In Harmojala mood


Kwa pamoja tutazame hapa tulipo,
Panatuonyesha picha ya mbali huko tuendako mpenzi.
Mengi utasikia yakisemwa usiyaweke moyoni,
Kuteleza inatokea mambo ya ndani usiyaweke hadharani.
Kama ndege juu turuke angani wote
Unishike nikushike ili tuwe wote mpenzi
Mvua ikinyesha iwe baraka ya penzi letu, lolote likitokea basi tuanguke na tufe wote.
Wengine amani tuliyonayo kidogo wanaiota hawana,
Tena pengine pesa si tatizo vipigo, kati yao upendo hakuna
Heri yetu sisi
Tushukuru kwa yote(tushukuru kwa yote)
Tushukuru kwa yote kipenzi changu
Tushukuru kwa yote
Asiyenipenda hakupendi hata siku moja,
Siku tunaachana ndo wanachongoja
Asiyenipenda hakupendi hata siku moja
Siku tunaachana ndo wanachongoja
Juzi nilikosea, nikakukuta unalia machozi Nilipokuomba radhi ukaelewa, samahani ikaokoa penzi.
Wengine amani tuliyonayo kidogo wanaiota hawana tena pengine pesa si tatizo vipigo kati yao upendo hakuna
Heri yetu sisi
Tushukuru kwa yote(tushukuru kwa yote)
Tushukuru kwa yote kipenzi changu
Tushukuru kwa yote
View attachment 2274391
Sent using
Jamii Forums mobile app