Selfika na JF: Snap it. Show it

Brother wala hakuna haja ya kufanya character assessment kupitia huu uzi, utawakosea warembo wa watu.

Waache wateme sumu zao wiki nzima waliteseka nyuzi zisizikuwa na mpango, fikiria mdada wa wa watu kapost picha yake mtu kaichukua kaizoom na kukandia sijui kavaa ndala na maneno mbovu mbovu kibao, lakini anasahau hao ni wadogo zetu ndo wamemaliza masomo au ndo wanaanza hustling za maisha, unaweza kumkosoa kwa kumfata pm au ukamkosoa in a good way lakini si kumbeza jukwaani kumdhihaki ili mradi tu.

Halafu kwenye haya maisha kweli unaweza kumdhihaki mtu kisa viatu sijui kiuchumi hayuko sawa, leo utamcheka kavaa ndala kesho yake unakatatika miguu kwa ajali hata hizo ndala huwezi kuvaa tena.
Haya maisha kuna watu wanajisahau sana hukatazwi kumsifia mwanamke wako offcourse ndo tunavyopendwa kusifiwa n wanaume zetu ila ukinisifia mimi siyo uwaponde wanawake wengine, thats not cool na msukuma wangu kaniambia haipo kwenye katiba ya kiumeni.
 

Sina uhakika kama haya uliyoyaandika yanahusiana kwa namna yo yote na comment yangu uliyoikwoti. Labda sijaelewa.

JF hapa, kama ilivyo huko mitaani, kuna watu wa kila aina. Hapa tumechangamana watu wa makuzi tofauti, elimu tofauti, uchumi tofauti, exposure tofauti, morals tofauti, mitazamo tofauti...na ukilijua hili basi hakuna kitakachokushangaza hapa. Na mimi naamini utofauti wetu huu ndiyo unaifanya JF kuwa hivi ilivyo. Nilichojifunza hapa ni kuvumiliana tu kwa sababu kamwe hatuwezi kuwa sawa.....

Anyway nimefurahi kusikia kuwa una dume la Kisukuma. Hakuna wanaume wanaojitambua kama Wasukuma; na wao wakipenda basi wamependa. Pamoja na "ushamba" wao lakini Wasukuma ndiyo mpango mzima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…