Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

20220326_212520.jpg
 
Kuna wawili hapo imebidi tu niscreenshot hii comment niwatumie whatsapp vinginevyo hizo tags zako wasingeziona zingeenda bure tu. Na nimewatumia maana hata mimi mwenyewe siyo siri nimemiss kuwaona humu.

Kiukweli mwenyewe huu uzi umenifanya nifahamiane na baadhi ya watu ambao nilikuwa nawakubali sana humu na nilikuwa sijui hata kama watakuja kukubali kufahamiana na mimi. But leo hii tumefahamiana and we are friends.

Sijawahi fahamiana na mkaka huku then akaja kuwa mpenzi wangu hilo nilishakataa na halikuwa lengo langu since the very first day najiunga jf na nashukuru Mungu nimefanikiwa hilo. So hakuna Mkaka ambaye nimewahi date naye humu.

Wengi niliofahamiana nao ni wanawake and some of them are like sisters to me now yaani tumekuwa kama ndugu. Kwa wanaume ambao nimefahamiana nao walionitongoza urafiki ulikufa hapo hapo kwa sababu sikutaka mahusiano.

Mie nilitaka urafiki tu na kama unavyojua wanaume huwa wakitongoza mwanamke akawakataa wanapotezea. Wenzetu huwa hawataki habari za kuwa friendzoned so automatically mawasiliano yanakufa maana hamna cha kuongea tena.

Na mimi ndicho huwa ninachotaka kwamba kama mwanaume ukiona hauwezi kuwa rafiki kwangu basi njia nyeupe kiroho safi tu. Maana sitaki mahusiano na vile vile huwa sibembelezagi mtu kwangu ni either uwe rafiki au salam zao tu na siyo kwa ubaya.

Ofcourse wapo wanaume wachache ambao Hawana tatizo kuwa friendzoned maana wanajua siyo sifa kukulana na kila mwanamke unayefahamiana naye na wanaume wa hivyo mimi huwa nawasalute ile mbaya yani. All in all this is JF mkuu.
Dada naomba nikutoe out, bill juu yangu
Umeongea kitu cha maana mno.
 
Haha ongea tu mama mchungaji mimi hili jambo muda mrefu sana huwa natamani nilianzishie uzi sema nakosa maneno mazuri ya kuweka ili nieleweke

Seriously mimi napenda sana kuwa na marafiki wa kiume zaidi kuliko wa kike yaani kwa lugha rahisi napenda zaidi kuwa na washikaji kuliko mashost

Ila tatizo moja tu hawa kaka zetu wanapofeli wanadhani kwamba kila mwanamke anapenda hayo mambo ya friends with benefit ama kukulana kimasihara kama wenyewe wanavyoita kumbe wengine wala hatuentertain hayo mambo
ila dada una upiga mwingi mnoo.
 
Em anzisha uzi siku moja; tusikie from men's perspective. Inawezekana sisi tumeshindwa kuwaelewa. Ila Mimi ninachoamini ni kwamba; urafiki wa dhati kati ya ke na me unawezekana kabisa, pasipo kuhusisha ngono.

Wakati mwingine unashindwa hata kumtreat me vizuri; maana ukimchekea tu anahisi huyu tayari ameshaingia laini, kumbe hata wazo huna
wee fidodido hebu soma hapa lol.
 
Sasa yeye atajuaje kama huyo mtu atamtongoza? Imagine mtu kakusalimia tu; unaanza kumwambia "sihitaji mahusiano kwa sasa". Kwamba Kila me anakuja tu kukutongoza? Au mimi ndiyo sielewi haya mambo, najifanya msemaji wa wanaume?
 
Boss Lady angekuwepo hapa usingeona mijadala hii ya ajabu ajabu. Picha yake moja tu inazima mijadala yote mara moja. Sijui leo kapotelea wapi. Shida tupu yaani!
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 nipo msukuma nivile nasoma tu na kupita mie sio muongeaji kabisa.... watu wana freedom of expression msukuma let them speak wasisahau kuutendea haki uzi tu..
 
Back
Top Bottom