Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

7274393A-D59B-48BB-935F-909C9C9CB32E.jpeg
 
Inshallah

Tukijaaliwa uzima na afya mama ...na mimi niyapate mawaidha yako mubashara

Yani basi purukushani tu nilikuwa hukoo wanapaita mlimba sijui



Haki Morogoro ni kubwa kuliko Tanzania.jamani nilikaa kwenye gari kutoka dar to moro Town..moro Town mpka ifakara,ifakara tu mlimba.mlimba tu ndani ndani huko..jamani jamani waaaahiii uvumilivu ukanishinda ikabidi nimuulize jirani yangu “samahani dada eti tunaenda mbinguni”kha!!
Morogoro ndani ndani huko kama barabara ni mbovu aise ni bora kusubiri jua liwake barabara ichangamke kwanza maana...

Sasa ngoja nikuchekeshe siku hiyo akati narudi mvua ilikuwa inanyesha niko kwenye boda natoka kijijini huko kwenda mlimba stand nikastuka boda anapunguza mwendo nikamuuliza Chief Vipi mbona umepunguza mwendo?akasema dada kuna mteremko na utelezi mkali hatua chache ..hapo mvua imekata kama dk 10 kumbukahata kabla sijamaliza kutafakari itakuwaje...nikajikuta niko chini na udongo ulivyo wa mfinyanzi...loh hapo Naendelea kuserereka tu usisahau niko juu ya kilima...napiga jicho kushoto na kulia simuon boda wala boda yenyewe

Ikabidi sasa nitumie mbinu za kivita na za kimkakati kuzuia kuserereka,kibegi kipo juu juu kama antena (jamani...)
Nikanasa,niko katikati ya giza totoro kumi na moja kasoro hiyo katikati ya mlima ikabidi nimuombe boda nae atumie mbinu za kivita ili asiendelee kuserereka akaniacha mwenyewe kilimani wooooiii namkuta chini kule amekula tope matata sana hakuna wa kumpa mwenzie lawama.ilibidi kubadilisha nguo nilipofika standna huo ndo ulikuwa utalii wangu wa ndani..khooooo

Tuondelee kuomba uzima na afya tutakuja kuonana nao tu.

Huwa sifurahishwi na watu kugombana gombana aise..kama mmeelewana ni vyema kabisa binafsi ninalifurahia hilo..ona jinsi ilivyovyema na kupendeza...ndugu wakae pamoja kwa umoja.

Yaani ni umenichekesha kupita maelezo jamani, pole kwa mkasa. Eti simuoni boda wala boda yenyewe
 
Hhaahahahaahaha endelea kuchochea karama yako ya uvumilivu. Umenichekesha sana hapo mwishoni.

Bana mimi huwa nikiamua kuonana na mtu, nanyoosha tu na milonjo yangu sina habari. Ni vile siku hizi nazeeka + majukumu, kuna muda nakwama. But tuombe uzima bana, tutaonana mdogo angu.


Dada sisi siyo mafeminist ila ni vile tu wanaume wa jf wakiishiwa hoja ndiyo wanatumia hilo neno kama defensive mechanism

Nakukubali sana dada yangu mzuri mzuri nkamu gwangu nawe ubarikiwe mpaka ushangae. Daah siku nikikuona sijui nitafurahije aise ila ndiyo najua siyo leo wala kesho wala mwaka huu.

Nilimaanisha hadi ufahamiane na mtu basi ni umempenda sanaaa au umemuamini sanaaa. Ndiyo maana mimi nikawa nawaza sijui nakuanzaje.

Au niendelee kumtazamia Bwana
 
Back
Top Bottom