Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Haki Morogoro ni kubwa kuliko Tanzania.jamani nilikaa kwenye gari kutoka dar to moro Town..moro Town mpka ifakara,ifakara tu mlimba.mlimba tu ndani ndani huko..jamani jamani waaaahiii uvumilivu ukanishinda ikabidi nimuulize jirani yangu “samahani dada eti tunaenda mbinguni”kha!!
Morogoro ndani ndani huko kama barabara ni mbovu aise ni bora kusubiri jua liwake barabara ichangamke kwanza maana...

Sasa ngoja nikuchekeshe siku hiyo akati narudi mvua ilikuwa inanyesha niko kwenye boda natoka kijijini huko kwenda mlimba stand nikastuka boda anapunguza mwendo nikamuuliza Chief Vipi mbona umepunguza mwendo?akasema dada kuna mteremko na utelezi mkali hatua chache ..hapo mvua imekata kama dk 10 kumbukahata kabla sijamaliza kutafakari itakuwaje...nikajikuta niko chini na udongo ulivyo wa mfinyanzi...loh hapo Naendelea kuserereka tu usisahau niko juu ya kilima...napiga jicho kushoto na kulia simuon boda wala boda yenyewe

Ikabidi sasa nitumie mbinu za kivita na za kimkakati kuzuia kuserereka,kibegi kipo juu juu kama antena (jamani...)
Nikanasa,niko katikati ya giza totoro kumi na moja kasoro hiyo katikati ya mlima ikabidi nimuombe boda nae atumie mbinu za kivita ili asiendelee kuserereka akaniacha mwenyewe kilimani wooooiii namkuta chini kule amekula tope matata sana hakuna wa kumpa mwenzie lawama.ilibidi kubadilisha nguo nilipofika standna huo ndo ulikuwa utalii wangu wa ndani..khooooo

Tuondelee kuomba uzima na afya tutakuja kuonana nao tu.

Huwa sifurahishwi na watu kugombana gombana aise..kama mmeelewana ni vyema kabisa binafsi ninalifurahia hilo..ona jinsi ilivyovyema na kupendeza...ndugu wakae pamoja kwa umoja.
Hadithi inasisimua sana.
Ila daaa!! Mkoa wa Morogoro ni mkubwa sana.

Tumetoka Dar saa 12 asubuhi tukaingia Moro mjini saa 2:00. Ifakara saa 7:30, Mahenge saa 1 usiku, Mwaya saa 4, Iputi saa 5, Ilonga Selous Game Reserve saa 6:30 usiku.
Mkoa huo huo mmoja unatembea masaa kibao
 
Hadithi inasisimua sana.
Ila daaa!! Mkoa wa Morogoro ni mkubwa sana.

Tumetoka Dar saa 12 asubuhi tukaingia Moro mjini saa 2:00. Ifakara saa 7:30, Mahenge saa 1 usiku, Mwaya saa 4, Iputi saa 5, Ilonga Selous Game Reserve saa 6:30 usiku.
Mkoa huo huo mmoja unatembea masaa kibao
Nakumbuka mwaka juzi tulifanya utalii wa ndani kutembelea udizungwa,kiukweli mkoa wa Morogoro ndio mkoa pekee naamini unastahili kugawanywa.
Yaan tumetoka Dar saa 2,kule tunaingia saa 1 jioni.

Ila nawapongeza sana waruguru kwa kutunza uoto wa asili,sema bado swala la barabara ni tatizo kubwa,yaan barabara ya kuunganisha wilaya moja kwenda nyingine inamagorongo!
Sijui wabunge wao kama wanajali sana.
 
Hadithi inasisimua sana.
Ila daaa!! Mkoa wa Morogoro ni mkubwa sana.

Tumetoka Dar saa 12 asubuhi tukaingia Moro mjini saa 2:00. Ifakara saa 7:30, Mahenge saa 1 usiku, Mwaya saa 4, Iputi saa 5, Ilonga Selous Game Reserve saa 6:30 usiku.
Mkoa huo huo mmoja unatembea masaa kibao
Km mnaenda Sumbawanga baasi nikiambiwa nauli kutoka Moro hadi Dar elf35 naguna!kumbe ni sawa baasi!
 
Samia suluhu hassan
IMG_20210411_144609.jpg
 
Hadithi inasisimua sana.
Ila daaa!! Mkoa wa Morogoro ni mkubwa sana.

Tumetoka Dar saa 12 asubuhi tukaingia Moro mjini saa 2:00. Ifakara saa 7:30, Mahenge saa 1 usiku, Mwaya saa 4, Iputi saa 5, Ilonga Selous Game Reserve saa 6:30 usiku.
Mkoa huo huo mmoja unatembea masaa kibao
Kiukweli nikiulizwa Tanzania na Morogoro ipi ni nchi😁😁nitasema Morogoro(kidding..)ila tuache masihara bhana nafikiri Morogoro Ndio mkoa mkubwa sana Tanzania jamani..

Ila kwa mchana ni pazuri sana unafanya utalii wa ndani..japo barabara ni changamoto..
 
