Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Mwafirika:
Jibu hoja hapa, hilo ndilo kubwa ili utueleze pumba ni zipi na mchele basi!

Hoja ni ipi mkuu wangu mongoiwe?

Nikiiona hoja nitaijibu bila kusita. Kwa sasa, unataka nijibu kitu kilichoandikwa JF na kikapatiwa majibu na wana JF?
 
Jamani lazima tuwe dynamic, mabadiliko ni jambo la msingi. Danda na Kufulila ni maafisa wadogo tu ktk chama, kama wameonyesha kiburi na kukosa nidhamu ni haki kuenguliwa ili kupisha wengine waendeleze chama.

Suala la kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba mwenyekiti ameitisha kikao cha kumfukuza kazi inaonyesha kuwa alikuwa na matatizo makubwa. Heko Dr. Slaa, chama lazima kiwe na watu serious. Akijirekebisha mrudisheni, kwasasa wapeni wengine. Bw. Lwakatare yupo hapo apewe cheo, tuufaidi utumishi wake.

Sasa tunataka utekelezaji wa operation sangara kwa ajili ya uchaguzi. Go chadema.
 
Mwafrika;

Samahani tena samahani sana. Baada ya kukusoma nimeona upeo wako au namna ya kujadili mambo ni sawa na Mama Sophia Simba wa CCM. Nimetanguliza samahani kama nimekutafsiri visivyo.

FP,

Nilikuwa sijaiona hii. Kama ndivyo unavyoona kuwa mimi ni kama Sophia Simba (is this name calling?) basi sidhani kama nina la kujibu hapo.

Hapa kinachojadiliwa ni kuwa, Je Mbowe hawezi kukaa meza moja na wanaotofautiana naye kimtizamo na kumaliza tofauti hizo?. Kwanini vikao vya siri visivyo rasmi?. Laiti angeitisha kikao rasmi yoote haya yasingekuwapo.

Una hakika hili halikufanyika?

Pia kwanini useme kuwa siwezi kufanya kazi na mtu?, Chadema sio kampuni ambayo lengo ni kutengeneza faida, hapa ni mitizamo tu mnakaa mezani mnayamaliza, tena ikibidi mnakaa ONE on ONE.

Hebu nakuomba tena fikiria OBJECTIVELY kwa manufaa ya TAIFA na si ya chama chenu.

Manufaa ya taifa ni yapi mkuu wakati wewe ushachagua upande - CCM?
 
Mwafrika akielezwa huwa mjuaji wa kila kitu, the best thing ni kuwa ameshakuwa marked na credibility yake ime slump down accordingly.

anatapatapa, hizi post atazijibu tu upende usipende

wait and see!

Hell yes nitazijibu.

Kama wewe uko kwenye mashindano ya umiss congeniality hapa basi utakuwa na long day in hell waiting.
 
Jamani lazima tuwe dynamic, mabadiliko ni jambo la msingi. Danda na Kufulila ni maafisa wadogo tu ktk chama, kama wameonyesha kiburi na kukosa nidhamu ni haki kuenguliwa ili kupisha wengine waendeleze chama.

Suala la kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba mwenyekiti ameitisha kikao cha kumfukuza kazi inaonyesha kuwa alikuwa na matatizo makubwa. Heko Dr. Slaa, chama lazima kiwe na watu serious. Akijirekebisha mrudisheni, kwasasa wapeni wengine. Bw. Lwakatare yupo hapo apewe cheo, tuufaidi utumishi wake.

Sasa tunataka utekelezaji wa operation sangara kwa ajili ya uchaguzi. Go chadema.
Matapishi ya CUF hayo..hana jipya..no other personalities besides him lol.
 
hutakiwi kumvumilia mtu anayetoa siri za chama huyo ni mhaini lazima afukuzwe la sivyo wapinzani wenu watapata faida.
 
Sioni tatizo kwenye hoja za Zitto, Slaa, na mwandishi wa habari hizi. This is all abotu speculations. Speculations from the media na kwa hao wanaodai wamefukuzwa kutoka katika chama. They should wait for the official letters if its true that they have been fired. Speculations za nini? Kama unajiamini wewe ni mpinzani wa kweli, unaanza kukurupuka nini? Start your own party for chrissake!
 
Kwanza hiyo 80% ya sample ya % ngapi? ukichaguliwa na watu sita kati ya watu 20 waliotakiwa wapige kura unasema mbele ya watu wenye akili timamu kuwa umeshinda?? labda udanganye kenge.
Mkuu, sometimes ushindi si lazima uwe umepata kura zote. Unaweza kushinda tu kwa kuwa hakuna aliepata kura nyingi kama wewe.

