Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Ningetaka kujipa ujiko ningesema kweli ni abroad ila ni vile tu haina maana,, Rovos huwa inakuja bongo kila mwaka mkuu na siku hiyo ilikuwa kama zali tu tumeingia kutoka mbeya tunaikuta pale tazara dar imepark ndiyo inajiandaa kuondoka huwa haikai sana hapa na ni bahati kuiona maana inakujaga bongo mara moja moja ndiyo maana nikaona nichukue tupicha twa ukumbusho maana moja ya ndoto zangu ni kuja kuipanda siku moja..

Cc Relief Mirzska
Inatokea nchi gani mkuu ?
 
Kitaa leo.. Kienyeji zaidi...
1573025004537.jpeg
 
Alifariki mmoja,, ila nimegundua gari ikipinduka juu chini chini juu ina uwezekano isiue watu wengi kuliko ikipinduka kiupandeupande..

Kuna siku nilienda kutembea milimani kule barabara ya chunya wakati narudi nakuta ajali ya basi ilikuwa imebeba wanajeshi wadogo wadogo ndiyo wametoka kupiga course tabora wanaenda mbeya kupewa ajira na hilo basi walikodiwa na jeshi ila ndiyo lilikuwa bovu hasa kwenye usukani

Ikafika sehemu likapinduka kiupandeupande,, kwa mara ya kwanza nilishuhudia live utumbo wa mtu unazolewa zilienda ambulance mbili na gari za jeshi ila maiti na majeruhi bado hawakuisha walikuwa wengi halafu ni vijana wadogo tu kwenye miaka 20 hivi

Walioumia sana na kufariki ni wale waliokuwa upande ambao lile basi lililalia baadaye ndiyo wakaja kulinyanyua,, ila ile barabara ya kuelekea chunya ni mbaya sana aise zile kona kona daah kama nyoka wenyewe huwa wanaziita kona za mkoa maana mkoa mzima hamna kona mbaya kama zile..
Kwenye hiyo ajali ya vijana wa jeshi nilimpoteza college mate wangu mmoja
 
Back
Top Bottom