Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Kwa hiyo kama ni kweli Ludovick alijihusisha, naye ni masalia?. Kama ni masalia. CHADEMA ina masalia wangapi?. Lwakatare ni nani?.

Vuta Subira Mwongo/Mnafiki Mpe muda..........soon mtabaki wa mnyama!:yo:
 
Kwa wale waliokuwa wanasema hiyo video siyo ya Lwakatare nafikiri jibu limepatikana vizuri ila point wanayoshikilia wanasheria ni kuhusu sound editing kama wanavyosema hapa chini.





Mkuu we ni mshamba sana, yaani una-quote maneno mwenyewe kwamba .......''video imewekewa baadhi ya maneno''......hapo hapo unafurahi eti wamekiri wenyewe kuwa sio fake.......ivi inapobadilishwa baadhi ya maneno inabaki kuwa origino.....we wa wapi aiseee
 
hawa nao wanabwabwaja tu, issue iko mahakamani hizo hoja wapeleke huko mahakamani. mwisho wa siku ule mkanda alichukua ndio hata dhamira inawasuta kwahiyo wakamtetee huko mahakamani sio humu au kwenye vyombo vya habari, unless anataka watu waandamane
 
Hivi sasa wanasheria wa CHADEMA wanafanya mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na tukio la Lwakatare na makosa ambayo alishitakiwa nayo.

Anaeleza kuwa kama ameshitakiwa kwa ugaidi lazima makosa hayo yawe ni ya kigaidi, ila makosa ya Kidnapping na abduction ni makosa ya kawaida ya jinai , na kama ili yawe ya kigaidi ni lazima hayo makosa yawe yamefanyika kwa malengo ya kigaidi , na hata hati ya mashitaka haina maelezo ya makosa ya ugaidi .


Nyongeza: kuhusu video amesema tayari kuna ushahidi wa kimawasiliano baina ya Mwigulu Nchemba ya tarehe 28.12.2012 wakiwasiliana na Ludovick saa 5:55 asubuhi , na Lwakatare amesema kuwa yeye alikutana na Ludovick kuanzia saa tano asubuhi tarehe 28.

Aidha , ameongeza kuwa tarehe 27.12.2012 Denis Msacky alimpigia simu Lwakatare wakati akiwa njiani kurejea akitokea Kagera , akiwa Morogoro na kumuuliza kama yupo DSM , akamjibu yuko njiani.

Tatu, tarehe 29.12.2012 Mwigulu Nchemba , akiwa na Zitto na Mtatiro Star Tv , kipindi cha tuongee asubuhi ndipo alisema kuwa ana mkanda wa viongoz i wa chadema wakipanga mauaji ......sasa haya yote yatajulikana mahakamani.

Ziada .

Maelezo aliyotoa Lwakatare polisi kuhusu maneno yaliyoko kwenye video alisema kuwa yeye anakumbuka siku ya tarehe 28, alikuwa nyumbani kwake na Ludovick ndio alienda kwake , ila picha ya video ni ya kwake , sura ni ya kwake ila baadhi ya maneno yaliyoko sio ya kwake na ameandika hivyo , kwa hiyo kuhusu ukweli wa mkanda majibu ya kina yanatakiwa kutoka polisi , Mwigulu na Denis ndio wanajua nini kipo kwenye mkanda . Hivyo picha limeanza kuonekana , na kwa taarifa zaidi ni kuwa polisi wana video yenye dakika 27.06 na maneno yanatofautiana sana na yaliyoko kwenye You tube iliyowekwa kwenye mitandao .

Sasa polisi nao waliulizwa ni kwanini hawajamkamata aliyeweka hiyo you tube kwenye mitandao walitoa majibu yao na mawakili wanaendelea na uchunguzi wao.

CHADEMA mnalo
 
Tundu Lissu siku ile alijidhalilisha sana pale mahakamani mpaka akachekwa na umati wa watu!!!
Mimi mwenyewe naona unajidhalilisha humu JF na ninakucheka, lakini kwa kuwa niko peke yangu siwezi kujiita kuwa mimi ni umati. Sasa ZeMarcopolo wewe ulimcheka Tundu Lissu peke yako halafu unajiita wewe ni umati?
 