Ukiweza kutimiza masharti ya ushindi na ukatangazwa mshindi na mamlaka zinazohusika kisheria, basi utakuwa mshindi kihalali.

Kinachotakiwa si kulumbana wenyewe kwa wenyewe. Bali kujua kinachohitajika kuwa mshindi na kuchukua hatua za kuupata ushindi huo. La sivyo, tutamlaumu FP kama ndie anaetangaza matokeo.
 
VIongozi wengi wa chadema wanasoma kinachoandikwa humu. Kumbuka kuwa hata Mbowe alikuwa anakuja humu kabla hajaanza kutukanwa matusi ya nguoni na kina GT, mswahili na mafundamentalist wenzake.

Asante kwa ushauri mzuri mkuu.

Now i get it, its not frustrations tu kumbe kuna mengine mengi.......
 
KUNRADHI MHESHIMIWA WA CHADEMA AMBAYE HAPO MWANZO NILIKUFANANISHA NA MTU ANAYEJIITA MWAFRIKA. NIMEGUNDUA NIMEKOSEA NA NAOMBA UNISAMEHE KWA HILO.

omarilyas
 
KULA TANO BABA, NIMEMWELEZA JANA ZITTO KWENYE POST MOJA , the very same ideas

KWA NINI TUSIANZISHE CHAMA CHA VIJANA kitakacho hit kila kona na kuleta mwanga na matumaini ya kizazi hiki na kijacho

why kung'ang'ania chama kinachoongozwa kwa misingi ya CCM na uzee uzee, vimekaa ki NGO NGO, familia familia, n.k

Vijana ni taifa la leo na ndio tuko wengi

Magezi that idea is superb

Wakuu Magezi, Paintruth na wengine wenye misimamo kama yenu.
Mkishaunda hicho chama, baada ya miaka kumi mtakuwa vijana bado eeh? Au mtawafukuza vijana watakaokuwa wananakuja? Hakuna sumu mbaya kama ya kuunda makundi ya umri ambao unapita kwa kasi ya ajabu, bora makundi ya jinsi, angalao itahitajika operesheni kubadili lol
 
Wakuu Magezi, Paintruth na wengine wenye misimamo kama yenu.
Mkishaunda hicho chama, baada ya miaka kumi mtakuwa vijana bado eeh? Au mtawafukuza vijana watakaokuwa wananakuja? Hakuna sumu mbaya kama ya kuunda makundi ya umri ambao unapita kwa kasi ya ajabu, bora makundi ya jinsi, angalao itahitajika operesheni kubadili lol

Labda watakuwa kama Nchimbi (anaendelea kujiita kijana) au Kikwete ambaye hadi leo miaka karibu 60 watu wanamwita raisi Kijana. Chama chao kitakuwa cha vijana ambao hawazeeki.
 
JF wakati mwingine tunasikitisha sana. Yaani kuanzia page ya 1 mpaka ya 12 ni malumbano ambayo hayana kichwa wala miguu. Huwa tunaanza ku-react kwenye mada kabla ya kupata full information.

Ninadhani ni mapema sana kutoa mchango kabla hatujajua kwanini Kafulila kavuliwa madaraka? Barua yake ndiyo inaweza kutoa sababu na based on the reasons za kutenguliwa uteuzi huo, ndipo tunaweza kuweka maswali na hoja za kueleweka.

Je, utenguzi huo umefuata Katiba ya Chadema?
Je, wamefuata taratibu na kanuni zao?
Je, tuhuma alizotuhumiwa nazo zina ukweli?
Je, walitumia njia gani kuzithibitisha ama ni yeye mwenyewe alikiri?
Je, alipewa nafasi ya kujitetea? Na mengineyo mengi.

Michango yetu hapa ni muhimu sana kwa vyama vyote vya siasa. Huwa kuna vingunge wa vyama vyote wanakuja kuchukua madesa na hoja. Tukianza kuleta ushabiki tutashusha hadhi ya JF.

JF ina jina kubwa sana kwenye politics za Tanzania.

Keil

Asante Sana, very objective. Wana JF tunawajibu kuimaintain heshima ya JF na credibility yake. Tupunguze personal attacks na character assasinations tuendelee kujikita kwenye issues.
 
