Jamani mbona tunatoa hukumu hata kabla ya kesi kusikilizwa? Haya ni maelezo ya upande mmoja wa utetezi, mbona tunafanya haraka kabla ya kusikia upande wa pili? Kwa maelezo haya natoa majibu ya baadhi ya maswali ambayo kwa hayo hayajatoa mwelekeo wa nani mkweli kati ya pande zote mbili.
Tumeelezwa kwenye uzi ule mwingine kuwa polisi wana clip ambayo ina utofauti na ya youtube, hivyo hatujui ni clip ipi ina mashitaka mahakamani, hivyo naona ni mapema kusheherekea. Wanasheria wanachokifanya naona ni kutafuta uhalisia wa hizo clip, kitu ambacho nadhani, huenda DPP alijilidhisha kabla ya kwenda mahakamani. Tukumbuke kuwa, kwa hapa mshitaki hajatoa vielelezo vyake. Kwangu mimi, baada ya hapo ndio nitaanza kujua mwelekeo wa kesi lakini sasa ni mapema sana, bado nipo gizani.