Nia yao siyo hicho kinachoelezwa na wanasheria bali ni udhalilishaji wa makusudi. ni kama mtu akuvue nguo kwa makusudi halafu aite watu wengine akishangilia ulivyo na akicheka!! maccm noma!!

Ss hapo anayedhalilika nani,km sio wao ambao wanazidi kuipa umaarufu cdm?
 
hawa nao wanabwabwaja tu, issue iko mahakamani hizo hoja wapeleke huko mahakamani. mwisho wa siku ule mkanda alichukua ndio hata dhamira inawasuta kwahiyo wakamtetee huko mahakamani sio humu au kwenye vyombo vya habari, unless anataka watu waandamane

Ulikuwa nambari wani kutaka kujua ukweli, na leo nakuona ni nambari wani kwa unafiki.......kwamba huhitaji tena kujua ukweli baada ya kupewa japo robo
 
Kwa hiyo kama ni kweli Ludovick alijihusisha, naye ni masalia?. Kama ni masalia. CHADEMA ina masalia wangapi?. Lwakatare ni nani?.

Sijui umri wako lakini kwa watu wazima kinachosemwa ni muhtasari ya mengi yaliyo kwenye maudhui. Kwangu mimi najua hatasalia hata masalia mmoja ndani ya CDM. Siyo kwa sababu Chadema ni wazuri sana kupambana na changamoto, bali ni kwa sababu msingi wao wa ukweli utanabahi unatoa fursa kubaini mambo mengi.

Kwenye uongozi kuna msingi wa mwongozo wa kutathmini hali (situation) unaitwa SWOT naamini unaujua. Nikianzia mwisho kwenye T CDM wanazisimamia kikamilifu Trends, O wanabaniwa sana, W wanazigeuza kuwa O, S yao ni kuaminika na umma. Niambia masalia watakatiza wapi.

Si vizuri kukukumbusha kuwa M<wigulu, Michuzi, Masalia, Ludo, Lwakatare ni watu siyo masuala/issues. Tulia jikite na issues kesi ya ugaidi, video, mahakama, polisi, CCM, TISS nk.
 
Pasco wa JF you have a best interest na hii kesi we are watching am optmistic wewe ni teja wa walio post video hiyo si bure kwa nini nasema hivyo unakatisha watu tamaa ,na unadhani mahakama kuu inafanya kazi ya suggestions za kwenye JF

How can one know if another have best interest in the case, if yourself dont have one?
 
Bila shaka wataeleza mahakamani hiyo yao wameitoa wapi!
Na hilo ndio kosa lililofanyika!
Ni dhahili hapa kuna mchezo mchafu!

Vedio ya You tube ni dakika 19.6,

Swari:

Je hii ya police wameitoa wapi?

Je Mwigulu kawapelekea police?
 
Kwa sasa wenye kujua hayo angalau kimazingira ni Ludo, Michuzi chini ya Mwigulu

Lwakatare kishamaliza kazi , mwenyewe kakiri baadhi ya maneno siyo ya kwake, ina maana mengine ni ya kwake mnataka nini mpaka hapo?
 
Mkuu Mpaka Kieleweke,
Kwanza poleni kwa yote!.
Pili mnayo team nzuri sana ya wanasheria, lakini nashauri, mara moja moja, muwe mnasikiliza maoni ya ma layman kama sisi kupitia humu jf.

Nasikitika kuwaambia kitendo cha kufungua kesi kuhoji mamlaka ya DPP, its a wastage of time!. Mamlaka ya DPP haihojiwi na mamlaka yoyote hata rais wa nchi, hawezi kuyahoji, hivyo you are fighting a loosing battle!.

Ni kweli timu yenu ya sheria is a good team, nashauri please seek legal opinion ya best criminal lawyers around, kwa sababu baadhi ya wanasheria wenu ni politiciancs, wajiangalie wasije wakaipoliticise hii kesi kuonekana its a political case, bali muendelee kuipigania iwe abduction na sio terrorisim!.

Mwisho mtake msitake, lazima Chadema kama chama, kitoe statement kuwa whatever mashitaka yanayomkabili Rwakatare, ni yake mwenyewe kama Rwakatare, vingenevyo hali ikiachwa ilivyo, kuna hatari ya jamii kuaminishwa kuwa hayo yaliiyotendeka, yamendwa kwa maelekezo ya chama, hivyo kuja kuwaingiza hata wasiokuwemo!.

