweze kukidhi mahitaji ya kifamilia hasa ukizingatia.kuwa kwenye chama inachukua muda kupata malipo.

Wakulima hapaswi kulazimishwa kupeleka mazao yote ushirika anaweza kushindwa hata kuhudumia familia

Naomba nikwambia tu ukweli hujui chochote kuhusu ushirika wala hujawahi hata kuwa karani katika ivyo vyama

ingekuwa hivyo tumbaku, pamba, korosho zisinge kuwa zinauzwa katika vyama vya ushirika wangeuza masoko huria.

Vyama haviruhusu mkulima kujigharamia pembejeo ingekuwa ni ruhusa basi wakulima wangeuza watakapo bila ya kupitia vyama vya ushirika.

unaongea hata usivyo vijua et"huwezi chukua mkopo kuliko thamani ya mazao" thamani ya mazao hujulikana baada ya kuuzwa (hapo unakuwa usha chukua mkopo) ingekua hivyo wakulima wasinge kuwa wanalaza madeni ya pembejeo.

mkuu huna uzoefu wowote na hili jambo nimekuwa karani wa vyama vya msingi kwa misimu 3 nafahamu nacho zungumza.
 
Back
Top Bottom