Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Bofya kwenye link hapo chini umtazame Tundu Lissu akielezea video ya Rwekatare na Joseph Ludovick kwenye kupanga ugaidi.

http://m.youtube.com/watch?client=mv-google&hl=en-GB&gl=US&v=yR_sm3UYJcY
 
Kwenye red hapo mkuu ina maana kuna tafsiri pana.

Kama Mwampamba alisema anamfahamu vizuri Ludovick na walikuwa wote katika uongozi wa CDM-DUCE basi upo uwezekano kuwa Shonza na Mwampamba ndio walikuwa wanatumika kuisambaratisha CDM. Sasa basi, maneno ya Ben Saanane yatakuwa na kiini fulani cha ukweli! Tunabakia na swali moja kwanini Ben Saanane alioona Zitto anastahili kuhojiwa?

Wewe ni great thinker!

Ongezea na hii Festo Richard Sanga (Original owner wa Id ya TUNTEMEKE) alikua CHASO kama kiongozi baada ya Uongozi wa Ludovick na wenzake

Mawasiliano ya Festo Sanga Jioni hii akiwa Mbeya na mtu mmoja akiwa Dar(Simtaji kwa sababu maalumu) anasema ana uhakika kabisa kwamba Lwakatare hachomoki kwenye hili suala.Richard Sanga ndiye anayesimamia shughuli zote za Blog ya William Malecela(Kiongozi ndani ya jumuiya ya Wazazi CCM aliyeko karibu sana na Nape na Mwigulu)

Tarifa za Akina Shonza,Mchange,Mwampamba na Sanga kupitia ID ya TUNTEMEKE za Tarehe 12 January (wiki mbili baada ya Mwigulu kudai anayo video)humu kwamba kuna video watakayoiweka itakayokimaliza CHADEMA kabisa na kuwakatisha Tamaa ni kielelezo kwamba walijua kilichokua kinaendelea.Wahojiwe incase hawajampata aliyeweka hiyo video Youtube

Mazingira aliyosemea Mwigulu yabaweza kuwa mazingira yaliyopangwa kwa umakini ili apingwe hapo hapo katika mazingira hayo hayo ili kuondoa suspicion ya mojawapo wa collaborator katika mchezo huo

Devis Msaki+ Mwigulu+MASALIA= - --- -- --- -
 
Unafiki mbaya sana!! unakuwa huaminiki kotekote! mwisho utaishi kiujanja ujanja kama akina Mtela Mwampamba na mkwapuaji simu maarufu hapa mjini!!
Loh!... Unalo! Ila hili hamtoki...
 
Hapo patamu ingawa meli ya CCCCM imeanza kuzama asubuhi na mapema. Sakata hili litavua watu nguo, muda ndo utasema.SUBIRINI
 
Hapo patamu ingawa meli ya CCCCM imeanza kuzama asubuhi na mapema. Sakata hili litavua watu nguo, muda ndo utasema.SUBIRINI

Naona humu ndani wameadimika kwelikweli. Wameanza kupata wasiwasi dhidi ya video yao ya kihindi. Unajua unapopambana na cdm unapaswa kufikiria kesho itakuwaje.
 
Tutarajie mengi hadi 2015 na hili ni kuelekea anguko kuu la CCM.
 
If wishes were horses.....!

Ni nani aliyeweka youtube?

Iko wapi video ya Mwigulu Nchemba?

Ni kwa nini polisi waweke video tofauti na ile iliyopo youtube?

Kwa hiyo watajikanyaga ni ile walisema wameitoa Jamii Forums au kuna nyingine tena duh mwaka huu hawachomoki Zitto anapaswa kuhojiwa
 
hawa nao wanabwabwaja tu, issue iko mahakamani hizo hoja wapeleke huko mahakamani. mwisho wa siku ule mkanda alichukua ndio hata dhamira inawasuta kwahiyo wakamtetee huko mahakamani sio humu au kwenye vyombo vya habari, unless anataka watu waandamane
Magamba, mnalo hilo mambo yamesha wachachia
 
Mimi sina wasiwasi hata kidogo kwamba hii sinema inawavua nguo ccm muda mfupi ujao.
Walidhani wao wajanja lakini wamepatikana mchana kweupe.
Pigeni kazi mawakili wetu tuna imani kubwa sana nanyi lakini pia ueledi wenu unatupa matumaini makubwa.
 
picha ndo kwanza linaanza wataumbuka wengi
 
"Tumekaa jopo la mawakili watano; tumeiomba mahakama kuu iingilie kati na kuitisha mafaili yote mawili ya kesi hii na kisha ijiridhishe kama sababu ya kufutwa kwa kesi ya kwanza ni kwa ajili ya maslahi ya taifa," alisema.
Alisema maombi mengine katika hati hiyo ni pamoja na kuiomba mahakama ichunguze ili kuona kama haki imetendeka kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, pia wameiomba ifute hati ya kufutiwa mashtaka kwa Lwakatare na ifute amri ya kumaliza kesi hiyo.
" Hii kauli imenifurahisha sana, inaonesha ni kwa kiasi gani cdm walivyo makini, hawataki ubabaishaji na hawataki ushindi wa mezani. Kinachotafutwa ni hukumu ya haki na si bora hukumu
 
Tundu Lissu ni special case jamani wenye wivu wapande miti wajinyoge. Sina hofu kabisa na ninajua chadema walivyo smart kwenye mambo yao hii ngoma ya watoto lazima ikifika jioni wote warudi majumbani mwao wakalale tubakie wakubwa mitaani
 
Naona humu ndani
wameadimika kwelikweli. Wameanza kupata wasiwasi dhidi ya video yao ya
kihindi. Unajua unapopambana na cdm unapaswa kufikiria kesho
itakuwaje.

wanajilaumu kimoyomoyo kwa nn waliitoa hii vdeo
 
Ukiangalia video vizuri nina hakika Ludovick alimweleza Lwakatare na wakaamua kuitengeneza hiyo video ili wampe nchemba. Inaonekana kabisa Lwakatare anaelewa kuwa anarekodiwa, tatizo waliifanya ionekano kweli bila kushirikisha wataalam wa editing.
Lwakatare aliongea na msacky na hatujui waliongea nini inawezekana alimweleza kwamba ikitoka video fulani usishangae.
Ludovick si msaliti kwa sasa mpaka kesi ikiisha, anaweza akawa ndo ana
mabomu zaidi ya kumlipua Nchemba na CCM, tusubiri
 
Mahakama Kuu isikubali wala kuruhusu kuingiliwa. Uhuru wa Mahakama ni Msingi mmojawapo wa utawala wa sheria. Kutoa mwanya kwa Ofisi ya DPP kuyumbisha Mahakama ni udhalilishaji wa Mhimili huu Mkubwa wa Serikali.
 
Kwa hiyo watajikanyaga ni ile walisema wameitoa Jamii Forums au kuna nyingine tena duh mwaka huu hawachomoki Zitto anapaswa kuhojiwa

huyo jamaa mwenye rangi nyekundu mimi ananikera sana kwa mwenendo
 
Uwongo ni kazi ngumu sana kuisimamia ionekane ni ukweli. Chemba! Ujinga si kitu cha kujaribu
 
Back
Top Bottom