Huu ni ushauri wa bure tuu toka kwa layman.

Pasco.

Kwanza nitoe ufafanuzi ufuatao,
Moja , kuwa Wanasheria wanahoji mamlaka ya DPP sio kweli , wao wanahoji jamo linaloitwa ..abuse of the court....hii ni kutokana na ukweli kuwa hakimu alipaswa kutoa hukumu juu ya kama kuna kesi ya kujibu ama laa, wao serikali wakaamua kufuta kesi namba 37 na kufungua nyingine ambayo kimsingi ni ileile , yaani kesi iliyofutwa ndio ilifunguliwa upya bila kuongezwa hata nukta ama neno lolote jipya , sasa hapo wanatumia hukumu iliyowahi kutolewa na Jaji Mroso wa mahakama ya Rufani kuhusu jambo hili na kuonekana kuwa kama DPP akifuta kesi bila kuzingatia maslahi ya umma ama bila kuonyesha kuwa lengo lilikuwa ni kuonyesha haki inatendeka , basi mahakama inamamlaka ya kuamua juu ya hilo.

Pili, ukisoma kifungu cha 245 (3) CPA utaona mamlaka ya mahakama kuhusu kutoa dhamana ama laa , jamo ambalo wanasheria wanaona kuwa jana kama hakimu angepata mwanya wa kutoa rulling yake basi hilo lingeweza kuamuliwa na akawa nje kwa dhamana halafu mpambano wa kesi uendelee huko mahakamani .

Naitafuta hukumu ya Jaji Mroso kuhusu Nolle , then mjadala utaenda vizuri.

Kuhusu hoja yako kuwa lazima Chadema itoe kauli kuhusiana na jambo hili na unataka iseme kuwa hayo yote ni ya Lwakatare , sio busara kwani kama chama kimewapa wanasheria wake suala hilo na wao wameshaweza kuanza kutoa ushahidi wa wazi jinsi ambavyo hii ni kesi ya kutunga na kubambikiana , sasa unawataka tena chama watoe kauli ya kukubaliana na kubambikiwa kesi kwa Lwakatare na wakina Mwigulu?

Kwa sasa wenye busara wanaweza kuelewa ni mchezo gani ulikuwa unachezwa , na hata kipindi cha star tv siku hiyo nasi,ia tayari kuna nyaraka zimenaswa za kuonyesha nani alihusika kufanya mwaliko wa kipindi na lengo lilikuwa nini , tusubiri muda ukifika itajulikana mbivu na mbichi.

Wapo wanaosema kuwa Dr.Slaa ameumbuka , hawa watakuwa ni majuha tuu , kwani alichosema yeye ni kuwa mkanda ni wa kutengeneza na walichosema leo wanasheria na alichosema Lwakatare polisi ni kuwa ni kwelii amelishwa maneno , sasa hapo kaumbuka vipi? Ni suala la kuelewa content na context tuu hapo.
 
Masaburi @ work!...

Mkuu Mpaka Kieleweke,
Kwanza poleni kwa yote!.
Pili mnayo team nzuri sana ya wanasheria, lakini nashauri, mara moja moja, muwe mnasikiliza maoni ya ma layman kama sisi kupitia humu jf.

Nasikitika kuwaambia kitendo cha kufungua kesi kuhoji mamlaka ya DPP, its a wastage of time!. Mamlaka ya DPP haihojiwi na mamlaka yoyote hata rais wa nchi, hawezi kuyahoji, hivyo you are fighting a loosing battle!.

Ni kweli timu yenu ya sheria is a good team, nashauri please seek legal opinion ya best criminal lawyers around, kwa sababu baadhi ya wanasheria wenu ni politiciancs, wajiangalie wasije wakaipoliticise hii kesi kuonekana its a political case, bali muendelee kuipigania iwe abduction na sio terrorisim!.

Mwisho mtake msitake, lazima Chadema kama chama, kitoe statement kuwa whatever mashitaka yanayomkabili Rwakatare, ni yake mwenyewe kama Rwakatare, vingenevyo hali ikiachwa ilivyo, kuna hatari ya jamii kuaminishwa kuwa hayo yaliiyotendeka, yamendwa kwa maelekezo ya chama, hivyo kuja kuwaingiza hata wasiokuwemo!.

