Nuzulati
JF-Expert Member
- Nov 25, 2020
- 10,675
- 39,092
Kuna wawili hapo imebidi tu niscreenshot hii comment niwatumie whatsapp vinginevyo hizo tags zako wasingeziona zingeenda bure tu. Na nimewatumia maana hata mimi mwenyewe siyo siri nimemiss kuwaona humu.
Kiukweli mwenyewe huu uzi umenifanya nifahamiane na baadhi ya watu ambao nilikuwa nawakubali sana humu na nilikuwa sijui hata kama watakuja kukubali kufahamiana na mimi. But leo hii tumefahamiana and we are friends.
Sijawahi fahamiana na mkaka huku then akaja kuwa mpenzi wangu hilo nilishakataa na halikuwa lengo langu since the very first day najiunga jf na nashukuru Mungu nimefanikiwa hilo. So hakuna Mkaka ambaye nimewahi date naye humu.
Wengi niliofahamiana nao ni wanawake and some of them are like sisters to me now yaani tumekuwa kama ndugu. Kwa wanaume ambao nimefahamiana nao walionitongoza urafiki ulikufa hapo hapo kwa sababu sikutaka mahusiano.
Mie nilitaka urafiki tu na kama unavyojua wanaume huwa wakitongoza mwanamke akawakataa wanapotezea. Wenzetu huwa hawataki habari za kuwa friendzoned so automatically mawasiliano yanakufa maana hamna cha kuongea tena.
Na mimi ndicho huwa ninachotaka kwamba kama mwanaume ukiona hauwezi kuwa rafiki kwangu basi njia nyeupe kiroho safi tu. Maana sitaki mahusiano na vile vile huwa sibembelezagi mtu kwangu ni either uwe rafiki au salam zao tu na siyo kwa ubaya.
Ofcourse wapo wanaume wachache ambao Hawana tatizo kuwa friendzoned maana wanajua siyo sifa kukulana na kila mwanamke unayefahamiana naye na wanaume wa hivyo mimi huwa nawasalute ile mbaya yani. All in all this is JF mkuu.