Samahani wdau huyu Kafulila ndio nani? katika Chadema.Na kafanya madudu gani mpaka uteuzi wake utenguliwe.
naomba datas.

kafulila ni afisa habari na uenezi wa chadema. hii njemba mwaka jana iliporomoka toka gorofa ya kumi ikagonga kichwa na tangu wakti huo akili yake haijaka sawa. inasadikiwa amedisko mlimani amekacha shule sasa anabangaiza akiutafuta ubunge mwakani. ameshindwa kazi ya uenezi kutokana na kuendekeza mikwaruzano na wandishi wa habali. sio hio tu ana bifu sana na mbowe na huwa anakataa katokato kutoa pres release inayompamba bosi wake. ameishia kuandika kwenye magazeti ya hoja na rai makala zilizogubikwa na chuki za kikabila . jamaa mtelezo sana na ameapa kwamba yuko radhi chama kife kama mbowe ataendelea kuwa myenyekiti. hio ndio imekuwa ajenda yake mahususi tangu alipokamatwa akijalibu kuiba kura za uwenykiti wa vijana akishirikiana na mtuhumiwa mwenzake dadi juju. ni sahihi kabisa kutoswa madarakani kwani katibu mkuu ndio mwenye huo uwezo kikatiba ya kuteua na kuengua maafisa wa sekritariat. slaa na mbowe mmechelewa sana hiki kibudu chenye sumu kilitakiwa kimwagwe long time!!!!
 
- Well kama hii habari ni ya kweli, then Mbowe ni Mwenyekiti ambaye Tanzania tunamuhitaji sana as opposed na Wenyekiti wa huko CCM, TLP na CUF. I mean mnyonge mnyongeni, mwanachama hawezi kubwa bigger than chama, ni lazima kila mwanachama afuate utaratibu wa chama, meaning katiba ya chama kama kuna mwanachama anavunja katiba kwa mwenendo wake usiofaa kwa chama then ni wajibu wa Mwenyekiti kuchukua hatua za haraka, ambazo zinaenda na katiba,

- Sio lazima kila mkutano wa chama cha siasa uwe wa public, sometimes kuna vikao lazima viwe vya siri Mwenyekiti wa chama cha siasa ana haki zote kikatiba kuita mkutano wa aina yoyote ile as long as analinda interest ya chama kile in the big picture na hana sababu ya kujibu swali la anybody kuhusu chama chake, lakini lazima demokrasia itendeke kwa maana ya matokeo ya kikao hicho cha siri kuendana na katiba ya chama kile.

- Ujumbe wangu kwa Mbowe, kwa kawaida huwa sikubaliani na mengi ya huko Chadema kwa sababu huwa hayaendani na katiba ya chama hicho, lakini on this one I am with you kama ni kweli, isipokuwa tu whatever the outcome ya hivi vikao vya siri, ni lazima iendane na katiba ya chama. Kuita vikao vya siri ni sawa kabisa wala haijavunjwa sheria ya jamhuri au ya chama, tatizo tu ni matokeo kama yataendana na katiba then hamna sababu ya kujali anything! kumbuka hiki ni kipindi kigumu sana cha kukaribia uchaguzi na kuna mengi sana yanayoandaliwa undeground na wasiolitakia mema taifa letu, lakini dalili zote ziko wazi kuwa wanashindwa, sasa wanatapa tapa na haya magazeti nayo ni lazima kuwa makini nayo sana maana nguvu zao nyingi maadui wa taifa hili zimepandwa huko. Huu ni wakati muafaka wa kutengeneza vyama viwe imara, kulinusuru taifa hili na dogs!

Respect.


FMEs!
 
Heee haya makubwa! nimekuwa msomaji tu maanake hii habvari nzima kaam kile kipindi cha kina mama Radio Clouds - HEKAHEKA!
Yangu macho, wasiojua kusoma na wasubiri muadhana!
 
JF wakati mwingine tunasikitisha sana. Yaani kuanzia page ya 1 mpaka ya 12 ni malumbano ambayo hayana kichwa wala miguu. Huwa tunaanza ku-react kwenye mada kabla ya kupata full information.

Ninadhani ni mapema sana kutoa mchango kabla hatujajua kwanini Kafulila kavuliwa madaraka? Barua yake ndiyo inaweza kutoa sababu na based on the reasons za kutenguliwa uteuzi huo, ndipo tunaweza kuweka maswali na hoja za kueleweka.

Je, utenguzi huo umefuata Katiba ya Chadema?
Je, wamefuata taratibu na kanuni zao?
Je, tuhuma alizotuhumiwa nazo zina ukweli?
Je, walitumia njia gani kuzithibitisha ama ni yeye mwenyewe alikiri?
Je, alipewa nafasi ya kujitetea? Na mengineyo mengi.

Michango yetu hapa ni muhimu sana kwa vyama vyote vya siasa. Huwa kuna vingunge wa vyama vyote wanakuja kuchukua madesa na hoja. Tukianza kuleta ushabiki tutashusha hadhi ya JF.

JF ina jina kubwa sana kwenye politics za Tanzania.

Hayo yote nimeuliza huko nyuma, Mwafrika ndo pekee akajitolea kutafuta majibu.

Wengine wakaanza kutukana.
 
Back
Top Bottom