Huu ni ushauri wa bure tuu toka kwa layman.

Pasco.
 
Nyongeza: kuhusu video amesema tayari kuna ushahidi wa kimawasiliano baina ya Mwigulu Nchemba ya tarehe 28.12.2012 wakiwasiliana na Ludovick saa 5:55 asubuhi , na Lwakatare amesema kuwa yeye alikutana na Ludovick kuanzia saa tano asubuhi tarehe 28.

Aidha , ameongeza kuwa tarehe 27.12.2012 Denis Msacky alimpigia simu Lwakatare wakati akiwa njiani kurejea akitokea Kagera , akiwa Morogoro na kumuuliza kama yupo DSM , akamjibu yuko njiani.

Tatu, tarehe 29.12.2012 Mwigulu Nchemba , akiwa na Zitto na Mtatiro Star Tv , kipindi cha tuongee asubuhi ndipo alisema kuwa ana mkanda wa viongoz i wa chadema wakipanga mauaji ......sasa haya yote yatajulikana mahakamani.

Ziada .

Maelezo aliyotoa Lwakatare polisi kuhusu maneno yaliyoko kwenye video alisema kuwa yeye anakumbuka siku ya tarehe 28, alikuwa nyumbani kwake na Ludovick ndio alienda kwake , ila picha ya video ni ya kwake , sura ni ya kwake ila baadhi ya maneno yaliyoko sio ya kwake na ameandika hivyo , kwa hiyo kuhusu ukweli wa mkanda majibu ya kina yanatakiwa kutoka polisi , Mwigulu na Denis ndio wanajua nini kipo kwenye mkanda . Hivyo picha limeanza kuonekana , na kwa taarifa zaidi ni kuwa polisi wana video yenye dakika 27.06 na maneno yanatofautiana sana na yaliyoko kwenye You tube iliyowekwa kwenye mitandao .

Sasa polisi nao waliulizwa ni kwanini hawajamkamata aliyeweka hiyo you tube kwenye mitandao walitoa majibu yao na mawakili wanaendelea na uchunguzi wao.


Mkuu Pasco

Kuna siku tutakuomba urudie yale maneno yako ya "bona fide genuine"

Soma hapo juu

Maana baada ya ili clip inawezekana wewe Pasco, Manyerere Jackton na maggid mlikuwa mmepagwa kuja kutuaminisha

BAHASHA BAHASHA NJAA MBAYA

 
Last edited by a moderator:
Bila shaka wataeleza mahakamani hiyo yao wameitoa wapi!
Na hilo ndio kosa lililofanyika!
Ni dhahili hapa kuna mchezo mchafu!

Mbona mnapenda kubahatisha mambo? Hizi propaganga tu kwamba dakika zinatofautina? zushi hakuna lolote hapo.
 
Hapo umeonesha jinsi usivyojua kusoma!

Mtahangaika sana ila sheria itachukua mkondo wake. SWALA LA MSINGI NI KWANINI APANGE KUTEKA WATU NA KUWAPA WATU DAWA ZA USINGIZI? HAIJALISHI VIDEO IMEPATIKANAJE. ILA NI KWANINI APANGE HAYO?
 
Hivi sasa wanasheria wa CHADEMA wanafanya mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na tukio la Lwakatare na makosa ambayo alishitakiwa nayo.

Anaeleza kuwa kama ameshitakiwa kwa ugaidi lazima makosa hayo yawe ni ya kigaidi, ila makosa ya Kidnapping na abduction ni makosa ya kawaida ya jinai , na kama ili yawe ya kigaidi ni lazima hayo makosa yawe yamefanyika kwa malengo ya kigaidi , na hata hati ya mashitaka haina maelezo ya makosa ya ugaidi .


Nyongeza: kuhusu video amesema tayari kuna ushahidi wa kimawasiliano baina ya Mwigulu Nchemba ya tarehe 28.12.2012 wakiwasiliana na Ludovick saa 5:55 asubuhi , na Lwakatare amesema kuwa yeye alikutana na Ludovick kuanzia saa tano asubuhi tarehe 28.

Aidha , ameongeza kuwa tarehe 27.12.2012 Denis Msacky alimpigia simu Lwakatare wakati akiwa njiani kurejea akitokea Kagera , akiwa Morogoro na kumuuliza kama yupo DSM , akamjibu yuko njiani.

