Sehemu gani Dar haujawahi kufika?

Sehemu gani Dar haujawahi kufika?

Magogoni Ikulu
Zamani tulikuwa wageni wa mikoani wakifika tulikuwa tunawapeleka kutembea posta,magogoni na ferry wakapande pantoni,ila tangu alipoingia Magufuli wakaziba zile fence na ulinzi mkali. Hatuwaoni tena tausi na wanyama wa mule ndani.
 
Pazuri sana mm nilikuw napita kila siku nikitoka kazini ili nione taus af nichungulie ofisi ya waziri mkuu pazuri sana sijawai ingia ndani ila nimekuona kwa nje iyo siku gets likikuwa wazi jioni wanafunga njia sasa nilitaka kufosi kupita siku iyo wanajeshi wakataka nizingua ikabidi nizunguke
Wakati niko primary nilikua na rafiki baba yake alikua anafanya kazi ikulu na walikua wanaishi humo ndani.
Tulikua tunaenda sometimes Ila getini unakaguliwa mno utafikiri umebeba bomu.
 
Ni jina tu baya ila kwa mparange na vitongiji vya buza ni Kati ya maeneo yaliyojengeka Sana kuliko sehemu nyingi sana maarufu zenye majina ya kuvutia.

Mitaa yote ina lami na inawaka taa usiku Kama ulaya. Nyumba Kali,Bei nafuu na access ya kufika sehemu nyingi za mji Kama kawe,makumbusho na CBD.

Buza ni moja ya fastest growing area kwa Temeke..Population na miundo mbinu rafiki
 
Back
Top Bottom