Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,752
- 218,339
Akizungumza mbele ya maelfu ya wananchi kwenye mkutano Mkubwa wa hadhara , Makamu Mwenyekiti wa Chadema , amesema kwamba , Tangu aliposhambuliwa kwa Risasi hakuna yeyote aliyekamatwa wala hakuna uchunguzi uliofanyika hadi sasa .
Amedai kwamba hapo awali , alidhani haukufanyika uchunguzi kwa vile aliyewatuma wauaji wakati huo alikuwa Rais , kwahiyo ingekuwa vigumu kujikamata na kwamba IGP wa wakati huo alikuwa Sirro , lakini sasa Rais ni Samia na IGP ni Wambura .
Tundu Lissu ameendelea kuhoji kwamba , Sasa kama viongozi wale wa zamani wamebadilika na wale wabaya wameondoka , hawa wema akiwemo tunayesema NANI KAMA MAMA , Mbona wahalifu hawa hawakamatwi ?
Ujumbe wake huu hapa