Tatu, tarehe 29.12.2012 Mwigulu Nchemba , akiwa na Zitto na Mtatiro Star Tv , kipindi cha tuongee asubuhi ndipo alisema kuwa ana mkanda wa viongoz i wa chadema wakipanga mauaji ......sasa haya yote yatajulikana mahakamani.

Ziada .

Maelezo aliyotoa Lwakatare polisi kuhusu maneno yaliyoko kwenye video alisema kuwa yeye anakumbuka siku ya tarehe 28, alikuwa nyumbani kwake na Ludovick ndio alienda kwake , ila picha ya video ni ya kwake , sura ni ya kwake ila baadhi ya maneno yaliyoko sio ya kwake na ameandika hivyo , kwa hiyo kuhusu ukweli wa mkanda majibu ya kina yanatakiwa kutoka polisi , Mwigulu na Denis ndio wanajua nini kipo kwenye mkanda . Hivyo picha limeanza kuonekana , na kwa taarifa zaidi ni kuwa polisi wana video yenye dakika 27.06 na maneno yanatofautiana sana na yaliyoko kwenye You tube iliyowekwa kwenye mitandao .

Sasa polisi nao waliulizwa ni kwanini hawajamkamata aliyeweka hiyo you tube kwenye mitandao walitoa majibu yao na mawakili wanaendelea na uchunguzi wao.


[h=1]TUNDU LISSU AFANYA MKUTANO NA WANAHABARI LEO[/h]


Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu akiongea na wanahabari (hawapo pichani).
Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu leo amefanya mkutano wa wanahabari. Katika mkutano huo, Lissu ameongea yafuatayo:
1. Atafungua kesi Mahakama kuu kuiomba iiamuru Mahakama ya Kisutu kuendelea kusikiliza kesi ya awali iliyofutwa na DPP katika kesi inayomhusu Lwakatare kwani DPP amevuka mipaka yake inayomruhusu kufuta kesi na isitoshe kesi aliyofungua ni ile ile hivyo Mahakama iamuru shauri la awali liendelee.
2. Kuhusu video iliyoonyeshwa kwenye mitandao Lissu anasema kuna mashaka makubwa sana kuhusiana na video ile na kisheria kesi hiyo ikifika mahakamani haitachukua hata nusu saa ataibuka mshindi.
Lissu anasema
- Hakuna mtu anayepanga mauaji katika hadhara mahali ambapo watu wanapitapita kama inavyoonekana kwenye video ile.
-Lwakatare kama alirekodiwa basi lazima ielezwe je ilikuwa ni kwa hiari yake kama si hivyo ni makosa
-Issa Michuzi Mpiga picha wa Rais alikuwa akipongezana na watu wa Ikulu wenzake kuwa TISS (Usalama wa Taifa) wamefanya kazi nzuri kwa kurekodi ile video. Kisheria usalama wa taifa hawatakiwi wala hawaruhusiwi kurekodi au kuvifanyia ushushu vyama vya siasa kwa maslahi ya Chama tawala.
-Ludovick baada ya kukutana na Lwakatale tarehe 28 Desemba mwaka jana saa 5 muda mfupi baadaye yaani saa 5:59 alimpigia simu Mwigulu Nchemba kwa kutumia namba ya simu ya Mwigulu ambayo ameiandikisha kwenye kumbukumbu na vitabu vya Bunge Lissu anadai wana rekodi ya mazungumzo yao.
-Siku iliyofuata tarehe 29 Desemba mwaka jana akiwa kwenye kipindi cha Tuongee asubuhi cha Star TV alidai ana mkanda wa video unaowaonyesha CHADEMA wakipanga mauaji.
-Pia amedai itabidi waambiwe video hiyo imerekodiwa studio gani, maneno gani yameondolewa na yapi yameongezwa.
Anamalizia kwa kusema walianza kwa kusema CHADEMA ni chama cha familia wakashindwa, wakasema ni chama cha wachaga wakashindwa, wakesema ni chama cha wakatoliki wakashindwa, wakasema ni chama cha wakristo wakashindwa, wakasema ni chama cha ukanda wakashindwa leo wanasema ni chama cha kigaidi WATASHINDWA.


 
Back
Top Bottom