Sehemu gani Dar haujawahi kufika?

Sehemu gani Dar haujawahi kufika?

Bandari kubwa mkuu.

Kuna Water front,Puma, namba tatu(TPA),Bima,namba nne,kwa mo,UDA,TICS(mama lishe) TRH,Malawi cargo, East coast,Mofed, alafu Kuna bandari geti la inakoingilia mizigo ya kwenda comoros,Zanzibar na TPA Tower.

Sijui unazungumzia bandari sehemu gani Kati ya hizo.
Mimi pia Bandari sijawahi kufika, naishia kuona zile Tower tu kwa mbali nikiwa naenda Kivukoni
 
Za jioni

Miaka 20 Dar sijawahi kufika maonesho ya Sabasaba.

Wapi haujawahi kufika au unapasikia kukaa kote Dar?

Mbopo napasikia.

Kina sehemu inaitwa king'ong'o kwa kweli hapa hapana sijawahi kufika.

Kijichi.

Kivule.


Hata sijui 7 7 ipo sehemu gani, yani sijafika sehemu nyingi kweli, Maisha ya Dar yanakuamulia mambo mengi sana.
 
Zamani tulikuwa wageni wa mikoani wakifika tulikuwa tunawapeleka kutembea posta,magogoni na ferry wakapande pantoni,ila tangu alipoingia Magufuli wakaziba zile fence na ulinzi mkali. Hatuwaoni tena tausi na wanyama wa mule ndani.
Jamaa alijiona spesho sana kwenye hii ardhi, kumbe tunapita tu na sasa kashapita
 
Uzi ushavamiwa na wamkoani
Wewe labda ndio ujishangae narudia tena dar es salaam ndio mkoa mdogo kuliko mikoa yote tanzania bara usichanganye mambo elewa kama nilivyo andika kama hujui uliza wenzio ulio karibu nao
 
Dar ni mkoa wa kipekee sana ni rahisi kuidentify hali zote za maisha watu.

Nashukuru nimeishi na watu wa hali zote , nimejifunza mengi mno.
 
Kuishi kwangu hapa kawe miaka ya kutosha
Kula pombe sana kila kiwanja...ajabu beach kidimbwi napasikia tu
 
Back
Top Bottom