Nakumbuka mwaka juzi tulifanya utalii wa ndani kutembelea udizungwa,kiukweli mkoa wa Morogoro ndio mkoa pekee naamini unastahili kugawanywa.
Yaan tumetoka Dar saa 2,kule tunaingia saa 1 jioni.

Ila nawapongeza sana waruguru kwa kutunza uoto wa asili,sema bado swala la barabara ni tatizo kubwa,yaan barabara ya kuunganisha wilaya moja kwenda nyingine inamagorongo!
Sijui wabunge wao kama wanajali sana.
Suala la kutunza mazingira Morogoro ni la kimila.
Misitu ya asili ya mkoa huo bado inatunzwa na kuzalisha mvua za kutosha kila siku.
Ndiyo maana mpaka sasa bado wameweza kuhifadhi maji mengi kwenye mito ya mkoa huo kuliko mkoa wowote ndani ya jamuhuri ya Tanzania.
 
Haki Morogoro ni kubwa kuliko Tanzania.jamani nilikaa kwenye gari kutoka dar to moro Town..moro Town mpka ifakara,ifakara tu mlimba.mlimba tu ndani ndani huko..jamani jamani waaaahiii uvumilivu ukanishinda ikabidi nimuulize jirani yangu “samahani dada eti tunaenda mbinguni”kha!!
Morogoro ndani ndani huko kama barabara ni mbovu aise ni bora kusubiri jua liwake barabara ichangamke kwanza maana...

Sasa ngoja nikuchekeshe siku hiyo akati narudi mvua ilikuwa inanyesha niko kwenye boda natoka kijijini huko kwenda mlimba stand nikastuka boda anapunguza mwendo nikamuuliza Chief Vipi mbona umepunguza mwendo?akasema dada kuna mteremko na utelezi mkali hatua chache ..hapo mvua imekata kama dk 10 kumbukahata kabla sijamaliza kutafakari itakuwaje...nikajikuta niko chini na udongo ulivyo wa mfinyanzi...loh hapo Naendelea kuserereka tu usisahau niko juu ya kilima...napiga jicho kushoto na kulia simuon boda wala boda yenyewe

Ikabidi sasa nitumie mbinu za kivita na za kimkakati kuzuia kuserereka,kibegi kipo juu juu kama antena (jamani...)
Nikanasa,niko katikati ya giza totoro kumi na moja kasoro hiyo katikati ya mlima ikabidi nimuombe boda nae atumie mbinu za kivita ili asiendelee kuserereka akaniacha mwenyewe kilimani wooooiii namkuta chini kule amekula tope matata sana hakuna wa kumpa mwenzie lawama.ilibidi kubadilisha nguo nilipofika standna huo ndo ulikuwa utalii wangu wa ndani..khooooo

Tuondelee kuomba uzima na afya tutakuja kuonana nao tu.

Huwa sifurahishwi na watu kugombana gombana aise..kama mmeelewana ni vyema kabisa binafsi ninalifurahia hilo..ona jinsi ilivyovyema na kupendeza...ndugu wakae pamoja kwa umoja.

Si unaziona ila akili zako

Khaa ndiyo nini kunichekesha hivi mtoto wa mwanamke mwenzio? Nimeanza huo mstari wa kwanza tu nimecheka kwa nguvu sasa hadi namaliza comment yote ikabidi niweke kwanza simu pembeni ili nimalize kucheka!

Eti Morogoro ni kubwa kuliko Tanzania daah kiukweli naungana na wale waliosema huo mkoa ugawanywe jamani. Kwa kweli huo utalii wa ndani nimeupenda yaani kama nakuona vile ulikuwa unaserereka na kibegi.

Mngekuwa maeneo ya mjini mjini halafu watu wangeona hilo tukio haki mngeshikwa uchawi maana wabongo hatuchelewi! Mie hizi safari ndefu za siku kadhaa ndiyo nazipenda ila tu huo usafiri uwe na kila kitu ndani mfano sehemu za kula na kulala ila siyo ule usafiri ambao utakulazimu kushuka kwenda kula au kulala na ndiyo maana mie napenda sana treni!

Hahaha nilimaanisha mwenye picha ndiye alinielewa tukayamaliza yule aliyesambaza kwa kweli sijawahi kumtafuta wala kumuuliza chochote hadi leo nimeona nimsamehe na nijikalie tu kimya! Ila kiukweli kupatana ni jambo jema sana mwenyewe huwa sipendi malumbano na nikiona naelekea kugombana na mtu basi ni either nitajishusha au nitakaa kimya tu ili tusifikie kwenye ugomvi!
 
hakika sijawahi kujua kama ninachoandika wakati mwingine kina kuwa kimekaa kikomedi


Yaani hata Khantwe naye anasemaga hivyo hivyo kuwa anashangaa kwanini watu wanacheka anayoyaandika wakati yeye anayaonaga ya kawaida. Ukiona watu wengi wanasema hivyo basi ujue kweli vinachekesha ila tu wewe mwenyewe unakuwa haunotice hicho kitu.
 
Back
Top Bottom